Halima Mdee na wenzake watinga Bungeni licha ya CHADEMA kutangaza kuwafukuza rasmi

Halima Mdee na wenzake watinga Bungeni licha ya CHADEMA kutangaza kuwafukuza rasmi

Hii post ndefu ni ya hoja za kulazimisha, naona kila mara unairudia ili kupotosha huku ukisema kigogo wa Cdm, na kuwa akina Halima waliogopa kumtaja. Kuna jambo linasemwa kila mara na unalikwepa kwa makusudi maana halibebi uzushi wako. Nusrat Hanje alikuwa magereza, na alitolewa usiku jambo ambalo halikubaliki kisheria, na akasafirishwa usiku kupelekwa Dodoma ili kuwahi kuapishwa. Je huyo kigogo wa Cdm ndiye aliyekuwa na nguvu kumtoa mtu gerezani usiku? Au Paskali bado unadhani watu ni wajinga wa hivyo?

Utetezi wa haya mauzishi yako ulikuwa unafanya hata baada ya shambulio la Lisu. Ulikuwa unaleta story ndefu na kuweka malink ya zamani ukidhani utafanikiwa kutupotosha kuhusu shambulio la Lisu. Tukawa tukikuhoji nani aliagiza askari wa getini kwenye makazi ya viongozi waondoke, na aliyeondoa CCTV camera zilizokuwa maeneo yale, huna majibu unalazimisha kuleta porojo zisizo na kichwa wala miguu. Huenda umepewa kazi ya kupotosha na kuhakikisha jamii inabaki na sintofahamu ya maovu ya serikali kwa faida yako binafsi, lakini kwa bahati mbaya watu wanauelewa mpana kiasi kwamba tunaishia kukudharau tu. Unataja matukio yako ya huko nyuma, sijui kumuuliza Magufuli ili kutaka tukuone una misimamo, au kama sehemu ya utetezi wa huu uzushi wako, lakini hakuna mjinga wa hivyo hapa.

Cc: Nguruvi3, joka kuu, mag3
Hawa wenye post ndefu achana nao wanaliloa Ruskington ya UN baba kwa serikali wakiwa na upinzani au kambi rasmi ya upinzani amabayo inaundwa kwa asilimia fulani na kuwa na kambi rasmi ya upinzani bungeni
 
Uchaguzi wa 2020 ulikuvuruga sana. Ulipata kipigo kibaya sana. Bado unakinyongo.

Sijawahi kugombea cheo chochote hata ndani ya familia yangu, ila uchaguzi wa 2020 chini ya dhalimu ulikuwa wa kihayawani kuliko maelezo. Kinyongo na dhalimu nilianza toka alivyoanza ulevi wa madaraka, uchaguzi wa 2020 ulisimika rasmi kinyongo na yeye. Imeisha hiyo.
 
KK ilikaa tarehe 11, Tarehe 13wakawepo BUNGENI, chadema wakati huo bado haijaandika barua rasmi kuiwakilisha BUNGENI,
Chadema watakapo andikia bunge barua ikafaamika rasmi na spika akapata kizunguzungu hapo ndipo tuta judge kunanini?, maana mchakato wa chadema ulikuwa wazi.
 
Kuhusu Lowassa kuhamia CHADEMA 2015 na kupewa nafasi ya kugombea urais, msingi ule ule wa Katiba, Viongozi, wanachama na vikao ulitumika kufanikisha hilo. Na huo unabakia kuwa ni uamuzi wa Chama. Upende au usipende.
Mnachekeshaga!

Sawa mlikaa mkakubaliana matokeo yake ni aliyekuwa makamu mwenyekiti wenu Chacha Wangwe, aliyekuwa makamu mwenyekiti wenu Zitto, aliyekuwa katibu wenu mkuu Dr. Slaa, waliyekuwa wenyeviti wenu wa Bavicha (, Shonza, Katambi, n.k) na Bawacha (Mdee). Na kadhalika na kadhalika.

Ni hivi, kwa attitude yenu ya kutojichunguza wenyewe na mifumo yenu na kulea vitabia vya kulaumu laumu wengine kwa matatizo yenu mnayojisababishia wenyewe, mtafukuzana wote hadi abaki mbowe peke yake ili ajifukuze mwenyewe.

Uneutral wangu au kutokuwa neutral wala si hoja ya msingi. Unaweza kuassume kwamba sipo neutral and that's fine. Na pengine sina sababu yoyote wala interest yoyote kwa nini hata nicomment hapa kuhusu chadema. Si mwanachama, sijawahi kuwa mwanachama na wala sijawahi kufikiria kuwa mwanachama. Sema tu ni hiki kitabia changu cha kuwa too analytical na vile naona watu wanavyoweza hata kuchukiana kiwango cha hatari kwa sababu ya mambo ya chadema na siasa zao zisizo za kisayansi na kuendeshwa king'ombe ng'ombe sometimes ni ngumu kupotezea na kuandika mawazo yangu. Na mawazo yangu ni kwamba Chadema mnahitaji radical reforms.
 
Siasa ni kuzidiana uhuni. Kama unadhani kunaustaarabu kwenye siasa basi huijui.
 
Acheni maneno yasiyo na ukweli[emoji116]
View attachment 2223608
Hawafukuziki wapi? Kama ni kwenye chama wameshafukuzwa. Huko bungeni ni jukumu la spika na wale waliohusika kuwaweka huko. Wakiamua kukaa nao bungeni hadi mwisho, yaani 2025, huo ni uamuzi wao. Kuwalipa pesa za mishahara na posho zingine pamoja na mafao ya mwisho, wabunge 19 si kitu sana, kodi zetu zipo, wacha waendelee kuwepo bungeni.
 
Kuna ugumu kwa muhimili kulitolea uamuzi swala hili. Kuwatoa bungeni ni kuiabisha Tume ya Uchaguzi kuwa ni kweli ilipeleka majina ambayo hayakuwasilishwa na Chadema. Hili si jambo dogo kwa chombo kilichoundwa kusimamia sheria za Uchaguzi. Tume haitakubali ionekana imekosa sifa za kufanya majukumu yake. Maadamu Chadema hawataki kutipoti jinai dhidi ya kashfa hii huenda Bunge/Tume imewashauri Akina Mdee waende mahakamani kutetea mchakato wa kupatikana kwao.
 
Samia awe makini sana hasa wakati huu anaposisitiza maridhiano, kitendo cha kuendelea kuwaweka bungeni hao wanawake itatafsiriwa ni dharau, muhimu awe na heshima kwa mwenzake kama naye anavyotaka kuheshimiwa.
Samia hana mamlaka ya kuwatoa watu bungeni, hilo ni jukumu la Spika.
 
Ukweli huu wote uliouandika kila mtu anaujua, na Paskali anaujua vyema, lakini ukweli huu si lolote si chochote kwake maana Cdm hawawezi kumpa cheo. Yeye hasimamii ukweli, anaangalia anayeweza kumpa madaraka. Hapo ndio Paskali Mayalla alipofikia!

Hizi post zake zote ni kujaribu kubaki relevant kwa post zake za huko nyuma za kuwasifia hao COVID-19, na akiangalia uamuzi uliochukuliwa umemkwaza sana kwani huenda anadhani anafahamu sana mambo ya ndani ya vyama. Hivyo uamuzi huu hauendani na uzushi wake wa huko nyuma. Kinachomfanya kwa sasa aanzishe uzi kila baada ya muda mfupi kuhusu maamuzi ya Cdm, ni vile watu wanamkejeli na kumdharau, hali hii inamuacha na msongo wa mawazo, hivyo anaanzisha uzi ili kutaka kuhalalisha uzushi wake.
AMEN
 
Kama bado wapo bungeni ni kashfa na aibu kwa Serikali ndani na nje ya nchi, kwa CHADEMA ni credit na turufu kisiasa ya kuonyesha ubovu wa Serikali kutozingatia sheria.
 
Ndugu Pascal Mayalla

Hivi ilikuwaje kwa yule dada Nusrat Hanje, aliyekuwa gerezani Singida, akatolewa saa tatu usiku na kusafirishwa usiku kwa usiku kuelekea Dodoma kuapishwa na kuwa mbunge!?

Hapa CHADEMA walifanyaje mkuu Pascal Mayalla
 
Huu ni mwaka wa pili katiba inavunjwa na hakuna kilichotokea.
Mamlaka zimeanza kulea hii tabia,Kuna siku zitawarudi wao,wanadhani wanawakomesha watu wa chache lakini wanatengeneza ubovu na uchochoro kwa watu wengine na hata taasisi zingine pia kuchezea katiba na sheria za nchi bila woga.

Hii mbegu aliyoipanda Ndugai na Mwendazake na wenzao wengine ya kuchezea katiba ya nchi na sheria zake bado inaota Kuna siku isiyo na jina itatugharimu sana,unamwingizaje bungeni mtu ambaye amepoteza uhalali wa kuwa mbunge!Hata theater haiingii mtu ambaye siyo daktari husika, hata news room haingii kila mtu,msikitini haingii asiye muislam, hata sisi wazee wa kwichi kwich hatuingizagi kila mtu bedroom wengine tunawapeleka gest na wengine tunamalizana nao hata kwenye magari huwezi ingiza kila mtu, sehemu nyeti kama hana vigezo vilivyowekwa.

Kesho wataingia watu ikulu wasio na uhalali wa kuwa ikulu kumbe sababu tu kwa ujinga wenye mamlaka wameanza kuharibu heshima ya katiba na sheria walizo kula kiapo kuzilinda na kuzitetea.

Kwa crises iliyokuwepo wakati Mwendazake ametangazwa kuondoka Kama Mabeyo na timu yake,wasinge kuwa na utiisho wa kutii katiba,sheria na itifaki za ki nchi na viapo vyao na kufanya maigizo na michezo Kama alivyofanya Ndugai na Sasa Tulia sasahivi tungekuwa na historia nyingine tofauti.
Hawa wehu wanachokifanya Sasa wanaipunguzia katiba ya nchi utiisho wake,historia itawahuku hata kwenye makaburu yao.
 
Kuna msemo unasema ukitenda sawa sawa na kwa haki unaitendea NAFSI yako.
Na vilevile ukitenda uovu hujamtendea mwingine ni umeitendea nafsi yako.

Muda waja yatakuja kutokea makubwa kwa upande wao na hawata kuwa na la kufanya wala hakuna kitakachotokea vilevile.

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
Wakina nani?!
 
Mlisema Magufuli ndiyo anawakingia kifua wasiondolewe,

Kwani bado yupo?
 
Mkuu Nguruvi3, the most important document kwenye utawala wa nchi ni katiba, na the most important document kwenye utawala wa chama cha siasa ni katiba zao. Kwenye utawala wa nchi, rais akivunja katiba, anashitakiwa na Bunge, anaondolewa madarakani. Lile swali langu kwa JPM pale Ikulu, kuwa amepata wapi mamlaka ya kwenda kinyume cha katiba, ni kama kusema JPM amevunja katiba, Bunge lingepaswa kumshitaki. Nilipoandika kuhusu Bunge, nyote mnakijua kilichonitokea, hivyo maadam Chadema ina katiba, there is no excuse why Chadema isifuate katiba yake. Kama kijikatiba hiki tuu kidogo cha Chadema inashindwa kukifuata, jee Chadema Ingekabidhiwa nchi na lile ji Katiba kubwa la JMT, wangeiweza?.

Mimi ni kada wa CCM, ila ni CCM contemporary, kuna ma CCM ambao ni ma burgeoges na kuna ma CCM ambao ni ma lumpenproletariat, sisi ma CCM Contemporary tunapenda haki, tunapenda CCM ishinde kwa haki, tunapenda Bunge letu liwe na opposition, tunawapenda baadhi ya baadhi ya wapinzani makini na tunapenda kuona Tanzania ina opposition makini, hivyo kuna wana CCM, mimi nikiwemo, hatufurahii kuona Bunge la Chama kimoja na mara baada ya uchaguzi, tuliwaombea kwa Mwenyekiti wetu, awateue baadhi ya wapinzani muhimu waingie bungeni Bunge jipya lina hali mbaya! Serikali itafanaje kuliokoa Bunge ili kuwa na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni? na Zitto nikamuombea uteuzi rasmi Ombi Maalum kwa Rais Magufuli: Mteue Zitto Kabwe kuwa Mbunge wa Bunge la JMT, ndiye mpinzani pekee mzalendo, Capable kuongoza PAC! hivi ninapoona Chadema inapoteza assets kama Halima Mdee na Esta Bulaya, kwa sababu za kijinga jinga, tunaumia!.

Kama kuna forgery yoyote, ili Chadema waweze kuipata nakala halisi ya barua ya uteuzi kutoka Chadema kwenda NEC iliandikwa na nani, ilisainiwa na nani, Chadema walipaswa kuripoti polisi ili uchunguzi wa kijinai ufanyike, Chadema haikufanya hivyo kwasababu inaujua ukweli kuwa hakuna forgery yoyote!. Voices from within, inanieleza yule "kigogo" baada ya Chadema kama Chama kususia kuteua wajumbe wa viti maalum, Halima Mdee akiwa ameandamana na Esta Bulaya, wali seek an audience na kigogo wa Chadema na ku consult umuhimu wa nafasi hizo, kigogo huyo akatoa a go ahead, ndipo Halima aka proceed kuwatafuta na kuwa organize. Kigogo akasaini na process ikaendelea. Mambo yalipochemka, kigogo akawaomba kina Halima wajitoe to save his face, wakamgomea. Kiukweli Halima ni Mwanamke wa shoka, shujaa aliyefundwa akafundika, na ana command a very high respect kwa hao wote 19 kwa kuwasihi wasifungue midomo yao kusema chochote kwenye Baraza Kuu, and take it from me, Halima ali consult na Kigogo, kigogo akamshauri wao wanyamaze na wasijibu kitu, yeye atawaombea msamaha, watasamehewa na kuendelea na ubunge wao, hivyo wakakubali, wakanyamaza na kutotoa siri ya kigogo wa Chadema, hivyo baada ya matokeo kutoka wamepigwa chini ndipo Mdee akajikuta wamefanyiwa uhuni!.

P
Ester Bulaya si asset bali ni pandikizi, hii fracas imesababisha aangaliwe kwa jicho la tatu hivyo kumtumia kama reference kunanifanya nihisi una agenda maalum kwenye mlolongo wa posts zako.

Uwepo wa Ester Bulaya ndiyo umem-mcopromise Halima Mdee, watu wenye nia njema na chama chao hawawezi kung'ang'ania kwenda kinyume na majority kwenye chama chao regardless taratibu za katiba zikoje. Mshikamano wa chama ni primary goal, sasa hawa wanaosababisha mpasuko wanafanya hivyo kwa faida ya chama gani?

Katika watu ambao walikuwa wakidai mtu wa opposition anaposhabikiwa na kuwa supported na chama tawala basi huyo si mpinzani wa kweli sasa leo hii unadhani hilo limemtoka kichwani? Malengo yao yako dhahiri na si bahati mbaya kwa CCM kuwakingia kifua lakini hata wakiendelea kuwa bungeni haisaidii kuwarudisha CDM na kamwe hawatarudi hivyo acha waendelee kuvuna pesa za bure kwa uwepo wao ambazo ni kodi za Watanzania.
Sasa Halima Mdee(this is according to your posts) atakuwa akishiriki vikao vya CDM kwa cheo chake ndani ya chama.
 
Ni Wakati rasmi kufungua kesi kuomba ufafanuzi wa hili atajulikana aliyekaa Nyuma yao
 
Back
Top Bottom