Hakuna ubishi, S2kizzy ni producer bora kuzidi mkongwe Master Jay

Hakuna ubishi, S2kizzy ni producer bora kuzidi mkongwe Master Jay

Aisee kwani una ugomvi na Master J? Kwanini yeye kati ya maprodyuza wote? Halafu, hivi hakukuwa na picha nyingine mpaka uweke hii?
Kwa sababu ni mkongwe anaependa kukashifu maprodyuza vijana anawaonea wivu sana yeye hajawai kutengeneza international hits kina s2kizzy washafanya mpaka na kina maluma
 
So point yako ni ipi? Masta jei kamzidi kitu gani zombie kwenye production zaidi ya ukongwe?
UNa umri wa miaka Mingapi?
Kwanini nakuuliza hivyo..
Pengine Kipindi cha miaka 2000s ulikuwa hujazaliwa so huenda hujui hata mazingira ya Muaka hiyo ilikuwje..

Sasa ngoja nikupe Mfano Dhahiri miaka ya 80s kulikuwa na Shule chache za secondary hivyo wanafunzi wengi tulifaulu ufaulu wa juu sana ila shule zilikuwa chache Tanzania nzima shule hazikuzidi 20..

Kwahyo unaweza kukuta mwanafunzi wa zamani enzi hizo akawa na maksi kubwa sana kuliko mwanafuzni wa sasa hivi, Mwanafunzi ili aende secondary ilibdi afaulu Kwa kupata maksi za juu sana..

Vivo hivyo hata secondary ilikuwa hivyo hivyo watu wengi waliopata Div 3 na 4 na hata wale wa 2 ilibdi waende kusoma ualimu Daraja la 3 maana hakukuwa na Nafasi sio kwamba walikuwa hawafaulu..
Ila siku hizi kuna shule nyingi mpaka 3 anasoma na kufika chuoni..

Sasa kwanini Nimekupa mfano wa hayo yote..
Kwa sababu Zamani na sasa ni tifauti sana kwa technolojia na vitu vingine pia..

kama umewahi kufanya Production miaka hiyo Na miaka ya sasa hivi utajua nachozungumzia ..

Master J yuko Juu sana kuliko S2kizz..

Ningependa tujikite kwenye hoja..
S2kizzy kamtoa msanii Gani kwa kutumia Jina lake?
Au yeye ndo kabebwa na Wasanii anaowatengenezea?
 
Bado inachekesha😂
Music production ya sasa imekua rahisi zaidi, kila kitu kimekua autamated and incorporated into user friendly softwares.
Kabisa mkuu, ukiachialia mbali unaweza kununua packs kibao, code progression kibao.
Kuna watu sasa wanajua Fl wanagonga beat wakati hata piano hawezi kupiga.
Muziki sasa umekuwa rahisi sana kwa beat makers.
Sampling pia imekuwa too much. Technology imerahisisha vitu na bado inaendelea kurahisisha.
Mfano kuna platfome moja unaweza kupiga kifaa kwa mdogo ukaaupload sauti yako halafu ukaupload na sample za kifaa mfano violon basi itageuza ile sauti uliyopiga kwa mdomo kusound kama violin.
Zombie ni bora ila akina master wametengeneza foundation na wale wajenga misingi huwa hawafaidi sana matunda
 
View attachment 2891931

S2kizzy aka Zombie ni producer mkali kuliko Master Jay.
Zombie ambaye ni Grammy nominated mara kadhaa na kafanya nyimbo ambazo ana international hits kuzidi Master Jay ambaye alikuwa akimiliki studio ya MJ production ambayo alitumia wataalam wa kutengeneza muziki kama Maron linje, Profesa Ludigo, Maundi na wengine kadhaa uku akiweka sign yake kwenye nyimbo aonekane kazitengeneza yeye.

Naandika haya ili kumpa maua yake S2kizzyy ili jamii ijue ukubwa alionao kuzidi mkongwe Master Jay ambaye tunamheshimu licha ya kuwa mzee mwenye mihemko sana anaependa kutrend ambae ana historia mbaya ya kutumia wasanii wa kike kama Shaa akiwarubuni kwa studio time.

Zombie apewe heshima yake sio kila aliyetangulia anamzidi wa sasa lazima tuelezane ukweli.
Hichi ni kichekesho ambacho hata Mama yako ukimwambia lazima acheke kabisa…
Hii ni futuhi 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
View attachment 2891931

S2kizzy aka Zombie ni producer mkali kuliko Master Jay.
Zombie ambaye ni Grammy nominated mara kadhaa na kafanya nyimbo ambazo ana international hits kuzidi Master Jay ambaye alikuwa akimiliki studio ya MJ production ambayo alitumia wataalam wa kutengeneza muziki kama Maron linje, Profesa Ludigo, Maundi na wengine kadhaa uku akiweka sign yake kwenye nyimbo aonekane kazitengeneza yeye.

Naandika haya ili kumpa maua yake S2kizzyy ili jamii ijue ukubwa alionao kuzidi mkongwe Master Jay ambaye tunamheshimu licha ya kuwa mzee mwenye mihemko sana anaependa kutrend ambae ana historia mbaya ya kutumia wasanii wa kike kama Shaa akiwarubuni kwa studio time.

Zombie apewe heshima yake sio kila aliyetangulia anamzidi wa sasa lazima tuelezane ukweli.
Ni sawa na kusema Hitboy ni mkali kuliko DJ Premier. Yaani unafananisha hawa wachoraji beat kwa kutumia mouse na watu waliokuwa wana-loop kanda za kaseti? You're out of your fu**in mind.
 
View attachment 2891931

S2kizzy aka Zombie ni producer mkali kuliko Master Jay.
Zombie ambaye ni Grammy nominated mara kadhaa na kafanya nyimbo ambazo ana international hits kuzidi Master Jay ambaye alikuwa akimiliki studio ya MJ production ambayo alitumia wataalam wa kutengeneza muziki kama Maron linje, Profesa Ludigo, Maundi na wengine kadhaa uku akiweka sign yake kwenye nyimbo aonekane kazitengeneza yeye.

Naandika haya ili kumpa maua yake S2kizzyy ili jamii ijue ukubwa alionao kuzidi mkongwe Master Jay ambaye tunamheshimu licha ya kuwa mzee mwenye mihemko sana anaependa kutrend ambae ana historia mbaya ya kutumia wasanii wa kike kama Shaa akiwarubuni kwa studio time.

Zombie apewe heshima yake sio kila aliyetangulia anamzidi wa sasa lazima tuelezane ukweli.
Mkuu,

Kanuni muhimu ya kulinganisha mambo ni kulinganisha vinavyolinganishika.

Ndiyo maana hata kwenye ndondi watu wanapiganishwa kwa uzito sawa, si kupiganisha mpiganaji ndondi yeyote kwa yeyote tu.

Huyo S2kizzy kafanya kazi mwaka gani mpaka mwaka gani? Master J kafanya kazi mwaka gani mpaka mwaka gani?

Katika miaka yao ya kufanya kazi, kuna miaka imeingiliana?

Nasema hivi ili ulinganishe vitu vinavyolinganishika, usije kulinganisha watu wawili waliofanya kazi katika masoko tofauti, teknolojia tofauti, miaka tofauti, mpaka ule ulinganisho wako ukakosa maana.

Yani usije kufanya kosa la kumlinganisha baba ambaye hajui kusoma ambaye amemsomesha mtoto shule mpaka mtoto akajua kusoma, halafu ukasema huyo mtoto ni zaidi ya baba, kwa sababu mtoto anajua kusoma, bila kujali kwamba mtoto huyo anayejua kusoma, kakua katika mazingira ya watu wote kujua kusoma, na asingeweza kujua kusoma bila kusomeshwa shule na baba asiyejua kusoma ambaye alikua katika mazingira ambayo karibu watu wote hawakujua kusoma.

Master J ni mtu wa kulinganishwa na Mika Mwamba, P Funk Majani, Marlon Linje, Bonny Luv, Enrico Figueiro, Roy Bukuku.

Unawajua hao watu?

Hao ndio watu waliokuwa wanafanya kazi siku hizo za Master J.
 
Shida imeanzia ulipojarbu kuwalinganisha, tuseme tu MJ ni balaa mimi huwa nikikaa nikasikiliza beat za enzi hizo mpaka nadata asee mfano ile Dhahabu ya Dully na zingine kibao.
Ila kwa zama hiz s2keezy ni habari ingine.
Namaanisha kila mmoja ni bira zaidi kwa zana zake lakini ni rahis sana MJ kufit hizi zama akiamua lakini haiwezekani s2keezy kufit zama za MJ. Yaani mkubwa ni mkubwa apewe heshima yake acha kiburi cha Amapiano na Miso misondo.
 
Tatizo unalinganisha Kizazi cha sasa Cha Automated softwares Na kizazi cha zaman unatumia Only FL studio (Fruits Loops) kutengeneza beats na unatumia softwares za Kuingiza vocal zinazoruhusu only Direct singing ambayo haina marudio..

Na ndo maana zaman ilikuwa lazma ukariri nyumbo yote uende ukaimbe sio siku hizi unaweza ukatunga na kuimba nyimbo na kurudia rudia kila kipande..
Sometimes tujue kulinganisha vitu na kutoa Appreciation kwa ma legend..

Ni sawa ulinganishe mtu aliyetengeneza Daraja mwaka 1961 ulinganishe na aliyetengeneza mwaka huu..
Tujifunze kutoa shukrani....

S2kizz mwepesi sana
lakini madaraja ya 61 yapo ya 2024 yashaanza kubomoka hata hayajazinduliwa
 
Ila wabongo bana yani kuna mtu ana amini hakuna msanii wa zaman wala wa sasa wa kumzidi diamond ila mtu huyo huyo pia haamini kua s2kizzy ni bora kuliko master jay
Wabongo wengi wana tatizo la kufikiri kwa muktadha wa "all or nothing at all".

Yani, wengi hatuna nuance ya kuona kwamba hapa kuna zama tofauti, na wale wakongwe walikuwa na changamoto tofauti sana za teknolojia, za biashara etc. Na wao ndio waliochanja njia mpaka kufanya hawa wa baadaye wapate urahisi.

Na hivyo, kuwalinganisha hawa wa sasa na wale ni kulinganisha vitu viwili tofauti kabisa.

Unalinganishaje watu walioanza kufanya experiment kwa vifaa duni, na wengine waliokuja baadaye na kuona experiment ya awali ilivyoenda na kufanikiwa kwa kuona matokeo ya hiyo experiment ya awali na kutumia vifaa bora zaidi?
 
Back
Top Bottom