Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

Mzee wang mohamed said..pole na hongera kwa mwezi huu mtukufu...ukipata picha ya mke wa mzee wetu yaan mke wa sykes ..miaka ya karibuni kabla ya umauti ..ilete tafadhali tuione
Escotter,
Wa kwanza kushoto ndiye Mama Daisy, mbele yake ni Bi. Titi Mohamed
na mbele ya Bi. Titi ni Bi Zainab aliyekuwa mke wa Tewa Said Tewa.

toW0HLKw0_eZRKHUURD38LIxZWcW5RXD7goNoYJWFVWEj8kMEyL1bPXqHWB5CmfrXmD1mA=w329-h566-no
 
Kwezisho,
Abdul Sykes hakupata kumsusa Nyerere hata siku moja.

Ikiwa umesoma kitabu changu utakuwa umesahau baadhi
ya vitu na hii ndiyo sababu unahangaishwa na hii ''kususa,''
au ungependa kuwa Abdul awe kasusa.

Mimi tabu mtu kunichokonoa.
Huwa siingii kwenye tundu nabaki mlangoni.

Rejea kwenye kitabu cha Abdul Sykes na soma Sehemu
ya Tatu ya Kitabu.

Uhuru ushapatikana 1961.
Palipitika majambo.

Soma kisha rejea katika mjadala.
Usiandikie mate na wino upo.
Aksante. Nimekisoma sana kitabu chako na pia majambo yalipitika nimeyaona ila yale matundu uliyoaacha ndio hayo sie twataka utujuze kwa undani.
 
Aksante. Nimekisoma sana kitabu chako na pia majambo yalipitika nimeyaona ila yale matundu uliyoaacha ndio hayo sie twataka utujuze kwa undani.

Kwezisho,
Kasome Sehemu ya Tatu ya Kitabu.
Maswali yako yote majibu yake yamo mle.
 
CtOKRwRzrB5mBzQ5Cb9hS_jD8pN0sOFV1B9UckVYU8i70_Q_XEgdcQvlLqtXwNIGW3VWYaLF4a3otlgbC7K9Em0h3Ei39ed7tspSVQ5gtgrZL5rX2su_TqGlyreZorkWRdRYWBJm9Hn-QodC4i5vw06b46UkgySmTNjczP8cj6bmXb4RA6T3qSC_BRU6IEc8Uk75bpciUYbt_YdFaT-dh7hXKdN7cAdD9DHdB4xKJnFGYL4kk1Re5KOjQb6dQbt6-W2QvuYpX7q_3wE2ayyasqEFYWkowgSSkAVFoSq7jL6StW7uicmeAbddSAD_lW0f1GKpvu4xqI9a4PI-bYpm_24kxvl6H8PB1jGH53J9kAbmKXXFPW9YH4qAATIs8DSUScqrg8cJFiy35i4w8jl_JY9uTugl2Aw44difR64FY7bDSEaxEnvJoAwt7M-fxGIG15Umq6XOPqn2rzgSW-lp0fZFNQw9Psx1PGIaIrPRkMAm9PszJcCMiwBkZ9tPSxmQbYeMWxj0yL1lzzPXdNCcTFcoGpAmatJ1uOku2ZCcVz5Si6WIiO58WJjxk8cC3pX-kibj3Y1fBK5co9QGLfLHjSh0zHTOmAOH=w579-h657-no

Chief Michael Lukumbuzya wa Ukerewe​

Nilikuwa naitafuta picha ya hayati Chief Michael Lukumbuzya kwa miaka mingi bila mafanikio. Sababu ya kuitafuta picha ya Chief Lukumbuzya ni kisa alichonihadithia Bi. Mwamvua biti Masha mke wa marehemu Abdulwahid Sykes maarufu akijuikana kwa jina la mwanae wa kwanza Daisy hivyo tukimuita Mama Daisy.

Nilikuwa kila nikipata fursa ya kuwa na mama yangu Bi. Mwamvua, yaani Mama Daisy nikipenda kumdodosa mambo yalivyokuwa wakati wa ukoloni walipokuwa wanapambana na Muingereza, kwanza kichinichini katika miaka ya mwanzo ya 1950 wakati wa TAA kisha wakipambana na mkoloni dhahiri baada ya kuunda TANU mwaka wa 1954.

Bi. Mwamvua
alikuwa wakati mwingine bila kutegemea akiniangushia habari muhimu kupita kiasi. Mfano siku aliponiambia kuwa nafasi ya president wa TANU nafasi ile ilikuwa ya Chief Kidaha Makwaia lakini alikataa ndipo bahati ikamuangukia Julius Nyerere.

IMG-20160406-WA0111%2B%25281%2529.jpg

Chief David Kidaha Makwaia​

Iko siku akanieleza taharuki iliyotokea nyumbani kwa Abdul Sykes baada ya Nyerere kula chakuka kilichomfanya tumbo limkate na ikadhaniwa kuwa amelishwa sumu.

Mkasa huu ulitokea wakati mama yake Nyerere, Bi. Mugaya Nyangombe yuko na Mama Maria Nyerere vilevile wamekaa uani na akina mama wengine na Abdul Sykes, Nyerere na viongozi wengine wako nyumba kubwa wanapanga mipango ya kupeleka harakati mbele.

Mama yake Nyerere alianza kulia akiamini kabisa kuwa mwanae katiliwa sumu katika chakula. Mama Daisy alikuwa na habari nyingi sana za nyakati zile. Historia ya TANU kama zilivyo nyaraka na picha zake nyingi zimo mikononi mwa watu.

Mfano mwingine ni wa mkutano wa kwanza wa Wanawake wa TANU uliokuwa ukifanyika Arnautoglo Hall na yeye alikuwa yuko nyumbani anafanya shughuli zake. Anasema, ‘’Aliporudi nyumbani Bwana Abdul kanikuta nimekaa, akaniuliza wewe hukwenda mkutanoni? Wenzako wote wako Arnautoglo…’’ Bi. Mwamvua anasema hapo hapo akachukua baibui lake na kuelekea mkutanoni.

Wasemaji wakuu walikuwa Bi. Titi Mohamed na Bi. Tatu biti Mzee. Huu ndiyo mkutano wa kwanza wa wanawake wa TANU.

toW0HLKw0_eZRKHUURD38LIxZWcW5RXD7goNoYJWFVWEj8kMEyL1bPXqHWB5CmfrXmD1mA=w329-h566-no

Kushoto Mama Daisy na mbele yake ni Bi. Titi Mohamed
na Bi. Zainab mke wa Tewa Said Tewa

Katika mazungumzo kama haya ndipo siku moja akanihadithia habari za Chief Luumbuzya. Anasema walitoka Dar es Salaam yeye mumewe kwenda Nansio, Ukerewe kumtembelea Hamza Mwapachu.

Anasema walipanda meli Mwanza pamoja na Chief Lukumbuzya kuelekea Nansio. Lukumbuzya alikuwa anatokea Makerere Uganda alipokuwa anasoma anarudi nyumbani likizo. Abdul Sykes na Michael Lukumbuzya hawakuwa wanajuana.

Hamza Mwapachu alikuwa amekusanya wananchi na kikundi cha ngoma kuja kumpokea bandarini Nansio President wa TAA Abdulwahid Sykes. Lukumbuzya alishangazwa kukuta sherehe bandarini akifanyiwa mtu ambae yeye hakuwa anamjua na akiuliza anaambiwa ni mgeni kutoka Dar es Salaam.

Lukumbuzya alipigwa na butwaa kuona mapokezi ya watu wake wa Ukerewe wakiwa katika nderemo wakati yeye chief hakuna hata mtu alikuwa anajua kuwa yumo katika meli ile ile. Baadae Hamza Mwapachu alimfahamisha yule mgeni waliokuja kumpokea pale alikuwa nani katika siasa za Tanganyika.

proxy

Hamza Kibwana Mwapachu​

Simulizi kama hizi zilinifikirisha sana katika kutaka kuwajua wazalendo wa wakati ule. Hamza Mwapachu alikuwa anafanya haya ya kukusanya wananchi kumpokea kiongozi wa Waafrika chini ya pua za Waingereza bila kujali nini kitampata licha ya kuwa yeye kupewa uhamisho kupelekwa kisiwani Ukerewe peke yake ilikuwa ni adhabu, kwa hakika ni kifungo khasa cha kumtia kuzuizini asiweze kuenedeleza mipango yake ya kuunda chama cha siasa.

Uhuru ulipopatikana Chief Michael Lukumbuzya alipelekwa nje ambako alikuwa balozi na mwisho akawa balozi Canada ambako huko ndiko umauti ulikomfika.

6La5FUdYcnEadMYf6JSIrrWhkpElkSUYiAFTlRs_Bz4mDSXPmSD4EMzk4gTvEnMGuvf8pxy__jBGacnsvJHLYxP_wyS0OA25OYba8__txYHDI2z5TOfGkl7O_IoMO3NAleFvmru20T-YQF39hdK_UD7K79l2x2k40bDIMbiMoIB_ArerygwQ5oIGK11itARq1AoviA_D4OZrLGJZ-mOTiDWEC0pNQPmQPCS-cXzyWVr9raFuGLLKTwCz1GYMrJwsoBIeqCiy_AoHfwRMiTgHgBNRPHowAkwTnbtPxlJ_q9CTx_Ny6xhgBxkIMIBwc9Y79KJA7DXbYcODNB5X-lEL7SxzUEASzHc9r77_ByOVTHcN0j-HCDs2tr7oGw85M3YPXBv0OHG_2pnc_yZefK7n9_UyaxLXX1pmIeP1p01hc6LGf1QcrRusRSirpgfDZrxPMGTwr3EcKUjvY8vh1Kj2_zL9VnkUc-uHdQCSgUi6JBUaZrDi_2LVFAy1ImbD9BwIspcf8aHvXSBLQFSWfC2m3EGmjIMKOU2CDUXZv8NTjsn7UCfaBiWfrRT4ab3OSNhVpvB2GqLU1Rgk5_YjnfJgAxeKukdqeFoc=w476-h657-no

Abdulwahid Sykes​
Mkuu unavitabu umeandika, ningependa kuvisoma.
 
Mkuu unavitabu umeandika, ningependa kuvisoma.
Menyidyo,
Soma kitabu ''Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes...''
Kinapatikana Ibn Hazm Media Centre Bookshop Msikiti wa Manyemana Mtoro,
Kariakoo bei shs: 10,000.

Kipo pia Soma Bookshop Mikocheni na Novel Idea Slip Way Masaki hapa wana
nakala ya Kizungu, ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes...''
 
Aksante. Nimekisoma sana kitabu chako na pia majambo yalipitika nimeyaona ila yale matundu uliyoaacha ndio hayo sie twataka utujuze kwa undani.
Kwezisho,
Nashukuru kuwa umesoma kitabu.
Hayo matundu usemayo mimi siyajui.

Nimejitahidi kutafiti na kuandika kadri ya uwezo wangu.

Mara nyingi hupata maswali ya sampuli yako na mimi
huwa najibu kuwa labda Nyerere angeliandika historia
yake na vipi alikutana na Abdul Sykes tungeweza kupata
mengi.

Lakini kwa bahati mbaya sana Nyerere hakuandika.

Kwa nini hakuandika historia hii muhimu katika maisha yake
hatutoweza kujua kwa uhakika ila tutafanya, ''speculation,'' tu.

Miaka michache iliyopita katika ukumbi huu huu palifumuka
vumbi kubwa niliposema kuwa hotuba ya Nyerere aliyosoma
UNO 1955 ilikuwa imetayarishwa 1950 na jopo la Abdul Sykes,
Hamza Mwapachu, Sheikh Hassan bin Amir, Stephen
Mhando, Dr.Vedasto, Kyaruzi
na timu nzima ya TAA Political
Subcommitee ambayo Abdul alikuwa katibu wake.

Waliofuatilia mnakasha ule watakumbuka.
Kwa wengi hii ilikuwa habari mpya.

Kuna baadhi walikuwa hawajasikia hata hilo jina la Abdul na
majina mengine niliyotaja kama Sheikh Hassan bin Amir na
Said Chaurembo.

Ilikuwa kama vile nimemtukana Mwalimu Nyerere.

Na kila nilipojaribu kueleza historia ya TANU kama niijuavyo
ndivyo nilivyozidisha ghadhabu za baadhi ya watu.

Sishangai kukuona unahangaika na kuwa katika hali ya kutotosheka
na niliyoandika.

Hauko peke yako katika hili.
Mwalimu wangu Prof. Haroub Othman yeye alikwenda mbali zaidi.

Prof. Haroub alimkabili Mwalimu Nyerere uso kwa macho kutaka
kusikia kutoka kinywani kwake ukweli katika yale niliyoandika.

Je ungependa kujua jibu la Mwalimu Nyerere?
 
Kwezisho,
Nasikitika kukufahamisha kuwa baada ya mimi kuandika
kitabu cha Abdul Sykes kumeingia ''disinterest'' kwa hii
historia ya Nyerere kwetu sote.

Nyerere amekuwa sasa si muhimu tena baada ya ukweli
kujulikana katika historia ya AA, TAA na TANU.

Na nadhani baada ya Abdul na Ally Sykes kupewa nishani
katika kumbukumbu ya miaka 50 wa uhuru wa Tanganyika
kutambua mchango wao katika kupambana wa ukoloni sasa
hakuna tena jipya.

Imekuwa kama vile katika ''show,'' pazia limeshushwa.

Wewe ni mbobezi na mtaalamu wa tafiti za kihistoria, kwa uelewa wangu mdogo historia zote dunia ambazo zinavuma huwa zinataja key figures katika jambo linalosimuliwa. Haiwezekani na haitakaa itokee historia itaje watu wooote kwa uzito Sawa katika events moja. Ulivyosema baada ya kitabu chako cha Abdul Sykes kumeibuka disinterest kwa Nyerere, japo sijakisoma huenda hiyo imeletwa na mtazamo wa mwandishi juu ya hao wawili! Cha msingi historia haiwezi kuwabeba watu wote kwa usawa! hata katika familia watu wakishatutoka hatuwakumbuki kwa uzito unaofanana na hiyo itategemea nani alikuwa nani kabla ya hapo. Mfano mzuri ni Zanzibar, Mzee Karume anatajwa sana kana kwamba yale mapinduzi aliyaandaa peke yake. Lakini ishu sio hiyo, ni kwa sababu miaka yote historia hum-feva kinara wa mwisho (the last key figure not initiators). Wewe waweza kuwa shahidi Kati ya mtu anayetoa wazo la jambo fulani na mtu anayetimiliza hilo wazo, Kati ya hao wawili ni yupi atafahamika zaidi. Hata nyie waandishi waweza pewa wazo zuri la kuandika kitu fulani ambalo hukuwahi kulidhani kama lingekuwa zuri lakini utakapoliandika na likapokelewa vizuri na jamii mtu atakayefahamika zaidi ni wewe uliyaandika hicho kitabu na wala huenda Jamii isimfahamu huyo mtoa wazo. Inawezekana kabisa hiyo ndo sababu ya Nyerere kutajwa zaidi kuliko hao wengine
 
Kwezisho,
Nashukuru kuwa umesoma kitabu.
Hayo matundu usemayo mimi siyajui.

Nimejitahidi kutafiti na kuandika kadri ya uwezo wangu.

Mara nyingi hupata maswali ya sampuli yako na mimi
huwa najibu kuwa labda Nyerere angeliandika historia
yake na vipi alikutana na Abdul Sykes tungeweza kupata
mengi.

Lakini kwa bahati mbaya sana Nyerere hakuandika.

Kwa nini hakuandika historia hii muhimu katika maisha yake
hatutoweza kujua kwa uhakika ila tutafanya, ''speculation,'' tu.

Miaka michache iliyopita katika ukumbi huu huu palifumuka
vumbi kubwa niliposema kuwa hotuba ya Nyerere aliyosoma
UNO 1955 ilikuwa imetayarishwa 1950 na jopo la Abdul Sykes,
Hamza Mwapachu, Sheikh Hassan bin Amir, Stephen
Mhando, Dr.Vedasto, Kyaruzi
na timu nzima ya TAA Political
Subcommitee ambayo Abdul alikuwa katibu wake.

Waliofuatilia mnakasha ule watakumbuka.
Kwa wengi hii ilikuwa habari mpya.

Kuna baadhi walikuwa hawajasikia hata hilo jina la Abdul na
majina mengine niliyotaja kama Sheikh Hassan bin Amir na
Said Chaurembo.

Ilikuwa kama vile nimemtukana Mwalimu Nyerere.

Na kila nilipojaribu kueleza historia ya TANU kama niijuavyo
ndivyo nilivyozidisha ghadhabu za baadhi ya watu.

Sishangai kukuona unahangaika na kuwa katika hali ya kutotosheka
na niliyoandika.

Hauko peke yako katika hili.
Mwalimu wangu Prof. Haroub Othman yeye alikwenda mbali zaidi.

Prof. Haroub alimkabili Mwalimu Nyerere uso kwa macho kutaka
kusikia kutoka kinywani kwake ukweli katika yale niliyoandika.

Je ungependa kujua jibu la Mwalimu Nyerere?

Ni kweli kabisa, hata mimi nilishangaa kusikia hivyo. Nikiri kwamba historia kamili ya wapigania uhuru wa Tanganyika nimekuja kuwafahamu nilipokuwa chuo kikuu chini ya mwl wangu wa HISTORY OF TANZANIA Dr Mkanachi. Waanzilishi wote wa chokochoko za ukombozi na kwamba Nyerere aliingia rasmi TAA 1953 baada ya kutoka masomoni Wingereza nilivijulia huko. Nachotaka kusema, ordinary historians si rahisi kufahamu initiators wa uhuru. Wanawafahamu zaidi key figure ambao walikuja kushika madaraka na hilo si kosa wala dhambi kwani ndo historia ya dunia ilivyo. Historia ya dunia ni tofauti na historia za dini ambazo Waanzilishi ndo waliozieneza kwa sababu mwenyezi Mungu alipanga iwe hivyo.
 
Kwezisho,
Nashukuru kuwa umesoma kitabu.
Hayo matundu usemayo mimi siyajui.

Nimejitahidi kutafiti na kuandika kadri ya uwezo wangu.

Mara nyingi hupata maswali ya sampuli yako na mimi
huwa najibu kuwa labda Nyerere angeliandika historia
yake na vipi alikutana na Abdul Sykes tungeweza kupata
mengi.

Lakini kwa bahati mbaya sana Nyerere hakuandika.

Kwa nini hakuandika historia hii muhimu katika maisha yake
hatutoweza kujua kwa uhakika ila tutafanya, ''speculation,'' tu.

Miaka michache iliyopita katika ukumbi huu huu palifumuka
vumbi kubwa niliposema kuwa hotuba ya Nyerere aliyosoma
UNO 1955 ilikuwa imetayarishwa 1950 na jopo la Abdul Sykes,
Hamza Mwapachu, Sheikh Hassan bin Amir, Stephen
Mhando, Dr.Vedasto, Kyaruzi
na timu nzima ya TAA Political
Subcommitee ambayo Abdul alikuwa katibu wake.

Waliofuatilia mnakasha ule watakumbuka.
Kwa wengi hii ilikuwa habari mpya.

Kuna baadhi walikuwa hawajasikia hata hilo jina la Abdul na
majina mengine niliyotaja kama Sheikh Hassan bin Amir na
Said Chaurembo.

Ilikuwa kama vile nimemtukana Mwalimu Nyerere.

Na kila nilipojaribu kueleza historia ya TANU kama niijuavyo
ndivyo nilivyozidisha ghadhabu za baadhi ya watu.

Sishangai kukuona unahangaika na kuwa katika hali ya kutotosheka
na niliyoandika.

Hauko peke yako katika hili.
Mwalimu wangu Prof. Haroub Othman yeye alikwenda mbali zaidi.

Prof. Haroub alimkabili Mwalimu Nyerere uso kwa macho kutaka
kusikia kutoka kinywani kwake ukweli katika yale niliyoandika.

Je ungependa kujua jibu la Mwalimu Nyerere?
Naam, sheikh napenda sana kujua. Ila bado naufikirisha sana ubongo wangu. Je, yumkini Abdulwahid Sykes aliogopa kilichompata mtu aliyemtaka awe Rais wa TANU Bwana David Kidaha Makwaia? Zote ni speculation ila ni vyema kujua kwa kuwa hizi ni zama za kutaka kujua zaidi.
 
Back
Top Bottom