KERO Hali ya upatikanaji wa maji baadhi ya maeneo ya Mbeya ni mbaya

KERO Hali ya upatikanaji wa maji baadhi ya maeneo ya Mbeya ni mbaya

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Chinu Mkodoli

Member
Joined
Apr 8, 2024
Posts
17
Reaction score
23
Habari za muda huu wana JF,

Licha ya kuwepo kwa mvua nyingi na vyanzo vingi vya maji katika mkoa wetu huu wa Mbeya lakini maeneo mengi yamekumbwa na ukosefu mkubwa wa maji.

Kwakweli hali ni mbaya, mfano, hapa mtaani kwangu ni kama mwezi hivi sasa hakuna maji na kama yakitoka basi hutoka usiku sana na speed huwa ni ndogo mithili ya mkojo wa paka.

Maeneo ya Airport, mtaa wa nyuma wa chuo cha TIA, kuzunguka Mzumbe na maeneo mengine mengi hali ya upatikanaji wa maji si nzuri.

Kwa sasa tunategemea maji ya mvua na maji ya visima ambayo si salama kwa afya zetu.

Najiuliza kama upatikanaji wa maji utakuwa hivi, itakuwaje kipindi cha kiangazi?

Nashangaa sana sehemu kama Mbeya kuwa na shida ya maji kwa kiwango hiki lakini cha ajabu sijawahi kusikia kiongozi yeyote akisema lolote kuhusiana na hali hii.

Ni kama jambo la kawaida tu na hakuna mtu yeyote anayestuka. Au labda sehemu iliyoathirika na uhaba huu ni ndogo kiasi kwamba hata viongozi wameshindwa kugundua tatizo? Lakini sehemu nyingine pia wanalalamika sana kutopata huduma hii.

Ni kama tupo katika dilemma kwasababu hatujui huduma hii itarudi lini.
 
Shida ni kuwa na Viongozi wenye vyeo vingi. Iliaminika Dr. Tulia atakuwa mkomboz wa Mbeya lakin kumbe hamna kitu.

Bora Mbeya turudi Kwa Sugu au mbunge mwingine yoyote asiye na mavyeo mengi.

Kwa kweli Tulia Mungu anakuona maana mara nyingi umekuwa na tabia ya kuwadhihak Wana Mbeya Kwa kutowajibika na kuishia kutoa misaada Uchwara. 2025 Kura yangu hutapata
 
Shida ni kuwa na Viongozi wenye vyeo vingi. Iliaminika Dr. Tulia atakuwa mkomboz wa Mbeya lakin kumbe hamna kitu.

Bora Mbeya turudi Kwa Sugu au mbunge mwingine yoyote asiye na mavyeo mengi.

Kwa kweli Tulia Mungu anakuona maana mara nyingi umekuwa na tabia ya kuwadhihak Wana Mbeya Kwa kutowajibika na kuishia kutoa misaada Uchwara. 2025 Kura yangu hutapata
Kabisa ndugu, yaani tunateseka Sana, hamna namna tu ya kufanya, ila kukosa hata maji ni kero kubwa sana. Tuwaombe viongozi wetu waliangalie hili kwa jicho la huruma
 
Habari za muda huu wana JF,

Licha ya kuwepo kwa mvua nyingi na vyazo vingi vya maji katika mkoa wetu huu wa Mbeya lakini maeneo mengi yamekumbwa na ukosefu mkubwa wa maji.

Kwakweli hali ni mbaya, mfano, hapa mtaani kwangu ni kama mwezi hivi sasa hakuna maji na kama yakitoka basi hutoka usiku sana na speed huwa ni ndogo mithili ya mkojo wa paka. Maeneo ya airport, mtaa wa nyuma wa chuo cha TIA, kuzunguka Mzumbe na maeneo mengine mengi hali ya upatikanaji wa maji si nzuri.

Kwa sasa tunategemea maji ya mvua na maji ya visima ambayo si salama kwa afya zetu. Najiuliza kama upatikanaji wa maji utakuwa hivi, itakuwaje kipindi cha kiangazi.

Nashangaa sana sehemu kama Mbeya kuwa na shida ya maji kwa kiwango hiki. Lakini cha ajabu sijawahi kusikia kiongozi yeyote akisema lolote kuhusiana na hali hii. Ni kama jambo la kawaida tu na hakuna mtu yeyote anaestuka. Au labda sehemu iliyoathirika na uhaba huu ni ndogo kiasi kwamba hata viongozi wameshindwa kugundua tatizo? Lakini sehemu nyengine pia wanalalamika Sana kutopata huduma hii. Ni kama tupo katika dilemma kwasababu hatujui huduma hii itarudi lini.
Kwakweli hali ni mbaya mno😩
 
Sio Mbeya tu ata Huku Goba Maji ni changamoto sana, ni aibu kwa Mji kama Goba hakuna Maji afu viongozi wapo tu
 
Back
Top Bottom