Halima Mdee bado una nafasi ya kutubu, Heshima na tamaa havikai pamoja

Halima Mdee bado una nafasi ya kutubu, Heshima na tamaa havikai pamoja

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
Ulikuwa umejijengea heshima ndani na nje ya nchi, ndani na nje ya bunge, tambua nguvu na heshima yako ilijengwa na sapoti ya wananchi waliokuzunguka hasa wanachama na viongozi wenzako wa Chadema ambao leo unataka kuwasaliti.

Kumbuka ulipokuwa jela ni wanachadema hawa hawa walikuchangia utoke sikumsikia Ndugai wala Mahera, ulipokamata kura feki ni wana Chadema hawa hawa walikuwa tayari kuumia na wewe, wale wanaokuona shujaa leo hasa wana CCM ndio waliokuwa wanakubeza na kukuzomea, ndio waliokucheka ulipovunjwa mkono na askari magereza.

Halima tambua nje ya umma utabaki Mdee wa kwenye mitandao ni sawa na samaki nje ya maji, alikuwepo Masumbuko Lwamwai akachagua tamaa, alikuwepo Mrema akachagua tamaa, na wewe umechagua njia hiyo.

Watawala wanaokutafuta leo ni kwa sababu uliteka mioyo ya wananchi wakishakunyang’anya hiyo nguvu ya umma kesho watagugeuza geuza kama chapati hutapata mtetezi.

Unashiriki kubomoa chama ulichokipigania kwa damu kwa miaka mingi kwa sababu ya ubunge wa miaka 5, hao watesi wako wa juzi ulioamua kuungana nao sio kwamba wanakupenda sana bali wanataka wakutumie baada ya hapo watakutupa kama mpira.

Uamuzi ni wako, karibu kwenye uwanja mpya wa mapambano, leo Ndugai ni rafiki kesho atakapoanza kukubeza bungeni usifedheheke, wananchi wakakapoanza kukuzomea mitaani ujue ndio njia uliyochagua.

Unafanya makosa lakini bado una nafasi, kama ulikwazika fikiria upya omba radhi kwa wananchi nafikiri watakusamehe.
 
Nikupe pole sana mdogo wangu hakuna Mdee kwa kuingia mkengenge bila kujitambua kwa kutunukiwa na CCM nawe ukawaingiza wenzako ukiwaaminisha kua hakuna wa kukugusa ndani ya chama kwamba na wewe umeota ndevu.

Halima Mdee umewaingiza wenzako mkenge bila kujali kesho zenu, kwa taarifa wengi mmewalazimisha kusaini na kuwaingiza kwenye list ya wanawake 19. Hawakua na la kufanya kwa vile wewe ni mwenyekiti wa BAWACHA ilikua ni lazima wakusikilize. Umemuingiza kwenye matatizo dada Nusrati Hanje ambaye alikua gerezani hakujua A wale B.

Lowassa na Membe ni wanachama wakongwe na wana michango mikubwa ndani lakini walopoleta fyoko wala CCM hakikujali kua kitagawanyika. Ilikua ni afya kwa CCM Lowassa kuondoka kuliko angebaki kipindi hicho, na Membe vile vile.

Miaka 5 ni kidogo sana, baada ya hapo mtajikuta katika hali mbaya sana ya kisiasa. Hamjui kwa vile sasa mnatafuta maslahi hamjaangalia future zenu.

Mnaenda kujifunza siasa mpya za CCM ghafla bila kujiandaa, itawachukua muda sana kuzizoea kuliko harakati zenu mlizokua nazo ndani ya CHADEMA ambapo mapambazuko yako njiani kutokana na wananchi kuichoka kabisa CCM ambayo kwa sasa inajitwalia madaraka kwa nguvu pande zote za bara na visiwani.

USHAURI WANGU
Bado ninayo nafasi ya kwenda kuomba radhi kwa viongozi wenu mkajiondoa kwenye yale majina 19, mtakua mmejijengea heshima kubwa sana kwa Watanzania ambao mpaka sasa hawawaungi mkono kwa maamuzi yenu.
 
Mwaka jana kulivuja sauti ya wabunge wa Chadema Said Kubenea na Anthony Komu wakipanga njama za kumuuwa Boniface Jacob ili hatimae wafanikishe adhima yao ya kumng'oa Freeman Mbowe kwenye uenyekiti wa chama.

Baada ya sauti hizo kuvuja mara moja chama kilitangaza kikao cha dharura cha kamati kuu kuwahoji ili waweze kuchukuliwa hatua kali sana ikiwa pamoja na kufukuzwa Chadema. Matokeo yake baada ya kikao cha kamati kuu hao wabunge wauaji walisamehewa na kutakiwa kuomba radhi tu!

Kama hali ni hiyo, wabunge wa viti maalum Chadema si wauaji na wala hawajatishia kumuuwa mtu yoyote ila wanajaribu tu kutumia haki yao ya kikatiba iweje wafukuzwe Chadema? Kweli kuwa mwanamke Chadema ni dhambi kubwa kuliko wapanga mauaji waliosamehewa??

Tusubiri na kuona kesho kikao cha kamati kuu chadema kitaamua nini, bila shaka Mbowe is going to be tested again na maamuzi tofauti na kufukuza yatamwimalisha ,na maamuzi ya kufukuza hao wanawake itakuwa ni kiss of death kwa Mbowe na Chadema kwa ujumla.
 
Hivi kati ya Wabunge walio teuliwa wa Chadema ni Halima Mdee pekee kwa nini lawama kwa Halima Mdee pekee.
 
Hallima Mdee YUKO SAHIHI KABISA.

Baadhi yetu watanzania tunaanza kutoa TAFSIRI isiyo sahihi ya ni nini USALITI KATIKA SIASA.

Mdee Hajasaliti...bali ameangalia MBALI KISIASA.

Zanzibar ni ndogo na waliokuwa wanachama wa CUF kule hawakuwa ni wengi Kama Hawa wa CHADEMA. CUF iliamua KUTOSHIRIKI UCHAGUZI wa mara ya pili kulikopelekea KUKAA NJE YA BARAZA LA WAWAKILISHI KWA MIAKA 5 mfululizo.

👉Hakukuzuia BARAZA LA WAWAKILISHI KUENDELEA NA KAZI ZAKE.

Bali kulisababisha CHAMA KIKOSE RUZUKU....
Bali kulisababisha WAWAKILISHI wakose "maslahi ya kazi yao walioichagua...".

Tusisahau kuwa SIASA NI KAZI..
Tusisahau kuwa NYUMA YA watu hawa 19 kuna AJIRA NYINGI....je tunataka AJIRA HIZO ZIFUTIKE?!!
Je, tunataka CHADEMA ifukuze WAFANYAKAZI wake nchi nzima kwa sababu ya "ukata" wa Kukosa RUZUKU?

MAMBO HAYA TUYAANGALIE KWA UHALISIA NA KUACHA HISIA.

CHADEMA wapunguze JAZBA kwani "siasa zetu Afrika" hazioani Sana na WENZETU waliokwishakutangulia KIDEMOKRASIA.

Tujikongoje sasa na huko MBELENI nasi TUTAFIKA LEVELS kubwa za KIDEMOKRASIA.

KUCHUTAMA SI UNAFIKI.
KUCHUTAMA SI USALITI
 
Swali kidogo, sheria za bunge la Tanzania haziruhusu wabunge wa kujitegemea, yaani wabunge binafsi, Jee hawa wabunge 19 watafanyaje au watafanywaje na bunge ikiwa jumamosi katika mkutano wao chadema wakiamua kuwafukuza uanachama?
 
.
Eti halima katunukiwa na CCM, kila mtu akivuruga cdm Basi kanunuliwa na CCM, ila akivuruga wa CCM amejitambua hajanunuliwa na upinzani, so sad
...yaani...we acha tu...

SAD
 
Wakiitisha maandamano hamjitokezi, wakiwekwa selo mnaishia kupiga hashtag Twitter ohh #freesomebody# upinzani wanawapigania watz ila nyinyi mko bize na kusaka mkate wenu, waacheni nao wasake matonge yao!
 
Eti halima katunukiwa na CCM, kila mtu akivuruga cdm Basi kanunuliwa na CCM, ila akivuruga wa CCM amejitambua hajanunuliwa na upinzani, so sad
Wewe mtu ulikuwa wapi? Mdee amesema mwenyewe mbele ya vyombo vya habari kuwa ameona kwa macho yake voti feki katika jimbo lake alokuwa anapigania, na kusema kuwa uchaguzi si wa haki, halafu leo anarudi kuingia bungeni kufanya kazi na alosema wamemuibia ubunge, hivi wewe hilo linakuingilia akilini? Mtu anakuibia shamba lako halafu anakwambia njoo na jembe tulime na unakubali tu?
 
Kapata nafasi ataacha vipi, huwezi ukawa masikini ukawa mwanasiasa bora, thus wenzetu huwezi ukawa masikini kisha wakupe uongozi never utahongwa. Thus Wana maendeleo.
 

Mdee alikuwa role model wa wengi.
Unadhani muhusika hajafikilia hilo kabla hajaenda kula kiapo acheni lawama. Usimuamini mwana siasa narudia tena usimuamini mwana siasa.
 
Back
Top Bottom