Tetesi: Handeni, walioiba silaha Ofisi za TAKUKURU ni TAKUKURU wenyewe

Tetesi: Handeni, walioiba silaha Ofisi za TAKUKURU ni TAKUKURU wenyewe

Kinoamiguu

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2018
Posts
11,936
Reaction score
15,196
Habari za mapumziko,

Inasemekana walioiba Silaha kwenye ofisi za TAKUKURU huko Handeni ni maafisa TAKUKURU wenyewe.

Chanzo chetu kutoka Handeni kinasema maafisa hao wakishirikiana na watu wa ishu/Majambazi walisuka njama za kuziiba silaha hizo huku wakiahidiwa kupewa donge nono.

Inasemekana siku ya tukio washukiwa walikuwa wote kwenye baa moja maarufu wilayani hapo wakikamilisha mpango huo.

Mnyetishaji wetu anasema hakukuwa na uvunjifu wowote na kutupwa kwa funguo ni geresha iliyopangwa na maafisa hao ili kuonesha kwamba walikuwa ni majambazi.

silaha hizo zilisafirishwa usiku na kupelekwa mkoa mmoja huko kaskazini mwa nchi ambako kuna ujambazi mwingi.

Tunazishauri mamlaka zinazohusika ziwabane MAAFISA TAKUKURU Ili wakaoneshe silaha zilipo kwani wao ndiyo wahusika kwenye mpango huu.

Nawasilisha
 
Njaa kali sana madili ya kubambikia watu kesi hakuna..bora waibe silaha wakauze tu.

Nchi yenyewe ishapoteza mwelekeo.

#MaendeleoHayanaChama
 
We umejuaje kama zilipelekwa usiku mkoa wa kaskazini mwa nchi.
 
Mwanza au kagera? Hii mikoa mbona haina ujambazi mwingi! Mtoa mada mshamba sana
Hiyo ni mikoa ya kanda ya ziwa,

Mikoa ya kaskazini ni arusha, manyara, kilimanjaro na tanga

Kanda ya kati kuna singida dodoma nazani na tabora

Kanda ya mashariki kuna pwani dsm na morogoro

Kanda ya kusini kuna lindi mtwara na ruvuma

Kanda yanyanda za juu kusini kuna iringa njombe mbeya na songwe

Kanda ya magharibi au ziwa tanganyika ni kigoma na rukwa na katavi

KAnda ya ziwa ni shinyanga simiyu mara geita mwanza na kagera
 
Mtoa thread tuseme hii taarifa imetoka chanzo kamili au nawe unataka kujua watu watajadili nn? Tuanzie hapo
 
Hiyo ni mikoa ya kanda ya ziwa,

Mikoa ya kaskazini ni arusha, manyara, kilimanjaro na tanga

Kanda ya kati kuna singida dodoma nazani na tabora

Kanda ya mashariki kuna pwani dsm na morogoro

Kanda ya kusini kuna lindi mtwara na ruvuma

Kanda yanyanda za juu kusini kuna iringa njombe mbeya na songwe

Kanda ya magharibi au ziwa tanganyika ni kigoma na rukwa na katavi

KAnda ya ziwa ni shinyanga simiyu mara geita mwanza na kagera
Hebu tuelezee mwenzetu katika pande za dunia lini hii kanda ya ziwa imeanza kutumika?
 
Hiyo ni mikoa ya kanda ya ziwa,

Mikoa ya kaskazini ni arusha, manyara, kilimanjaro na tanga

Kanda ya kati kuna singida dodoma nazani na tabora

Kanda ya mashariki kuna pwani dsm na morogoro

Kanda ya kusini kuna lindi mtwara na ruvuma

Kanda yanyanda za juu kusini kuna iringa njombe mbeya na songwe

Kanda ya magharibi au ziwa tanganyika ni kigoma na rukwa na katavi

KAnda ya ziwa ni shinyanga simiyu mara geita mwanza na kagera
Umesoma jiografia mkuu? Kusini, Kaskazini, Mashabiki na Magharibi, haya hiyo Kanda ya ziwa iko wapi kwenye hizo nne?
 
Back
Top Bottom