Halima Mdee: Walichofanya wajumbe wa Baraza Kuu CHADEMA ni Uhuni! Mimi ni CHADEMA, nitaendelea kuwa CHADEMA

Halima Mdee: Walichofanya wajumbe wa Baraza Kuu CHADEMA ni Uhuni! Mimi ni CHADEMA, nitaendelea kuwa CHADEMA

Kina Halima watafanya delaying techniques, wataenda Mahakamani.

So bado wana nafasi za kula hela ya nchi kidogo.

Unless otherwise iwe ni makubaliano kati ya Mbowe na Samia kua watimue na bungeni tuwatimue mlete wengine.
Points sana umeongea, yaan wewe no kichwaa 'na km Samia akiamua kuweka kifua hata hiyo kesi itapigwa danadana mpya 2025, yaan mwenye maamuzi hapo Samia 'na wala sio Mbowe 'na kamati kuu
 
Ndiyo maana Mahakama zipo kwa ajili ya kupambana na wahuni.

Mbunge Halima Mdee ameendelea kusisitiza yeye na wenzake 18 bado ni wanachama halali wa Chadema.

Kilichotokea kwenye kikao cha Baraza Kuu ni Uhuni.

Wabunge hao wana Haki ya Kikatiba kupinga Uhuni Mahakamani.
 
oday2.png
 
Kina Halima watafanya delaying techniques, wataenda Mahakamani.

So bado wana nafasi za kula hela ya nchi kidogo.

Unless otherwise iwe ni makubaliano kati ya Mbowe na Samia kua watimue na bungeni tuwatimue mlete wengine.
Katiba ua CHADEMA inazuia mtu kwenda mahakamani kwa masuala yanayohusiana na chama, labda kama masuala hayo ni ya jinai.

Hapo kwa suala la uwanachama wao, ndipo lilipoishia.
 
Mkuu, unatakiwa kujua kua mahakama ndie muamuzi wa mwisho kwenye jambo lolote nchi hii.

Kwa hiyo wana haki ya kwenda mahakamani wakitaka. Kumbuka ishu ya Zitto.

Nachokisema, inawezekana mahakama ikakubaliana na uamuzi wa chadema 100% na hilo halina ubishi.

Ila kwa kitendo cha kwenda mahakamani, wanafanya mchezo wa kuchelewesha ama delaying techniques. Kwa hiyo hata Bunge haliwezi kuwafukuza maana bado ni wanachama hadi mahakama itoe majibu, tayari huo muda unakua umeenda na kama ni vikao vya bunge 2 ama 3 wnaakua wamekula hela zetu.

Tusubiri tuangalie.
Ndugu yangu, kumbe hata basics za sheria huzijui kiasi hiki?

Ukishapatikana una hatia na chombo chochote kwa mujibu wa kanuni, katiba yenu au sheria, unaendelea kuwa na hatia (hata kama umekata rufaa), mpaka siku ile mahakama au chombo cha juu kinapotengua.

Hayo mawazo yako yangekuwa yapo hivyo, gerezani kusingekuwa na wafungwa, maana ingekuwa baada ya kuhukumiwa na mahakama, unakata rufaa, unakuwa huru, kusubiria hukumu ya rufaa!!

Ukishapatikana na hatia na mahaka ya mwanzo, ukahukumiwa kifungo, siku ile ile unafungwa, hata kama utasema unakata rufaa. Hata wakati rufaa yako inaendelea kysikilizwa na mahakama ya juu, wewe utaendelea kuwa mfungwa, mpaka siku ile mahakama ya juu itakapotengua ule uamuzi wa mahaka ya chini.

Mdee na wenzake wataendelea kuwa siyo wanachama, mpaka siku ambayo chombo kingine kitakuwa na uwezo wa kuwarudishia uwanacha wao. Na chombo hicho, hakipo kwa sababu katiba ya CHADEMA inatamka wazi kuwa mamlaka ya mwisho ya maamuzi kuhusiana na masuala ya wanachama na wanachama ni Baraza Kuu, na Mdee analijua hilo.
 
Hawa watu hasa huyu Mdee bado sijajua kwanini walikubali kudanganyika wakasaliti maamuzi ya chama chao, kama kilikuwa kiburi cha uwepo wa mwendazake pole yao.

Kinachomkuta sasa hivi hakuna yeyote mwanye akili atakayemuelewa na utetezi wake, walipewa ruhusa ya kujitetea kwenye KK wakagoma kwenda.

Kile kiburi walichoonesha pale ndio ulikuwa uhuni wenyewe, na ule uhuni ndio umeleta hii hasira kwa wajumbe wa Baraza Kuu "kuwachinjia baharini" kwa kura zakutosha toka kwenye kila kanda.

Kama walikuwa na nafasi ya kuomba msamaha ilikuwa ni wakati ule, pale anagalau wangeweza kusikilizwa, lakini kugoma kwao kwenda kwa kisingizia cha kitoto "usalama wao" 'ile ilikuwa ni dharau kwa wajumbe wa KK.

Hakuna mjumbe kichaa wa KK wa kuwafanyia fujo, wamevuna walichopanda, sasa waende mahakamani kama wakipenda, ingawa naamini wanajua hata huko mahakamani hawatavuna heshima yoyote, simply wameshapotea.
Shetani siku zote ana ushawishi.
Inahitaji imani thabiti kumshinda shetani.

Mwendazake alikuwa ni shetani mwenye vivutio vingi kwa yeyote atakayekubali kumsujudia. Wengi walianguka na kuangamia kwenye dhambi wakati wa uhai wake.

Fikiria waliokubali hata kuwaua, kuteka na kuwabambikia kesi binadamu wenzao ili kumfurahisha na kumridhisha Mwendazake, hapo ndipo utajua nguvu ya shetani.
 
Sasa tunasubiria majina ya hao 19 wa mbadala hapo chadema wasije wakaleta kutafutiana ulaji
Watapelekaje majina wakati walikataa uchaguzi haukuwa huru?
Au tumesahau?
Anyway,ebu tutibu majeraha ya uchaguzi na kazi ziendelee.
 
Ndugu yangu, kumbe hata basics za sheria huzijui kiasi hiki?

Ukishapatikana una hatia na chombo chochote kwa mujibu wa kanuni, katiba yenu au sheria, unaendelea kuwa na hatia (hata kama umekata rufaa), mpaka siku ile mahakama au chombo cha juu kinapotengua.

Hayo mawazo yako yangekuwa yapo hivyo, gerezani kusingekuwa na wafungwa, maana ingekuwa baada ya kuhukumiwa na mahakama, unakata rufaa, unakuwa huru, kusubiria hukumu ya rufaa!!

Ukishapatikana na hatia na mahaka ya mwanzo, ukahukumiwa kifungo, siku ile ile unafungwa, hata kama utasema unakata rufaa. Hata wakati rufaa yako inaendelea kysikilizwa na mahakama ya juu, wewe utaendelea kuwa mfungwa, mpaka siku ile mahakama ya juu itakapotengua ule uamuzi wa mahaka ya chini.

Mdee na wenzake wataendelea kuwa siyo wanachama, mpaka siku ambayo chombo kingine kitakuwa na uwezo wa kuwarudishia uwanacha wao. Na chombo hicho, hakipo kwa sababu katiba ya CHADEMA inatamka wazi kuwa mamlaka ya mwisho ya maamuzi kuhusiana na masuala ya wanachama na wanachama ni Baraza Kuu, na Mdee analijua hilo.
Mkuu, unaweza kunielewesha Zitto aliendeleaje kua mbunge wakati alikua kafukuzwa chadema?
 
Lakini wanaendelea kuwa wabunge hadi kesi iamuliwe ina maana Chadema hawatakuwa na uwezo wa kuteua wabunge wengine
Bora waendelee kukaa Bungeni kwa amri ya mahakama ila chama chao kimemaliza kazi yake kwa mujibu wa katiba.
 
Hapa patamu sana.

Ok, tukisema tumewasamehe CCM kwa zile rafu walizofanya makusudi kwenye uchaguzi mkuu uliopita, rafu ambazo zimesababisha leo hii wakina Mdee wamefukuzwa chamani tukiwaita wasaliti, kwanini basi na wakina Mdee wasisamehewe?

Kwangu, uamuzi wowote utakaosema yaliyopita si ndwele tugange yajayo, basi lazima uende moja kwa moja na kusamehe na kutibu yale majeraha yote yaliyosababishwa na kosa la msingi [rafu za uchaguzi 2020].

Je, utakuwa tayari kuwasamehe kina Mdee ili tuanze wote kwa pamoja? if No, kwanini uwagomee kina Mdee lakini uwasamehe CCM kwa zile rafu zao za makusudi?

Yes, ni CCM coz wakati ule wakitufanyia uhuni, Samia alikuwa mgombea mwenza, kama alikuwa hataki yale maovu angejiondoa kugombea, lakini nae akasikika akisema; "hata kama wasipotupigia kura bado tutangazwa washindi"

Hayo maswali unayoyaogopa kwangu ni suala dogo, nimeona next time wamesema Chadema watakutana na CCM na serikali yake kwa pamoja, hapa lazima CCM wakubali makosa yao na wafanye jambo kuyafuta, sijui kwanini unawatetea wasirudie uchaguzi? why unawahurumia?

Ujinga walioufanya wakati ule una gharama kubwa, na gharama hizo ndio wakati wao kuzilipa, na pesa za uchaguzi sio zao, ni za walipa kodi wa nchi hii.
Mtu husamehewa aliyeomba msamaha. Covi 19 wangeomba msamaha yaishe
 
Ukweli ni kwamba Mbowe na Mnyika wanajua wamewasaliti kina Mdee. Mawasiliano ya simu yapo na sauti. Subirini labda wasiende mahakamani.
Wangeyasema kwa wajumbe kuhusu huo uhuni na kuzitoa hizo sauti za akina Mnyika ushahidi kama sehemu ya rufaa. Wamekosa fursa nzuri ya kutetea hoja za rufaa zao
 
Wapange trip kwenda Chato kuhiji kisha Kongwa kuchunga mbuzi - maisha yanakwenda kwa kasi saana. Wanajua fika mama Samia hawezi kuwavumilia tena.
 
Mwache mzee Halima aendelee na ubishi wake this time atanyolewa vyuuzzz bila maji wala wembe.
 
Sio kweli, huwezi kufungua kesi ya kupinga matokeo ya Urais mahakamani.

Marais hawashitakiwi wakiwa madarakani au nje ya mdaraka.
Mkuu, unatakiwa kujua kua mahakama ndie muamuzi wa mwisho kwenye jambo lolote nchi hii.

Kwa hiyo wana haki ya kwenda mahakamani wakitaka. Kumbuka ishu ya Zitto.

Nachokisema, inawezekana mahakama ikakubaliana na uamuzi wa chadema 100% na hilo halina ubishi.

Ila kwa kitendo cha kwenda mahakamani, wanafanya mchezo wa kuchelewesha ama delaying techniques. Kwa hiyo hata Bunge haliwezi kuwafukuza maana bado ni wanachama hadi mahakama itoe majibu, tayari huo muda unakua umeenda na kama ni vikao vya bunge 2 ama 3 wnaakua wamekula hela zetu.

Tusubiri tuangalie.
 
Dar es Salaam. Aliyekuwa mwanachama wa CHADEMA, Halima Mdee amesema hakukuwa na uhuru kwa wajumbe wa Baraza Kuu la chama hicho katika upigaji wa kura na kwamba, kilichofanyika ndani ya Baraza hilo ni uhuni. Na Mbowe anajua ni Uhuni. Nitaongea siku nyingine kwa Urefu leo sio siku mwafaka. Mimi Halima Mdee ni CHADEMA na nitaendelea kuwa chadema
Matokeo ya jumla

Idadi ya wajumbe 423

Waliokubalina na maamuzi ya Kamati ya kuwafukuza Uanachama ni 413 sawa 97.6%

Wasiokubaliana na uamuzi wa Kamati kuu ni 5 sawa na 1.2%

Wasiofungamana na upande wowote ni 5 sawa na 1.2%

Pia, soma;


====

UPDATES ;

=====
View attachment 2221245
Habari zaidi kutoka Gazetini;

Dar es Salaam. Aliyekuwa mwanachama wa Chadema, Halima Mdee amesema hakukuwa na uhuru kwa wajumbe wa Baraza Kuu la chama hicho katika upigaji wa kura na kwamba, kilichofanyika ni uhuni.

Mdee ambaye amepata kuwa mbunge wa Jimbo la Kawe na Katibu wa Baraza la Wanawake wa Chadema, Bawacha, ni miongoni mwa makada walifukuzwa baada ya Bazara Kuu kubariki uamuzi wa Kamati Kuu ya Chadema kuwafukuza ndani ya chama kwa kukubali kwenda kuapishwa na kuwa wabunge kinyume cha matakwa ya chama hicho.

Matokeo ya jumla

Idadi ya wajumbe 423

Waliokubalina na maamuzi ya Kamati ya kuwafukuza Uanachama ni 413 sawa 97.6%

Wasiokubaliana na uamuzi wa Kamati kuu ni 5 sawa na 1.2%

Wasiofungamana na upande wowote ni 5 sawa na 1.2%

Chanzo: Mwananchi
HALIMA HALIMA...UMESHAWAPONZA WENZIO WAMEFUKUZWA CHAMA KWA TAMAA ZAKO HALIMA
 
Back
Top Bottom