Halima Mdee bado una nafasi ya kutubu, Heshima na tamaa havikai pamoja

Halima Mdee bado una nafasi ya kutubu, Heshima na tamaa havikai pamoja

Kwamba kwa vile miaka yote mnaiba mlikuwa mmezoea matokeo?

Kwa sasa mnasema mbona miaka mingine tuliiba lakini hamkufanya hivi, hivyo mnaomba tutumie misimamo ile ile kwa sababu wizi ni ule ule?

Maajabu ya firauni.

Haya si ndiyo yale ya kuiba tumekwiba lakini kukiri ng'o!

Hukusikia safari hii kuwa:

Ukhanithi basi au Sasa basi?

Ukhanithi basi! Sasa basi! Hayo ndiyo habari kamili.

Uzee mwisho chalinze - Friday, 0800 27th Nov 2020!
Jibu hoja acha porojo
 
Halima na wenzake wote wako under surveillance ya tiss , kila wanachokifanya wanakifanya kwa maelekezo ya Mhutu na tiss yake . Hata kuja kwenye kamati kesho mpaka waruhusiwe , inategemea Jiwe atakuwa kaamkaje iyo kesho umeelewa ?

Mkuu yanaeleweka hayo. Lakini ni heri busara ikawa rejea.

Kukumbuka ulikotoka ni muhimu zaidi kuliko kuegamia kule unakodhani unakwenda.

Wanasema "tamaa mbele, mauti nyuma."
 
Mkuu kwa hiyo hao wamechaguliwa na CCM? shida CDM haina msimamo rejea 2015 Slaa vs Lowassa, siamini Kama hao wamama wamejiamulia wenyewe tu, siamini Kama hii inshu mbowe alikuwa haijui mapema
Katibu Mkuu kasema hao hawana baraka za chama na kamati kuu ambayo ndio yenye uwezo wa kuteua wabunge viti maalum haijakaa!
Ndio maana hata Spika aliwasurprise waandishi,waliitwa viwanja vya bunge bila kujua spika anawaitia nini!
Hii ni dhahiri huu mchezo ulipangwa na spika ameshiriki!
CDM isipowaadhibu vikali kwa kuwafuta uanachama basi mimi ndio itakuwa mwisho kuwa mfuasi wake!Nitahamia Chauma!
 
Wataacha vipi kugomea kama pori jipya nyani wale wale?
Yes, walikuwa wanagomea matokeo lakini wanakubali kuingia bungeni kwa kuwa walikuwa wanaume (wafanya maamuzi); sasa wanawake wamepata nafasi ya kuingia bungeni minjemba inapinga kwa kuwa haitaingia bungeni!
#hakisawakwawote
 
Katibu Mkuu kasema hao hawana baraka za chama na kamati kuu ambayo ndio yenye uwezo wa kuteua wabunge viti maalum haijakaa!
Ndio maana hata Spika aliwasurprise waandishi,waliitwa viwanja vya bunge bila kujua spika anawaitia nini!
Hii ni dhahiri huu mchezo ulipangwa na spika ameshiriki!
CDM isipowaadhibu vikali kwa kuwafuta uanachama basi mimi ndio itakuwa mwisho kuwa mfuasi wake!Nitahamia Chauma!
Mkuu jiandae kisakolojia kesho hiyo ngoma ni 50-50
 
Sawa mwisho wa yote utamkuta mbowe bora tu hili wapunguze mihemko ya mitandao busara inahitajika zaidi achana na danadana za uchaguzi lakini hii mitandao imechangia zaidi kukiumiza chadema

Mkuu CDM ni imara kuliko unavyoweza kudhani. CDM ni people driven. Hamkujifunza hata katika kampeni? Ni watu watakaoamua hatima yao hawa kesho.

Kwamba nani kahusika? Tumewaomba wawe wazi hata kama wahusika ni Jiwe, Pole pole, bashiri, Mbowe, Mnyika nk na watajwe tu!

Tatizo liko wapi hapo hadi tuanze kupiga ramli hadi wino upo?
 
Mabibi na mabwana na hasa wale walio wazalendo. Ni ukweli ulio wazi kuwa maji yakishamwagika huwa hayazoleki. Hata hivyo tunaweza kuganga yajayo.

Ni ukweli usiopingika kuwa, Bi. Halima ni mmoja kati ya makamanda shupavu kabisa walioipigania CDM kwa uaminifu mkubwa, licha ya kupitia katika changamoto nyingi.

Wandugu, kujikwaa si kuanguka na kosa moja halifukuzishi mke!

Siyo siri kuwa, tukio hili lililopelekea mtafaruku huu, limetusikitisha na kutusononesha mno. Kwa hakika itakuwa vyema sana kama tutashirikiana sote kulimaliza suala hili kistaarabu kwa mustakabala mwema wa chama chetu.

Ni furaha iliyo je mbinguni, mwenye dhambi mmoja akitubu?

Msingi wa hoja kama chama ni kutokutambua haramu ya uchaguzi 2020 na yote yatokanayo nao. Huu haupingiki aliye na hoja tofauti na atushawishi kwa hoja. Hiyo ndiyo demokrasia.

"Hapa pana namna ambayo suala hili Bi. Halima, litakwisha na adui yetu akatepeta na kulegea vilivyo:

1.Ombeni radhi kwa dhati kabisa mkijutia yote yaliyotokea.
2. Wekeni wazi bila kuficha kama ni Hadaa, ghiliba, ahadi, vitisho, nk na mkiwaweka wazi wote waliohusika na sarakasi hii. Koleo na likaitwe kwa jina lake.
3. Tuunganeni sote kumshambulia na kumwaibisha mbaya wetu.
4. Mengine kama yatakavyo shauriwa na waungwana wengine."

Sote tu wakosaji, shuruti tuwe tayari kusamehe 7x70.

Hayupo aliyepanga kukufukuzeni. Chonde chonde uamuzi wa kutofika huko mnao pia mikononi mwenu.

Ashindwe mbaya wetu na washirika wake wote.

Washindwe na walegee!
Watu wasisahau pia mchango mkubwa wa hawa wanawake. Sisis ni binadamu na kunawakati kulingana na hali inavyokwenda hata wewe ungeamua kama walivyoamua wao. Kosa hili lisitufanye sisi kuwachukulia kama ni wasaliti. Pia tutakuwa wizi wa fadhila ikiwa tutasahau mchango wao katika kupigania demokrasia nchini.
 
Yes, walikuwa wanagomea matokeo lakini wanakubali kuingia bungeni kwa kuwa walikuwa wanaume (wafanya maamuzi); sasa wanawake wamepata nafasi ya kuingia bungeni minjemba inapinga kwa kuwa haitaingia bungeni!
#hakisawakwawote

Mnajishaua sana. Ila habari mlikuwa nayo mapema tu:

Ukhanithi basi! Sasa basi!

Mlidhani maana yake business as usual? Kweli mburula ni mburula tu!
 
Naona sasa unataka kujaza reply kwenye siredi tu 😅

Mstari wa kwanza kwenye uzi ulitanabaisha wazi nani uzi huu haumfai:

"Mabibi na mabwana na hasa wale walio wazalendo."

Hapa chini kulikuwab na kionjo zaidi kwenu:

IMG_20201126_180144_563.jpg


Kwa hakika "mboga mboga" huu uzi hauwahusu. Huoni wenzio wengi wamepita kimya kimya?

Umburula kweli nao ni kipaji!
 
Watu wasisahau pia mchango mkubwa wa hawa wanawake. Sisis ni binadamu na kunawakati kulingana na hali inavyokwenda hata wewe ungeamua kama walivyoamua wao. Kosa hili lisitufanye sisi kuwachukulia kama ni wasaliti. Pia tutakuwa wizi wa fadhila ikiwa tutasahau mchango wao katika kupigania demokrasia nchini.

Wanasema waungwana, "kosa si kutenda kosa, bali kurudia kosa."

Ajabu na kweli ni kuwa uelekeo wowote wa maelewano ikiwamo katika mtafaruku huu, ni msiba mchungu kwa kina "mboga mboga."

Kama wanatubu na kujirudi. What is the issue?

Mtu mzima uswahilini akisha sema "samahani," kesi yote huishia hapo!
 
Halima na wenzake wote wako under surveillance ya tiss , kila wanachokifanya wanakifanya kwa maelekezo ya Mhutu na tiss yake . Hata kuja kwenye kamati kesho mpaka waruhusiwe , inategemea Jiwe atakuwa kaamkaje iyo kesho umeelewa ?
Kwa hiyo, hao ni mateka na siyo waasi?
 
Kwa nini mnataka waombe radhi?? Kwa kosa gani.Yaani kutekeleza kwa takwa la maamuzi ya kamati kuu imekuwa taabu

Umesoma uzi hukuona kosa lao? Au ndiyo hii ya kukurupuka kutoka mashimoni. Kumbuka uzi huu umezingatia hili:

"Mabibi na mabwana na hasa wale walio wazalendo."

Yawezekana haumo kwenye kundi hili. Kama ni hivyo ulione vipi kosa lao?

Acha nijaribu tena. Kosa lao liko kwenye mada na liko kwenye bold. Rejea ukasome kule kama hujasoma.
 
Back
Top Bottom