Halima Mdee na wenzake Washinda kesi dhidi ya CHADEMA. Waendelea kuwa wanachama wa CHADEMA. Kuendelea na Ubunge wao

Halima Mdee na wenzake Washinda kesi dhidi ya CHADEMA. Waendelea kuwa wanachama wa CHADEMA. Kuendelea na Ubunge wao

Kwa jinsi hukumu ilivyotolewa bila kutaja Vifungu vyovyote au kusoma Katiba ya Chadema juu ya Wajumbe wanaounda Baraza Kuu ni wazi Hukumu ilipangwa kimkakati.Ushauri kwa Chadema.Maadamu Kama Chama tayari Kamati Kuu na Baraza Kuu limewafukuza Halima na Genge Lake achaneni nao endeleeni na Mipango mingine binafsi naamini hata Baraza Kuu likikaa na kuwafukuza mkakati waliopangiwa na CCM ni kukataa Rufaa tena na Bunge halitawafukuza mpaka RUFAA yao isikilizwe na itakuwa Mwaka 2026.CCM inaona AIBU ikiwafukuza Bungeni kina HALIMA kwani walikubaliana kuwalinda mpaka 2025.

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
Sisi wengine tulishaliona hilo tangu mwanzo !
Hakuna geni hapo ! Akina Mdee wapo sana mpaka 2025 !!
 
Halima Mdee na wenzake Wana uwezo wa kutoa tsh 1m kwa kila mjumbe wa Baraza Kuu
Hata bila kutoa kitu !!
Wale wapo wapo sana tu kwa njia zozote zile including ku-buy time kwenye mashauri mengine yeyote yatakayoletwa kuhusu hilo shauri !!

Tuliwaambiaga tangu mwanzo !!
 
Tuna uandishi wa kikasuku usiozingatia taaluma. Yani mtu anaokota habari bila kuilewa vizuri anaichapa. Ndio maana baadhi ya vyuo vya habari kama SAUT ukisoma uandishi lazima usome Media Law, Human Rights Law na Constitutional Law. Pia kuna option za Criminal Procedure Law na Law of Evidence ili ukiripoti mambo ya kisheria usiwe tabula rasa (angalau uwe na uelewa kidogo).

Anyway; ngoja nitoe shule kidogo maana wengi wamepotoshwa eti akina Halima wamerudishiwa uanachama. SI KWELI. Kwanza ieleweke hawakufukuzwa uanachama na Baraza Kuu, bali Kamati kuu (angalia next slide). Kamati Kuu iliwafurusha tar.27/11/2020 na uamuzi huo kutangazwa na Mwenyekiti Mbowe tar.28/11/2020.

Akina Halima wakakata rufaa Baraza kuu ambalo liliketi tar.12 May 2022 na kubariki maamuzi ya Kamati kuu. Akina Halima wakaenda Mahakamani kupinga maamuzi ya Baraza kuu.

Hoja zao;
1. Hawakupewa haki ya kusikilizwa.
2. Suala lao kushughulikiwa kwa dharura
3. Kuhofia usalama wao
4. Wajumbe wa Kamati kuu kuwa pia wajumbe wa Baraza kuu na hivyo kuathiri maamuzi (law of impartiality).

Leo Jaji Cyprian Mkekha ametoa maamuzi yafuatayo;

1. Kuhusu haki ya kusikilizwa amesema waleta maombi (akina Halima) walipewa haki ya kusikilizwa lakini wakaamua kutokuitumia.

2. Kuhusu suala lao kushughulikiwa kwa dharura, amesema Chadema walikua na haki ya kushughulikia kwa dharura kwa mujibu wa Katiba yao ibara ya 6.5.1(d)

3. Kuhusu kuhofia usalama wao, Jaji Mkekha amesema hoja hiyo haina mashiko maana waleta maombi (akina Halima) hawakuripoti kwenye chombo chochote cha usalama.

4. Kuhusu "Law of Impartiality" hapa ndo pameleta shida. Jaji Mkekha amesema haikua sahihi wajumbe wa Kamati kuu (iliyowafukuza uanachama akina Halima), kushiriki kikao cha Baraza kuu ambacho kilisikiliza rufaa zao. Amebatilisha maamuzi ya Baraza kuu kwa sababu ya kuhudhuriwa na wajumbe wa Kamati kuu.

Kwa kifupi Jaji Mkekha amesema Baraza kuu la Chadema likae tena (bila uwepo wa wajumbe wa Kamati kuu) na lipitie upya rufaa za akina Halima. Kwahiyo akina Halima bado SIO WANACHAMA WA CHADEMA mpaka Baraza kuu litakapopitia upya rufaa zao. Kama hujaelewa muite Miso Misondo umuulize Malisa amepigaje hapo?View attachment 2842875View attachment 2842876

Sent using Jamii Forums mobile app
Huu ndio usahihi wa hukumu hii...
 
Rudi shule Mangi ,mzee mbowe alikuwa mwenyekiti kwenye vikao vyote ,elewa neno Mwenyekiti

..kinachotakiwa kuzingatiwa ni kama Katiba ya Chadema imefuatwa wakati wa kuwafukuza uanachama.

..Jaji amejiongeza kitu ambacho hakutakiwa kukifanya ktk maamuzi yake.
 
Mnapenda Sana kuwafananisha CCM na wapinzani. Acheni unafiki. Unajua kwamba bungeni pamejaa CCM asilimia 94% then unalazimisha kuweka na upinzani, tuwe serious.
Kuwafananisha kwenye nini? Mie nimeeleza kuwa hao wabunge kwa pamoja wote huwa kitu cha kwanza ni masilahi yao(au ya chama) kisha ndio hufuata masilahi ya wananchi, na siku zote huwa na umoja kwenye suala la masilahi yao bila kujali upinzani au ccm.
 
Back
Top Bottom