Halmashauri nyingine ziige hili la jiji la Mbeya kujenga English medium za Serikali

Halmashauri nyingine ziige hili la jiji la Mbeya kujenga English medium za Serikali

Wala hilo halijaanzia huko Mbeya ,Tunduma zipo tena 2 alafu hapo Mbeya kuna shule iko jirani na stand Kuu ilijengwa na Serikali miaka mingi na pia ziko pia mikoa mingine.

Kama unafuatilia utasikia wazuri huwa anazizungumzia hizo shule,pia zingine zilijengwa kama shule za mifano wakati wa Kikwete chini ya ufadhili wa Umoja wa Umoja wa Mataifa kama pilot project ya malengo ya Millenia.

Sema hivi ,kumeanza kuzuka huo mtindo kwa Halmashauri kujenga shule za mchepuo wa Kiingereza kwa kutumia pesa za walipakodi afu kwenye udahili zinageuzwa za biashara na chanzo cha mapato kwa Halmashauri husika.

Hii tabia haiwatendei haki walipakodi wote na inakuwa leta conflicts of interests na sekta binafsi.Kazi ya serikali ni kutoa huduma sio kufanya biashara.

Athari yake ni kwamba watoto wa maofisa na watu wenye uwezo ndio watasomesha watoto wao hapo huku Halmashauri husika ikitumia mapato waliyokusanya kutoka kwa wananchi kuhudumia vizuri hizo shule na kutelekeza shule zingine,zitafanywa bora liende.Hii sio sawa Kabisa na Serikali ipige marufuku.

Mwisho walimu wa hizo shule watakuwa wale wazuri na wako paid vizuri afu vilaza wanaletwa shule za kayumba ambako pia watoto wamerundikana madarasani hadi kukaa chini.
Umetumia kigezo gani kuwaita vilaza hao walimu
 
Haina maana kulazimisha jambo. Tutumie kiswahili na English kwapamoja. English au lugha yoyote kuijua inataka ufatuliaji binafsi.

Mimi leo nipo 100% kwenye English na sijawahi soma English medium schools..... Na kuna rafiki zangu wengi tu wamesoma English medium schools ila wana ongea English broken kabisa ingawa wakisoma na kusikiliza wanaelewa.

Uchawi wa English au lugha yoyote ni kujitengea muda kila siku na kujifunza maneno mapya ambayo yanatumika sana kimaongezi.

Pia kuwa na watu ambao hautakuwa uncomfortable kuongea nao English ili kuwa familiar na pronunciation ya maneno hayo lakini pia kuwa fluent unapozungumza na mtu anaetaka kuwasiliiana na wewe kupitia kugha husika.

Tazama sana movies za Hollywood au za uingereza maana wao ndio wana lugha utelezi. Ingawa English ya lafudhi (accent) ya Marekani imekaa poa sana na ipo very smooth kutumia.

Sasa hawa watoto wa siku hizi waogaaaaaaa kujifunza lugha, wanatazama haya maCD ya kutafsiriwa na wakalimani wa uswazi wasiojua wanachosema makelele mtindo m'moja.

Hawapendi kusoma vitabu na kujifunza maneno mapya, hawasikilizi nyimbo kujifunza matamshi.

Nina ndugu yangu tunazama movie ya kimarekani, yaani anapata shida kuielewa maana wanachoongea ni ile English ya utelezi yaani laini ambayo inatumika na wamarekani kwenye jamii yao au kama vile viongozi wao wakiwa wanaongea kwenye taarifa za habari kama CNN, yy anapata shida kuelewa akisikilizia neno hadi apate tafasiri tayari movie imeshamuacha. Mimi huku nikitazama movie hiyo hiyo ni kama natazama bongo movie. Its like wanaongea kiswahili yaani every word wanasema mimi tayari linakuwa translated automatically bila kutumia nguvu yoyote.


So madogo na serikali muache visingizio sijui shule zifundishe lugha moja, that's crap. Mtu kujua lugha ni matokeo ya juhudi binafsi.
 
Pia tusisahau mbeya ndio sehemu ya pili yenye vyuo vingi zaidi Tanzania

MUST
MCHAS (tawi la udsm)
UCC (tawi la udsm)
MZUMBE
TIA
SAUT
ADEM
CBE
TUMAINI
TEKU

Hivi vingine vya ufundi na afya kwa ngazi za chini vipo kama utitiri.
 
Pia tusisahau mbeya ndio sehemu ya pili yenye vyuo vingi zaidi Tanzania

MUST
MCHAS (tawi la udsm)
UCC (tawi la udsm)
MZUMBE
TIA
SAUT
ADEM
CBE
TUMAINI
TEKU

Hivi vingine vya ufundi na afya kwa ngazi za chini vipo kama utitiri.
UDSM wamefanya jambo kubwa sana kuanzisha chuo cha Afya.
 
Pia tusisahau mbeya ndio sehemu ya pili yenye vyuo vingi zaidi Tanzania

MUST
MCHAS (tawi la udsm)
UCC (tawi la udsm)
MZUMBE
TIA
SAUT
ADEM
CBE
TUMAINI
TEKU

Hivi vingine vya ufundi na afya kwa ngazi za chini vipo kama utitiri.
Mbeya hakuna UCC ilishadanja
 
Back
Top Bottom