MNISOME VIZURI :
Kila MTU ni shahidi kuwa Awamu hii ndiyo awamu iliyoletwa na Mungu kwa ajili ya kuondosha uovu Tanzania :
Kwanza 2015 watu waliomba Sana juu ya Uchaguzi ule lakini wengi wakiwemo wale wanaojiita mitume na manabii Ambao ni makada wa CCM wa wazi kama Gwajima,Lusekelo, n.k. na baadhi ya mashekhe walikua wanaomba huku mawazo yao yakiwa kwa Lowassa.
Mungu akawabadili lugha zao ndani ya CCM Lowasa akakatwa . JK akiwa upande wa Asha Rose au Membe. Kinana akiwa na Lowassa . Nape akiwa na Kinana aliyemuachia Jimbo la Mtama ambalo amelifanya mali yake sasa na yupo tayari kumkatakata mtu yeyote kwa mapanga aliyoyaita mitama alimradi apate ubunge.Kosa kubwa!!
Mkapa akiwa na JPM.Wazee walikua na Lowassa.
Wengine hawakua na nguvu zaidi ya kusikilizia upepo wa wajumbe wengi unakwendaje.
Mwaka huo 2015 roho wa Madaraka na utawala akamwingia Mkapa akapindua meza na upepo wa madaraka na utawala ukamwangukia JPM kwa ghafla na mchezo ukaisha JPM akapita katikakati ya Lowasa na Membe.
Mwanzo wa Tanzania mpya iliyokua inamsubiri Kiongozi wake ajaye.
Baada ya maombi ,sala na dua za watanzania Mungu akamleta Yohana ili asawazishe njia kwa ajili ya Kiongozi ajaye.
Lowasa akakimbilia upinzani na kupata kura nyingi sana japo masanduku ya kura za magumashi yalikua yamejazwa kila mahali . Bado ilikua alimanusura JPM abwagwe.
JPM akaingia madarakani kwa ahadi nyingi nzuri zenye mvuto kwa wanafunzi wa vyuo ,wafanyakazi,wafugaji,wakulima, wafanyabiashara, kuwaunganisha watanzania bila kujali makabila yao vyama vyao.
Mwanzo wa Tanzania mpya isiyo na uovu ni pamoja na Tanzania isiyo na imani za kukifanya Chama cha mapinduzi kuwa ni kikubwa kuliko Mungu. Tumeona watu wakitekwa ,kununuliwa kwa rushwa za fedha na ahadi za madaraka. Wakurugenzi na maDC na maRC kugeuka kuwa watenda uovu mkuu juu ya wanadamu walioumbwa kwa mfano wa Mungu kwa sababu tu ya kutetea CCM na kusema kuwa itakaa madarakani Milele kama Mungu muumba wa Vyote! Uovu mkuu!!
Watu wakajiona kukaa ndani ya CCM ni kuwa salama kuliko kukaa ndani ya Mungu hata wale waliojiita manabii na mitume na maaskofu feki waliofundisha kuwa ukiwa ndani ya Yesu una ulinzi wakageuka na kutafuta ulinzi na amani yao kwa mwanadam na chama cha mapinduzi ikawa ndiyo ngao yao ili waweze kueneza injili . Yaani Bila kuunga mkono juhudi hata dini zilitishiwa kufutiliwa mbali na kulipishwa kodi walizokua wanadaiwa. Sikuwa nafahamu kuwa dini nazo zinalipa ada kwa watawala ili wapewe kibali cha kumtangaza Mwenye Dunia yaani Mungu. Mungu anapewa masharti ya kukanyaga Tanzania. Uovu mkuu!!
Mungu akabadili ndimi zao kuelekea kwenye Tanzania mpya kwa kuanza safari ya kuiangusha CCM ,ambayo ndiyo Babiloni mkuu kwa Tanzania. Katibu mkuu Komredi Kinana wakati huo akawa hapendezwi na Matumizi ya nguvu ktk siasa. Akaomba kustaafu akakubaliwa.
Akateuliwa Bashiru Ally mkereketwa wa Upinzani kuwa katibu Mkuu wa CCM. MTU ambaye hajawahi kuipenda CCM na dhulma zake na wizi wake wa kura na uonevu wake ,ghafla akawa katibu mkuu na akageuka kuitumikia katika misingi yake ya uovu. Bashiru aliyeamini katika haki kwa miaka mingi ghafla akageuka kuwa msimamozi wa dhulma na siasa chafu za kuhujumu watu kwa kutaifisha Mali zao. Yeye anapata Mapesa mengi kwa kuunga mkono dhulma anasahau kuwa wengine wamepata Mali kwa kujinyima na hata kulala mitaroni na kwenye mapango wakisaka Mali ili waendeshe maisha yao na familia zao. Yeye Bashiru anakuja kuwanyanganya mali zao ili watoto wake waishi maisha mazuri kwa kumfurahisha MTU mmoja na familia yake. Uovu mkubwa.
Akateuliwa Hamfrey Polepole kuwa msemaji mkuu wa CCM. MTU ambaye alipigania Katiba mpya na mfumo wa bora wa uongozi unaopunguza madaraka ya Rais kuteua kila MTU mwenye nafasi ya juu katika kufaidi keki ya taifa. Mfumo mbaya unaoweza kutuletea dikteta kwenye utawala. Hamfrey akabadilika na kujiunga na uovu wa CCM bila kujali Damu ya Dr.Sengondo Mvungi iliyomwagwa na majambazi kutokana na msimamo wake wa Kutetea katiba mpya. R.I.P Dr. Sengondo Mvungi( uliowaachia Jukumu LA kudai Katiba mpya wamerejea walikotoka kulinda Mali zao walizochuma kutokana na pesa walizopata wakati wa mchakato wa Katiba mpya)
Polepole akawaasi wa Tanzania kwa sabu ya kutetea tumbo lake akajiunga na misimamo ya Dhulma ya chama cha mapinduzi. Akaendesha siasa za Rushwa ya madaraka na ubabe wa kila namna huku akiwatisha wakurugenzi. Uovu mkuu!!
Wakaja wakina Kitilia Mkumbo ,Kabudi , Kafulila na wengine wakapewa nafasi ya kuongoza mapambano ya kuhakikisha haki na usawa katika Taifa hili vinafutika ili CCM iendelee kulinda makada wake waliopora Mali za Taifa hili kuanzia vyama vya ushirika ,viwanda ,nyumba za serikali, mashirika ya umma n.k . na Nchi ikawa kama kuku aliyenyonyolewa manyoya yote wakati wa Baridi na kuwekwa kwenye nyumba yenye A.C kwa kuaminishwa kuwa nyumba bora ni yenye A.C. na ndio maendeleo.
Mbunge wa Moshi kwa miaka Mingi akafariki ghafla mtu aliyekua nguzo kuu ya upinzani hasa Chadema. Bilionea aliyekua na mali zake bila kuonea mtu. Wasiwasi ukatujaa kuwa ni kwa nini CCM na serikali yake walizuia kwa nguvu kubwa sana Wanachama na wabunge wenzake Wasiuage Mwili wa marehemu Ndesamburo kwenye uwanja wa mashujaa pale Moshi. Yaani CCM na watawala wake wakahamishia uovu wao kwa marehemu na kuweka pingamizi mpaka LA kuaga maiti asiye na kauli tena!! Uovu mkuu!! Hayo yote yaliganywa na CCM ikijiaminisha kuwa itatawala milele bila ridhaa ya wanadam zaidi ya ridhaa ya Risasi na mabomu. Wakasahau kuwa Mabomu na risasi ni vinatengenezwa na binadamu lakini Binadamu ameumbwa na Mungu. Hivyo binadamu ni lazima aheshimiwe kwanza.
CCM wakatangaza soko la wanasiasa wa upinzani wanaotaka kurudi CCM kwa Rushwa ya wazi na ahadi za vyeo.
Wwkatumia dhulma kuwapitisha mpaka wakapoteza maisha ya Akwilini bila kujali haki. Dhulma ikapiteza maisha ya mtoto wa maskini ili Walioshiba ndani ya CCM wazidi kushiba ! Uovu mkuu!!
Wapinzani Maslahi wakakimbilia vyeo na ubunge wa Dhulma kule CCM.
Hofu ikatanda Nchi nzima. Kila mtu akakaa kimya mbele ya kuwekwa ndani,kufilisiwa, kuuawa,kutekwa na kuteswa. Na kila aina ya uovu dhidi ya binadamu. Wabunge na bunge lao wakafurahia maisha hayo ya kudhulumu wapinzani ili wao waendelee kubaki Bungeni. Majaji wakafurahia teuzi na maslahi yao wanayopata wakajitenga na haki na kukaa upande wa Dhulma hata walipoambiwa wahukumu kesi ya Tume huru ili uchaguzo uwe huru na haki wakatupilia mbali na kutangaza kuwa tume ipo huru.Wakajiunga na dhulma ili wapate raha na familia zao kupitia mpango wa CCM wa kutawala milele pamoja na Mungu.
Uovu mkuu!!
Watu wasiojulikana wakaunga mkono juhudi kwa kumpiga Lisu Risasi. WanaCCM wakalipuka kwa Shangwe kwa kuona kuwa sasa hawana tena mpinzani Tanzania watatawala milele kama Mungu. Uovu mkuu!!
Mungu akaamua kusimama Mwenyewe ili aonyeshe kuwa yeye ndiye aliyewaumba wanadamu wote na hakuwapa Chama cha siasa Bali amri zake Kumi na sheria za haki. Haki haina Chama wala kabila. Mungu ni Mungu wa haki. Haki huinua Taifa. Mungu akamponya Lisu.
Lisu akarudi Tanzania . Njia ya kuifanya Tanzania mpya ikaanza kung'aa. Watu wakarejeshewa furaha mioyoni mwao. Nchi imelipuka kwa furaha , vyama vya siasa vimeanza kunawiri. Haki inaanza kuonekana itarejea.
Hofu imewageukia akina Bashiru. Wanawayawaya wanawatisha watu ,wanaogopa mahakama ya kimataifa inawanyemelea. Wametumia vibaya madaraka na mamlaka waliyoyapewa. Kama sio leo lakini kesho watavuna walichopanda. Heshima Polepole na Bashiru waliyojijengea kwa kupigania Haki na Katiba yenye misingi ya haki na utawala bora wameipoteza kwa sababu ya ubinafsi wa kuweka mtu mmoja mbele badala ya Taifa na vizazi vijavyo.
Mungu akaikinga Tanzania na Korona ili Uchaguzi ufanyike Tanzania mpya izaliwe .
Mungu alimtanguliza Yohana ili kuiandaa mioyo ya wa Tanzania kuwa kitu kimoja katika kuileta Tanzania Mpya yenye haki itakayowaunganisha wote bila kujali makabila na vyama na dini. Haki kila mtu anaitaka mana hakuna anayependa kudhulumiwa . Hata hao watu wa Tume wabaotumiwa na CCM kudhulumu watanzania kura zao hawapendi kudhulumiwa.
.
Tanzania mpya inakuja.
Watanzania wote tumchague Lisu ili tuachane na Tanzania ile ya dhulma na kutishana ,kuoneana ,kufitiniana kwa sababu ya kujipendekeza, unafiki, kutekana ,kufilisi watu waliotafuta mali zao kutokana na chuki tu za kisiasa na kukomoana .
IPO wazi kabisa Endapo Mpinzani atapata kura nyingi na wabunge wengi atatangazwa.
Mfano Lisu akitangazwa siku hiyo hiyo dola lote linahamia kwake. Tume inakua huru na hakuna wa kuigusa. Bashiru hana ubavu wa kuzuia Mtu asitangazwe mana anaootangazwa Lisu kuwa Rais basi nguvu ya JPM inakua imepotea na Polepole anabaki kama mjumbe tu wa kamati ya Harusi.Ghafla Lisu ndio anakua na Power yote. Tukumbuke uongozi na madaraka ya kupitia kampeni na Uchaguzi unakuwa na watu nyuma yake ndani na nje ya vyombo vyote vya dola . Hofu ni pale watu wanapodhani kuwa mtu atakosa kura hivyo kumuunga mkono wazi wazi haiwezekani.
Watu wamchague Lisu kwa kura nyingi mana hata wale watu wa Tume wameapa kwa Mungu kutenda haki. Haki zao zipo kikatiba na Mungu ndiye anyeweza kuwalinda dhidi ya waovu kama alivyomlinda Lisu.