Halaand sio binadamu, ameweka rekodi kuwa mchezaji wa kwanza kwenye historia ya EPL kufunga mabao 70 mapema zaidi

Halaand sio binadamu, ameweka rekodi kuwa mchezaji wa kwanza kwenye historia ya EPL kufunga mabao 70 mapema zaidi

Ronaldinho alichowazidi Messi na Ronaldo ni skills tu

unapozungumza skills una maana gani?

ROnaldonho amewazidi hao jamaa kwa kila kitu zaidi ya magoli mengi na mataji mengi waliobeba.

Kuanzia Pasi refu, fupi, chenga, dribbling, kila kitu
 
Huyu dogo ana mahaba na halland hata cr7 wakati anacheza man utd hajamuona.

hivi unaazaje kumlinganisha CR7 na halland mkuu? unajua kama huu msimu ukimaliza kuna uwezekano mkubwa kuwa Halland atakua ameshamfikia magoli yote ronaldo aliyoyafunga EPL kwa misimu mitatu tu wakati Ronaldo alifunga kwa misimu 8?
 
😂😂😂😂😂😂Ronaldinho alikua na skills tu ila hakuwa best playmaker.
Messi anatambulika kama BEST PLAYMAKER IN HISTORY.
Messi ana assist nyingi kuliko Ronaldinho je unalijua hilo!??
Messi amekua akihudumu namba tatu hadi sasa.namba 8,10 na 9.
Na tangia kuondoka kwa Xavi na Iniesta alihudumu kiungo mchezeshaji na kiungo mshambuliaji hadi sasa.
Huyo halland aliwahi kucheza namba 8 hata siku moja!??
Messi kipindi cha Ernesto Valverde namba 8 ndio ilikua namba yake.
Akichezesha timu kwa kuipandisha na kuishusha.
Alichofanya Messi HALLAND HAWEZI FANYA HATA ROBO YAKE MPAKA ANAINGIA KABURINI.
Labda kama ulikua hufuatilii mpira.
Enzi hizo messi anakokota mpira kuwapiga chenga wachezaji mpaka watano na kufunga.
Na messi is the best dribbler in history.
Mwambie huyo Halland a dribble hata wachezaji watatu kama anaweza.

acha porojo mkuu, hata Mc tominay anacheza namba tofauti uwanjani so what?
 
Mtu anazubaa yard 20 karibia na goli asubiri kufunga tu mnataka kumfananisha na Messi au Ronaldo watu ambao walikua wanautafuta mpira popote na wanafunga angle zozote!??

more than 10 years sasa Ronaldo ni mviziaji tu
 
Kaka naona unaanza kukosa adabu kwa wakubwa.
Unamfananisha Halland mtu wa box na Ronaldo ambaye alikua akiisakia matokeo Man united!?
Aliyoyafanya Ronaldo Halland kamwe hatayafikia.
HAlland atabakia kuwa best scorer ila Ronaldo is a complete player.
Leo hii umwambie Halland autafute mpira apore atengeneze nafasi hawezi.
Ila Ronaldo alikua akiwania mipira,akipora na akitengeneza nafasi.
Hivi kaka mpira umeanza kufuatilia juzi nini!??

KAzi ya striker ni nini mkuu? hayo mengine ni mbwembwe tu.
 
Kwa Ronaldo siwezi sema ila kwa Messi ninaweza kusema wapi kamzidi Ronaldinho.
Messi ni mwepesi wa kudribble na ana dribble za kasi na zilizofupi kuliko Ronaldinho,ndio maana walimuita messi the best dribbler in history.
Messi ana accuracy katika dead ball kuliko Ronaldinho.

Best dribbler in history? Uliwahi muona Maradona mkuu?
 
KAzi ya striker ni nini mkuu? hayo mengine ni mbwembwe tu.
😂😂😂😂Kama ni mbwembwe muulize Guardiola kwanini hadi sasa anasema timu yake inamkosa mtu muhimu kama messi??
Hayo unayoyaita mbwembwe ndio yanaamua mechi ikiwa ngumu.
more than 10 years sasa Ronaldo ni mviziaji tu
Umri umeenda he is on his peak of his career.
 
Haaland ni striker mzuri sana. Ila mafanikio yake yamechangiwa na timu anayochezea. Ni nzuri na inampa service nzuri. Uchezaji wa Messi ni wa aina nyingine, ie kiungo na anajua kucheza na mpira. Ronaldo naye ni mchezaji mwenye uchotara wa Striker, winger na elements za kiungo.

mafanikio ya Halland yanachangiwa na timu anayocheza, vipi kuhusu Messi na Ronaldo? hao jamaa walicheza na wachezaji bora zaidi kuliko anaocheza nao Halland.
 
Sikuhizi soka limekuwa ujinga sana

Linaangalia magoli tu yaani namba sasa halaand hana kipaji cha soka kabisa ila ni vile tu basi tu

Pep mwenyewe alishasemaga "sometimes football is beyond the number"

Haland wa kawaida sana

Ronaldo na Messi waliishi kwa magoli, kwanini kwa wengine iwe nongwa? au mumeshasahau mulipokuwa munatuhesabia 50 goals a season hapa?
 
Mfano mechi ya Man City vs West Harm alifanya nini haswa uwanjani tofauti na kufunga magoli tu? Hana vigezo vya ubora kufikia akina Cr7 na Messi hata kwa 25% tu, Haaland wa kawaida sana tu.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.

hayo magoli ndio ubora wenyewe mkuu, asingeyafunga City mpaka mda huu wangekua na vikao vya kujitafakari
 
Najua litapingwa hili ila Aguero alikuwa ni mzuri kuliko hata huyu Haaland anaeshinda hizi goli nyingi

sasa mbona aguero alishindwa kufunga gole nyingi kama za Halland?
 
Mkuu hao jamaa nje ya ya career zao Real na Barca ni wakawiada sana, messi alifunga goli 6 Psg kwa aibu kabisa
Mchezaji mkubwa always ni kwa ajili ya timu kubwa maana unacho ongea ni sawa na kusema Pele nje ya Santos hana kitu,maana maisha yake yote ya soka kwenye ubora wake aliichezea Santos,alivyo enda US hakufunga magoli mengi. Mpira haupimwi hivyo.Halafu hizo goli sita za Messi PSG ni total kwa misimu yote miwili?
 
Mchezaji mkubwa always ni kwa ajili ya timu kubwa maana unacho ongea ni sawa na kusema Pele nje ya Santos hana kitu,maana maisha yake yote ya soka kwenye ubora wake aliichezea Santos,alivyo enda US hakufunga magoli mengi. Mpira haupimwi hivyo.Halafu hizo goli sita za Messi PSG ni total kwa misimu yote miwili?

sasa goli 6 kwa msimu mmoja ni majivuno?
 
unapozungumza skills una maana gani?

ROnaldonho amewazidi hao jamaa kwa kila kitu zaidi ya magoli mengi na mataji mengi waliobeba.

Kuanzia Pasi refu, fupi, chenga, dribbling, kila kitu
Huyo Dihno mwenye kwenye ubora wake, alimtabiria Messi kipindi yupo kijana kabla hajawa na namba ya kudumu kwenye timu ya wakubwa,yakuwa atakuwa bora zaidi yake na kweli leo yametimia.

Messi anauwezo wakupiga pasi yoyote kwa usahihi, katafute Asists zake zaidi ya 350+,Dribbling Messi ni bora kulio mchezaji yoyote, Messi ana solo goli na assists zaidi ya mia,tena nyingine anapunguza watu zaidi ya watano na sizani kama kuna mchezaji anaye weza kupiga penetration pasi katikati ya msitu wa watu na ikafika zaidi ya Messi simuoni.
 
Back
Top Bottom