Hakuna Taifa lililoendelea kwa kujipendekeza na kujidharau

Hakuna Taifa lililoendelea kwa kujipendekeza na kujidharau

Siyo peke yako uliyewahi kuishi huko, kama kweli uliwahi kukaa huko.

Uliyoandika hapa ni kama ni mwenyeji wa huko, au umeolea huko, na pengine kuwa na maslahi binafsi na huko.

Ndiyo, yapo waliyofanikiwa kuyafanya vizuri, mfano mzuri ni elimu yao iko imara zaidi, lakini hilo haliifanyi nchi hiyo iwe "...juu sana kwenye mambo mengi," kama unavyodai
"Raia kujitambua," una maana gani? Umefika kule Baringo ukakuta raia wapo tofauti sana na hawa waliopo Liwale katika kujitambua?
Unachukulia tu kakikundi uliko-'interact' nako hapo ulipofanya vikozi vyako ndiyo ukadhani kuna "seriousness, bidii na uwajibikaji, professionalism", ambayo huku Tanzania haipo mahali popote? Umefanya utafiti ukakupa majibu hayo?

Halafu unachekesha kweli: yaani hata "utembeaji" wa watu unauwekea uzito wai kuonyesha tofauti zilizopo kati ya watu walioko Nairobi na hawa , sijui wa Dar es Salaam au Tanzania yote?
Yaani unataka Tanzania twende Nairobi, tukajifunze kutembea kama wao? Hapo hali zetu ndipo zitakapoonekana kuwa nafuu kidogo kama wao?

Ninachohimiza waTanzania tujitahidi kukifanya kwa bidii zaidi kuliko kitu kingine kwa haraka zaidi, ni kuifanya elimu yetu iwe imara. Elimu yetu inaupungufu sana, na ndio maana, kama huyu 'Executive Sister' ni mTanzania kama inavyoonekana anadai yeye, anadiriki kuandika vitu vya ajabu sana kama alivyoandika hapa. Msingi wake wa elimu ulikuwa duni sana, licha ya kwamba hata hivyo vikozi alivyofanya huko Nairobi inaonyesha havikumsaidia kitu, kutokana kuwa na msingi mbovu tokea mwanzo.
Siko hapa kushindana kuishi ughaibuni. Na wala hakuna sehemu niliyosema ni mimi tu nipo ughaibuni au kuishi au kuwahi kufika huko. Soma uelewe. Hayo umeanzisha mwenyewe. Kuna maelfu ya watanzania ughaibuni. Nakuona weye huna hoja unataka leta ubishi wa kitoto. Hivyo napuuzia ulichoandika. Samahani sana sipo kubishana. Nipo kujenga hoja kwa watu waelewa waliona mawazo ya kujenga.
 
Siko hapa kushindana kuishi ughaibuni. Na wala hakuna sehemu niliyosema ni mimi tu nipo ughaibuni au kuishi au kuwahi kufika huko. Soma uelewe. Hayo umeanzisha mwenyewe. Kuna maelfu ya watanzania ughaibuni. Nakuona weye huna hoja unataka leta ubishi wa kitoto. Hivyo napuuzia ulichoandika. Samahani sana sipo kubishana. Nipo kujenga hoja kwa watu waelewa waliona mawazo ya kujenga.
Sasa angalia upuuzi huu. Kenya nayo unaiita "ughaibuni"?

Mimi nimemjibu 'Executive Sister', hapa wewe 'Wilderness Voice' ni kipi kinachokuhusu?

Lakini hata kama ni wewe unayetumia majina mbalimbali humu, ninaridhika kabisa kwamba jibu nililokupa limekuondoa fahamu kabisa na kujiona jinsi ulivyoandika upuuzi katika bandiko lako nililolijibu.

Hili liwe ni fundisho kwako na wenzako, msiwe mnajiandikia tu vitu vya kipuuzi puuzi kudhalilisha taifa lenu (kama kweli nawe ni mTanzania mwenzangu).

Mnaudhi sana.

Utajengaje hoja kwa kulidhalilisha taifa lako, tena kwa mambo ya uongo? Nani atafaidika na hoja za namna hiyo?
 
Wewe uwezi ondoa ufahamu wangu kwa kuandika pasipo kuzingatia hoja. Na kisaikolojia mtu anapom attack mtu kwa maneno anakuwa na upungufu wa hoja. Kikubwa shusha hoja si shambulizi kwa mtu. Leta hoja ipimwe. Simaneno ya mipasho.
Kwa kifupi siko kama unavyofikiri, uwa sibabaiki kwa vijineno. Bali ninamkubali mtu anaejenga hoja nikaona hapa kweli pana hoja. Vijimaneno neno kwangu, uwa napuuza.
Karibu ujenge hoja.
 
Wewe uwezi ondoa ufahamu wangu kwa kuandika pasipo kuzingatia hoja. Na kisaikolojia mtu anapom attack mtu kwa maneno anakuwa na upungufu wa hoja. Kikubwa shusha hoja si shambulizi kwa mtu. Leta hoja ipimwe. Simaneno ya mipasho.
Kwa kifupi siko kama unavyofikiri, uwa sibabaiki kwa vijineno. Bali ninamkubali mtu anaejenga hoja nikaona hapa kweli pana hoja. Vijimaneno neno kwangu, uwa napuuza.
Karibu ujenge hoja.
Mkuu 'Widerness Voice', nadhani kuna kutoelewana hapa.

Mimi sikujibishana nawe mahali popote.
Hiyo uliyoni'quote' nilikuwa namjibu Executivesister, na wala sio wewe, sasa tatizo limetoka wapi?

Lakini, kama wewe ndiye unafahamika kwa jina lingine la Executivesister; bado sioni kama nilikushambulia binafsi bila ya kuishambulia hoja yako.
Jambo linaloumiza, kama wewe hujui, ni kuidhalilisha nchi yetu, kuidharau, kama Executivesister alivyofanya. Huko sio kujenga hoja, bali ni kutufanya sote tuonekane duni kwa hao unaowasifia, jambo ambao sio kweli kabisa.
Kenya hawatuzidi kiasi cha kuwaona wao ni bora zaidi yetu sisi.
 
Mkuu 'Widerness Voice', nadhani kuna kutoelewana hapa.

Mimi sikujibishana nawe mahali popote.
Hiyo uliyoni'quote' nilikuwa namjibu Executivesister, na wala sio wewe, sasa tatizo limetoka wapi?

Lakini, kama wewe ndiye unafahamika kwa jina lingine la Executivesister; bado sioni kama nilikushambulia binafsi bila ya kuishambulia hoja yako.
Jambo linaloumiza, kama wewe hujui, ni kuidhalilisha nchi yetu, kuidharau, kama Executivesister alivyofanya. Huko sio kujenga hoja, bali ni kutufanya sote tuonekane duni kwa hao unaowasifia, jambo ambao sio kweli kabisa.
Kenya hawatuzidi kiasi cha kuwaona wao ni bora zaidi yetu sisi.
Ok, Nimekuelewa ndugu yangu Kalamu 1: Samahani kwa nilipokukosea. Ni binadamu na kunakughafirika. Na Naamini Kenya sio wa kubabaikiwa!
 
Tanzania ndo Taifa pekee hasa kwa miaka ya sasa ambapo kuanzia viongozi wake na wananchi ujidharau na kusifia mataifa mengine kwa kujipendekeza.

Wakati wa Baba wa Taifa haya mambo hayakuwepo. Hatukubembeleza mtu au Taifa. Hata Jomo Kenyatta enzi hizo alionja shubiri za Nyerere. Si mara ya kwanza Tanzania kuwa na vita ya maneno na ya kiuchumi na Kenya.

Rais Kamuzu Banda pia aliwahi onja joto ya jiwe. Nakumbuka mashuleni hadi tuliimba. "Banda wa malawi katuvalia ngozi simba, kututishia watanzania hatujali...hatujalii. Watanzania tulisimama wamoja. Banda kwa mkwara tu akafyata mkia. Lakini bado Tanzania tulibaki imara (Kwa sauti ya Msechu)

Viwanda viliendelea, tulisoma bure kuanzia chekechea au vidudu hadi chuo kikuu. Tulisafirishwa bure kwa wale wa boarding. Tulipewa daftari na kalamu shuleni. Kulikuwa pia na magari ya shule. Maduka ya serikali na mabasi ya serikali kila mkoa. Kulikuwa na viwanda mikoa mingi. Mabus ya wafanyakazi. Kulikuwa na bustani au park zilitunzwa vizuri. Watu tulienda kupumzika mandhari nzuri na familia. Miji ilipangiliwa. Barabara nyingi zilikuwa na miti pembeni. Leo hakuna kitu. Sijui vilienda wapi.

Pamoja na kiburi chetu hakuna kubembeleza. Tulifunga balozi hadi za uingereza na kukataa misaada yao. Ujerumani Mashariki nao tukawagomea. Israel na wengineo lkn bado Tanzania tulieshimika duniani.

Leo tumekuja na siasa za kubembeleza. Kujipendekeza, kusifia wengine. Leo Watanzania tunaona Wakenya kama ndo wakombozi wa uchumi wetu. Miungu wetu. Leo tunawapa rukhsa waingie mbungani kwetu. Wawe huru. Wawekeze kila sehemu. Ni vizuri. Lakini tunaijua vema Kenya? Nani alivunja umoja wa Afrika mashariki? Nani alidhurumu mali za umoja huo? Nani alitumiwa na majasusi kuvunja huo umoja?

Eti leo economic democracy yetu ni kujiona sisi wajinga ila mataifa mengine ni wajanja. Kazi yetu ni ziara za kusaini mikataba tunayopewa kusaini. Hata hatuna muda wakufikiria. Kisa hatutaki hudhi mtu.

Naomba ziara zingine watanzania tuwe tuna taarifiwa kabla ili tujue nini kinaenda fanyika na pia kama ni mikataba ijadiliwe kwanza bungeni na watanzania tuelewe.

Mtamsema sana vibaya Mwl. Nyerere lakini hatabaki kuwa mdiplomasia wa hali ya juu. Alikuwa mbabe lkn bado aliheshimika na mataifa makubwa.

Mtamsema vibaya na kumtukana Magufuli lkn nchi nyingi zilimtambua kuwa alisimama kwa masilahi mapana ya Tanzania. Hata Mkapa hakuwa na siasa za kubembeleza mataifa ya nje.

Angalia marekani, Uchina, Uingereza, Ujerumani na mataifa mengine wapi wanasera za kubembeleza na kusifia mataifa mengine. USA ilifikia sehemu kuweka vikwazo katika biashara na nchina japo USA inamtegemea China kwa biashara. Kikubwa ni kuangalia maslahi mapana ya nchi.

Eti leo tunasifia wakenya wanademokrasia zaidi ya Tanzania. Ni vizuri. Watanzania wanabaki kujidharau. Wanajiona wao si kitu. Kweli katika kukua tunaona mengi. Kujipendejeza sio kusifiwa ni kuzidi kudharaulika tu. Magufuli alikuwa mkorofi na mbabe. Lakini Tanzania iliheshimika. Hakuongea kiingereza lkn hotuba zake zilifatiliwa dunia nzima kusikia nini atasema. UN wenyewe walikubali kuwa alikuwa mtu aliependa Taifa lake na Afrika.

Korea kaskazini aijipendekezi lkn Marekani wanaogopa na kuheshimu Korea kaskazini. Duniani hapa mataifa makubwa yenye nguvu yote yalitumia ubabe.

Hata ukoloni ulifanyika kwa ubabe ili watawala wapate watakacho. Hata katika Biblia watawala hakuna alie kuwa lele mama. Hakuna alie jipendekeza na kusifia wengine.

Haya twendelee na kusifia, kubembeleza na kujipendekeza tuone hayo maendeleo. Hii awamu ya (-6<+4) imenikumbusha mbali hesabu za mlinganyo na magazijuto.

Hongera Rais wetu Samia Suluhu Hassan. Nakupenda ila kuwa makini na washauri wako. Hasa huyo ambae wakati wake nchi ilimshinda. Hata alipoulizwa kwanini Tanzania ni masikini wakati ina kila kitu. Alijibu hata yeye hajui na anashangaa kwanini Tanzania ni masikini. Ulikiri mwenyewe hotuba yako ya Bungeni kuwa anakushauri sana pamoja na yule bwana aliesema ataendeleza majengo alojenga babake lakini hakashindwa akabakiza majungu tu kule kwetu minazini.

Baba yake alikuwa na aakili kubwa. Ange kuwepo kule minazini kungekuwa dubai ndogo. Tusisingizie Muungano. Tunapotezwa tu. Yule baharia aliijenga nchi yetu ya minazini wakati huo huo wa muungano. Hata Dar wakati huo haikujengwa kama baharia alivyo ijenga minazini. Leo tunabaki lalamikia muungano badala ya kujikita kuijenga nchi yetu.

Yangu macho. Twendelee kujipendekeza. Kusifia na kuona sisi hatuwezi jenga uchumi wetu isipokuwa wawekezaji. China ilikuwa sawa na Tanzania miaka ya nyuma. Leo ni Taifa kubwa. Je, walitumia sera ya kujipendekeza na kusifia wengine na kujidharau?

Wachina walifanya kazi hawakutegemea wawekezaji uchwara kama Kenya. Walisomesha vijana wao nje, wakaiba tekinolojia toka mataifa makubwa. Wakaunda tekinolojia yeo. Rushwa ikapigwa vita ni kunyongwa tu. Taifa likasimama.

Watanzani leo hatuna scholarship kwa ajili ya Watanzania pekee kama yalivyo mataifa mengine. Mfano Afrika Kusini, Nigeria, Ethiopia na mengineyo hasa kwenda kusoma nje. Nashangaa balozi zetu hazina ubunifu.

Viongozi wengi tulionao leo walipelekwa kusoma nje na serikali. Leo wamekuwa wabinafsi.

Tanzania tu vijana wanaakili kwenye ubunifu na sayansi. Tuwatumie hawa. Tuwajari. Nchi imebaki majungu. Nchi imekuwa siasa kila kitu. Tunajenga shortcut ya maisha.

Viongozi tuwe na maono. Maendeleo hayaji kwa kujipendekeza. Watu watapata machungu ya maisha ila baadae wataenjoy. Nchi zote upitia huko. Ndo tutaona maendeleo ya kweli.

Karibu tena Ikulu kwa remote control. Nawe waziri wa mambo ya nje ulikuwa katibu Mkuu wa wizara ya mambo ya nje wakati wa team Msoga. Uliishia kutuletea Bush, Obama na hatukuona tija. Tulipata neti za mbu pekee.

Rais na baraza na taasisi waliishia kwenda nje. Nakuomba ubadilike. Mshauri vizuri mama. Najua anashaurika na akitulia ni kiongozi na Rais mzuri.
Na hao wachina wanasema no hardship that will break you.
Burning spirit ilikuwa mapinduzi makuu ya uchumi kwa kwenda nchi jirani na kuibua ujuzi kutoka huko.
 
Back
Top Bottom