Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

CtOKRwRzrB5mBzQ5Cb9hS_jD8pN0sOFV1B9UckVYU8i70_Q_XEgdcQvlLqtXwNIGW3VWYaLF4a3otlgbC7K9Em0h3Ei39ed7tspSVQ5gtgrZL5rX2su_TqGlyreZorkWRdRYWBJm9Hn-QodC4i5vw06b46UkgySmTNjczP8cj6bmXb4RA6T3qSC_BRU6IEc8Uk75bpciUYbt_YdFaT-dh7hXKdN7cAdD9DHdB4xKJnFGYL4kk1Re5KOjQb6dQbt6-W2QvuYpX7q_3wE2ayyasqEFYWkowgSSkAVFoSq7jL6StW7uicmeAbddSAD_lW0f1GKpvu4xqI9a4PI-bYpm_24kxvl6H8PB1jGH53J9kAbmKXXFPW9YH4qAATIs8DSUScqrg8cJFiy35i4w8jl_JY9uTugl2Aw44difR64FY7bDSEaxEnvJoAwt7M-fxGIG15Umq6XOPqn2rzgSW-lp0fZFNQw9Psx1PGIaIrPRkMAm9PszJcCMiwBkZ9tPSxmQbYeMWxj0yL1lzzPXdNCcTFcoGpAmatJ1uOku2ZCcVz5Si6WIiO58WJjxk8cC3pX-kibj3Y1fBK5co9QGLfLHjSh0zHTOmAOH=w579-h657-no

Chief Michael Lukumbuzya wa Ukerewe​

Nilikuwa naitafuta picha ya hayati Chief Michael Lukumbuzya kwa miaka mingi bila mafanikio. Sababu ya kuitafuta picha ya Chief Lukumbuzya ni kisa alichonihadithia Bi. Mwamvua biti Masha mke wa marehemu Abdulwahid Sykes maarufu akijuikana kwa jina la mwanae wa kwanza Daisy hivyo tukimuita Mama Daisy.

Nilikuwa kila nikipata fursa ya kuwa na mama yangu Bi. Mwamvua, yaani Mama Daisy nikipenda kumdodosa mambo yalivyokuwa wakati wa ukoloni walipokuwa wanapambana na Muingereza, kwanza kichinichini katika miaka ya mwanzo ya 1950 wakati wa TAA kisha wakipambana na mkoloni dhahiri baada ya kuunda TANU mwaka wa 1954.

Bi. Mwamvua
alikuwa wakati mwingine bila kutegemea akiniangushia habari muhimu kupita kiasi. Mfano siku aliponiambia kuwa nafasi ya president wa TANU nafasi ile ilikuwa ya Chief Kidaha Makwaia lakini alikataa ndipo bahati ikamuangukia Julius Nyerere.

IMG-20160406-WA0111%2B%25281%2529.jpg

Chief David Kidaha Makwaia​

Iko siku akanieleza taharuki iliyotokea nyumbani kwa Abdul Sykes baada ya Nyerere kula chakuka kilichomfanya tumbo limkate na ikadhaniwa kuwa amelishwa sumu.

Mkasa huu ulitokea wakati mama yake Nyerere, Bi. Mugaya Nyangombe yuko na Mama Maria Nyerere vilevile wamekaa uani na akina mama wengine na Abdul Sykes, Nyerere na viongozi wengine wako nyumba kubwa wanapanga mipango ya kupeleka harakati mbele.

Mama yake Nyerere alianza kulia akiamini kabisa kuwa mwanae katiliwa sumu katika chakula. Mama Daisy alikuwa na habari nyingi sana za nyakati zile. Historia ya TANU kama zilivyo nyaraka na picha zake nyingi zimo mikononi mwa watu.

Mfano mwingine ni wa mkutano wa kwanza wa Wanawake wa TANU uliokuwa ukifanyika Arnautoglo Hall na yeye alikuwa yuko nyumbani anafanya shughuli zake. Anasema, ‘’Aliporudi nyumbani Bwana Abdul kanikuta nimekaa, akaniuliza wewe hukwenda mkutanoni? Wenzako wote wako Arnautoglo…’’ Bi. Mwamvua anasema hapo hapo akachukua baibui lake na kuelekea mkutanoni.

Wasemaji wakuu walikuwa Bi. Titi Mohamed na Bi. Tatu biti Mzee. Huu ndiyo mkutano wa kwanza wa wanawake wa TANU.

toW0HLKw0_eZRKHUURD38LIxZWcW5RXD7goNoYJWFVWEj8kMEyL1bPXqHWB5CmfrXmD1mA=w329-h566-no

Kushoto Mama Daisy na mbele yake ni Bi. Titi Mohamed
na Bi. Zainab mke wa Tewa Said Tewa

Katika mazungumzo kama haya ndipo siku moja akanihadithia habari za Chief Luumbuzya. Anasema walitoka Dar es Salaam yeye mumewe kwenda Nansio, Ukerewe kumtembelea Hamza Mwapachu.

Anasema walipanda meli Mwanza pamoja na Chief Lukumbuzya kuelekea Nansio. Lukumbuzya alikuwa anatokea Makerere Uganda alipokuwa anasoma anarudi nyumbani likizo. Abdul Sykes na Michael Lukumbuzya hawakuwa wanajuana.

Hamza Mwapachu alikuwa amekusanya wananchi na kikundi cha ngoma kuja kumpokea bandarini Nansio President wa TAA Abdulwahid Sykes. Lukumbuzya alishangazwa kukuta sherehe bandarini akifanyiwa mtu ambae yeye hakuwa anamjua na akiuliza anaambiwa ni mgeni kutoka Dar es Salaam.

Lukumbuzya alipigwa na butwaa kuona mapokezi ya watu wake wa Ukerewe wakiwa katika nderemo wakati yeye chief hakuna hata mtu alikuwa anajua kuwa yumo katika meli ile ile. Baadae Hamza Mwapachu alimfahamisha yule mgeni waliokuja kumpokea pale alikuwa nani katika siasa za Tanganyika.

proxy

Hamza Kibwana Mwapachu​

Simulizi kama hizi zilinifikirisha sana katika kutaka kuwajua wazalendo wa wakati ule. Hamza Mwapachu alikuwa anafanya haya ya kukusanya wananchi kumpokea kiongozi wa Waafrika chini ya pua za Waingereza bila kujali nini kitampata licha ya kuwa yeye kupewa uhamisho kupelekwa kisiwani Ukerewe peke yake ilikuwa ni adhabu, kwa hakika ni kifungo khasa cha kumtia kuzuizini asiweze kuenedeleza mipango yake ya kuunda chama cha siasa.

Uhuru ulipopatikana Chief Michael Lukumbuzya alipelekwa nje ambako alikuwa balozi na mwisho akawa balozi Canada ambako huko ndiko umauti ulikomfika.

6La5FUdYcnEadMYf6JSIrrWhkpElkSUYiAFTlRs_Bz4mDSXPmSD4EMzk4gTvEnMGuvf8pxy__jBGacnsvJHLYxP_wyS0OA25OYba8__txYHDI2z5TOfGkl7O_IoMO3NAleFvmru20T-YQF39hdK_UD7K79l2x2k40bDIMbiMoIB_ArerygwQ5oIGK11itARq1AoviA_D4OZrLGJZ-mOTiDWEC0pNQPmQPCS-cXzyWVr9raFuGLLKTwCz1GYMrJwsoBIeqCiy_AoHfwRMiTgHgBNRPHowAkwTnbtPxlJ_q9CTx_Ny6xhgBxkIMIBwc9Y79KJA7DXbYcODNB5X-lEL7SxzUEASzHc9r77_ByOVTHcN0j-HCDs2tr7oGw85M3YPXBv0OHG_2pnc_yZefK7n9_UyaxLXX1pmIeP1p01hc6LGf1QcrRusRSirpgfDZrxPMGTwr3EcKUjvY8vh1Kj2_zL9VnkUc-uHdQCSgUi6JBUaZrDi_2LVFAy1ImbD9BwIspcf8aHvXSBLQFSWfC2m3EGmjIMKOU2CDUXZv8NTjsn7UCfaBiWfrRT4ab3OSNhVpvB2GqLU1Rgk5_YjnfJgAxeKukdqeFoc=w476-h657-no

Abdulwahid Sykes​
samahani swali langu liko nje ya mada kidogo. nauliza je, ni wewe mzee mohamed said ndiye uliyetunga kitabu cha NYOTA YA REHEMA?
 
Onxy,
Swali lako limekwenda mbali na mbele zaidi kuwa kwa nini
Abdul hakupewa cheo kikubwa serikalini.

Kuna mambo mengi sana mimi yakikuwa yananitatizo wakati
nafanya utafiti wa kitabu chake.

Jambo la kwanza nnilikuwa najiuliza kwa nini yeye alikuwa na
nafasi nzuri ya kuchukua uongozi wa TAA kuanzia mwaka wa
1951 alipokaimu nafasi ya president wa TAA lakini yeye akawa
anataka nafasi ile aishike Chief David Kidaha Makwaia.

Na ilipofika mwaka wa 1952 alipokutana na Nyerere na mwaka
wa 1953 alitaka kauli ya mwisho ya Hamza Mwapachu kuwa
yeye amuuunge mkono Nyerere achukue nafasi ya president
wa TAA na yeye amsaidie Nyerere kukubalika kwa Waislam wa
Dar es Salaam.

Kote nilipopita sikuona mahali popote ambapo baada ya uchaguzi
wa yeye na Nyerere 17 April 1953 na Nyerere akapita kwa shida
hakuna mahali popote pale Abdul alisimama kutaka nafasi katika
TAA na baadae TANU.

Ukipitia historia ya Abdul unaona kuwa kutoka 1953 hadi kuunda
TANU 1954 akawa yeye kabakia zaidi kama ''party financier,''
akitoa fedha nyingi sana kupeleka TANU na kwa Nyerere kuliko
yeye mwenyewe kuwa ''active,'' katika siasa kama alivyokuwa kati
ya 1947 hadi 1954.

Mwaka wa 1960 Nyerere alipotaka jina la mmoja katika vijana wa
Dar es Salaam kutoka kwa Abdul kuingia katika serikali ya kwanza
Abdul alipendeleza kwa Nyerere jina la Tewa Said Tewa.

Inawezekana labda huku kuwapeleka wengine mbele ndiko khasa
kulikofanya asiwe katika nafasi za uongozi wa serikali baada ya uhuru.

Inawezekana hizi ndizo sababu rafiki kwa ukarimu wake jina la utani,
''The Sweet Abdulwahid Sykes.''
Hapo ndio utaona tofauti ya kiongozi na mtawala mungu amuweke mahala pema peponi yy pamoja wazee wetu wengine mshume kiante mwijuma kambi hamza mwapachu juma mzee jumbe ally kirro mama daisy bibi titi mohamed said tewa nk
60c2a7813b1466ad56d4a5df9f364b26.jpg
6f4abd5c271ee6f556b7a8717cfc076b.jpg
 
Ni muhimu sana kuzihifadhi historia za watu mbali mbali walio na umuhimu katika historia ya Tanzania. Na moja ya hayo ni mchango mkubwa anaoufanya mzee Mohammed Said kwa utafiti mbali mbali ikiwa na pamoja na kukaa na kuzungumza na wazee walio kuepo wakati huo na kurekodi maelezo yao ambayo vinginevyo yatapotea pindi hawa wazee watakapo fariki.

Mambo na matukio mengi muhimu ya kihistoria hayaku haririwa ipasavyo kwa sababu mbali mbali zikiwamo za kisiasa.
 
Mzee Mohamed Said, ingawa umejibu lakini yaonekana zipo sababu nyingine zaidi. Jibu lako bado halijatosheleza kiu ya watu wanafuatilia harakati za uhuru na kwa nini baadhi ya watu hawamo katika "historia rasmi". Napata shida sana kulimeza jibu lako.
Mzee wangu, haiwezekani muungwana kama Abdulwahid Sykes 'akasusa' na 'kukataa'(?) kujumuika na wenzake ili kuendeleza kile walichokiamini na kukipigania huku akichotumia muda, nguvu na raslimali kubwa.
Je kwa nini Julius Nyerere hakupenda kuwatumia kina Sykes katika kukiendeleza kile walichokiamini na kukipigania (Uhuru wa Tanganyika) ila ikawa vyepesi sana kuwatumia kina Mwapachu?

Kwezisho umenishangaza, tatizo naona lipo kwenye story za mitaani ambazo msingi wake sio mzuri sababu hizo unazo taka kuamini hazina proof yoyote. Mwenzio kufanya utafiti na kakujibu swali lililoulizwa wewe hutaki kuamini! sema unachoamini ulekebishwe Mkuu! Kumbuka wazee wetu waliopigania uhuru wengi hawakuwa na uchu wa madaraka. Kiu yao Kubwa ilikuwa ni kumuondoa mkoloni! Hivyo madaraka baada ya uhuru kwao haikuwa ishu sana kama unavyoshangaa Abdul Sykes kutokuwa kwenye safu ya uongozi. Kwake yawezekana haikuwa ishu ilimladi mkoloni kuondoka basi. Tuheshimu tafiti tusipende Kuongea pasipo kutafiti
 
Daaa kwahiyo Nyerere aliibuka Kuwa mwenyekiti wa TANU kama JPM alivyo ibuka kugombea na kuwa Rais wa JMT yaani hawakuwa walengwa ...
Kajembejr,
Mwalimu Nyerere
hakuibuka.

Mwalimu Nyerere tayari katika maisha yake toka udogo alionyesha
uwezo wa akili ambao haukuwa wa kawaida.

Hamza Mwapachu ambae walikuwa wote Tabora School na Makerere
alikuwa anaujua vyema uwezo wa Nyerere na ndiyo sababu alimuomba
Abdul amchukue Nyerere katika TAA kwenye safu ya uongozi hapo HQ
New Street.
 
Mkuu samahani sana, swali lilikuwa hivi:
Kwanini Abdul hakupewa cheo kikubwa serikalini
Nawe wasema hivi:
Kwezisho umenishangaza, tatizo naona lipo kwenye story za mitaani ambazo msingi wake sio mzuri sababu hizo unazo taka kuamini hazina proof yoyote. Mwenzio kufanya utafiti na kakujibu swali lililoulizwa wewe hutaki kuamini! sema unachoamini ulekebishwe Mkuu! Kumbuka wazee wetu waliopigania uhuru wengi hawakuwa na uchu wa madaraka. Kiu yao Kubwa ilikuwa ni kumuondoa mkoloni! Hivyo madaraka baada ya uhuru kwao haikuwa ishu sana kama unavyoshangaa Abdul Sykes kutokuwa kwenye safu ya uongozi. Kwake yawezekana haikuwa ishu ilimladi mkoloni kuondoka basi. Tuheshimu tafiti tusipende Kuongea pasipo kutafiti
Uncle Jei Jei, mie naheshimu sana tafiti za kihistoria nawe pia umeniongezea kitu kwa kusema kiu kubwa ya wazee wetu ilikuwa ni kumuondoa mkoloni. Ila kidogo naomba kutofautiana nawe kwamba, watu waliojumuika na Julius Nyerere baada ya kuikomboa Tanganyika walikuwa na "uchu wa madaraka".
Hili neno uchu wa madaraka linanipa ukakasi na kunikwaza na hata mtafiti wetu Mzee Mohamed Said hapendi kulitumia katika hoja zake. Mzee wetu, Mohamed Said ni gwiji na hazina yetu hilo sote tunaliafiki.
Mimi nilitaka kufahamu kwa nini Abdulwahid Sykes na kizazi chake hawakutaka kujumuika na Julius Nyerere kama ilivyo kwa Mwapachu na familia yake? Je kuna kitu cha ziada au kina Sykes walikuwa na kiu ya kumuondoa mkoloni kisha hawakutaka kulijenga taifa walililolipigania? Yawezekana zipo sababu nyingine za ziada, hebu tujaribu kumdadisi na kumfikirisha Mzee Mohamed Said aendelee na utafiti wake ili aje atujuze.
 
Mzee Mohamed Said, ingawa umejibu lakini yaonekana zipo sababu nyingine zaidi. Jibu lako bado halijatosheleza kiu ya watu wanafuatilia harakati za uhuru na kwa nini baadhi ya watu hawamo katika "historia rasmi". Napata shida sana kulimeza jibu lako.
Mzee wangu, haiwezekani muungwana kama Abdulwahid Sykes 'akasusa' na 'kukataa'(?) kujumuika na wenzake ili kuendeleza kile walichokiamini na kukipigania huku akichotumia muda, nguvu na raslimali kubwa.
Je kwa nini Julius Nyerere hakupenda kuwatumia kina Sykes katika kukiendeleza kile walichokiamini na kukipigania (Uhuru wa Tanganyika) ila ikawa vyepesi sana kuwatumia kina Mwapachu?
Kwezisho,
Unasema yawezekana zipo sababu nyingine zaidi.
Ndiyo inawezekana zikawepo sababu nyingine zaidi.

Mimi nimejitahidi kujibu kadri ya uwezo na ufahamu wangu.

Na ni vizuri katika utafiti wowote ikaachwa nafasi ya mtafiti
mwingine kueleza yale ambayo mtafiti wa mwanzo labda kwa
sababu za kibinadamu zimempita.

Wenye taarifa zaidi ya historia ya kipindi kile wanaweza na wao
wakajazia pale ambapo mimi nimeishia.

Huenda kwa majibu ya wengine ikawa hiyo kiu ikakatika.

Kuhusu shida uinayo kuhusu jibu langu wala hapana haja ya wewe
kupata hiyo shida.

Nichukulie mimi kama mtu wa kawaida mwenye kikomo cha uwezo
na kwa ajili hii ipo nafasi kubwa sana ya kukosea.

Umetumia neno ''kususa'' na ''kukataa.''

Katika utafiti wangu sikukumbana na hali yoyote iliyoonyesha kuwa
Abdul ''alisusa'' au ''kukataa.''

Abdul kama walivyokuwa wenzake wengine katika wale wafadhili
wakubwa wa TANU waliendelea kukisaidia chama hadi uhuru 1961.

Hilo swali la kwa nini Nyerere hakupenda kuwatumia akina Sykes
kama alivyowatumia akina Mwapachu hili swali lako halijakaa vyema.

Halijakaa vyema swali lako kwa sababu sasa hapa unakuja kwa watoto
wa Hamza Mwapachu na watoto wa Abdul na Ally Sykes.

Swali hili lingemstahiki Mwalimu Nyerere mwenyewe kulijibu.
Mimi siwezi kumsemea.
 
Kwezisho,
Unasema yawezekana zipo sababu nyingine zaidi.
Ndiyo inawezekana zikawepo sababu nyingine zaidi.

Mimi nimejitahidi kujibu kadri ya uwezo na ufahamu wangu.

Na ni vizuri katika utafiti wowote ikaachwa nafasi ya mtafiti
mwingine kueleza yale ambayo mtafiti wa mwanzo labda kwa
sababu za kibinadamu zimempita.

Wenye taarifa zaidi ya historia ya kipindi kile wanaweza na wao
wakajazia pale ambapo mimi nimeishia.

Huenda kwa majibu ya wengine ikawa hiyo kiu ikakatika.

Kuhusu shida uinayo kuhusu jibu langu wala hapana haja ya wewe
kupata hiyo shida.

Nichukulie mimi kama mtu wa kawaida mwenye kikomo cha uwezo
na kwa ajili hii ipo nafasi kubwa sana ya kukosea.

Umetumia neno ''kususa'' na ''kukataa.''

Katika utafiti wangu sikukumbana na hali yoyote iliyoonyesha kuwa
Abdul ''alisusa'' au ''kukataa.''

Abdul kama walivyokuwa wenzake wengine katika wale wafadhili
wakubwa wa TANU waliendelea kukisaidia chama hadi uhuru 1961.

Hilo swali la kwa nini Nyerere hakupenda kuwatumia akina Sykes
kama alivyowatumia akina Mwapachu hili swali lako halijakaa vyema.

Halijakaa vyema swali lako kwa sababu sasa hapa unakuja kwa watoto
wa Hamza Mwapachu na watoto wa Abdul na Ally Sykes.

Swali hili lingemstahiki Mwalimu Nyerere mwenyewe kulijibu.
Mimi siwezi kumsemea.
Mzee wangu nashukuru sana kwa jibu lako. Na vyema tukawapa fursa watafiti wengine wakaendelea pale ukomo wetu ulipofikia. Ila kwa ufahamu wangu, unayo mahusiano mazuri sana na hii familia ya Sykes, sio vibaya kuwauliuza labda wanaweza kutufahamisha.
 
Mkuu samahani sana, swali lilikuwa hivi:

Nawe wasema hivi:

Uncle Jei Jei, mie naheshimu sana tafiti za kihistoria nawe pia umeniongezea kitu kwa kusema kiu kubwa ya wazee wetu ilikuwa ni kumuondoa mkoloni. Ila kidogo naomba kutofautiana nawe kwamba, watu waliojumuika na Julius Nyerere baada ya kuikomboa Tanganyika walikuwa na "uchu wa madaraka".
Hili neno uchu wa madaraka linanipa ukakasi na kunikwaza na hata mtafiti wetu Mzee Mohamed Said hapendi kulitumia katika hoja zake. Mzee wetu, Mohamed Said ni gwiji na hazina yetu hilo sote tunaliafiki.
Mimi nilitaka kufahamu kwa nini Abdulwahid Sykes na kizazi chake hawakutaka kujumuika na Julius Nyerere kama ilivyo kwa Mwapachu na familia yake? Je kuna kitu cha ziada au kina Sykes walikuwa na kiu ya kumuondoa mkoloni kisha hawakutaka kulijenga taifa walililolipigania? Yawezekana zipo sababu nyingine za ziada, hebu tujaribu kumdadisi na kumfikirisha Mzee Mohamed Said aendelee na utafiti wake ili aje atujuze.
Kwezisho,
Baada ya ufafanuzi huu wako sasa nimekuelewa.
Labda nami nijibu swali lako kwa kukuuliza swali.

Naamini umesoma historia ya TANU na uhuru wa
Tanganyika kuna mahali popote ametajwa Abdul?

Unasema Abdul hakutaka kujumuika na Nyerere.

Kwa nini isiwe labda Nyerere hakupenda kujumuika
na Abdul?

Lakini katika kundi hilo hakuwa Abdul peke yake.

Alikuwapo Sheikh Hassan bin Amir vile vile ambae
pia alitoa mchango mkubwa wa kukiongoza chama
vizuri na kumpa ''support'' kubwa Nyerere kati ya
1954 - 1961.

Iweje Nyerere alikuwa kimya kuhusu watu hawa
kama vile hakupata kujuananao?

Sasa hapa msiniachie mimi nifikiri peke yangu sote
tupige kichwa kufikiri.
 
Alhabyb Mohammed Said naomba nikuite jina hili kuanzia Leo "gurudumu la tarekh" hakika ww ni gogo Al bahri mashallah
Kwezisho,
Unasema yawezekana zipo sababu nyingine zaidi.
Ndiyo inawezekana zikawepo sababu nyingine zaidi.

Mimi nimejitahidi kujibu kadri ya uwezo na ufahamu wangu.

Na ni vizuri katika utafiti wowote ikaachwa nafasi ya mtafiti
mwingine kueleza yale ambayo mtafiti wa mwanzo labda kwa
sababu za kibinadamu zimempita.

Wenye taarifa zaidi ya historia ya kipindi kile wanaweza na wao
wakajazia pale ambapo mimi nimeishia.

Huenda kwa majibu ya wengine ikawa hiyo kiu ikakatika.

Kuhusu shida uinayo kuhusu jibu langu wala hapana haja ya wewe
kupata hiyo shida.

Nichukulie mimi kama mtu wa kawaida mwenye kikomo cha uwezo
na kwa ajili hii ipo nafasi kubwa sana ya kukosea.

Umetumia neno ''kususa'' na ''kukataa.''

Katika utafiti wangu sikukumbana na hali yoyote iliyoonyesha kuwa
Abdul ''alisusa'' au ''kukataa.''

Abdul kama walivyokuwa wenzake wengine katika wale wafadhili
wakubwa wa TANU waliendelea kukisaidia chama hadi uhuru 1961.

Hilo swali la kwa nini Nyerere hakupenda kuwatumia akina Sykes
kama alivyowatumia akina Mwapachu hili swali lako halijakaa vyema.

Halijakaa vyema swali lako kwa sababu sasa hapa unakuja kwa watoto
wa Hamza Mwapachu na watoto wa Abdul na Ally Sykes.

Swali hili lingemstahiki Mwalimu Nyerere mwenyewe kulijibu.
Mimi siwezi kumsemea.
 
Mzee wangu nashukuru sana kwa jibu lako. Na vyema tukawapa fursa watafiti wengine wakaendelea pale ukomo wetu ulipofikia. Ila kwa ufahamu wangu, unayo mahusiano mazuri sana na hii familia ya Sykes, sio vibaya kuwauliuza labda wanaweza kutufahamisha.

Kwezisho,
Nasikitika kukufahamisha kuwa baada ya mimi kuandika
kitabu cha Abdul Sykes kumeingia ''disinterest'' kwa hii
historia ya Nyerere kwetu sote.

Nyerere amekuwa sasa si muhimu tena baada ya ukweli
kujulikana katika historia ya AA, TAA na TANU.

Na nadhani baada ya Abdul na Ally Sykes kupewa nishani
katika kumbukumbu ya miaka 50 wa uhuru wa Tanganyika
kutambua mchango wao katika kupambana wa ukoloni sasa
hakuna tena jipya.

Imekuwa kama vile katika ''show,'' pazia limeshushwa.
 
Kwezisho,
Baada ya ufafanuzi huu wako sasa nimekuelewa.
Labda nami nijibu swali lako kwa kukuuliza swali.

Naamini umesoma historia ya TANU na uhuru wa
Tanganyika kuna mahali popote ametajwa Abdul?

Unasema Abdul hakutaka kujumuika na Nyerere.

Kwa nini isiwe labda Nyerere hakupenda kujumuika
na Abdul?

Lakini katika kundi hilo hakuwa Abdul peke yake.
Alikuwapo Sheikh Hassan bin Amir vile vile ambae
pia alitoa mchango mkubwa wa kukiongoza chama
vizuri na kumpa ''support'' kubwa Nyerere kati ya
1954 - 1961.

Iweje Nyerere alikuwa kimya kuhusu watu hawa
kama vile hakupata kujuananao?

Sasa hapa msiniachie mimi nifikiri peke yangu sote
tupige kichwa kufikiri.
Nashukuru kwa kunielewa. Mimi ni msomaji wa historia na nimeisoma historia ya TANU na nimebahatika kuvisoma baadhi ya vitabu vya Nyerere. Ila hili suala linanitatiza sana na kwa bahati mbaya hakuna majibu. Wengi wanajiuliza na hawapati kiini cha kujitoa (kususa?) kwa familia ya Sykes baada ya kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika.
 
Alhabyb Mohammed Said naomba nikuite jina hili kuanzia Leo "gurudumu la tarekh" hakika ww ni gogo Al bahri mashallah
Alhabib Bafa,
Ngoka nikueleze kitu.
Wallahi nakuapia si kama mimi ni mjanja kushinda wengine.

Bahati iliyonikuta mimi ni kuwa nimezaliwa na watu hawa na
kwa wakati ule.

Haya yanatendeka yanatendwa na watu ambao wazee wangu
wakiwajua na mimi nikaja kuwana kwa macho yangu.

Na yapo yaliyokuwa yakizungumzwa mimi mdogo nayasikia
ingawa haikunipitikia kuwa nilikuwa nashuhudia kitu kikubwa
sana katika historia ya Tanganyika.

Mimi nina picha alinipiga Mzee Shebe mwaka wa 1952 au 1953.
Huyu Mzee Shebe akaja kuwa mpiga picha wa TANU na Nyerere
wakati wa kudai uhuru.

20140129_133419.jpg


Siku mama yangu alipokuja kunambia historia ya picha ile nilishtuka.

Mzee Shebe
alinipiga picha ile katika studio yake iliyokuwa Mtaa wa
Livingstone na Kipata.

Alhabib,
Ahsante kwa kunitunuku jina.
 
Nashukuru kwa kunielewa. Mimi ni msomaji wa historia na nimeisoma historia ya TANU na nimebahatika kuvisoma baadhi ya vitabu vya Nyerere. Ila hili suala linanitatiza sana na kwa bahati mbaya hakuna majibu. Wengi wanajiuliza na hawapati kiini cha kujitoa (kususa?) kwa familia ya Sykes baada ya kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika.
Kwezisho,
Abdul Sykes hakupata kumsusa Nyerere hata siku moja.

Ikiwa umesoma kitabu changu utakuwa umesahau baadhi
ya vitu na hii ndiyo sababu unahangaishwa na hii ''kususa,''
au ungependa kuwa Abdul awe kasusa.

Mimi tabu mtu kunichokonoa.
Huwa siingii kwenye tundu nabaki mlangoni.

Rejea kwenye kitabu cha Abdul Sykes na soma Sehemu
ya Tatu ya Kitabu.

Uhuru ushapatikana 1961.
Palipitika majambo.

Soma kisha rejea katika mjadala.
Usiandikie mate na wino upo.
 
Ukiongelea tanu na taa..bila kumtaja abdul sykes ..ni sawq ni sawa na kuongelea mapinduzi bila kumtaja che guevara..

Pumzika kwa amani mzee wetu abdulwaheid sykes
Escotter,
Allahuma Amin.
 
Back
Top Bottom