Halima Mdee na wenzake watinga Bungeni licha ya CHADEMA kutangaza kuwafukuza rasmi

Halima Mdee na wenzake watinga Bungeni licha ya CHADEMA kutangaza kuwafukuza rasmi

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
1652427366743.png

Dodoma. Baadhi ya wabunge kati ya 19 waliofukuzwa uanachama na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wakiingia bungeni tayari kuendelea na shughuli za Bunge jijini Dodoma, leo Ijumaa Mei 13, 2022.

Jumatano ya Mei 11, 2022 Baraza Kuu la Chadema lilitupilia mbali rufaa za wabunge hao 19 kupinga uamuzi wa Kamati Kuu ya chama hicho kuwafukuza uanachama kwa tuhuma za usaliti kwa kukubali kwenda kuapishwa kuwa wabunge kinyume na msimamo wa chama hicho kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa 2020.
 

Dodoma. Baadhi ya wabunge kati ya 19 waliofukuzwa uanachama na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wakiingia bungeni tayari kuendelea na shughuli za Bunge jijini Dodoma, leo Ijumaa Mei 13, 2022.​

View attachment 2222525

Jumatano ya Mei 11, 2022 Baraza Kuu la Chadema lilitupilia mbali rufaa za wabunge hao 19 kupinga uamuzi wa Kamati Kuu ya chama hicho kuwafukuza uanachama kwa tuhuma za usaliti kwa kukubali kwenda kuapishwa kuwa wabunge kinyume na msimamo wa chama hicho kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa 2020.
Posho za leo wanatafuna bure tuu
 
Mshawafukuza basi inatosha msiendelee kuwafatafata. Wanasiasa wa kweli ni wachache sana walio wengi ni njaa tu. Wajinga ni wale waliopata majera, kufa au kufungwa jela kwaajili ya kupigania siasa za njaa kama za hawa wapinzani wa TZ.
 
hii nchi mwendazake alitaka kuiharibu vibaya sana, sema mkono wa Bwana umetuokoa !! mambo kama haya ni aibu kubwa kimataifa, looks like we're not organized & uncivilized.
Unataka kusemaje wewe, Jiwe ana mwaka amekufa bado amewashikilia masikio? Jiwe amekaa nao miezi minne tuu akiwa na mamlaka..... nyie mmekaa nao mwaka mzima na ushehe mkiwa na mamlaka yote. .bado mnamlaumu
 
Spika atasema kwamba hajapata barua rasmi kutoka Chadema inayo mtaarifu kwamba wamefukuzwa uanachama.

Ama kama amepata barua kutoka chadema, atasema kwamba hana taarifa rasmi kutoka kwa msajili wa vyama vya siasa.

Baada ya hapo bunge litalipuka kwa shangwe na kisha spika atatangaza kwamba yeye anawatambua kama wabunge halali wa chadema.
 
Back
Top Bottom