Hakuna uhusiano wowote kati ya demokrasia na maendeleo

Hakuna uhusiano wowote kati ya demokrasia na maendeleo

Ingekuwa hivyo, Bara la Africa ndiyo lingekuwa tajiri zaidi duniani na Bara la Ulaya ndiyo masikini wa kutupwa
Misingi ya utajiri na demokrasia iliyopo sasa ulaya haikujengwa kidemokrasia ilijengwa na misuguano ya muda mrefu sana
 
Tabia ya demokrasia ni kuweka mlolongo wa mambo ambapo hata maamuzi mazuri na yenye tija bado yanahitaji maamuzi ya wengi ili yatekelezwe tofauti na mahali ambako hakuna demokrasia mnyororo wa maamuzi ni mfupi hivyo mambo yote yenye tija huamuliwa kirahisi na kutekelezwa.

Kwa maoni yangu maendeleo ni matokeo ya kuongozwa na kiongozi/ viongozi mwenye upeo wa kuona mbali na mwenye usimamizi madhubuti wa utekelezaji wa hayo maoni.
Na huo mlolongo ndio huondoa uwezekano wa kujitokeza mtu kuhodhi maamuzi kama ilivyotokea Tanzania. Angels are not born here.
 
Tabia ya demokrasia ni kuweka mlolongo wa mambo ambapo hata maamuzi mazuri na yenye tija bado yanahitaji maamuzi ya wengi ili yatekelezwe tofauti na mahali ambako hakuna demokrasia mnyororo wa maamuzi ni mfupi hivyo mambo yote yenye tija huamuliwa kirahisi na kutekelezwa.

Kwa maoni yangu maendeleo ni matokeo ya kuongozwa na kiongozi/ viongozi mwenye upeo wa kuona mbali na mwenye usimamizi madhubuti wa utekelezaji wa hayo maoni.
Una kiwango gani cha elimu?
 
Na huo mlolongo ndio huondoa uwezekano wa kujitokeza mtu kuhodhi maamuzi kama ilivyotokea Tanzania. Angels are not born here.
Ikiwa atatokea mtu mwenye uthubutu upeo na maono huu mlolongo utambana sana. Nadhani ndio maana katika historia ya nchi yetu imewahi kubuniwa nafasi ya naibu waziri mkuu
 
Madicteta wanao pandikizwa ndio wanao shindwa kuleta maendeleo kutokana na miongozo wanayopewa na wanaowapa nguvu.

Dicteta anaetafutia nchiyake maendeleo halisi anauwezo wakufanikiwa kuendeleza nchi katika muda mfupi mfano libya.

Nchi za ulaya na marekani wanaendelea kwa spidi kilasiku sababu ya ukiukwaji mkubwa wa democrasia wanaoufanya katika nchi za wanyonge kwa kupora mali za wahusika na kuwawekea viongozi wanao kubaliana na dhuluma zao.
bwasheeeee, tukomee hapa.
uwe na siku njema.
 
Madicteta wanao pandikizwa ndio wanao shindwa kuleta maendeleo kutokana na miongozo wanayopewa na wanaowapa nguvu.

Dicteta anaetafutia nchiyake maendeleo halisi anauwezo wakufanikiwa kuendeleza nchi katika muda mfupi mfano libya.

Nchi za ulaya na marekani wanaendelea kwa spidi kilasiku sababu ya ukiukwaji mkubwa wa democrasia wanaoufanya katika nchi za wanyonge kwa kupora mali za wahusika na kuwawekea viongozi wanao kubaliana na dhuluma zao.
Zilindelea zaidi baada ya kuacha udikteta au kabla ?
 
Hakuna dikteta keshawahi letea watu maendeleo, madikteta wapo kwa ajili ya interest zao binafsi
Hitler aliivuruga ujeruman na kujirudisha nyuma kimaendeleo. Mleta nada ana mentality za udicteta hata kama hana nafasi ya kutekeleza.
 
Tatizo sio dictator shida ni ubinafsi mbona libya waliongozwa na dictator ila walikua na hali nzuri Hadi kufikia hatua ya kufadhili umoja wa africa!?
Aliekuwa anafadhili ni Ghadafi na si Libya. Utajili wa nchi ulikuwa mikononi mwake na si kwa wananchi.
 
Kwahiyo Gadaffi hakuwa mbinafsi? Naona umekuja na utetezi ule ule wa kutetea watu waovu ili waendelee kutawala, kisha ukiona limejengwa daraja useme ni kwakuwa kiongozi aliyepo ana maono hata kama hajali demokrasia, kana kwamba kukiwa na demokrasia bado daraja halitajengwa.
Na madikiteta hujitanabaisha na jamii wa wajinga na kuwaaminisha ni mkombozi wao.
 
Nimewaza huu ujinga wetu miafrika ..

Yaan Rais anatoa bilion34 kujenga kariakoo only...wakati fedha hizo zingetosha kutuwekea maji Safi mikoa ya Lindi na Mtwara na Ruvuma ambapo 75%tunakunywaji maji ya tope..

Na bei ya dumu la maji Ni 500 Sasa...Toka naanza awali miaka ya 1990 mpk leo tunamkamua chura ...

Ni aibu Sana ....Kuna mdau aliandika humu Viongozi wa Afrika hawana Future Plans na hata hiyo mipango Plans ya Taifa haifuatwi...

Pumbavu kabsaaaa...Demokrasia Afrika Ni Pasua Kichwa...kwa viongozi..
Viongozi wa kiafrika ni wezi. Kuna hazina mbili, moja ipo chini ya rais na hata CAG haikagui. Ndio chimbuko la rais Magufuli, Mama Samia katoa hela kufanikisha hiki au kile.
 
Kama Libya walikuwa na hali nzuri kwa nini waliandamana kwa mamilioni kumuondoa?
Tatizo sio dictator shida ni ubinafsi mbona libya waliongozwa na dictator ila walikua na hali nzuri Hadi kufikia hatua ya kufadhili umoja wa africa!?
 
Hao wapinzani ' wachache' walikuwa na madai gani?
Hakuwahi kuishi vibaya na walibya kilichotokea ni baada ya wapinzani wachache kuchochewa tokea nje ya nchi, kitu ambacho katika uongozi ni kawaida tu, hata ingekua unakubarika kiasi gani hilo linaweza Kutokea mf ni uasi wa wabunge ndani ya chadema haimaanishi kwamba kuna ugomvi binafsi na mbowe ila ni ushawishi wa nje umechochea huu uasi!!
 
Kuna watu wenye akili timamu wanaamini Gaddafi alikuwa mwanademokrasia?

Ukitaka Kujua Hilo Hauitaji Kuwa Genius Angalia Libya Ya Gaddafi Angalia Na Libya Ya Sasa,
 
Mataifa mengi yaliyowahi kuwa makoloni ni pamoja na China, Korea Kusini, India, Indonesia, Vietnam, Singapore, Brunei, Malaysia.

Haya ni baadhi ya mataifa yaliyowahi kuwa makoloni kwa muda mrefu ila yameshaachana na ujinga wa kusingizia wakoloni badala yake yanachuana kiuchumi na wakoloni wao kwa sasa.

Tatizo la Africa kudumaa kimaendeleo ni uongozi mbaya, usio na maona, unaotanguliza maslahi binafsi ya watu wachache.Tusiendelee kujificha kwenye kichaka cha ukoloni, tunaonekana wajinga tu.
No! Hapana! Umasikini wa Afrika haukutokana na ukosefu au kutokuwepo kwa demokrasia BALI umetokana na WIZI, UPORAJI NA UNYONYAJI ULIOKITHIRI wa mali na rasilimali za Afrika by hao Wazungu na Wasia kwa kutumia nia nyingi nyingi ikiwa ni pamoja na mikataba ya kinyonyaji dhidi ya akina Chief Kimweri na wenzao ZAMA ZA KALE.

Leo kuna wizi wa wazi wazi wa rasilimali zetu ikiwa ni pamoja na madini yetu (almasi, dhahabu, shaba, chuma, tanzanite na mengineyo), mali asili ikiwa ni pamoja na mbao za thamani sana kama mninga au mitiki na mengineyo na hata wanyama wetu ZAMA ZA LEO! Na kwa karibuni na hata sasa ni kwa kutumia misaada wanayotupa. Say wanakopesha $1.0bi/= lakini at the end of the day unaishia kulipa hata say $2. 0bi/=! Kwani utalipa riba, service charges kwa ajili ya huo mkopo, na zaidi ya hayo, utalipa mishahara na migharama mingine mingi kwa ajili ya "wataalamu" wanao ambatana na huo mkopo! Achilia mbali kuwa utanunua hata vifaa vingine vya hiyo miradi kutoka kwao kwa bei za KURUKA! Kwa njia hiyo mipesa inarudi kwa hao waliotukopesha!

Chunguzeni mikopo hii mtaona kuwa kuna njia nyingi za kinyonyaji na wizi ndani yake na hivyo kuufanya huo mkopo au hata msaada usiwe na manufaa kwetu na hivyo kuzidi kutufanya kuwa masikini! Kuna mtu mmoja aliwahi kusema "mikopo inatufanya tuzidi KUSIKINIKA na watoa mikopo na wazidi KUTAJIRIKA!
 
Libya ya sasa ndio inaonyesha Libya ya Gaddafi ilikuwa ya Kidemokrasia??
Ukitaka Kujua Hilo Hauitaji Kuwa Genius Angalia Libya Ya Gaddafi Angalia Na Libya Ya Sasa,
 
Back
Top Bottom