Hannibal Barca: Jenerali bora wa wakati wote kutoka Africa

Hannibal Barca: Jenerali bora wa wakati wote kutoka Africa

zitto junior

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2013
Posts
20,537
Reaction score
31,729
Habari za asbuhi wana jukwaa bila kupoteza muda embu twende moja kwa moja kwenye mada
images (31).jpg


MWANZO
Hannibal barca alizaliwa mnamo mwaka 247 BC... alikua jenerali wa jeshi la CARTHAGE yaani Tunisia ya leo na alipata umaarufu hasa kwenye vita vyake dhidi ya dola ya kirumi na mataifa mengine makubwa ya ulaya kwa wakati huo zilizofahamika kama PUNIC WARS
images (32).jpg

Jenerali huyu Alitoka afrika na kuweza kuvamia bara la ulaya kupitia Iberia yaani ureno na spain akiwatandika wote waliomzuia njiani kwa kutumia mbinu za kimedani bora zaidi kuwahi kushuhudiwa wakati ule.... Na umaarufu ulipanda zaidi alipovamia ITALIA kwenye moyo kabisa wa dola la kirumi na kushinda vita tatu muhimu dhidi ya dola hiyo kwenye miji ya trebia,trasimene na cannae. Nguvu zake ziliweza kuitia hofu dola hii kiasi walikuwa wakisikia jina lake wanatetemeka!!!

Katika moja ya vita kubwa kabisa ni vita ya cannae ambayo kihistoria ndio vita ambavyo Dola ya kirumi ilipoteza wanajeshi wengi zaidi kati historia ambapo wanajeshi elfu 80 walifia hapo huku masenator 80 wakichinjwa.... Kibaya zaidi alilizunguka jeshi zima la Rumi hivyo hakuna masalia waliopona na tokea hapo jeshi la Rumi liliogopa kupigana vita ya uso kwa uso na Hannibal Barca

Hannibal Barca Aliendelea kuitawala italia kwa miaka 15 lakini jambo ambalo mimi najiuliza mpaka leo na nimekosa majibu ni kwanini General Hannibal Barca aliyeogopeka dunia nzima ya kale aliwatandika warumi kwenye vita zote alizokutana nao ila alisita kuvamia Rome?? Je nini kilimzuia asivamie?? Aliogopa nini??

MBINU ZAKE VITANI
A005002.jpg

Hannibal anafahamika zaidi kwa kutumia tembo kwenye uwanja wa vita.... Alikuwa anatumia tembo mkubwa wa jamii ya syria ambao kwa sasa wametoweka hivyo ukubwa wake ulikuwa ni kama vifaru vya kijeshi vya sasa..... Aliwatanguliza mbele tembo kama 80 kiasi kwamba mpaka mnamalizana na tembo mnakuta mshazingirwa na kupewa kipigo cha mbwa mwizi

MWISHO WAKE
Baada ya kupata taarifa kuwa nchini mwake wamevamiwa ikabidi arudi kuokoa jahazi na kufikia muda huo mbinu zake za medani zilikwisha somwa vizuri na jenerali scipio Africanus wa dola ya Rumi ambaye alitaka kulipa kisasi baada ya Hannibal kumjeruhi vibaya baba yake kwenye ile vita ya trebia hivyo akampiga hannibal huko mjini ZAMA nchini Carthage (Tunisia) na baada ya hapo Hannibal Barca aliranda randa sana ulaya na mwishowe alisalitiwa na kurudishwa kwa warumi ila aliamua kujiua kwa kunywa sumu ili kuepuka dhahama ya kuangukia mikononi mwa maadui zake.

HITIMISHO
Jenerali huyu anatazamiwa kuwa mwanajeshi bora kuwahi tokea katika historia za kijeshi hapa duniani ila swali nalotaka mnisaidie great thinkers je ni kwanini General Hannibal pamoja na kuwatandika dola ya rumi huko italia aliogopa kuvamia roma ambayo ingeifuta rasmi dola ya kirumi kwenye uso wa dunia????

Naomba kuwasilisha
images (30).jpg
 
Asante kwa mada nzuri...kuna kitu kikubwa nimegundua kuna maarifa mengi hatufundishwi ....hasa maarifa yanaipa Afrika na watu wake utukufu
Sana mkuu hata huyu Hannibal alikuwa mixture ya Phoenicia na Nubia yaani sudan ya sasa ila wazungu huwa wanadai alikuwa mzungu mwenzao mpaka pale ushahidi huu ulipokuja kuwaumbua....
Screenshot_2018-07-08-14-10-20-1.png


mtu chake
 
Sana mkuu hata huyu Hannibal alikuwa mixture ya Phoenicia na Nubia yaani sudan ya sasa ila wazungu huwa wanadai alikuwa mzungu mwenzao mpaka pale ushahidi huu ulipokuja kuwaumbua....
View attachment 805753
Hawa wanubi wana historia kubwa na dunia hii..kuna mahali tulikengeuka na kuwaachia wazungu watuandikie ya kwetu
 
Mkuu asante kwa hoja nzuri na yenye kuchangamsha akili. Lakini kama kawaida yangu mimi nitakupa majibu kwa kutumia kitabu pendwa nikipendacho kuliko vyote, yaani "BIBLIA"; kitabu hichi kina majibu yote ya swali ulilouliza ingawa watu wengi wanakidharau.

Iko hivi utawala wa Rumi ni moja kati ya tawala tano kubwa zilizotabariwa au kuruhusiwa na MUNGU kuwepo hapa duniani, rejea kitabu cha DANIEL 2:36-44 ambapo utaona Danieli anamfafanulia Mfalme Nebukadreza ile ndoto yake ya sanamu kubwa. Katika ile ndoto, sehemu moja ya ile sanamu ilikuwa ni Ufalme wa Rumi, yaani ile miguu ya chuma.

Nebukadreza.jpg

Sanamu hii ndiyo ndoto aliyoota Mfalme Nebukadreza na tafsiri yake.
Sasa basi kwa kuwa Ufalme wa Rumi ulikuwa umeshatabiliwa na MUNGU kuwa utatawala dunia yote kwa wakati ulioamuriwa, isengekuwa rahisi kwa General Hannibal pamoja na jeshi lake kuivamia Roma na kuuangusha Ufalme wa Rumi. Fahamu kwamba nyuma ya hizi falme kubwa huwa kuna nguvu ya ajabu inayoziongoza, nguvu hiyo inaweza ikawa imetoka kwa MUNGU au inaweza ikawa imetoka kwa yule Mwovu Lusifer Ibilisi.

Kwa Ufalme wa Rumi, hata kama ulitabiriwa na MUNGU, lakini nguvu yake ilikuwa inatokana na Lusifer Ibilisi; rejea kitabu cha UFUNUO 13:1-2 .........yule joka(Lusifer) akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi(Ufalme) na uwezo mwingi(Nguvu za kijeshi). Hivyo basi kutokana na nguvu alizopewa Rumi, isingekuwa rahisi kwa General Hanniba kuivamia Rumi na kuindoa kwenye utawala wa dunia.

Utaona kwamba hata baada ya kifo cha General Hannibal bado utawala wa Rumi uliendelea kuwepo kwa miaka zaidi ya elfu moja. Isitoshe Hannibal Barca yeye na utawala wake hawakutabiriwa kuitawala dunia hata kama walikuwa na nguvu kiasi gani.

Mkuu zitto junior kitabu hichi BIBLIA kina majibu yote, hata kama utaamini au hautaamini, lakini UKWELI ndiyo huo.
 
Mkuu asante kwa hoja nzuri na yenye kuchangamsha akili. Lakini kama kawaida yangu mimi nitakupa majibu kwa kutumia kitabu pendwa nikipendacho kuliko vyote, yaani "BIBLIA"; kitabu hichi kina majibu yote ya swali ulilouliza ingawa watu wengi wanakidharau.

Iko hivi utawala wa Rumi ni moja kati ya tawala tano kubwa zilizotabariwa au kuruhusiwa na MUNGU kuwepo hapa duniani, rejea kitabu cha DANIEL 2:36-44 ambapo utaona Danieli anamfafanulia Mfalme Nebukadreza ile ndoto yake ya sanamu kubwa. Katika ile ndoto, sehemu moja ya ile sanamu ilikuwa ni Ufalme wa Rumi, yaani ile miguu ya chuma.

View attachment 805760
Sanamu hii ndiyo ndoto aliyoota Mfalme Nebukadreza na tafsiri yake.
Sasa basi kwa kuwa Ufalme wa Rumi ulikuwa umeshatabiliwa na MUNGU kuwa utatawala dunia yote kwa wakati ulioamuriwa, isengekuwa rahisi kwa General Hannibal pamoja na jeshi lake kuivamia Roma na kuuangusha Ufalme wa Rumi. Fahamu kwamba nyuma ya hizi falme kubwa huwa kuna nguvu ya ajabu inayoziongoza, nguvu hiyo inaweza ikawa imetoka kwa MUNGU au inaweza ikawa imetoka kwa yule Mwovu Lusifer Ibilisi.

Kwa Ufalme wa Rumi, hata kama ulitabiriwa na MUNGU, lakini nguvu yake ilikuwa inatokana na Lusifer Ibilisi; rejea kitabu cha UFUNUO 13:1-2 .........yule joka(Lusifer) akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi(Ufalme) na uwezo mwingi(Nguvu za kijeshi). Hivyo basi kutokana na nguvu alizopewa Rumi, isingekuwa rahisi kwa General Hanniba kuivamia Rumi na kuindoa kwenye utawala wa dunia.

Utaona kwamba hata baada ya kifo cha General Hannibal bado utawala wa Rumi uliendelea kuwepo kwa miaka zaidi ya elfu moja. Isitoshe Hannibal Barca yeye na utawala wake hawakutabiriwa kuitawala dunia hata kama walikuwa na nguvu kiasi gani.

Mkuu zitto junior kitabu hichi BIBLIA kina majibu yote, hata kama utaamini au hautaamini, lakini UKWELI ndiyo huo.
Aseee hii nondo imeshiba sana ubarikiwe mkuu nmejifunza kitu kipya hapa na nikiri tu sikuwa nimefahamu biblia ilitabiri ujio wa dola ya kirumi asante kwa kunifumbua macho.....
 
Karthago walikuwa wanampango wa kuvamia na kufika Roma tangu kwenye vita ya kwanza (The First Punic War) na walipiga sana Sicily lakini katikati ya vita (The Siege of Syracuse) walikumbwa na ugonjwa wa ndui (Smallpox) na wakafaraiki sana. Ndiyo safari ya Karthago kwenda Roma iliishia hapo, lakini bila hivyo leo tungekuwa na historia nyingine kabisa.
 
Mkuu asante kwa hoja nzuri na yenye kuchangamsha akili. Lakini kama kawaida yangu mimi nitakupa majibu kwa kutumia kitabu pendwa nikipendacho kuliko vyote, yaani "BIBLIA"; kitabu hichi kina majibu yote ya swali ulilouliza ingawa watu wengi wanakidharau.

Iko hivi utawala wa Rumi ni moja kati ya tawala tano kubwa zilizotabariwa au kuruhusiwa na MUNGU kuwepo hapa duniani, rejea kitabu cha DANIEL 2:36-44 ambapo utaona Danieli anamfafanulia Mfalme Nebukadreza ile ndoto yake ya sanamu kubwa. Katika ile ndoto, sehemu moja ya ile sanamu ilikuwa ni Ufalme wa Rumi, yaani ile miguu ya chuma.

View attachment 805760
Sanamu hii ndiyo ndoto aliyoota Mfalme Nebukadreza na tafsiri yake.
Sasa basi kwa kuwa Ufalme wa Rumi ulikuwa umeshatabiliwa na MUNGU kuwa utatawala dunia yote kwa wakati ulioamuriwa, isengekuwa rahisi kwa General Hannibal pamoja na jeshi lake kuivamia Roma na kuuangusha Ufalme wa Rumi. Fahamu kwamba nyuma ya hizi falme kubwa huwa kuna nguvu ya ajabu inayoziongoza, nguvu hiyo inaweza ikawa imetoka kwa MUNGU au inaweza ikawa imetoka kwa yule Mwovu Lusifer Ibilisi.

Kwa Ufalme wa Rumi, hata kama ulitabiriwa na MUNGU, lakini nguvu yake ilikuwa inatokana na Lusifer Ibilisi; rejea kitabu cha UFUNUO 13:1-2 .........yule joka(Lusifer) akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi(Ufalme) na uwezo mwingi(Nguvu za kijeshi). Hivyo basi kutokana na nguvu alizopewa Rumi, isingekuwa rahisi kwa General Hanniba kuivamia Rumi na kuindoa kwenye utawala wa dunia.

Utaona kwamba hata baada ya kifo cha General Hannibal bado utawala wa Rumi uliendelea kuwepo kwa miaka zaidi ya elfu moja. Isitoshe Hannibal Barca yeye na utawala wake hawakutabiriwa kuitawala dunia hata kama walikuwa na nguvu kiasi gani.

Mkuu zitto junior kitabu hichi BIBLIA kina majibu yote, hata kama utaamini au hautaamini, lakini UKWELI ndiyo huo.
Huwa napata jibu moja tu mtu anaposema hakuna Mungu na anapojitahidi kwa hoja dhaifu kubisha kwa nguvu sana, kwangu hawa nawaona ni waamini waliokengeuka na ambao vitu kama hivi hawajawahi kuvisoma ama la walisoma lakini hawakuelewa
 
Karthago walikuwa wanampango wa kuvamia Roma tangu kwenye vita ya kwanza (The First Punic War) na walipiga sana Sicily lakini katikati ya vita (The Siege of Syracuse) walikumbwa na ugonjwa wa ndui (Smallpox) na wakafaraiki sana. Ndiyo safari ya Karthago kwenda Roma iliishia hapo, lakini bila hivyo leo tungekuwa na historia nyingine kabisa.
Aseee kwahyo ugonjwa ndio ulizuia wasisogee basi dunia haiko fair mbona kwenye campaign ya kwanza kupitia alps alipoteza karibu nusu ya jeshi walivuka mito ambayo wengi walizama ila hakukata tamaa na aliweza kuwatandika warumi huko kaskazini sasa iweje hapa ndio akate tamaa kirahisi sana ....... Dah rome ina mambo kwakweli nikifikiria huyu na huko baadae ottoman kushindwa kuivamia naweza amini huu ufalme ulikuwa una nguvu nyingine kwa nyuma
 
Mkuu asante kwa hoja nzuri na yenye kuchangamsha akili. Lakini kama kawaida yangu mimi nitakupa majibu kwa kutumia kitabu pendwa nikipendacho kuliko vyote, yaani "BIBLIA"; kitabu hichi kina majibu yote ya swali ulilouliza ingawa watu wengi wanakidharau.

Mkuu zitto junior kitabu hichi BIBLIA kina majibu yote, hata kama utaamini au hautaamini, lakini UKWELI ndiyo huo.

Ukisoma historia za Wayahudi wanaseme Alexander Mkuu wa Ugiriki baada ya kuvamia Yerusalemu alikutana na makuhani waliomsihi sana asiwaue bali na watakubali kumtumikia. Kuhani Yadua alimpeleka hekaluni na kumwonesha maandiko ya Nabii Danieli yaliyozungumzia kwamba kuna mfalme atakuja kuuangusha ufalme wa Umedi na Uajemi. Alaxander akajua ndiyo yeye na akatoa sadaka ya kuteketeza na akaenda kumvamia Dario na ndiyo ukawa mwisho wa hadithi ya Umedi na Uajemi.

NB: Tuyaache haya tujikite kwenye utafiti wa anthropolojia zaidi.
 
Aseee kwahyo ugonjwa ndio ulizuia wasisogee basi dunia haiko fair mbona kwenye campaign ya kwanza kupitia alps alipoteza karibu nusu ya jeshi walivuka mito ambayo wengi walizama ila hakukata tamaa na aliweza kuwatandika warumi huko kaskazini sasa iweje hapa ndio akate tamaa kirahisi sana ....... Dah rome ina mambo kwakweli nikifikiria huyu na huko baadae ottoman kushindwa kuivamia naweza amini huu ufalme ulikuwa una nguvu nyingine kwa nyuma


"In 395 B.C Carthage had sent its military forces to the Island of Sicily to attack the city of Syracuse. During the Siege, many soldiers in the Carthaginian army fell ill, covered with pustules and many died, forcing the army to retreat" - Diseases and Human Evolution, by Ethne Barnes, pg 228.

 
Mungu Ni Mwema Wakati Wote
Safari Ya Kuyajua Yaliyofichwa Na Ukweli Wake
Hakuna Shaka Bado Ni Ndefu Sana

Yaani Kuna Watu Wengi Sana Weusi Toka Africa
Habari Zao Zimekuwa Kwenye Kificho Sana
Mkuu Zito Junior Bila Shaka
Hii Thread Ni Madini Mengine Zaidi Ya Tanzanite

Basi Yale Magazine Ya Udaku Tafadhali
Mkija Mje Kwa Staha
 
Back
Top Bottom