Halima Mdee bado una nafasi ya kutubu, Heshima na tamaa havikai pamoja

Halima Mdee bado una nafasi ya kutubu, Heshima na tamaa havikai pamoja

Future ipo chadema? Ulisikia wapi?
Mdee ana uhakika wa ajira ya miaka mitano, mshahara mono na uhakika wa kuinua mgongo!
Alafu hivi ni viti ni nafasi ya wanawake, mbona mma gubu nyinyi
 
Msimtisha bhana, leo mnasahau huyu dada alivunjwa mkono akikipigania chama, leo mnamuona hafai. Mwisho wa chadema kesho kama misimamo yenu ndiyo hii
Usisahau Yuda alikesha na kuomba pamoja na Yesu, lakin mwisho alimsaliti Yesu

Unasungumzia kuvunjwa mkono? Waliokufa wamepata nini?
 
Bwana MBOWE...

MWENYEKITI huyu hajapatapo KUTUBU baada ya KUIBADILISHA GIA ANGANI mbele ya mshenga Dr.Gwajima....

Mbowe hajapatapo KUTUBU kuhusu TUHUMA za kuwapendelea "baadhi ya wabunge wa viti maalum"

Kama iko AUDIO ama VIDEO akitubu tafadhali TUWEKEENI HAPA!!
 
Chadema ndio inajingiza matatizoni kama isipokuwa makini, siku zote ukiwa mwanasiasa usijaribu kujingiza matatizoni na kundi la wanawake. Hata wanaotaka Chadema ife wanajuwa ukitikisa kundi la kina mama, ndio umetikisa Chadema yote. Jaribu kutafuta suluhisho kuliko kuleta mabavu ambayo utayajutia mbeleni.
 
Hallima Mdee si msaliti...

Je na wale CHADEMA waliokacha MAANDAMANO ya AMANI kupinga matokeo ya uchaguzi TUWAITEJE?!!
 
Halima kashindwa life la kitaa bila ubunge.haahaa wanasiasa wetu ni shida. Chadema fukuzeni hao wamekula vya kutosha
 
Hallima Mdee amekacha kuwa STAMP ya kuwapitisha WABUNGE WA VITI MAALUM WALIO MBELEKO ya mfume dume wa mh.Mbowe...
 
Hivi ilikuwaje polisi hawakuwachukulia hatua?

Hivi ni nani alimvunja mdee mkono?

Hivi ni nani alimbambikia kesi Nusrati?

Hivi ni nani alimuweka matiko ndani miezi 2?

Hivi ni nani aliwaibia mdee, matiko, bulaya na wengine wanawake wengi wa chadema kwenye uchaguzi

Endelea na unafik wako maana ndo unakupa kula
 
Mdee alikuwa role model wa wengi.
Wangeanza kutubu wale ndugu zangu walionajisi uchaguzi na kupelekea yote haya. Usimbebeshe mmojawapo wa waathirika wa uchafuzi huu na ukawaacha wahusika. Nadhani wao kwenda bungeni wameonyesha ukomavu kisiasa. Acha maisha yaendelee mkuu.
 
Kukacha kwenda BUNGENI Ni kukacha RUZUKU YA CHAMA...

Chadema Hawa ambao WAMEKUWA WAKIPITISHA BAKULI kuomba KUCHANGIWA sasa wanataka waendelee KUWAKAMUA WATANZANIA kipindi hichi cha "uchumi huu wa kati"?!!!
 
Haahaa life la kitaa limemshinda mdee, kesho aulizwe swali moja tu, unataka kuwa mbunge au mwanachadema full stop.Akitaka kuwa mwanachadema aandike barua ya kujiuzulu ubunge nje ya hapo chadema wamalizane naye.
 
Wangeanza kutubu wale ndugu zangu walionajisi uchaguzi na kupelekea yote haya. Usimbebeshe mmojawapo wa waathirika wa uchafuzi huu na ukawaacha wahusika. Nadhani wao kwenda bungeni wameonyesha ukomavu kisiasa. Acha maisha yaendelee mkuu.
Ukomavu gan mkuu?
 
Hallima Mdee si MSALITI wala si MNAFIKI....

Kuna msaliti anayekesha RUMANDE kila UCHAO?!!

Nusrat HANJE si msaliti.....amepata madhila KIBWENA....

Esther Matiko Amedhalilishwa mno...mpaka VIDEO zipo ONLINE,naye ni MSALITI?!!

HUYO MTAKATIFU HAJAZALIWA BADO....
 
Hivi ilikuwaje polisi hawakuwachukulia hatua?

Hivi ni nani alimvunja mdee mkono?

Hivi ni nani alimbambikia kesi Nusrati?

Hivi ni nani alimuweka matiko ndani miezi 2?

Hivi ni nani aliwaibia mdee, matiko, bulaya na wengine wanawake wengi wa chadema kwenye uchaguzi

Endelea na unafik wako maana ndo unakupa kula
Usisahau na yule aliyempiga dole la kundu Ester Matiko.
 
David Silinde alisema SIASA Ni maisha yake...it's true...SIASA NI AJIRA kwani nyuma ya wanasiasa Kuna WATU WENGI wanaoishi....

Hallima Mdee ameanza harakati toka sisi wadogo hadi leo TUNAMUONA akiwa DADA MTU MZIMA....

Dada wa watu amededicate maisha yake kwa CDM kufikia mpaka kutokuwa na MUME NA WATOTO....

Mume wake ni CHADEMA....
Watoto wake ni CHADEMA....

LEO HII ANATUKANWA NA KUDHALILISHWA hivi?!!

So sad....
 
Ulikuwa umejijengea heshima ndani na nje ya nchi, ndani na nje ya bunge, tambua nguvu na heshima yako ilijengwa na sapoti ya wananchi waliokuzunguka hasa wanachama na viongozi wenzako wa Chadema ambao leo unataka kuwasaliti.

Kumbuka ulipokuwa jela ni wanachadema hawa hawa walikuchangia utoke sikumsikia Ndugai wala Mahera, ulipokamata kura feki ni wana Chadema hawa hawa walikuwa tayari kuumia na wewe, wale wanaokuona shujaa leo hasa wana CCM ndio waliokuwa wanakubeza na kukuzomea, ndio waliokucheka ulipovunjwa mkono na askari magereza.

Halima tambua nje ya umma utabaki Mdee wa kwenye mitandao ni sawa na samaki nje ya maji, alikuwepo Masumbuko Lwamwai akachagua tamaa, alikuwepo Mrema akachagua tamaa, na wewe umechagua njia hiyo.

Watawala wanaokutafuta leo ni kwa sababu uliteka mioyo ya wananchi wakishakunyang’anya hiyo nguvu ya umma kesho watagugeuza geuza kama chapati hutapata mtetezi.

Unashiriki kubomoa chama ulichokipigania kwa damu kwa miaka mingi kwa sababu ya ubunge wa miaka 5, hao watesi wako wa juzi ulioamua kuungana nao sio kwamba wanakupenda sana bali wanataka wakutumie baada ya hapo watakutupa kama mpira.

Uamuzi ni wako, karibu kwenye uwanja mpya wa mapambano, leo Ndugai ni rafiki kesho atakapoanza kukubeza bungeni usifedheheke, wananchi wakakapoanza kukuzomea mitaani ujue ndio njia iliyo hatua.

Unafanya makosa lakini bado una nafasi, kama ulikwazika fikiria upya omba radhi kwa wananchi nafikiri watakusamehe.
Mkuu imewapa USHAURI mzuri Sana,rudisha kila kilicho Chao, jiondoeni, ombeni msamaha kwa wanachama na chama, mtaeleweka ,vinginevyo mtapotea kisiasa, mtaandamwa na masononeko kwenye nyoyo zenu, mtaanza kujinyanyapaa na Jamii zenu zilizowazunguka nazo zitawanyanyapaa,
 
Kwa nini atubu na kwa nini chama kisimuache aendelee kuwakilisha watanzania wanyonge

Hawezi kuachiwa wakati hakuteuliwa na chama chake kama kuna kikundi kilichomdanganya aondoke na hicho kikundi chake
 
Enph_OsXMAALX-I.jpeg


Wanadamu wana utamaduni wao mzuri tu. Unaweza kufanya mambo kadhaa mazuri wakaponda,au wakakaa kimya tu wakibaki kuyaona yale mabaya unayofanya.

Sisi watu wa kuhojihoji tumekuwa tunauliza kwa nini usubiri nife ndio unisifie? Nisifie sasa bwana.
Funzo analotoa Halima Mdee juu ya usaliti aliofanya linatukumbusha kuwa na akiba ya sifa. Tusubiri mtu afe kwanza ndio tumsifie. Kwa sababu baada ya kifo hatakusaliti tena juu ya sifa ilizompa. Unaweza kumpa mtu sifa nzito nzito kesho akafanya kituko usijue unaficha wapi sura yako.

Achana na heshima ya muda mrefu aliyojijengea Halima Mdee kwa muda mrefu toka akiwa viti maalumu.
Ni juzi kati tu hapo aliwadis sana kina Lijualikali juu ya usaliti waliofanya! Ni jana kati tu hapo alimkana Shemasi Kigogo mwenye Twita yake kwamba aache kumtungia ujinga.
Hayo yalitufanya mimi na wenzangu tukamsifia sana. Tukasema huyu ni jembe kuliko hata wale wabunge wanaume. Tazama mtu anaacha mamilioni sababu ya kulinda utu wake.

Yaliyotokea juzi ni aibu kubwa.

Kwa hivyo MwanaJF nitakusifia siku ukifa. Watu wangu @MshanaJr The bold Tundu Lissu John Mnyika nitaendelea kuwakubali tu ila nitawasifia siku mkifa.

Enl3asmXEAAfhLf.jpeg

Screenshot_20201126-164005_Chrome.jpg
 
Kuna tofauti ya HARAKATI na SIASA....

Mh.Mdee amefanya HARAKATI MIAKA YOTE....leo hii ameamua kufanya SIASA anaonekana ni KIZINGITI....
 
Back
Top Bottom