Hakuna ubishi, bila biblia, hakuna uislam. Kama ukristo ungedukua na kukopi na kupaste quran, hali ingekuwaje?

Hakuna ubishi, bila biblia, hakuna uislam. Kama ukristo ungedukua na kukopi na kupaste quran, hali ingekuwaje?

Soma vizuri torati au agano la kale au taurat ulinganishe, pia jikumbushe uislam unavyomkubali Yesu wakati ukristo ukigoma kutofanya hivyo. Jielimishe kwanza badala ya kuhoji bila kujua unachohoji mwanangu. Simpo.
Uislamu unamkubalije Yesu na Ukristo unamkataa vipi Yesu ?

YESU ndiye mwanzilishi wa Ukristo

Waislamu hawamtambui Yesu kama mwana wa Mungu na anayeondoa dhambi

Waislamu wanamtambua jamaa mmoja anaitwa Isa ,ambaye ni tofauti kabisa na Yesu
 
Umewahi Kufika China?
Tamaduni za Kichina Unazijua?
Sijakataa Ni jamii kinachozungumzwa Ni majority..
Asilimia 80 ya Wachina hawana Dini ya Ukristo wala Uislamu..
Nakuelewa ila uliposema wasihusishwe wachina kwa sababu wana dini yao ndio nikakumbusha tu kwamba hiyo ni jamii hivyo wapo waislamu na wakristo miongoni mwao.
 
Hapo kinachoangaliwa ni Asili
Wanaoshiriki hiyo Asili ni Watatu
Wote Wana Asili Moja,sifa Moja na wanafanya kitu kimoja kwa wakati mmoja,

Binadamu ni Asili na wanaoshiriki hiyo Asili ni wawili
Mwanaume na mwanamke
Hao wanafanana kila kitu wote ni fresh na intelligent

Kungekua na viumbe tofauti wanaoshiriki hii Asili ndio tungesema tupo wengi

Kwa mfano huo nadhani angalau umeelewa!
Nilivyoelewa mimi hapo umefanya kuwa kuna Uungu na kuna hao watatu wanaoshiriki hiyo asili ya Uungu, na ndipo najiwa na swali la hao watatu ni kina nani ambao ndio hushiriki uungu? Maana ukitamka binaadamu inajulikana unazungumzia mtu na watu tupo wengi.

Lakini pia hao watatu wenye kushiriki asili ya uungu tumekuwa tukiona wakielezwa kufanya mambo tofauti kati ya mmoja na mwengine kwa nyakati tofauti au wana majukumu tofauti.
 
Uislamu unamkubalije Yesu na Ukristo unamkataa vipi Yesu ?

YESU ndiye mwanzilishi wa Ukristo

Waislamu hawamtambui Yesu kama mwana wa Mungu na anayeondoa dhambi

Waislamu wanamtambua jamaa mmoja anaitwa Isa ,ambaye ni tofauti kabisa na Yesu
Kama Yesu ni tofauti na Isa japo waislamu humkusudia Yesu wanapomtaja Isa, sasa mbna majini huwa mnasema ndio malaika waiyoasi japo waislam wenyewe wanasema majini ni viumbe tofauti na malaika na binaadamu? Huo ufanani wa majini na malaika waliyoasi ni upi?
 
Kama Yesu ni tofauti na Isa japo waislamu humkusudia Yesu wanapomtaja Isa, sasa mbna majini huwa mnasema ndio malaika waiyoasi japo waislam wenyewe wanasema majini ni viumbe tofauti na malaika na binaadamu? Huo ufanani wa majini na malaika waliyoasi ni upi?
Mm sio muislamu
 
Vatican mungu wao nani

kutoka Kitabu cha Ufunuo (Revelation) katika Biblia, hasa Ufunuo 13:1-10, ambapo "joka" linawakilisha Shetani na "mwanamke" ni mnyama au mfumo wa kisiasa na kidini.

Katika sura hii, mnyama ambaye ni "mwanamke" anapata nguvu na mamlaka kutoka kwa "joka," na inatajwa kuwa anawashinda watakatifu wa Mungu. Kwa kawaida, hii inahusishwa na mfumo wa kishetani, kwa upande mwingine, inaweza kumaanisha mapambano kati ya mafundisho ya kweli na ya uongo.
 
Kwa mara nyingine Tena makafiri wameshamkumbuka Papa wao kutoka Vatican na tayari vinyeo vimeshaanza kuwawasha hapa ndugu mtazamaji wanakusanyika kwa wingi hapa na kuanza kumchokonoa Baasha ili aje awakune ila mpaka sasa naona mabaasha hawajotekea nadhani wako vibanda umiza wanaabgalia Game ya Mabaasha wakuu wakicheza na Utopolo haya ngoja tuone kwa hali hii naona Makafiri yakipata tabu na kuruka ruka wakidai wanawashwa sijui nani ajitokeze awaondoe huu wahka unaowakuta ndugu makafiri.Nikilipoti kutoka kusikojulikana mi mimi ripota inch 9 wa kitaa media.
Nawewe ni muumini wa Dini ya Mwenyezi Mungu?
 
Ni vitu common kweli, sasa nashangaa inakuaje inaoneka uislamu umekopy maandiko ya wakristo kwa kumaanisha biblia hali ya kuwa biblia huo mkusanyiko wake una vitabu hadi ambavyo vilikuwepo kabla ya ukristo?

Na hapo ndipo inapokuja hoja ya kujimilikisha vitabu au maandiko ambayo yalikuwepo kabla hata ya kuwepo ukristo.
Ukristo umetokana na KRISTO sasa utaitenga vipi Bible AGANO la Kale n AGANO JIPYA? Aliyeandika vitabu 5 vya mwanzo ni Musa na huyo ni mmoja ya uzao wa waisrael na ndiye aliyetumwa kuwatoa huko Egypt na YESU kazaliwa katika mlolongo huo unatenga vipi?
 
Ukristo umetokana na KRISTO sasa utaitenga vipi Bible AGANO la Kale n AGANO JIPYA? Aliyeandika vitabu 5 vya mwanzo ni Musa na huyo ni mmoja ya uzao wa waisrael na ndiye aliyetumwa kuwatoa huko Egypt na YESU kazaliwa katika mlolongo huo unatenga vipi?
Yenyewe imejitenga kwa maana hakuna kitabu cha Mungu chenye kuitwa biblia, ndio maana ni muhimu kuzingatia biblia imekusanya vitabu hadi barua. Sijazungumzia ukristo umetokana na nini bali ukristo umeanza lini.
 
Ukatoliki ulianzisha Uislamu kama njia ya kisiasa na kidini ya kudhoofisha nguvu za Ukristo na Uprotestanti. Matukio mbalimbali, kama vile Constantine (306-337 AD), Mapinduzi ya Uprotestanti (1500s), Migogoro ya Dola la Ottoman (1200-1300s), na Kuanzishwa kwa Uislamu (622 AD) yanaweza kuunganishwa kupitia mtindo wa kudhoofisha nguvu za dini na kisiasa, na kuonyesha jinsi mikakati ya Ukatoliki ilivyokuwa na athari kwa kuanzishwa kwa Uislamu.
Unachokiongea Unakijua??
Au Niulize tena Hivi Ulichokiandika Ulikisoma Kabla ya Kukituma?

Yaani Ulichoandika Ni sawa na Mtu mwenye akili timamu asimame aseme..
"CCM ilianzishwa baada ya Tanu na ASP kuungana Ili kuweza Kushindana na CHADEMA.."

Nitaona Hauko Serious na Una matatizo ya Akili kwa Sababu How comes CCM iliyoanzishwa mwaka 1977 iundwe kwa ajili ya Kupingana na Chama Kilichoundwa maaka 1992 ??

Sasa hicho ndo ulichoandika wewe..

Kwamba Uislamu ulianzishwa kwa ajili ya Kupunguza Nguvu ya Uprotestant yaani Uliposema Tu hivyo nilipata akili ya kusema nikupuuze ila kuna Sauti nyingine moyoni ikaniambia kuwa Huenda kweli hujui na Nikueleweshe..

Uprotestant ulianza rasmi Miaka ya 1517s wakati Martin Luther, kasisi wa Kikatoliki kutoka Ujerumani, alipoweka Theses 95 kwenye mlango wa Kanisa la Wittenberg. Hati hizo zilikuwa na malalamiko dhidi ya Kanisa Katoliki, hasa kuhusu malipizi ya misamaha ya dhambi (indulgences). Na Hapa ndo chanzo cha Matengenezo au Protestant Reformation..na baadae ndo wakaja kina John Calvin na Huldrych Zwingli na wengineo na Ndiyo chanzo cha Uprotestant..

Sasa Kaka yangu Hamisi Uislmu imeanzishwa mwaka 622 AD
wakati Huo uprotestant umekuja Uislamu ukiwa Tayari umeshashamili Na Una miaka 900 na Sehemu yaani Una miaka 1000 ndo uprotestant ukaja..
Huwezi kusema kuwa Uislamu ulikuja Kuua Uprotestant wakati uprotestant umeukuta Uilslamu..
 
Back
Top Bottom