mbenge
JF-Expert Member
- May 15, 2019
- 4,864
- 10,483
Baadhi ya maeneo ya Kinondoni Kaskazini yamekosa umeme toka saa tatu asubuhi mpaka ninapotuma huu uzi hivi sasa.
Je! Kuna changamoto yoyote ile iliyojitokeza, na pengine imekwisha kutolewa taarifa hapo kabla na uongozi wa TANESCO siku ya leo ya tarehe 02-06-2024. Pengine taarifa hiyo imenipita huku baadhi ya wadau wameisikia.
Kwa muda sasa kulikuwa hakuna tena tatizo katika katika umeme ya muda mrefu kama huu, na hata kama iliwahi kutokea basi ilikuwa kwa kipindi kifupi, ama taarifa kutolewa kabla endapo changamotp ilikuwa ni kubwa, hasa ikitokea katika Grid ya taifa.
Sasa leo kwa upande wangu sina taarifa yoyote ile, na kila nikijaribu kupiga katika namba zao, napata majibu kuwa simu yako itapokelewa hivi punde, kwani watoa huduma wao kwa sasa wanaongea na wateja wengine.
Kama kuna mwanajukwaa anatambua uwepo wa changamoto yoypte ile ambayo imejitokeza tafadhali naomba anijuze.
Je! Kuna changamoto yoyote ile iliyojitokeza, na pengine imekwisha kutolewa taarifa hapo kabla na uongozi wa TANESCO siku ya leo ya tarehe 02-06-2024. Pengine taarifa hiyo imenipita huku baadhi ya wadau wameisikia.
Kwa muda sasa kulikuwa hakuna tena tatizo katika katika umeme ya muda mrefu kama huu, na hata kama iliwahi kutokea basi ilikuwa kwa kipindi kifupi, ama taarifa kutolewa kabla endapo changamotp ilikuwa ni kubwa, hasa ikitokea katika Grid ya taifa.
Sasa leo kwa upande wangu sina taarifa yoyote ile, na kila nikijaribu kupiga katika namba zao, napata majibu kuwa simu yako itapokelewa hivi punde, kwani watoa huduma wao kwa sasa wanaongea na wateja wengine.
Kama kuna mwanajukwaa anatambua uwepo wa changamoto yoypte ile ambayo imejitokeza tafadhali naomba anijuze.