Hali ya Chid Benz Inasikitisha sana

Hali ya Chid Benz Inasikitisha sana

Chunga wanao na masela Mavi sio watu wazuri

Katika vifo vilivyoniuma zaidi ni KIFO cha Pancho Latino wale Jamaa eti anazama wanamuona wanamuacha tu wanaanza kulialia na clip Video wanachukua Ile iliniuma kishenzi

Weka wanao mbali sana na masela Mavi

Hili neno naona umejifunza leo basi ndo limekuwa chorus.
 
Nataka kukumbusha tu kua wabongo wengi wanapitia hali ngumu hatujui kwasababu wao sio maarufu kama huyo Chid Benz. Street life ni gumu halafu kila mtu yuko busy na maisha yake na familia yake nobody cares about anybody else. Sasa hivi hata ukipoteza channel ya maisha familia, ndugu zako na watu wako wa karibu wanakuangalia tu hadi uugue ufe ili wakulilie na kukuzika fasta uwape gap la kusonga na maisha yao. Everybody is frustrated aseeh. Zamani familia hasa wazazi walikua karibu sana na watoto wao kiasi ambacho ni rahisi kupata msaada wa hali na mali, ushauri na counseling lakini sasa hivi watoto/ vijana wanalelewa na marafiki, wazazi wako busy kutafuta pesa ama unakuta hata hiyo familia haipo kabsa maana mtoto/ kijana analelewa na mzazi mmoja tu familia ishasambaratika (talaka). Inamana dogo akikutana na marafiki wazuri huko mtaani ni bora yake ila akikutana na marafiki wabaya anapotea mazima maana kumbuka hao ndo anashinda nao muda wote huko magetoni kwao so hata akipata changamoto yoyote itategemea watamshauri nini, wakimshauri upuuzi ndo hayo tunayoyaona kutopea kwenye uraibu wa madawa ya kulevya, ulevi na umalaya. Kwakifupi vijana siku hizi wanajilea wenyewe tu, nafasi ya wazazi na familia imekua ndogo sana na tunakoelekea ndo hatari zaidi maana ile bond kati ya mzazi na mtoto inazidi kupungua sana, I mean wazazi wanawakatia tamaa watoto wao mapema sana kwenye issue ya malezi. Nini kifanyike?! Kila mmoja akiwa mzazi ama mzazi mtarajiwa atafakari kwa kina nafasi yake kwa familia yake. Tuwemo!!
 
Chid mboni alishapona au wewe unazungumzia nini Chid kinachomsumbua sasa hivi ni tungi anakunywa sana na alishashauriwa na Daktari aache mitungi Ila Mzee anarudi kule kule sababu ni masela wanaomzunguka wale masela wa Ilala wote anabidi awapige chini ndio wanaomrudisha SHIMONI
Amepona vipi na unaambia anakaa maskani na mateja..
 
Haya maisha yamejaa mambo mengi sana usipokua makini utakufa kwa stress.... Mfano mm haya maisha ninayoishi ni tofauti kabisa na matarajio yangu, najiona kabisa nime underachieve.... Naamua tu ku-smile coz nikileta tu ujuaji nitajikuta nazungumzwa kwenye topic moja na wakina child benz
Ndio usitoke kwenye mstari ukaungana na kampani za kishamba utarudishwa shamba ukiwa hujitambui
 
Haya maisha yamejaa mambo mengi sana usipokua makini utakufa kwa stress.... Mfano mm haya maisha ninayoishi ni tofauti kabisa na matarajio yangu, najiona kabisa nime underachieve.... Naamua tu ku-smile coz nikileta tu ujuaji nitajikuta nazungumzwa kwenye topic moja na wakina child benz
Ucjal mkuu mamb yatakaa sawa tu.
 
Pole yake.mama ajitathimini uongozi wake.kwa Nini kipindi hiki tu chake kumekuwa na wimbi kubwa la waathirika wa madawa ya kulevya ikiwemo chidibenz?mama thibiti madawa ya kulevya unatuharibia wasanii wetu
 
Hali ya Msanii wa Hiphop Rashidi Makwilo (Chidibenz) inasikitisha sana sana, Siku za hivi karibuni amekua akiishi Msasani (Maandazi road) maskani moja na mateja, Kinachonisikitisha zaidi jamaa anaonekana hayuko sawa kiafya miguu imevimba, anaonekana aliumia na hajapona vizuri,miguu ameifunga bandage na anatembelea ndala, Nimemuona leo asubuhi nikiwa naelekea kazini atembea kwa msaada wa watu wanampa support (Nahisi alikuwa amelewa sana) Uso wake ni kama hauna matumaini

Nitoe wito kwa wasanii wenzake na Familia yake wamfuate pale msasani coz anaishi maskani na hana mtu wa kumuangalia, Sina uhakika ila kuna uwezekano labda amerudi tena kwenye wimbi la madawa ya kulevya

Kwa inavyoonekana ni kama wasanii wenzake wamemsusa, hawana time naye tena Lakini naona sio sahihi coz ni Msanii mwenzao inabidi wakubali kubeba hili jukumu la kumlinda na kumtunza Chidibenz, Juzi kwenye show ya Serengeti pale K/nyama viwanja vya posta, Chidibenz alipanda Wakimtenga hivi depression inaweza ikammaliza kabisa, Kwa upande wa Familia yake sijui wao wamejipangaje coz inaumiza sana kumuona Ndugu au mtu wako wa karibu akiwa anapitia kipindi kigumu

Vijana tujitahidini sana kuishi kwa nidhamu, Ujana una mambo mengi bila yakua na nidhamu ni rahisi kuanguka
Huyu bwana ni example of poor life choices wakati wa mafanikio
 
Mimi sikubaliani na wewe. Enzi akiwa kwenye peak alikuwa ni msanii ambaye alikuwa ana shows nyingi ana make ela ndefu shida ni pale alipotaka kuishi maisha aliyokuwa anayaona kwenye TV ya kutembea na msululu wa watu na kuwalisha na kuwanywesha na kuishi the same lifestyle kama la black American movies.
Haya ni matokeo ya kufanya uchaguzi mbovu maishani. Kwa kipindi chake na pesa aliyokuwa anapata kwa kipindi hicho ilikuwa nyingi angefanya kitu. Sidhani mtu kama Jay Mo alipata pesa nyingi kuliko Chid, but alifanya uamuzi sahihi.
Sasa hivi ni vigumu sana kumsaifia Chid kwanza kila anayetaka kumsaidia anageuka adui. Refer kisa chake na Diamond. Kaingiza vocal kwenye wimbo wake kumboost, kweli wimbo ukaenda hata mimi nilikuja kuusikiliza baada ya kuona ile performance yao, later anamkandia.
Chid kutumia madawa kaanza kuyatumia akiwa kwenye peak, akitumia madawa na pombe. So pesa imekata tayari ashakuwa addicted na madawa.
Ukifanya tathimini utagundua madawa ya kulevya wayamewadhuru wasanii wengi sana.

Ngwair, langa, chiddy Benz, Ray C, O-ten,Mr.blue,Banza stone, majina mengine sijayakumbuka hapa ila ni wengi mno.
 
Hali ya Msanii wa Hiphop Rashidi Makwilo (Chidibenz) inasikitisha sana sana, Siku za hivi karibuni amekua akiishi Msasani (Maandazi road) maskani moja na mateja, Kinachonisikitisha zaidi jamaa anaonekana hayuko sawa kiafya miguu imevimba, anaonekana aliumia na hajapona vizuri,miguu ameifunga bandage na anatembelea ndala, Nimemuona leo asubuhi nikiwa naelekea kazini atembea kwa msaada wa watu wanampa support (Nahisi alikuwa amelewa sana) Uso wake ni kama hauna matumaini

Nitoe wito kwa wasanii wenzake na Familia yake wamfuate pale msasani coz anaishi maskani na hana mtu wa kumuangalia, Sina uhakika ila kuna uwezekano labda amerudi tena kwenye wimbi la madawa ya kulevya

Kwa inavyoonekana ni kama wasanii wenzake wamemsusa, hawana time naye tena Lakini naona sio sahihi coz ni Msanii mwenzao inabidi wakubali kubeba hili jukumu la kumlinda na kumtunza Chidibenz, Juzi kwenye show ya Serengeti pale K/nyama viwanja vya posta, Chidibenz alipanda Wakimtenga hivi depression inaweza ikammaliza kabisa, Kwa upande wa Familia yake sijui wao wamejipangaje coz inaumiza sana kumuona Ndugu au mtu wako wa karibu akiwa anapitia kipindi kigumu

Vijana tujitahidini sana kuishi kwa nidhamu, Ujana una mambo mengi bila yakua na nidhamu ni rahisi kuanguka
Kama kweli ni mteja, mtu pekee anayeweza kumsaidia Chidi Benz ni Chidi Benz.
 
Ukifanya tathimini utagundua madawa ya kulevya wayamewadhuru wasanii wengi sana.

Ngwair, langa, chiddy Benz, Ray C, O-ten,Mr.blue,Banza stone, majina mengine sijayakumbuka hapa ila ni wengi mno.
Sana mkuu wengi sana. Sijui huwa wanaingia kwa kujua au kuna watu huwa wanawategeshea then wanajikuta tayari washaingia maana wana mifano mingi ya wenzao waliopotezwa na hiki kitu.
 
Tumchangie pesa ya matibabu aende India. Mazombi rusheni pesa ya matibabu kwenye namba Ile Ile.
Linachomsumbua chiddy kwasasa ni depression sio uteja kama awali. Vita ya uteja ameshaishinda kwa kiwango kikubwa, kwa sasa anachohangaika nacho ni kukubaliana na hali kuwa yeye sie tena yule chiddy Benz aliyekuwa kwenye Peak level za kimataifa, kwasasa amechafua image yake jamii inamtazama kama teja au muathirika wa madawa.

Hiyo sio vita ndogo. Imagine kuwa katika hiyo aina ya depression halafu uwe hauna pesa na unaona wasanii kama akina diamond ambao juzi kati uliwaona wakiwa wanatembea kwa miguu kwenda studio hawana hata mia mfukoni leo wana mafanikio makubwa kukushinda na wamekupiga bonge la gepu.

Hiyo lazima imletee msongo wa mawazo na ndicho kinachomfanya awe busy na unywaji pombe usio na ratiba.
 
Hali ya Msanii wa Hiphop Rashidi Makwilo (Chidibenz) inasikitisha sana sana, Siku za hivi karibuni amekua akiishi Msasani (Maandazi road) maskani moja na mateja, Kinachonisikitisha zaidi jamaa anaonekana hayuko sawa kiafya miguu imevimba, anaonekana aliumia na hajapona vizuri,miguu ameifunga bandage na anatembelea ndala, Nimemuona leo asubuhi nikiwa naelekea kazini atembea kwa msaada wa watu wanampa support (Nahisi alikuwa amelewa sana) Uso wake ni kama hauna matumaini

Nitoe wito kwa wasanii wenzake na Familia yake wamfuate pale msasani coz anaishi maskani na hana mtu wa kumuangalia, Sina uhakika ila kuna uwezekano labda amerudi tena kwenye wimbi la madawa ya kulevya

Kwa inavyoonekana ni kama wasanii wenzake wamemsusa, hawana time naye tena Lakini naona sio sahihi coz ni Msanii mwenzao inabidi wakubali kubeba hili jukumu la kumlinda na kumtunza Chidibenz, Juzi kwenye show ya Serengeti pale K/nyama viwanja vya posta, Chidibenz alipanda Wakimtenga hivi depression inaweza ikammaliza kabisa, Kwa upande wa Familia yake sijui wao wamejipangaje coz inaumiza sana kumuona Ndugu au mtu wako wa karibu akiwa anapitia kipindi kigumu

Vijana tujitahidini sana kuishi kwa nidhamu, Ujana una mambo mengi bila yakua na nidhamu ni rahisi kuanguka
Wasanii wanaishi kisanii,wanasubiri wasikie kazima utaona watakavyomiminika msibani,wengine wakilia kwa uchungu utafikiri walikua hawajui aliyokua anapitia...
 
Back
Top Bottom