Halima Mdee: Deni la Taifa limefika Tsh. 71 trillion, maana yake kila mtanzania anadaiwa Tsh. 1 million na ushee

Kama vipi ile noa yangu kwenye zile hela za barick waizuie wasinipe tumemalizana
 
Mbunge asiyefungamana na upande wowote...hahahaha..
Hii nchi ina upuuzi mwingi sana.
Alafu mwingine alipe kodi huku watu wanazitumbua tu.....huu ni upumbavu wa hali ya juu.
 
Yawezekana sisi tuliingizwa uchumi wa kati kwa kuangalia wastani wa deni kwa nchi za uchumi wa katinji kiaso gani? Wakaona tumefikia kiwango.
 
nchi ina madeni lukuki huku wabunge wanalipwa posho za kijinga kbs wakati hawana tija yoyote

mie sidaiwi watajua wenyew waliokopa
Mkuu unalipa bila kujua unalipa deni. Hebu fikiria sukari ilikuwa inauzwa buku kg 1 wakati wa jk baada ya kuingia mawimbi yalee tunauziwa 2,600/kg. Sasa hivi ukinunua sukari unalipa deni au haulipi? Huo ni mfano tu wa bidhaa moja kuna nyingine nyingi tukizinunua tunajikuta tunalipia deni bila kujua
 
Kama millioi moja kila Mtanzania basi deni letu ni himilivu Serikali iendeleze miradi yote ya kimkakati.
 
Hio Milioni Moja Laki Moja Na Themanini Yenyewe Ni Mshahara Wangu Nilioubana Mwaka Mzima Baada Ya Kubana Matumizi na Kujinyima Angalau Nidundulize Nijenge Kibanda cha 20M Niepuke Manyanyaso ya Baba Mwenye Nyumba.

Tutakoma.
 
Wangeweka account namba sisi wenye hela tulipe madeni yetu
 
Tatizo la wasomi kama mdee ni ujinga .Baadhi ya Vyuo vyetu vinazalisha watu wenye IQ ndogo mno.Wansona deni utafikiri wakopeshaji badala ya kuona vitu vilivyofanywa na hiyo Trilioni 71 imefanya kazi hukua hiyo hela ambayo iko kwenye miradi kamilika au endelea halafu gawia Kila mtanzania kwa hiyo miradi yote ya barabara na majengo nk halaf ujue kila mmoja anamiliki mali ya kiasi gani kwenye ndege zote zilizonunuliwa na barabara zote zilizojengwa ikiwemo miradi ya umeme na hospitali nk

Kuangalia nchi inadaiwa kiasi gani hiyo hasa ni kazi ya mkopeshaji wewe mkopaji unatakiwa kuangalia kilichofanyika ukigawa wananchi wako kila mmoja ana Asset kiasi gani kwa makert value ya sasa

Tatizo la wasomi wetu ni kumeza tu notisi vyuoni logic wengi wako zero akiwemo.Mdee nk huko bungeni ndio maana hadi bungeni akina msukuma na kibajaji ambao ni darasa la saba wanawaporomoshea matusi wasomi mchana kweupe
 
Ngoja nikaplipe kwanza 80000, hizi 1100000 nitalipa mwezi wa 9
 
Huyu mzee kafilisi nchi asee
Hizo pesa Trilioni 71 alipeleka kwenya akaunti zake binafsi za uswisi? very poor argument.Barabara zilizojengwa huzioni? umeme kila kijiji huuoni? Elimu bure huioni? Ndege huzioni? Vituo vya afya nchi nzima huvioni? nk wewe kipofu?
 
Hivi wale jamaa waliosema kwamba wanajenga kwa pesa za.ndani wanaweza tueleza deni limefikaje hapo?
 
Wewe unaulizwa hilo deni kama nani? Au ni wale covid 19?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…