DOKEZO Hali ni mbaya sana kwa walemavu tuliosoma, Si Serikali wala kampuni binafsi ambazo ziko tayari kutuajiri. Tunabaguliwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Hua wakati mwingi nawaza ni kwa namna gani ntaweza kusaidia hata na wengine!! Siamini bado falsafa ya "survival for fittest" naamin kweny creation ya fittest ili a survive
 
Pole sana mkuu
Nadhani viongozi wataona hii taarifa walifanyie kazi
Pole sana Mungu awasaidie
Siyo kwa viongozi hawa sana sana wataleta kiroba cha unga na debe mbili za maharage mbele ya camera ndio imetoka hiyo, kinyume cha hilo ni vimikopo visivyo na tija.
 
Kwenye kutoa ajira watu hawaangalii huruma hiyo ni risk kubwa sana.
 
Mkuu, angalau mabenk wanajari, nina rafiki zangu walemavu wa viungo wameajiriwa NMB, CRDB japo sijaona kiziwi hata hivyo hawa wamejazana kule kwenye ajira za ualimu.

Kingine ningeshauri pia muangalie mazingira na kazi za kuomba kuendana na hali zenu haya mambo ya usawa na huruma wakati mwingine hayafanyi kazi kila sehemu.
 
Tatizo lilianzia kwa wazazi. Ilibidi wajue mbele kunani hivyo wawape elimu ya ujasiriamali
 
Tatizo lilianzia kwa wazazi. Ilibidi wajue mbele kunani hivyo wawape elimu ya ujasiriamali
Historia ni ndefu San!! Lakn kwasisi wakt mwingne badhi ya wazaz hasa baba... Wanakuwa Kama hawatuamini Kama tutakuja saidia familia kwahio! Sikuwahi kuwa karibu na mzee
 
Hii jamii ya walemavu ni wachache sana!! Hakukuwa na haja ya kuwapa competition kubwa kweny kutafuta ajira!!! Ingefaa wakitoka chuo wapewe nafasi serikalini
 
Siyo kwa viongozi hawa sana sana wataleta kiroba cha unga na debe mbili za maharage mbele ya camera ndio imetoka hiyo, kinyume cha hilo ni vimikopo visivyo na tija.
Umejuaje kaka!! Yaani mi ni shuhuda wa Hilo!! Japo hata hicho kidog huwa tunashukuru
 
Huko tayari tumepita hakuna mweny jibu!! Wanaishia kuitwa kweny semina ili wapate posho za semina
Sasa hata walemavu pia mnasalitiana kwa kulambishwa sukari Basi hàkuna haja ya kulaumu wasio walemavu kuwabagua, acheni kwanza kubaguana ninyi kwa ninyi ndo muanze kuwalaumu wasio walemavu.
 
Hakuna watu wakorofi kazini kama walemavu.

Nimekoma.
 
Pole sana..
Lakini je hata ungekuwa wewe ,ungeweza kumuacha mtu ambaye si mlemavu ukaajiri mlemavu?
Mkuu, kwani huko makazini wanakwenda kupigana mieleka?

Taaluma nyingi walizosoma hawa ndugu zetu wala sio za kutumia akili na nguvu.
 
Pole Mkuu Mungu awasaidie!
Sasa hivi kwa sababu ya uchache wa ajira,kilichobaki ni Strugle of mass for existence! Hii ina result for Survival for the fittest!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…