Halima Mdee: Walichofanya wajumbe wa Baraza Kuu CHADEMA ni Uhuni! Mimi ni CHADEMA, nitaendelea kuwa CHADEMA

Halima Mdee: Walichofanya wajumbe wa Baraza Kuu CHADEMA ni Uhuni! Mimi ni CHADEMA, nitaendelea kuwa CHADEMA

Points sana umeongea, yaan wewe no kichwaa 'na km Samia akiamua kuweka kifua hata hiyo kesi itapigwa danadana mpya 2025, yaan mwenye maamuzi hapo Samia 'na wala sio Mbowe 'na kamati kuu
Samia hawezi kuendekeza upuuzi wa akina Halima Mdee yuko bussy kuirudisha nchi kwenye msitari.Huo ulikuwa ni mojawapo ya uchafu.
 
Waliposimamishwa na kamati kuu walikuja mbio mbio kusema kuwa kamati kuu iliwasimamisha bila kuwasiliza (wakati waliitwa kujieleza lakini wakapotea mitini), hivyo wakasema wanakata rufaa baraza kuu, walipoenda baraza kuu wakapewa nafasi kujieleza wakaishia kukaa kimya.

Wakina mdee ni wapuuzi sana.
 
Hoja hizi zinajadilika sana, kwa bahati mbaya muda wa kutuliza akili juu yake ni shida sana.

Akina Halima ni swala ndani ya chama moja kwa moja. "Uchafuzi" uliofanyika 2020 ni zaidi ya CHADEMA, ni swala la nchi nzima. Mhusika mkuu wa 'uchafuzi' kwa kudra za Mwenyezi hayupo tena. Hawa wasaidizi wake, wengine tayari wanamkana waziwazi.

Kuwaondoa akina Halima kwa ushiriki wao katika kukihujumu chama chao ni swala ambalo limo ndani ya uwezo wa chama chenyewe, bila ya kuhusisha watu wengine nje ya chama. Ni haki ya chama kufanya maamuzi wanayoona yanafaa, kama ilivyo haki ya chama hicho kuamua kutoitambua serikali iliyotokana na 'uchafuzi' au kuamua kushirikiana na serkali hiyo kutafuta suluhu ya maswala ambayo ni muhimu kwa taifa ili ule uchafuzi usijirudie tena.

Mbowe, kama kiongozi wa chama, anao wajibu wa kueleza na kushawishi viongozi wenzake na chama kwa ujumla kufanya maamuzi wanayoona yanafaa kwa kwenda mbele, na kutoshikilia yote yaliyopita.
Huu utakuwa ni uamzi utakaofanyika ndani ya chama hicho.
Nitakujibu kwa kila paragraph uliyoandika.

- Sawa, wakina Halima ni suala la ndani ya chama, na chama chao kimeshawashughulikia na kimemelizana nao. Uchaguzi wa 2020 ulioharibiwa ulikuwa ni wa kitaifa, sawa, lakini hata kama ulikuwa wa kitaifa, mbona kina Mdee wameadhibiwa kwa athari za uchaguzi huo?

Hata kama muhusika alifariki, hawa waliopo wanatakiwa kufuta makosa ya yule muhusika kwasababu alitoka ndani ya chama chao, na wengine wao walikuwa ndani ya serikali yake. Kutafuta suluhu lazima kuendane moja kwa moja na kufukia mashimo yaliyosababishwa na ule uchafuzu, ikiwemo kurudia uchaguzi mkuu.

- Hoja yako ya pili;

Kwanini basi, chama hicho kikae na yule aliyewasababishia matatizo ndani ya chama chao mpaka wakafukuzana, ili kutafuta maridhiano, lakini walishindwa kutafuta maridhiano na wale wanachama wake waliowafukuza?

Hapa unaonesha upendeleo, unaipenda sana serikali ya CCM iliyotuharibia uchaguzi, huku ukiwaona kina Halima walioadhibiwa kwa matokeo ya kuharibiwa uchaguzi ule ndio wenye makosa na kuadhibiwa na chama chao, coz ni suala lililopo ndani ya uwezo wa chama chao, unakosea.

Nakuona kuna jambo unalikwepa, hutaki hawa jamaa warudie uchaguzi, bila kurudia uchaguzi ni kutwanga maji kwenye kinu. CCM wataendeleza mazoea yao ya rafu za uchaguzi kila mwaka, labda wapunguze "scale" ya rafu hizo. Nataka tutafute solution ya hili tatizo moja kwa moja, ili wakae wakijuwa, wakiharibu tena uchaguzi, utarudiwa [fundisho].

- Hoja yako ya tatu;

Mbowe kama kiongozi wa chama aliyesimamia kufukuzwa kina Mdee, leo Mbowe huyo huyo arudi tena kukishawishi chama chake walegeze misimamo yao kuhusu matokeo ya ule "uchafuzi" wa 2020 nitamshangaa sana kwa ukigeugeu wake.

Jambo lolote linalohusu maamuzi ndani ya chama huamuliwa na vikao halali vya chama, Mbowe kama atapeleka hiyo agenda huko vikaoni asubiri jambo hilo lipigiwe kura.

Kama wengi watakubaliana na hoja yake, then wakumbuke athari zilizosababishwa na jambo hilo walilopigia kura, ikiwemo kuwafukuza wenzao chamani, wasiwe wabinafsi wa kuibembeleza serikali ya CCM.

NB.

Kati ya yote uliyoandika, nakuona unaikwepa sana hoja muhimu ya kurudiwa uchaguzi, kurudiwa uchaguzi ndio suluhisho la haya matatizo yote.

- Haki za walioporwa ushindi wao majimboni zitapatikana.

- Viti maalum watapelekwa wanaostahili.

Zaidi, pesa za kurudia uchaguzi sio za CCM na serikali yake, ni mali ya walipa kodi wa nchi hii, usiwahurumie hawa, waache wavune walichopanda.
 
Katiba ua CHADEMA inazuia mtu kwenda mahakamani kwa masuala yanayohusiana na chama, labda kama masuala hayo ni ya jinai.

Hapo kwa suala la uwanachama wao, ndipo lilipoishia.
Kwa hiyo chadema imekuwa FIFA!?
Kwenda mahakamani ni haki ya msingi. Haiwezi kupotea kwa matakwa ya katiba ya chadema. Lau ingekuwa ni katiba ya nchi ingekuwa sawa.

Sent from my SM-G5500 using JamiiForums mobile app
 
Dar es Salaam. Aliyekuwa mwanachama wa CHADEMA, Halima Mdee amesema hakukuwa na uhuru kwa wajumbe wa Baraza Kuu la chama hicho katika upigaji wa kura na kwamba, kilichofanyika ndani ya Baraza hilo ni uhuni. Na Mbowe anajua ni Uhuni. Nitaongea siku nyingine kwa Urefu leo sio siku mwafaka. Mimi Halima Mdee ni CHADEMA na nitaendelea kuwa chadema
Matokeo ya jumla

Idadi ya wajumbe 423

Waliokubalina na maamuzi ya Kamati ya kuwafukuza Uanachama ni 413 sawa 97.6%

Wasiokubaliana na uamuzi wa Kamati kuu ni 5 sawa na 1.2%

Wasiofungamana na upande wowote ni 5 sawa na 1.2%

Pia, soma;


====

UPDATES ;

=====
View attachment 2221245
Habari zaidi kutoka Gazetini;

Dar es Salaam. Aliyekuwa mwanachama wa Chadema, Halima Mdee amesema hakukuwa na uhuru kwa wajumbe wa Baraza Kuu la chama hicho katika upigaji wa kura na kwamba, kilichofanyika ni uhuni.

Mdee ambaye amepata kuwa mbunge wa Jimbo la Kawe na Katibu wa Baraza la Wanawake wa Chadema, Bawacha, ni miongoni mwa makada walifukuzwa baada ya Bazara Kuu kubariki uamuzi wa Kamati Kuu ya Chadema kuwafukuza ndani ya chama kwa kukubali kwenda kuapishwa na kuwa wabunge kinyume cha matakwa ya chama hicho.

Matokeo ya jumla

Idadi ya wajumbe 423

Waliokubalina na maamuzi ya Kamati ya kuwafukuza Uanachama ni 413 sawa 97.6%

Wasiokubaliana na uamuzi wa Kamati kuu ni 5 sawa na 1.2%

Wasiofungamana na upande wowote ni 5 sawa na 1.2%

Chanzo: Mwananchi
hayo ni maneno tu ya mfa maji nakumbuka hata zitto kabwe alisema mi nitakuwa wa mwisho kutoka CHADEMA lakini cha ajabu yeye ndo akawa wa kwanza kutoka.

kuna point ikifika huwa mtu anakuwa anaongea asichokifikiria. hakuna apendae chama kuliko maisha yake. lakini kuna wakati ili kuonyesha unapenda maisha yako basi penda zaidi kile kinachoyapendezesha maisha yako.
YESU atakayeipenda nafsi yake ataiangamiza bali yule atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu ataikombo.

Halima mdee na wenzake wakati kelele zinapigwa na kila mwanachama na mpenda maendeleo wao walipenda zaidi nafsi zao hata hawakuwahi kustuka kuwa jamani mbona tumekengeuka(nimemkumbuka komando urio) wakaona raha kula ela za kinafki huku wakijua mwisho utakuwa mtamu. Sasa sijajua ni akili za wanawake samahani hapo nimejiuliza tu au ni akili za pesa au ni akili za kushkiwa na marehemu mpaka halima kweli asitambue kama amekosea.

Haya mwana kulitafuta mwana kuliget. Sasa watulie baadae waombe radhi watasamehewa kwakuwa ni wanawake. Maana inawezekana walifata msemo wao kuwa wakiwezeshwa wanaweza hvyo marehemu akawawezesha wakaona dezo kuingia bungeni.
 
Toka alipozaliwa.
Na mademu zake hao(japo ni rumors tu) huwa vipi, mbona hawi na mwanaume? Panapofuka moshi huwa tunaamini kuwa chini kuna moto, nitaendelea kuamini kuwa ni ME until proved wrong.
 
Mkuu, unatakiwa kujua kua mahakama ndie muamuzi wa mwisho kwenye jambo lolote nchi hii.

Kwa hiyo wana haki ya kwenda mahakamani wakitaka. Kumbuka ishu ya Zitto.

Nachokisema, inawezekana mahakama ikakubaliana na uamuzi wa chadema 100% na hilo halina ubishi.

Ila kwa kitendo cha kwenda mahakamani, wanafanya mchezo wa kuchelewesha ama delaying techniques. Kwa hiyo hata Bunge haliwezi kuwafukuza maana bado ni wanachama hadi mahakama itoe majibu, tayari huo muda unakua umeenda na kama ni vikao vya bunge 2 ama 3 wnaakua wamekula hela zetu.

Tusubiri tuangalie.
Na Chadema wakichemka wakaandika wao barua kwenda bungeni kuwa wamewafukuza,watafanya kosa kubwa la kiufundi. Na spika hatawafukuza kwani yeye majina ya wabunge huletewa na tume ya uchaguzi. Si vyama.

Sent from my SM-G5500 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom