Hali ya Chid Benz Inasikitisha sana

Tumchangie pesa ya matibabu aende India. Mazombi rusheni pesa ya matibabu kwenye namba Ile Ile.
 
It's all about business sababu ni Biashara kwani mshauri wa wasanii ni nani au hii NCHI wasanii hawana mshauri?
 
Kwa hali yake kumlaumu kwa anavyokuwa kwa sasa ni kumuonea tu, huyo tayari sio mzima/timamu kwahiyo ni ngumu sana yeye binafsi kuona kuwa anakosea.
 
Kupona uraibu wa madawa sio rahisi hivyo hasa km bado anarudi kwenye kampani ileile iliyomuingiza huko, mtu aliyeshakuwq mraibu wa madawa sasa hivi mraibu wa pombe kurudi kwwnye madawa ni kugusa
 
Inauma sana kwa kweli. Nimewakumbuka Salasala boy, Cowboy, Pancho Latino mafia. Kifo hakina huruma
Chunga wanao na masela Mavi sio watu wazuri

Katika vifo vilivyoniuma zaidi ni KIFO cha Pancho Latino wale Jamaa eti anazama wanamuona wanamuacha tu wanaanza kulialia na clip Video wanachukua Ile iliniuma kishenzi

Weka wanao mbali sana na masela Mavi
 
Mfumo wa nchi hii haujawahii kumpa nafuu kijana yyte yule mpambanaji kwenye seckta yyte ile..
Tunaishi kimachale chale sana..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…