Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Kumbe Hamisi Kigwangalla aliwahi kuandika barua za kujiuzulu Uwaziri mara mbili akiwa Wizara ya Maliasili, akidai sababu ni vitu vya kipuuzi na masuala ya umbeya. Barua ya kwanza ilichanwa mbele yake, na ya pili hajui iliishia wapi, lakini hakuondolewa baada ya vikao kadhaa.
"Mimi nimewahi kuandika barua za kujiuzulu mara mbili, sababu ni vitu vya kipuuzi. Ya kwanza ilichanwa mbele yangu na kuambiwa, 'nenda kafanye kazi.' Sababu kubwa mara zote mbili ilikuwa uwongo. Bila kulindana, mnajikuta mnamalizana. Wazee wa zamani walikuwa wanalindana. Kwenye serikali, siasa na uongozi, watu wanaumizana sana, wanapigana shoti sana. Mpaka ikutokee ndio utajua. Mimi tangu ianze kunitokea, nimepunguza sana ku-judge watu".
"Mimi nimewahi kuandika barua za kujiuzulu mara mbili, sababu ni vitu vya kipuuzi. Ya kwanza ilichanwa mbele yangu na kuambiwa, 'nenda kafanye kazi.' Sababu kubwa mara zote mbili ilikuwa uwongo. Bila kulindana, mnajikuta mnamalizana. Wazee wa zamani walikuwa wanalindana. Kwenye serikali, siasa na uongozi, watu wanaumizana sana, wanapigana shoti sana. Mpaka ikutokee ndio utajua. Mimi tangu ianze kunitokea, nimepunguza sana ku-judge watu".