Uchaguzi 2020 Hali si shwari ndani ya CCM, Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Bashiru Ally amekemea vikali baadhi ya wanachama wanaopanga kukisaliti chama

Uchaguzi 2020 Hali si shwari ndani ya CCM, Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Bashiru Ally amekemea vikali baadhi ya wanachama wanaopanga kukisaliti chama

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
Katibu Mkuu wa CCM Ndg Bashiru Ally Kakurwa amekemea vikali tabia za baadhi ya wanachama wa CCM wanaopanga kukisaliti Chama katika kipindi hiki cha Uchaguzi Mkuu kwa maslahi yao binafsi. Ameahidi kuwachukulia hatua kali watakaobainika kusaliti Chama ikiwemo kuwafukuza Uanachama.

"Wanaohama CCM wakidhani wananguvu, wakitoka wanageuka kama vichaa, wafuatilieni wote waliohama CCM, hakuna mwanaCCM maarufu kuliko CCM, ukijiona maarufu ujue umeazimwa umaarufu na CCM , siku Chama kikikutupa ama ukikitupa umaarufu unakoma. Wapo watakaookota makopo nawahakikishia" Bashiru Ally.



2020-09-19 (1).png

Maoni ya Kada wa CCM.

Wakuu, Katibu Mkuu wa Ccm ametishia kuwafukuza wanaccm ambao wamepanga kumpa kura tundu lisu na kufikia mahali Ya kusema kuwa, watafukuzwa na watataifishwa Mali zao.

Unajua watu wanafanya mzaha na siasa za kutisha na kutumia manguvu pasipo ueredi na mwisho kutatokea anguko kubwa lisilotegemewa, siasa inataka akiri sio nguvu, Katibu badala Ya kutumia maneno Ya busara anatishia watu kuwa atawafukuza huku akijua kuwa kupiga kura ni Siri ya mtu mmoja, hupaswi kutisha watu kisa watapiga kura Kwa mtu mwingne huku ukijua kuwa kura ni Siri, Katibu alipaswa kutafuta sababu Kuu Ya wanaccm kupanga kupiga kura upinxani

Nimeshukuru Sana Ccm kugundua kuwa watu wamepanga kupiga kura Kwa upinzani nikiwemo Mimi Mwana Ccm Kada na kuna watu nawajua zaid ya Mia watapiga kura upinzani, Katibu ameshindwa kutambua kuwa kuweka haya hadharani ameshtua wengne waliokuwa wakinyanyaswa na Mwenyekiti kujiunga kwenye huo msafara

Naomba kumuuliza Katibu kuwa Mwenyekiti Alikuwa anachukua wapinzani anawapa vyeo anatuacha sisi miaka Yote, anawachukua anawapa nafasi za kugombea ubunge huku sisi akikataza katakata hata kuwapinga Leo hiii anatutisha? Haingiii akirini Mimi na watu Wangu tulihangaishwa na upinzani Mwaka 2015 hadi tukafanikiwa kumweeka madarakani halafau akatudharau kusema kuwa yeye ni Ccm Mpya akatutenga Halafu tuingie kwenye sanduku la kura tumpigie haiwezekani, tutapiga kura Kwa wingi Sana Kwa upinzani liwalo liwe hata atutishie afanye anachofanya sisi tutaonesha hasira zetu kwenye sanduku
 
Mwambie Bashiru asitutishe! Nani aliwaambia wafanye ubabe na kutuona wanaCCM ni wajinga? Inakuwaje tunachagua watu wanawakata? Inakuwaje wanachapisha fomu moja ya uraisi na kuzuia watu wasigombee uraisi?

Mwambie pia wanaCCM tuna uhuru kama wananchi wa Tanzania wa kumuunga mgombea urais, ubunge na udiwani wa Chama chochote kile na wala sio dhambi.
 
Wajiulize kwanini wanachama wanasaliti na wakipata jibu wadeal na hiho sababu na si watu. Naamini wapo wanachama wengi wanamapenzi na Lissu na sera zake na watampigia kura hiyo tar 28.
 
Mwambie Bashiru asitutishe! Nani aliwaambia wafanye ubabe na kutuona wanaCCM ni wajinga? Inakuwaje tunachagua watu wanawakata? Inakuwaje wanachapisha fomu moja ya uraisi na kuzuia watu wasigombee urais?

Mwambie pia wanaCCM tuna uhuru kama wananchi wa Tanzania wa kumuunga mgombea urais, ubunge na udiwani wa Chama chochote kile na wala sio dhambi.
jingalao, johnthebaptist Elitwege, stroke, njooni huku kuna ujumbe wenu.
 
Quinine,
Unawatishia wanachama? Waliotia Nia kugombea ccm na kukosa kura au kukatwa majina yao 100% wapo upinzani. Watumishi wa Umma wako upinzani 100% watumishi wa umma walio tia Nia kugombea na kukatwa mishahara yao,kutolipiwa madeni ya bank na kuwachangia uchaguzi fedha zaidi ya milion moja kila mjumbe wako upinzani 100% vyeti feki wako upinzani 100% wafanyabiashara wako upinzani 100% waliokuwa na maduka yakubadilishia fedha wako upinzani 100% walio hitimu vyuo wako upinzani 100% wakulima na wafugaji usiseme. Tafuteni suluhu na haya makundi mkitaka chama kiwe salama. Hali sio shwari.
 
Unawatishia wanachama? Waliotia Nia kugombea ccm na kukosa kura au kukatwa majina yao 100% wapo upinzani. Watumishi wa Umma wako upinzani 100% watumishi wa umma walio tia Nia kugombea na kukatwa mishahara yao,kutolipiwa madeni ya bank na kuwachangia uchaguzi fedha zaidi ya milion moja kila mjumbe wako upinzani 100% vyeti feki wako upinzani 100% wafanyabiashara wako upinzani 100% waliokuwa na maduka yakubadilishia fedha wako upinzani 100% walio hitimu vyuo wako upinzani 100% wakulima na wafugaji usiseme. Tafuteni suluhu na haya makundi mkitaka chama kiwe salama. Hali sio shwari.
Hali hii ikiendelea Hadi 2025 CCM itakuwa KANU
 
Mbona hawaguzi waZanzibari huko ambako CCM wanakaribia kutowaroho kama washatoana roho, yele yale ya Mwalimu Nyerere ukimaliza kuwabaguwa wengine utaanza kubaguwa hata ndani mwako ndio ilipofikia CCM leo hii.
Mwenyekiti wa CCM Taifa anatokea,Mkoa wa Geita Kanda ya ziwa, jirani na mkoa wa Geita ni mkoa wa kagera anatokea katibu mkuu wa chama, Kanda ya ziwa. Katibu mwenezi anatokea mkoa wa Mara ,Kanda ya ziwa.mnategemea ccm iko salama?
 
Back
Top Bottom