Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

UncleE="Uncle Jei Jei, post: 16461586, member: 34691"]Wewe ni mbobezi na mtaalamu wa tafiti za kihistoria, kwa uelewa wangu mdogo historia zote dunia ambazo zinavuma huwa zinataja key figures katika jambo linalosimuliwa. Haiwezekani na haitakaa itokee historia itaje watu wooote kwa uzito Sawa katika events moja. Ulivyosema baada ya kitabu chako cha Abdul Sykes kumeibuka disinterest kwa Nyerere, japo sijakisoma huenda hiyo imeletwa na mtazamo wa mwandishi juu ya hao wawili! Cha msingi historia haiwezi kuwabeba watu wote kwa usawa! hata katika familia watu wakishatutoka hatuwakumbuki kwa uzito unaofanana na hiyo itategemea nani alikuwa nani kabla ya hapo. Mfano mzuri ni Zanzibar, Mzee Karume anatajwa sana kana kwamba yale mapinduzi aliyaandaa peke yake. Lakini ishu sio hiyo, ni kwa sababu miaka yote historia hum-feva kinara wa mwisho (the last key figure not initiators). Wewe waweza kuwa shahidi Kati ya mtu anayetoa wazo la jambo fulani na mtu anayetimiliza hilo wazo, Kati ya hao wawili ni yupi atafahamika zaidi. Hata nyie waandishi waweza pewa wazo zuri la kuandika kitu fulani ambalo hukuwahi kulidhani kama lingekuwa zuri lakini utakapoliandika na likapokelewa vizuri na jamii mtu atakayefahamika zaidi ni wewe uliyaandika hicho kitabu na wala huenda Jamii isimfahamu huyo mtoa wazo. Inawezekana kabisa hiyo ndo sababu ya Nyerere kutajwa zaidi kuliko hao wengine[/QUOTE]
Uncle,
Nakushauri usome kitabu kwanza kabla hujatoa uamuzi katika historia hii.

Ningeweza kusema mengi lakini sipendi kuathir fikra yako nataka uwe huru
uje utueleze ulichoona.
 
Naam, sheikh napenda sana kujua. Ila bado naufikirisha sana ubongo wangu. Je, yumkini Abdulwahid Sykes aliogopa kilichompata mtu aliyemtaka awe Rais wa TANU Bwana David Kidaha Makwaia? Zote ni speculation ila ni vyema kujua kwa kuwa hizi ni zama za kutaka kujua zaidi.
Kwezisho,
Shida inayokupata wewe nadhani ni kuwa hii historia ni ngeni kwako.

Abdul
hakuwa mtu wa kutishwa na Nyerere si wakati wa kudai uhuru
wala wakati uhuru ushapatikana.

Ukweli wa historia ya TANU ushajulikana na ndiyo maana nikakueleza
kuwa kwetu sisi hii historia ishafika mwisho.

Tatizo lilikuwa pale ambapo tulikuwa kimya.

Lakini baada ya kuieleza dunia historia ya kweli ya TANU kisa hiki sasa
kimefika mwisho.
 
hilo baibui alilovaa bi mwamvua(mama daisy) liko wapi hapo pichani?

"anasema hapo hapo akachukua baibui lake na kuelekea mkutanoni"
Mtanganyika...
Unachanganya matokeo mawili tofauti.

Suala la baibui ni 1955 wakati wa kuunda Umoja wa Wanawake wa TANU.
Siku hizo hata Bi. Titi alikuwa anapanda kuhutubia kavaa baibui.

Baadae mabaibui yaliwekwa pembeni.
Hiyo picha nilolweka hapo ni maandamano ya TANU baada ya uhuru.
 
Kwezisho,
Shida inayokupata wewe nadhani ni kuwa hii historia ni ngeni kwako.

Abdul
hakuwa mtu wa kutishwa na Nyerere si wakati wa kudai uhuru
wala wakati uhuru ushapatikana.

Ukweli wa historia ya TANU ushajulikana na ndiyo maana nikakueleza
kuwa kwetu sisi hii historia ishafika mwisho.

Tatizo lilikuwa pale ambapo tulikuwa kimya.

Lakini baada ya kuieleza dunia historia ya kweli ya TANU kisa hiki sasa
kimefika mwisho.
Sheikh Mohamed, mimi sio mgeni wa historia na ni mfuatiliaji mzuri wa mabandiko yako pamoja na vipindi vya TV ila kinachonitatiza ni ushiriki wa familia ya Abdulwahid Sykes baada ya kuikomboa Tanganyika. Na hapo juu umegusia kwamba Abdul hakuwa mtu wa kutishwa na Nyerere si wakati wa kudai Uhuru au baada.
Ila kwa ufahamu wangu mdogo hili suala kama ulivyoelekeza ni suala linaloonesha bado kuna jambo au mambo hayapo wazi ingawa kwenye kitabu chako umegusia kuna mambo yalipitika, tunahitaji kujiuliza na kujua kwa nini ushiriki wa hii familia baada ya ukombozi.
Hebu tuwaombe wenye ufahamu kama Mzee wetu Mohamed Said watujuze.
 
Sheikh Mohamed, mimi sio mgeni wa historia na ni mfuatiliaji mzuri wa mabandiko yako pamoja na vipindi vya TV ila kinachonitatiza ni ushiriki wa familia ya Abdulwahid Sykes baada ya kuikomboa Tanganyika. Na hapo juu umegusia kwamba Abdul hakuwa mtu wa kutishwa na Nyerere si wakati wa kudai Uhuru au baada.
Ila kwa ufahamu wangu mdogo hili suala kama ulivyoelekeza ni suala linaloonesha bado kuna jambo au mambo hayapo wazi ingawa kwenye kitabu chako umegusia kuna mambo yalipitika, tunahitaji kujiuliza na kujua kwa nini ushiriki wa hii familia baada ya ukombozi.
Hebu tuwaombe wenye ufahamu kama Mzee wetu Mohamed Said watujuze.
Kwezisho,
Uamuzi ni wako.

Elimu haina mwisho ikiwa wako watakaojazia pale nilipoacha mie hiyo
ni kheri.
 
Tupe jibu la mwalimu Nyerere
Onyx,
Mwaka wa 1974 Ali Muhsin Barwani alifunguliwa kutoka jela za Bara ambako
Nyerere alimfunga kwa miaka 10 baada ya serikali ya Zanzibar kupinduliwa
mwaka wa 1964.

Hakupita muda Ali Muhsin alitoroka kwa kuvuka mpaka wa Horohoro kwa njia za
panya kwa miguu usiku wa manane akisaidiwa na wasamaria wema na hivyo
kuweza kufika Mombasa kisha Nairobi na kupata msaada wa UNHCR waliomsaidia
kufika Cairo kuungana na familia yake.

Ali Muhsin alitoroka Tanzania mwezi Mtukufu wa Ramadhani kama huu.
Mwaka wa 1997 aliandika kitabu, ''Conflicts and Harmony in Zanzibar.''

Unaweza kumjua Ali Muhsin kwa kuingia hapo chini:
Mohamed Said: KUTOKA JF: KUMBUKUMBU ZA ALI MUHSIN BARWANI: ''CONFLICTS AND HARMONY IN ZANZIBAR''
Mohamed Said: TUJIKUMBUSHE: SHEIKH ALI MUHSIN BARWANI MMOJA WA WAPIGANIA UHURU WA ZANZIBAR
Mohamed Said: MAISHA YA SIASA YA SHEIKH ALI MUHSIN BARWANI (1919 - 2006) - KUMBUKUMBU YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

ZDu_tcL44sInB5Squy6d_xNPetNWvp0p940_8HXbvHYClXF0XMrMn0fo_nSSk1NCKhEAhXIYL4X9Glt2L6LaX_os58klgYxCxgCBRhM3Ei5lOntFl7RMzu03bkomM1cAVC350oHv9GCnJSD0

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa U Thant akisalimiana na
Waziri Mkuu wa Zanzibar Mohamed Shamte na Waziri wa
Mambo ya Nchi za Nje Ali Muhsin Barwani mwaka wa 1963
New York


Katika kitabu chake hicho Ali Muhsin alimueleza Nyerere kwa namna
ambayo haikuwahi kufanywa kabla.

Kitabu hiki kilipigwa marufuku kimya kimya kuingia Zanzibar lakini photo
copy ya kitabu iliweza kupenyezwa na kuwafikia baadhi ya watu.

Kila aliyekisoma alipata mshtuko wa aina yake na mmoja wa wasomaji
wa kitabu hiki alikuwa Prof. Haroub Othman.

Mara tu baada ya kutoka kitabu cha Ali Muhsin ndipo kikatoka kitabu
cha Abdul Sykes mwaka wa 1998.

Kama ilivyokuwa kwa kitabu cha Ali Muhsin, kitabu hiki nacho kilikuja
na mengine ambayo yalionekana kuwataabisha baadhi ya watu na
mmoja katika hao waliotaabika alikuwa Prof. Haroub Othman.

Hakuweza kustahamili ndipo alipofunga safari hadi nyumbani kwa
Mwalimu Nyerere na kumuomba akijibu kitabu cha Ali Muhsin
Barwani
na kitabu cha Mohamed Said kwani vikiachiwa bila majibu
vitaharibu ''legacy'' yake.

Mwalimu Nyerere alikuwa kasoma vitabu vyote viwili na jibu alilompa
Prof. Haroub ni kuwa yeye Haroub atengeneze kamati na yeye atakuja
kueleza yote ili wao waandike historia yake.

Kamati ilitengenezwa lakini hakuna kilichofanyika hadi Mwalimu Nyerere
alipofariki dunia mwaka 1999.

Kitabu cha Ali Muhsin Barwani kinapatikana Tanzania Publishing House,
Ibn Hazm Media Centre Msikiti wa Mtoro na Manyema na Elite Bookshop
Mbezi Samaki na Soma Bookshop Mikocheni kwa bei ya shs: 10,000 hadi
shs 13,000.
 
Ni kweli kabisa, hata mimi nilishangaa kusikia hivyo. Nikiri kwamba historia kamili ya wapigania uhuru wa Tanganyika nimekuja kuwafahamu nilipokuwa chuo kikuu chini ya mwl wangu wa HISTORY OF TANZANIA Dr Mkanachi. Waanzilishi wote wa chokochoko za ukombozi na kwamba Nyerere aliingia rasmi TAA 1953 baada ya kutoka masomoni Wingereza nilivijulia huko. Nachotaka kusema, ordinary historians si rahisi kufahamu initiators wa uhuru. Wanawafahamu zaidi key figure ambao walikuja kushika madaraka na hilo si kosa wala dhambi kwani ndo historia ya dunia ilivyo. Historia ya dunia ni tofauti na historia za dini ambazo Waanzilishi ndo waliozieneza kwa sababu mwenyezi Mungu alipanga iwe hivyo.
Uncle...
Kusema kuwa ati historia inayojulikana ni ya walioshika madaraka
hiyo si kweli na hakuna ushahidi wa kisomi wa hiyo dhana yako.

Historia haijali haiba ya mtu labda iwe ''official history.''
Historia itaeleza yale yaliyotokea na waliohusika.

Kwa historia hii tunayoijadili hapa hiyo iliyoandikwa na watafiti wetu
historia hii ni ''official history,'' watafiti walielekezwa kipi cha kuandika
na kipi cha kuacha.

Fanya utafiti kidogo tu uangalie ni watu gani walifutwa katika historia
ya uhuru wa Tangnayika na jiulize ni kwa sababu gani?

Nimeeeleza haya kwa urefu na mapana katika kitabu cha Abdul Sykes.
Iweje mtu avishwe kilemba na joho si lake na asione vibaya?

Hebu ingia hapa:
Mohamed Said: UPINZANI DHIDI YA HISTORIA YA KWELI YA TANU NA UHURU WA TANGANYIKA 4

SAM_0322.JPG


Dr. Khamisi Mkanachi na mimi Dodoma
 
Ahsante mzee wangu mohammed said siku zote huwa sichok kusoma maandish yko maana najifunza mungu akupe afya njema na akulipe kla la kheir inshaallah
 
Onyx,
Baada ya uhuru Nyerere alimtia Chief Kidaha kizuizini Tunduru
chini ya Dentition Act of 1962.

Chief Kidaha alipoachiwa akahamia Kenya.

Kwa habari zaidi ingia:
Mohamed Said: CHIEF DAVID KIDAHA MAKWAIA
Mohamed Said: Chief David Kidaha Makwaia 1922 - 2007

Reading between lines, dhamira yako ya kumdharaulisha Nyerere bado inaendelea.
Nyerere "alimtiaje" ndani chief David Kidaha?
Je ni sahihi kuandika historia ya sasa kuhusu Sheik Ponda kuwa alipigwa risasi na Kikwete, kwa vile tu tukio lilitokea wakati utawala wa Kikwete?
 
CtOKRwRzrB5mBzQ5Cb9hS_jD8pN0sOFV1B9UckVYU8i70_Q_XEgdcQvlLqtXwNIGW3VWYaLF4a3otlgbC7K9Em0h3Ei39ed7tspSVQ5gtgrZL5rX2su_TqGlyreZorkWRdRYWBJm9Hn-QodC4i5vw06b46UkgySmTNjczP8cj6bmXb4RA6T3qSC_BRU6IEc8Uk75bpciUYbt_YdFaT-dh7hXKdN7cAdD9DHdB4xKJnFGYL4kk1Re5KOjQb6dQbt6-W2QvuYpX7q_3wE2ayyasqEFYWkowgSSkAVFoSq7jL6StW7uicmeAbddSAD_lW0f1GKpvu4xqI9a4PI-bYpm_24kxvl6H8PB1jGH53J9kAbmKXXFPW9YH4qAATIs8DSUScqrg8cJFiy35i4w8jl_JY9uTugl2Aw44difR64FY7bDSEaxEnvJoAwt7M-fxGIG15Umq6XOPqn2rzgSW-lp0fZFNQw9Psx1PGIaIrPRkMAm9PszJcCMiwBkZ9tPSxmQbYeMWxj0yL1lzzPXdNCcTFcoGpAmatJ1uOku2ZCcVz5Si6WIiO58WJjxk8cC3pX-kibj3Y1fBK5co9QGLfLHjSh0zHTOmAOH=w579-h657-no

Chief Michael Lukumbuzya wa Ukerewe​

Nilikuwa naitafuta picha ya hayati Chief Michael Lukumbuzya kwa miaka mingi bila mafanikio. Sababu ya kuitafuta picha ya Chief Lukumbuzya ni kisa alichonihadithia Bi. Mwamvua biti Masha mke wa marehemu Abdulwahid Sykes maarufu akijuikana kwa jina la mwanae wa kwanza Daisy hivyo tukimuita Mama Daisy.

Nilikuwa kila nikipata fursa ya kuwa na mama yangu Bi. Mwamvua, yaani Mama Daisy nikipenda kumdodosa mambo yalivyokuwa wakati wa ukoloni walipokuwa wanapambana na Muingereza, kwanza kichinichini katika miaka ya mwanzo ya 1950 wakati wa TAA kisha wakipambana na mkoloni dhahiri baada ya kuunda TANU mwaka wa 1954.

Bi. Mwamvua
alikuwa wakati mwingine bila kutegemea akiniangushia habari muhimu kupita kiasi. Mfano siku aliponiambia kuwa nafasi ya president wa TANU nafasi ile ilikuwa ya Chief Kidaha Makwaia lakini alikataa ndipo bahati ikamuangukia Julius Nyerere.

IMG-20160406-WA0111%2B%25281%2529.jpg

Chief David Kidaha Makwaia​

Iko siku akanieleza taharuki iliyotokea nyumbani kwa Abdul Sykes baada ya Nyerere kula chakuka kilichomfanya tumbo limkate na ikadhaniwa kuwa amelishwa sumu.

Mkasa huu ulitokea wakati mama yake Nyerere, Bi. Mugaya Nyangombe yuko na Mama Maria Nyerere vilevile wamekaa uani na akina mama wengine na Abdul Sykes, Nyerere na viongozi wengine wako nyumba kubwa wanapanga mipango ya kupeleka harakati mbele.

Mama yake Nyerere alianza kulia akiamini kabisa kuwa mwanae katiliwa sumu katika chakula. Mama Daisy alikuwa na habari nyingi sana za nyakati zile. Historia ya TANU kama zilivyo nyaraka na picha zake nyingi zimo mikononi mwa watu.

Mfano mwingine ni wa mkutano wa kwanza wa Wanawake wa TANU uliokuwa ukifanyika Arnautoglo Hall na yeye alikuwa yuko nyumbani anafanya shughuli zake. Anasema, ‘’Aliporudi nyumbani Bwana Abdul kanikuta nimekaa, akaniuliza wewe hukwenda mkutanoni? Wenzako wote wako Arnautoglo…’’ Bi. Mwamvua anasema hapo hapo akachukua baibui lake na kuelekea mkutanoni.

Wasemaji wakuu walikuwa Bi. Titi Mohamed na Bi. Tatu biti Mzee. Huu ndiyo mkutano wa kwanza wa wanawake wa TANU.

toW0HLKw0_eZRKHUURD38LIxZWcW5RXD7goNoYJWFVWEj8kMEyL1bPXqHWB5CmfrXmD1mA=w329-h566-no

Kushoto Mama Daisy na mbele yake ni Bi. Titi Mohamed
na Bi. Zainab mke wa Tewa Said Tewa

Katika mazungumzo kama haya ndipo siku moja akanihadithia habari za Chief Luumbuzya. Anasema walitoka Dar es Salaam yeye mumewe kwenda Nansio, Ukerewe kumtembelea Hamza Mwapachu.

Anasema walipanda meli Mwanza pamoja na Chief Lukumbuzya kuelekea Nansio. Lukumbuzya alikuwa anatokea Makerere Uganda alipokuwa anasoma anarudi nyumbani likizo. Abdul Sykes na Michael Lukumbuzya hawakuwa wanajuana.

Hamza Mwapachu alikuwa amekusanya wananchi na kikundi cha ngoma kuja kumpokea bandarini Nansio President wa TAA Abdulwahid Sykes. Lukumbuzya alishangazwa kukuta sherehe bandarini akifanyiwa mtu ambae yeye hakuwa anamjua na akiuliza anaambiwa ni mgeni kutoka Dar es Salaam.

Lukumbuzya alipigwa na butwaa kuona mapokezi ya watu wake wa Ukerewe wakiwa katika nderemo wakati yeye chief hakuna hata mtu alikuwa anajua kuwa yumo katika meli ile ile. Baadae Hamza Mwapachu alimfahamisha yule mgeni waliokuja kumpokea pale alikuwa nani katika siasa za Tanganyika.

proxy

Hamza Kibwana Mwapachu​

Simulizi kama hizi zilinifikirisha sana katika kutaka kuwajua wazalendo wa wakati ule. Hamza Mwapachu alikuwa anafanya haya ya kukusanya wananchi kumpokea kiongozi wa Waafrika chini ya pua za Waingereza bila kujali nini kitampata licha ya kuwa yeye kupewa uhamisho kupelekwa kisiwani Ukerewe peke yake ilikuwa ni adhabu, kwa hakika ni kifungo khasa cha kumtia kuzuizini asiweze kuenedeleza mipango yake ya kuunda chama cha siasa.

Uhuru ulipopatikana Chief Michael Lukumbuzya alipelekwa nje ambako alikuwa balozi na mwisho akawa balozi Canada ambako huko ndiko umauti ulikomfika.

6La5FUdYcnEadMYf6JSIrrWhkpElkSUYiAFTlRs_Bz4mDSXPmSD4EMzk4gTvEnMGuvf8pxy__jBGacnsvJHLYxP_wyS0OA25OYba8__txYHDI2z5TOfGkl7O_IoMO3NAleFvmru20T-YQF39hdK_UD7K79l2x2k40bDIMbiMoIB_ArerygwQ5oIGK11itARq1AoviA_D4OZrLGJZ-mOTiDWEC0pNQPmQPCS-cXzyWVr9raFuGLLKTwCz1GYMrJwsoBIeqCiy_AoHfwRMiTgHgBNRPHowAkwTnbtPxlJ_q9CTx_Ny6xhgBxkIMIBwc9Y79KJA7DXbYcODNB5X-lEL7SxzUEASzHc9r77_ByOVTHcN0j-HCDs2tr7oGw85M3YPXBv0OHG_2pnc_yZefK7n9_UyaxLXX1pmIeP1p01hc6LGf1QcrRusRSirpgfDZrxPMGTwr3EcKUjvY8vh1Kj2_zL9VnkUc-uHdQCSgUi6JBUaZrDi_2LVFAy1ImbD9BwIspcf8aHvXSBLQFSWfC2m3EGmjIMKOU2CDUXZv8NTjsn7UCfaBiWfrRT4ab3OSNhVpvB2GqLU1Rgk5_YjnfJgAxeKukdqeFoc=w476-h657-no

Abdulwahid Sykes​
Ahsante kwa historia nzuri ya Taifa letu Ndugu Mohamed Said.u
Ningelipenda kujua ktkt harakati za uhuru upande kina mama kama una habari yeyote ya Chiku bint Said Kisusa wa New Street enzi hizo ambaye alikuwa mke wa Sharif Said Al attas (ulishawahi mtaja kwenye simulizi zako) .
 
Ahsante kwa historia nzuri ya Taifa letu Ndugu Mohamed Said.u
Ningelipenda kujua ktkt harakati za uhuru upande kina mama kama una habari yeyote ya Chiku bint Said Kisusa wa New Street enzi hizo ambaye alikuwa mke wa Sharif Said Al attas (ulishawahi mtaja kwenye simulizi zako) .
Kambaresharubu,
Bahati mbaya sina taarifa za bi. mkubwa huyu.
 
Reading between lines, dhamira yako ya kumdharaulisha Nyerere bado inaendelea.
Nyerere "alimtiaje" ndani chief David Kidaha?
Je ni sahihi kuandika historia ya sasa kuhusu Sheik Ponda kuwa alipigwa risasi na Kikwete, kwa vile tu tukio lilitokea wakati utawala wa Kikwete?
Nanren,
Thomas Molon
ameandika kitabu: ''Nyerere The Early Years.''

Ameeleza sintofahamu iliyokuwapo kati ya Chief Kidaha na
Nyerere iliyodumu kwa miaka mingi.

Naamini Molon hakuwa na nia ya kumdhalilisha Nyerere kwa
kueleza ugomvi ule.
 
Onyx,
Mwaka wa 1974 Ali Muhsin Barwani alifunguliwa kutoka jela za Bara ambako
Nyerere alimfunga kwa miaka 10 baada ya serikali ya Zanzibar kupinduliwa
mwaka wa 1964.
Mkuu Maalim
Mohamed Saidasante kwa taarifa, kutujulisha kumbe enzi zile ni Nyerere ndio alikuwa anatia watu jela na kuwafunga tuu!, ila haikusemwa watu hao waliofungwa na Nyerere, walikuwa wanafunguliwa na nani kutoka vifungo hivyo vya Nyerere?!. Mimi nilidhani ungesema ni serikali ya Nyerere!, kumbe ni Nyerere!, asante!.

Kwa msio jua kilichotokea Zanzibar baada ya mapinduzi yale matukufu ya 1964, wapinzani wa Karume walikuwa wana vanish into thin air, hata unywele haukuonekana (taarrifa zisizothibitishwa zilisema walininginizwa majiwe shingoni, kutiwa ndani ya magunia na kutoswa baharini). Kufuatia Mwalimu Nyerere kuwa ni mcha Mungu, hakuridhishwa na kinachoendelea kule, hivyo ili kuwanusuru waliotofautiana na Karume, aliwachukua na kuwafunga huku bara ambayo hiyo ndio salama yao!, hivyo ndivyo Nyerere alivyowanusu wengi akiwemo Col. Mafudha, Abrahman Mohamed Babu na baadhi ya Makomredi, vinginevyo saa hizi, tungekuwa tunazungumza mengine!.

Kiukweli shukrani ya punda ni mateke!, asingekuwa Nyerere na Muungano, baada ya yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, sijui ingelikuwaje kwa race fulani kule Zanzibar, halocust ingekuwa ni afadhali maana angalau ulipatikana japo mfupa au hata majivu!, Zanzibar hata unyayo tuu ulipokanya mara ya mwisho,usingeonekana, sii unywele wala ukucha!. Badala ya kushukuru ndio kwanza watu humu wanabeza!.

Kwa amsiomjua Nyerere, japo nchi yetu ina adhabu ya kifo, katika utawala wake wa miaka 23, alisaini hati moja tuu ya kunyongwa kwa Mwamwindi!. Aliyefuatia ni swala tano!, uliza alisaini hati ngapi na watu wakanyongwa!.

Vitu vingine bora tuacheni tuu!, harakati za kumtangaza Nyerere ni Mwenye Heri, zinaendelea!.

Pasco
 
Kajembejr,
Mwalimu Nyerere
hakuibuka.

Mwalimu Nyerere tayari katika maisha yake toka udogo alionyesha
uwezo wa akili ambao haukuwa wa kawaida.

Hamza Mwapachu ambae walikuwa wote Tabora School na Makerere
alikuwa anaujua vyema uwezo wa Nyerere na ndiyo sababu alimuomba
Abdul amchukue Nyerere katika TAA kwenye safu ya uongozi hapo HQ
New Street.
Ahsante MZEE Mohamed
 
Back
Top Bottom