Hannibal Barca: Jenerali bora wa wakati wote kutoka Africa

Hannibal Barca: Jenerali bora wa wakati wote kutoka Africa

Karthago walikuwa wanampango wa kuvamia Roma tangu kwenye vita ya kwanza (The First Punic War) na walipiga sana Sicily lakini katikati ya vita (The Siege of Syracuse) walikumbwa na ugonjwa wa ndui (Smallpox) na wakafaraiki sana. Ndiyo safari ya Karthago kwenda Roma iliishia hapo, lakini bila hivyo leo tungekuwa na historia nyingine kabisa.
Warumi walikuwa wajanja sana na Vita yao Barca ilianzia kwa Barca(baba wa Hannibal)

Ushushushu haukuanza leo na udhaifu mkubwa waligundua upo kwa familia yake hivyo bada ya kuwazidi kete kule Alps wao wakatawanya majeshi kurudi kwao na Hannibal...............

Ila mke pia alimponza maana kibaraka wake mmoja alikuwa ni pandikizi la Rome...

Bila shaka ujasusi wa warumi uliwasaidia zaidi kuliko historia ya utabiri wa nguvu zao
 
Huwa napata jibu moja tu mtu anaposema hakuna Mungu na anapojitahidi kwa hoja dhaifu kubisha kwa nguvu sana, kwangu hawa nawaona ni waamini waliokengeuka na ambao vitu kama hivi hawajawahi kuvisoma ama la walisoma lakini hawakuelewa
Kabisa mkuu Mshana Jr wengi wanataka mpaka wamuone MUNGU kwa macho yao ndiyo waamini, kumbe hata bila kumuona kwa macho matendo yake makuu yanajitosheleza.
 
Warumi walikuwa wajanja sana na Vita yao Barca ilianzia kwa Barca(baba wa Hannibal)

Ushushushu haukuanza leo na udhaifu mkubwa waligundua upo kwa familia yake hivyo bada ya kuwazidi kete kule Alps wao wakatawanya majeshi kurudi kwao na Hannibal...............

Ila mke pia alimponza maana kibaraka wake mmoja alikuwa ni pandikizi la Rome...

Bila shaka ujasusi wa warumi uliwasaidia zaidi kuliko historia ya utabiri wa nguvu zao

Warumi walikuwa wako vizuri kwasababu ilikuwa ni jamii iliyowekeza sana kwenye kujifunza hata kutoka kwa maadui zao pale ilipowabidi. Intelijensia ya Karthago ilikuwa na nguvu kuliko ile ya Roma kwasababu Hannibal pamoja na jeshi lake dogo aliweza kupigana ndani ya nchi isiyo yake dhidi ya jeshi kubwa zaidi lenye uzoefu wa vita (Huu ni uthibitisho tosha kabisa). Ile vita Roma alishinda baada ya Scipio Africanus kutumia mbinu za Hannibal mwenyewe kumpigia, kuanzia kwenye mikakati ya kivita (War Strategy) na mbinu za kijasusi (Methods of Strategic Espionage)

Kabla ya kuvamia Roma alituma majasusi kwenye makabila ambayo ni maadui wa Roma na wakayapanga kabisa kwamba watakapovamia hayo makabila yafanye nini. Wanasema alituma majasusi kwenye kambi za Roma na hadi Roma kabisa, walijifunza hadi lugha ngeni za kilatini. Sasa wakati wako Roma hawa majamaa walifundishwa kutengeneza nakala feki (Forging of documents), kuandika maneno ya siri (coding), kuwafuatilia maadui na mwenendo wa jeshi (Surveillance and Reconnaissance) na kutuma ujumbe wa siri.

Baba yake Hannibal na wengine ndiyo walifanikiwa kutoa ubashiri kwamba siku moja Roma lazima atakuja kuwa adui yao kwasababu amevamia (Sicily) sehemu ambayo walikuwa wanaitegemea kimkakati. Wanasema alikuwa anatumia maneno ya siri (Codes) ambayo aliaandika kwenye vijini vya mwanzi na kumtumia Hannibal. Kule Roma kuna majasusi waliwahi kukamatwa wakakatwa mikono na warumi ili kutuma ujumbe. Warumi ndiyo wakajua kwamba wasipobadilisha mkakati itakula kwao. Maana kuna mchezo walichezewa na Hannibal kwenye vita ya ziwa Trasimene (The Battle of Lake Trasimene), ambapo wanajeshi wa Roma walifuatiliwa na Hannibal na walivyofika hilo eneo Hannibal aliwasha vijinga vya moto kwenye msitu wakati wa Usiku na Roma wakajua kwamba jeshi limepumzika pale basi wawavamie (They were dead wrong, na walikufa wanajeshi 15,000 kwa mpigo na wengine kama 10000 kufanywa mateka)

Warumi walikuja na michezo michafu sana, wakawa wanachanganya diplomasia, ujasusi na propaganda huku wanamsoma tu Hannibal. Walienda kwenye kambi yake kama mabalozi wa amani wakiwa na watumwa waliowasindikiza, kumbe wale watumwa ni wanajeshi. Ilifika hadi kipindi ili kuwadanganya Waroma ilibidi wale watumwa wachapwe viboko na wale mabalozi wa kirumi. Basi wale watumwa wakawa wanazunguka kwenye ile kambi na Wakarthago wakihisi kwamba wale ni wanajeshi kumbe wanachora ramani ya kambi. Usiku ulipofika Scipio Africanus akaanzisha moto kwenye kambi wakarthago wakatoka nje bila silaha wakihisi kwamba ni moto wa kawaida na hamna kitu kutokana na yale mazungumzo ya amani yalikuwa yakiendelea na walijua Roma kashashindwa. Kutoka huko wakachinjwa kweli kweli.

NB 1: Huko Roma nako vita vya kipropaganda vilipigwa sana vikiongozwa na Bwana Marcus Porcius Cato au Cato the Elder. Huyu ndiyo alitumia mchezo kama ule wa Joseph Goebbels (Waziri wa Propaganda wa Hitler) kwamba "If you repeat saying a lie on regular basis it becomes the truth". Jamaa alikuwa akiongea chochote kile hata kwenye Bunge lazima amalizie na kusema "Furthermore, i consider that Carthage must be destroyed". Sasa ikafika kipindi huko Roma watu hata wakisalimiana "Habari za asubuhi" lazima wamalizie kwa kusema "Karthago lazima iangamizwe". Walicheza huu mchezo ikafika kipindi Roma nzima walikuwa wakawa wanaamini kwamba "Karthago ikiwepo basi hakuna Roma"

NB 2: Warumi walikuwa wakilipiga jeshi lolote lile lenye nguvu, basi wanawaacha baadhi ya wanajeshi wa adui zake ili wajifunze mbinu zao za kivita. Hivyo baada ya Punic Wars, Warumi walitoka na utaalamu mzito sana kijeshi na Kijasusi. Japo kushinda hii vita kwa Warumi kulichangiwa sana na Hannibal kutotaka ushauri kutoka kwa wanajeshi wake. Ambao wengine walisema kwamba umeipiga Roma basi utumie ushindi wako vizuri na usivamie Roma kwa kipindi hiki mpaka uje na mkakati mwingine.
 
Warumi walikuwa wako vizuri kwasababu ilikuwa ni jamii iliyowekeza sana kwenye kujifunza hata kutoka kwa maadui zao pale ilipowabidi. Intelijensia ya Karthago ilikuwa na nguvu kuliko ile ya Roma kwasababu Hannibal pamoja na jeshi lake dogo aliweza kupigana ndani ya nchi isiyo yake dhidi ya jeshi kubwa zaidi lenye uzoefu wa vita (Huu ni uthibitisho tosha kabisa). Ile vita Roma alishinda baada ya Scipio Africanus kutumia mbinu za Hannibal mwenyewe kumpigia, kuanzia kwenye mikakati ya kivita (War Strategy) na mbinu za kijasusi (Methods of Strategic Espionage)

Kabla ya kuvamia Roma alituma majasusi kwenye makabila ambayo ni maadui wa Roma na wakayapanga kabisa kwamba watakapovamia hayo makabila yafanye nini. Wanasema alituma majasusi kwenye kambi za Roma na hadi Roma kabisa, walijifunza hadi lugha ngeni za kilatini. Sasa wakati wako Roma hawa majamaa walifundishwa kutengeneza nakala feki (Forging of documents), kuandika maneno ya siri (coding), kuwafuatilia maadui na mwenendo wa jeshi (Surveillance and Reconnaissance) na kutuma ujumbe wa siri.

Baba yake Hannibal na wengine ndiyo walifanikiwa kutoa ubashiri kwamba siku moja Roma lazima atakuja kuwa adui yao kwasababu amevamia (Sicily) sehemu ambayo walikuwa wanaitegemea kimkakati. Wanasema alikuwa anatumia maneno ya siri (Codes) ambayo aliaandika kwenye vijini vya mwanzi na kumtumia Hannibal. Kule Roma kuna majasusi waliwahi kukamatwa wakakatwa mikono na warumi ili kutuma ujumbe. Warumi ndiyo wakajua kwamba wasipobadilisha mkakati itakula kwao. Maana kuna mchezo walichezewa na Hannibal kwenye vita ya ziwa Trasimene (The Battle of Lake Trasimene), ambapo wanajeshi wa Roma walifuatiliwa na Hannibal na walivyofika hilo eneo Hannibal aliwasha vijinga vya moto kwenye msitu wakati wa Usiku na Roma wakajua kwamba jeshi limepumzika pale basi wawavamie (They were dead wrong, na walikufa wanajeshi 15,000 kwa mpigo na wengine kama 10000 kufanywa mateka)

Warumi walikuja na michezo michafu sana, wakawa wanachanganya diplomasia, ujasusi na propaganda huku wanamsoma tu Hannibal. Walienda kwenye kambi yake kama mabalozi wa amani wakiwa na watumwa waliowasindikiza, kumbe wale watumwa ni wanajeshi. Ilifika hadi kipindi ili kuwadanganya Waroma ilibidi wale watumwa wachapwe viboko na wale mabalozi wa kirumi. Basi wale watumwa wakawa wanazunguka kwenye ile kambi na Wakarthago wakihisi kwamba wale ni wanajeshi kumbe wanachora ramani ya kambi. Usiku ulipofika Scipio Africanus akaanzisha moto kwenye kambi wakarthago wakatoka nje bila silaha wakihisi kwamba ni moto wa kawaida na hamna kitu kutokana na yale mazungumzo ya amani yalikuwa yakiendelea na walijua Roma kashashindwa. Kutoka huko wakachinjwa kweli kweli.

NB 1: Huko Roma nako vita vya kipropaganda vilipigwa sana vikiongozwa na Bwana Marcus Porcius Cato au Cato the Elder. Huyu ndiyo alitumia mchezo kama ule wa Joseph Goebbels (Waziri wa Propaganda wa Hitler) kwamba "If you repeat saying a lie on regular basis it becomes the truth". Jamaa alikuwa akiongea chochote kile hata kwenye Bunge lazima amalizie na kusema "Furthermore, i consider that Carthage must be destroyed". Sasa ikafika kipindi huko Roma watu hata wakisalimiana "Habari za asubuhi" lazima wamalizie kwa kusema "Karthago lazima iangamizwe". Walicheza huu mchezo ikafika kipindi Roma nzima walikuwa wakawa wanaamini kwamba "Karthago ikiwepo basi hakuna Roma"

NB 2: Warumi walikuwa wakilipiga jeshi lolote lile lenye nguvu, basi wanawaacha baadhi ya wanajeshi wa adui zake ili wajifunze mbinu zao za kivita. Hivyo baada ya Punic Wars, Warumi walitoka na utaalamu mzito sana kijeshi na Kijasusi. Japo kushinda hii vita kwa Warumi kulichangiwa sana na Hannibal kutotaka ushauri kutoka kwa wanajeshi wake. Ambao wengine walisema kwamba umeipiga Roma basi utumie ushindi wako vizuri na usivamie Roma kwa kipindi hiki mpaka uje na mkakati mwingine.
Tangu mwanzo ilikuwa ni lazima Warumi washinde kwa sababu hii ilikuwa ni vita ya kiutawala(kila mmoja alitaka kuitawala dunia na ukumbuke ya kuwa kipindi cha uimara wa Carthage adui yake mkubwa alikuwa ni lile kabila la matambiko mengi la Waetruria ambao walikuwa wamejijegea utawala karibu Africa yote lakini kuibuka kwa wakathaga kukawapoteza kabisa na wakabaki na kinyongo huku jamii zile zikitawanyika na kupotea katika historia ya utawala.

Wakathaga walikuwapo miaka 60 kabla ya dola ya Warumi kujitokeza na baada ya warumi kuwako nao wakatak kujiweka fiti kwa kumpiga Hamilcar Barca na kuichukua Sicily na hapo warumi hawakuwa wazembe wakaendelea kujipanga na kuweka ushushu kila pahali kwa kuwa waliamini Wakathaga watarudi na kweli kule Spain Hamilcar akajenga tena ngome upya ikawa ni Spain na North Africa viko chini yake

Kuibuka kwa Hannibal kukaja na kuibuka kwa mzee wa proganda Spicio.

Lakini kwa nini nasema lazima ilikuwa ishinde Roma kwa sababu mbinu za kuiga za kutumia ushushushu wa ndani ya adui uliwasaidia sana na hapo ndipo wakaamua kumtumia mke wa Hannibal kama njia yao

Imilce (mke wa Hannibal) alikuwa anatokea kwenye jamii za Etruria kwenye kabila la Iberia na alikuwa ni Eberian princess na alioolewa tu ule utawala wa baba yake ukaangushwa na kuwa chini ya Hannibal (Hii ni North Africa)jamii ile ikazidi kuwa na chuki zaidi lakini pia propaganda za Quinter Fabius Maximus kuitwa dikteta na wenzie ama wananchi wake na kuzua chuki ya kuigiza hivyo wa Rome wengi wakawa wanaenda kuishi kwa Wakathaga na wengine kujiunga na jeshi la Hannibal (hilo ni kosa analojutia had leo huko kaburini)

Na alivyowapiga kupitia milima ya Alps nadhani Scipio aliwaachia Rome kisha Trebia na Trasnene ila ni kimkakati na hiyo ni baada ya taarifa kutoka upande wa mke wa Hannibal kuthibitika ya kuwa watu wa Iberian na Etruria kiujumla hawapo upande wa Hannibal hivyo akakimbia na kuja kuanzisha propaganda nyingine ndani ya jamii za North Africa Adui wa wakathaga na alifanikiwa maana alitengeneza jeshi kubwa

Lakini pia kwa njia hiyo ilikuwa ni lazima ashinde kwa sababu Hannibal aliwekeza nguvu Spain na huku kwao Africa akaweka mtawala ambae alikuwa ni shemeji yake(mme wa mdogo wa Hannibal) aliitwa Hasdrubal
Hasdrubal hakuwa na nguvu ndio maana Scipio alimpiga ahsubuh na mapema na Hannibal alipopata habari akarudi kwao kusaidia na Scipio akakutana nae kwenye ile vita waliita BATTLE OF ZAMA
hapo ndipo Hannibal akagundua kosa lake la kuwachukua waroma kama jeshi lake wakamgeuka na kumpiga vibaya sana na akakimbilia Ephesus (uturuki ya leo)
Huko akapewa cheo cha ushauri wa kijeshi

Hapa ndipo mpanga propaganda zote CATO THE ELDER akiwa hoi kitandani akasema KATHAGO LAZIMA IANGAMIZWE"na hapo ndipo jiji la Wakathago likavamiwa na kuharibiwa kabisa na raia wake kujiua wengine kutekwa na Hannibal akatafutwa huko uturuki na Ugiriki ya Leo nae akajiua

So tukihitimisha utaona kabisa kwa akili nyingi walizotumia Warumi ilikuwa lazima washinde na kumaliza mzizi wa fitina kizazi cha wakathago kikapigwa kwa nia ya kuangamizwa hii ni sababu iliofanya ushindani wa kimamlaka ufe kabisa maana pengine wangeachwa ingelikuwa ni Vita kila kukicha.

Baada ya miongo miwili ndo akaja mtu kutoka Rome aliitwa Yurio Kaiser akalifufua jiji lile na kueneza ukristo lakini kwa kuogopa kuinuka tena kwa Wakathago Waroma wakauharibu kabisa mji ule hadi leo ni migofu tu imetamalaki na watalii haweindi kwa sana kwa sababu hamna cha kujifunza mle

Maana hata yule mungu wao waliemwita Baali alivunjwa na Yurio Kaiser
 
Baada ya miongo miwili ndo akaja mtu kutoka Rome aliitwa Yurio Kaiser akalifufua jiji lile na kueneza ukristo lakini kwa kuogopa kuinuka tena kwa Wakathago Waroma wakauharibu kabisa mji ule hadi leo ni migofu tu imetamalaki na watalii haweindi kwa sana kwa sababu hamna cha kujifunza mle

Maana hata yule mungu wao waliemwita Baali alivunjwa na Yurio Kaiser

Marekebisho kidogo mkuu,
Julius Caesar hakueneza Ukrtisto Karthago kwasababu ameishi kipindi ambazo ukristo ulikuwa bado haujazaliwa duniani 100 BCE hadi 44BCE. Dola la Mroma kipindi hiki lilikuwa lina dini zile za kipagani amazo Wagiriki walikuwa nazo.
 
historia nzuri sana hii. Kingine huyu jamaa ili kuvamia Italy ilimbidi apite Iberia na kuiingilia Italy upande wa kaskazini kwenye milima ya Alps. Sasa Tembo wake ambao alikuwa akiwategemea sana jeshini wengi walikufa sababu ya baridi huko milimani. Hili lilimpunguzia sana nguvu. Ni sababu moja alishindwa kufika Roma.

Huyu jamaa alikuwa mfeonike ambayo leo ni Lebanon. Ni kweli unavyosema kuwa alicganganya na damu ya kinubi?
 
"Those who cannot remember the past are Doomed to repeat it''.
kuna maana sana ya kufunua hizi elimu.

Baba yake Hannibal Barca Hemircal Barca alishindwa vita vya kwanza na kulazimika kulipa kodi kwa utawala wa kirumi Talanta 440 kwa miaka kumi, mgogoro mwingine ulipotokea Sardinia Warumi walitangaza vita, baba yake akiwa kiongozi akaogopa na kuzuia vita akaahidi kuilipa dola ya kirumi kodi ya talanta 1200 zaidi huku akisalimisha na maeneo ya Sardinia na Corsica.

Huyu mzee alikuwa na watoto watatu wa kiume Hannibal, Hasdrubal na Mago. Mtoto wake Hannibal akiwa na miaka 9 aliapishwa mbele ya Madhabahu kiapo kwamba lazima aje alipize kisasi kwa hicho Rumi walichowafanyia.

Hapo unaweza kujifunza umuhimu wa mipango ya Muda mrefu. Na unaweza kuona siri ya mafanikio ni matokeo ya mipango tangu jemedali huyo akiwa kinda wa miaka 9.


Mzee huyu kumuandalia mazingira bora ya Ushindi baadae alivamia eneo la spain. akaweka kambi na kulifanya kuwa eneo lao la utawala. Akahamishia huko watoto wake watatu ili baade miaka mingi ijayo Mtoto wake aje alipe kisasi kutokea huko katika vita vya pili kati ya dola hilo na dola la kirumi. Ikumbukwe vita vya kwanza vilivyoendeshwa na baba walishindwa vibaya.
 
historia nzuri sana hii. Kingine huyu jamaa ili kuvamia Italy ilimbidi apite Iberia na kuiingilia Italy upande wa kaskazini kwenye milima ya Alps. Sasa Tembo wake ambao alikuwa akiwategemea sana jeshini wengi walikufa sababu ya baridi huko milimani. Hili lilimpunguzia sana nguvu. Ni sababu moja alishindwa kufika Roma.

Huyu jamaa alikuwa mfeonike ambayo leo ni Lebanon. Ni kweli unavyosema kuwa alicganganya na damu ya kinubi?
Yeah mkuu nilisoma paper credible kuhusu hiyo taarifa kuwa interaction ilikuwepo kati ya wafoenike wa kathago na numidia iliokuwa na watu weusi hata jeshi lake lilichukua mercenaries kutokea huko pia hta tembo wengi aliowatumia jamii yao ilitokea kwenye pembe ya afrika hivyo huyo mwanahistoria aliconclude kuwa katika hizo interaction ndipo muingiliano wa kindoa ulitokea na Hannibal akazaliwa akiwa mixture na hata History channel walienda mbali zaidi na kusema alikuwa pure dark skinned kwenye documentary yake waliweka a pure negroe to act as Hannibal barca na walichukua hayo kutoka kwa maandiko ya wasomi kadhaa credible wa kigiriki waliosema ''phoenicians were tall,dark skinned.....'' Ingawa bado ni taarifa inayohitaji utafiti zaidi
 
Mkuu zitto junior ahsante kwa mada nzuri. Nachoshindwaga kuelewa ni hizi vita zilizoandikwa kwenye bibilia zilivyokuwa zikipiganwa. Inavyoonekana kwa teknolojia ya wakati ule ilikuwa ni kutumia panga, rungu, Mikuki na mishale. Na ilikuwa ni vita ya kupigana ana kwa ana. Yaani hawa wanatoka huku na wale wanatokea kule na kuja kukutana katikati na kuanza kupigana mapanga na mashoka marungu nk.

Vita za aina hii ni za kipumbavu sana. Sijajua ni maslahi gani walikuwa wakiyataka au ni ubabe tu. Maana kwa kupigana kule vifo vilikuwa ni vingi sana na sijui population ya wakati huo ilikuwa vipi. Maandiko mengi kwenye biblia kwangu yanakuwaga magumu sana kuelewa naana kwa akili za kawaida unaona kama haiwezekani.
 
Mkuu zitto junior ahsante kwa mada nzuri. Nachoshindwaga kuelewa ni hizi vita zilizoandikwa kwenye bibilia zilivyokuwa zikipiganwa. Inavyoonekana kwa teknolojia ya wakati ule ilikuwa ni kutumia panga, rungu, Mikuki na mishale. Na ilikuwa ni vita ya kupigana ana kwa ana. Yaani hawa wanatoka huku na wale wanatokea kule na kuja kukutana katikati na kuanza kupigana mapanga na mashoka marungu nk.

Vita za aina hii ni za kipumbavu sana. Sijajua ni maslahi gani walikuwa wakiyataka au ni ubabe tu. Maana kwa kupigana kule vifo vilikuwa ni vingi sana na sijui population ya wakati huo ilikuwa vipi. Maandiko mengi kwenye biblia kwangu yanakuwaga magumu sana kuelewa naana kwa akili za kawaida unaona kama haiwezekani.
mkuu usiseme hivyo.
hawa jamaa licha ya aina ya silaha zao, mbinu zao za kivita, kijasusi na kiutawala zilikuwa ni za viwango vya juu kuliko yawezekana hata hizi unazoziona sasa.

Mfano katika WW2 jenerali wa jeshi la Adolf Hitler Rommel alitumia mbinu za Hannibal Barca huyu mdau tunayemjadili, na kuyashinda majeshi ya washirika huko afrika kaskazini ktk mji wa Tobruk (Libya).
Kuna mbinu za kiuchumi za kisasa ambazo ni copy paste za hawa manguli pia mkuu.
 
Mkuu asante kwa hoja nzuri na yenye kuchangamsha akili. Lakini kama kawaida yangu mimi nitakupa majibu kwa kutumia kitabu pendwa nikipendacho kuliko vyote, yaani "BIBLIA"; kitabu hichi kina majibu yote ya swali ulilouliza ingawa watu wengi wanakidharau.

Iko hivi utawala wa Rumi ni moja kati ya tawala tano kubwa zilizotabariwa au kuruhusiwa na MUNGU kuwepo hapa duniani, rejea kitabu cha DANIEL 2:36-44 ambapo utaona Danieli anamfafanulia Mfalme Nebukadreza ile ndoto yake ya sanamu kubwa. Katika ile ndoto, sehemu moja ya ile sanamu ilikuwa ni Ufalme wa Rumi, yaani ile miguu ya chuma.

View attachment 805760
Sanamu hii ndiyo ndoto aliyoota Mfalme Nebukadreza na tafsiri yake.
Sasa basi kwa kuwa Ufalme wa Rumi ulikuwa umeshatabiliwa na MUNGU kuwa utatawala dunia yote kwa wakati ulioamuriwa, isengekuwa rahisi kwa General Hannibal pamoja na jeshi lake kuivamia Roma na kuuangusha Ufalme wa Rumi. Fahamu kwamba nyuma ya hizi falme kubwa huwa kuna nguvu ya ajabu inayoziongoza, nguvu hiyo inaweza ikawa imetoka kwa MUNGU au inaweza ikawa imetoka kwa yule Mwovu Lusifer Ibilisi.

Kwa Ufalme wa Rumi, hata kama ulitabiriwa na MUNGU, lakini nguvu yake ilikuwa inatokana na Lusifer Ibilisi; rejea kitabu cha UFUNUO 13:1-2 .........yule joka(Lusifer) akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi(Ufalme) na uwezo mwingi(Nguvu za kijeshi). Hivyo basi kutokana na nguvu alizopewa Rumi, isingekuwa rahisi kwa General Hanniba kuivamia Rumi na kuindoa kwenye utawala wa dunia.

Utaona kwamba hata baada ya kifo cha General Hannibal bado utawala wa Rumi uliendelea kuwepo kwa miaka zaidi ya elfu moja. Isitoshe Hannibal Barca yeye na utawala wake hawakutabiriwa kuitawala dunia hata kama walikuwa na nguvu kiasi gani.

Mkuu zitto junior kitabu hichi BIBLIA kina majibu yote, hata kama utaamini au hautaamini, lakini UKWELI ndiyo huo.
mkuu Bibilia pia inasehemu ya Jibu kwa nini Rumi haikushindwa.
Ilitabiliwa haitashindwa katika mfululizo wa tawala zile nne.
Pia nguvu ya rumi haitakwisha kabisa hadi Yesu anarudi.
Pia Hakutakuwa na Dola jingine kubwa zaidi ya Rumi ya wakati wake duniani, hata US ananguvu lkn zinamipaka sio kama zile na wenda nguvu yake inakuwa boosted na rumi hiyohiyo.
Note:
Msingi wa Ufafanuzi wa Unabii uliouweka wa Daniel 4, 7 na Ufunuo 13 ni Day/Year approach in interpretation of Biblical prophesies.
Msingi huo licha kuwa msimamo wa Wasabato, Waprotestant wa enzi za karne ya 16 waliamini (ukiacha hawa wa sasa ambao wengi ni product ya counter-reformation). Hata Commentaries za Mzee Jerome mkristo wa huko Uyahudi aliyecompile Bibilia ya awali kwa kilatini kibovu VULGATE alikuwepo siku Dola hilo linaanza kuanguka na commentary Yake alionyesha kabisa kinachotokea ni Utimilifu wa Unabii wa Daniel. Sio yeye tu na wengine wengi hadi wanasiasa wakina napoleon na wakina Hitler walielewa historia hizo.
Na hata mwanahistoria wa Muda wate wa kiingereza Gibbon kaeleza hayo katika maandishi yake ambayo ulaya nzima wanaamini maandiahi yake ni source za kuaminika za kihistoria. Kaeleza kwa kina katika series za Volumes zake za RISE AND FALL OF ROMAN EMPIRE.

Maoni Kwa Nini Huyu Mwafrika Hakufika ROME na KUTAWALA Dunia ya wakati huo.

*Isingewezekana kwa sababu haikuwahi kutabiriwa hivyo katika unabii wa Muda mrefu hadi Dunia Inapota (sababu ya kiimani).
*Kwa Mujibu wa wananzuoni Marhabar alimwambia Hannibar, " You know how to gain a Victory, But Hannibal You know not how to use one''.

Kushinda Vita ni kitu kimoja, lkn kutakeadvantage ya huo ushindi ili kusukuma malengo makubwa ya kidola ni kitu kingine.
Wananzuoni wanamchambua Hannibal wakisema, Alikuwa amebobea kwenye MBINU ZA USHINDI, LAKINI HAKUWA NA MIKAKATI BAADA YA USHINDI.
Hata mipango yake mingi ilikuwa ya kimbinu zaidi (tactics) huku ikikoswa mikakati (Stratergies).
Mfano.
Alipigana vita mahususi na kupata ushindi ambao kama angekuwa na mikakati na maono ya mbele angeingia Roma na kutawala licha ya kuwa na jeshi dogo. Katika Ushindi wake pale CANNAE. Habari hizo za ushindi ule ziliwatetemwsha warumi wote, waliogopa sana na kama angeamua kusonga mbela akeiteka Rumi lkn hakuwa na mikakati na hakuona nje ya mbinu zake za kivita, akaamua kurudi Hispania alikotokea.

*Sababu nyingine Kulikuwa na mgawanyiko katika utawala wa Carthage. Wakati Barca anatafuta Ushindi mkubwa na kutawala njia zote za kiuchumi eneo hilo ambazo zilishikiliwa na Rumi, wakati huo akipambana kutokea Hispania alipokulia na kuandalia mikakati. Baadhi ya watu wa utawala huko Tunisia sehemu ya dola ya Carthage hakuunga mkono hilo wakiogopa vita kama vile vya kwanza enzi za baba yake Hannabal. hivyo hiki nacho kikawa ni kigezo. Ni sawa na kuwa na serikali yenye watu wenye maono makubwa huku wengine au baadhi ya watendaji kuyapinga.

*Sababu nyingine ni Mgawanyiko. Kikosi kilichoongozwa na kaka yake Hasdrubal Barca kilibaki Hispania. kulinda hiyo ngome yao huku Barca yuko huko italia anapambana na kikosi chake kidogo chenye mbinu za uhakika. Warumi walijua kumdhohofisha ni kwenda kushambulia na kupashohofisha maana wasingeweza kudhubutu kushambulia kutokea tunisia kwa sababu ufukweni hao carthage wangeshindwa. Hayo yalikuwa maono ya Cornelius na Scipio (mtoto wake alitimiza hayo maono), na hiyo ndiyo ilikuwa njia pekee ya kumtoa humo italia.

*Sababu nyingine Barca hakupata uungwaji mkono mkubwa na baadhi ya makabila huko italia kama alivyowashawishi wahispania kujiunga na jeshi lake. inasemekana wale jamaa hawakuonyesha ushirikiano wa kutosha hivyo kumfanya akose nguvu kiasi.

*Sababu nyingene Tofauti na waCarthage warumi wao walikuwa na umoja na maono yao waliyaunga mkono wote licha ya changamoto. Objective ya Taifa la warumi ilikuwa moja Tu, wao waendelee kuwepo kwa kutokuwepo kwa Hannibal Barca kwa gharama yoyote. Wakazi wa rumi wote hadi watumwa wao walikuwa nyuma ya serikali yao. Walijitolea hata kulipa kodi za ziada ili Jeshi lao lifanikiwe.

Umoja ni Nguvu
zitto junior
Malcom Lumumba
Red Giant

wakuu karibuni kwa kudadavua zaidi,
 
Marekebisho kidogo mkuu,
Julius Caesar hakueneza Ukrtisto Karthago kwasababu ameishi kipindi ambazo ukristo ulikuwa bado haujazaliwa duniani 100 BCE hadi 44BCE. Dola la Mroma kipindi hiki lilikuwa lina dini zile za kipagani amazo Wagiriki walikuwa nazo.
Malcom Lumumba sidhani kama mimi na wewe tunamzungumzia Caesar ama Kaisar mmoja

Nimejaribu kukuandikia kirefu ili walau unisaidie kujua kama wanaufanano ama ni mtu mmoja

“Roma ya Afrika”

Ilionekana kwamba Carthage ilikuwa imefikia mwisho wake kabisa. Lakini, karne moja tu baadaye, Yulio Kaisari aliamua kuanzisha koloni huko. Ili kumtukuza, koloni hiyo iliitwa Colonia Julia Carthago. Wahandisi wa Roma walisogeza udongo upatao meta mchemraba 100,000. Walifanya sehemu ya juu ya Byrsa kuwa jukwaa kubwa tambarare na kuondoa magofu yote. Mahekalu na majengo ya umma yenye madoido yalijengwa kwenye eneo hilo. Muda ulipopita, Carthage likawa ‘mojawapo ya majiji yenye ufanisi mwingi katika milki ya Roma.’ Lilikuwa jiji la pili kwa ukubwa katika eneo la Magharibi, baada ya Roma. Ukumbi wa maonyesho, viwanja duara vya maonyesho, mabafu makubwa ya maji moto, mfereji wenye urefu wa kilometa 132, na kiwanja cha sarakasi ambacho kingeweza kutoshea watazamaji 60,000 kilijengwa ili kutosheleza mahitaji ya wakazi 300,000 wa jiji hilo.

Ukristo ulifika Carthage yapata katikati ya karne ya pili W.K. na ukasitawi haraka. Yule mwanatheolojia maarufu na mtetea-imani Tertullian, alizaliwa huko Carthage wapata mwaka wa 155 W.K. Kutokana na maandishi yake, Kilatini kikawa lugha rasmi ya makanisa ya Magharibi. Cyprian, askofu wa Carthage wa karne ya tatu, aliyeunda mfumo wa vyeo vya makasisi vya madaraja saba, alikufa kama mfia-dini katika jiji hilo mnamo mwaka wa 258 W.K. Mtu mwingine kutoka Afrika ya Kaskazini, Augustine (354-430 W.K.), aliyetajwa kuwa mtu mwenye akili nyingi zaidi katika Ukristo wa kale, alihusika sana katika kuchanganya mafundisho ya kanisa na falsafa za Kigiriki. Uvutano wa kanisa hilo la Afrika Kaskazini ulikuwa mwingi sana hivi kwamba kasisi mmoja alisema hivi: “Ni wewe, Ee Afrika, unayeendeleza harakati za imani yetu kwa bidii nyingi sana. Unachoamua hukubaliwa na Roma na kufuatwa na wakuu wa ulimwengu.”

Hata hivyo, Carthage ingefikia mwisho wake. Kwa mara nyingine tena, mambo yaliyopata jiji hilo yalihusiana na mambo yaliyoipata Roma. Milki ya Roma ilipofifia, ndivyo na Carthage. Mnamo mwaka wa 439 W.K., jiji hilo lilitekwa na kuporwa na Wavandali. Wabyzantium walipoteka jiji hilo karne moja baadaye, jiji hilo liliponea kuharibiwa kwa muda mfupi. Lakini halikuweza kuwazuia Waarabu walioshambulia Afrika Kaskazini. Mnamo mwaka wa 698 W.K., jiji hilo lilitekwa, na baada ya hapo, mawe yake yalitumiwa kujenga jiji la Tunis. Katika karne zilizofuata, mawe ya marumaru na matale ambayo hapo zamani yaliremba jiji hilo la Roma, yaliporwa na kupelekwa hadi nchi nyingine ili kujenga makanisa makuu ya Genoa na Pisa nchini Italia, na yawezekana pia Canterbury, nchini Uingereza. Carthage liliacha kuwa jiji la kale lenye utajiri na uwezo mwingi zaidi, liliacha kuwa milki iliyokaribia kutawala ulimwengu. Hatimaye, jiji la Carthage likawa rundo la magofu lisilo na maana......

zitto junior
 
"Those who cannot remember the past are Doomed to repeat it''.
kuna maana sana ya kufunua hizi elimu.

Baba yake Hannibal Barca Hemircal Barca alishindwa vita vya kwanza na kulazimika kulipa kodi kwa utawala wa kirumi Talanta 440 kwa miaka kumi, mgogoro mwingine ulipotokea Sardinia Warumi walitangaza vita, baba yake akiwa kiongozi akaogopa na kuzuia vita akaahidi kuilipa dola ya kirumi kodi ya talanta 1200 zaidi huku akisalimisha na maeneo ya Sardinia na Corsica.

Huyu mzee alikuwa na watoto watatu wa kiume Hannibal, Hasdrubal na Mago. Mtoto wake Hannibal akiwa na miaka 9 aliapishwa mbele ya Madhabahu kiapo kwamba lazima aje alipize kisasi kwa hicho Rumi walichowafanyia.

Hapo unaweza kujifunza umuhimu wa mipango ya Muda mrefu. Na unaweza kuona siri ya mafanikio ni matokeo ya mipango tangu jemedali huko akiwa kinda wa miaka 9.


Mzee huyu kumuandalia mazingira bora ya Ushindi baadae alivamia eneo la spain. akaweka kambi na kulifanya kuwa eneo lao la utawala. Akahamishia huko watoto wake watatu ili baade miaka mingi ijayo Mtoto wake aje alipe kisasi kutokea huko katika vita vya pili kati ya dola hilo na dola la kirumi. Ikumbukwe vita vya kwanza vilivyoendeshwa na baba walishindwa vibaya.
Kaka samahani naona kama kuna huyu Hasdrubal ni mwana wa Hamalcar ama alikuwa ni mkwe wake?!

Lakini pia nineoma tena umesema kuhusu namna alivyotawala alikuwa ni North Africa ama alikuwako Spain?!

Basi kama kuna utata kutakuwa kuna mahali historia zao hazijawekwa sawa japo zimejaribu kutufanya tumjue Hannibal na familia yake kiujumla tangu walivyochukua utawala kutoka kwa Tiro wa Etruria
 
Kaka samahani naona kama kuna huyu Hasdrubal ni mwana wa Hamalcar ama alikuwa ni mkwe wake?!

Lakini pia nineoma tena umesema kuhusu namna alivyotawala alikuwa ni North Africa ama alikuwako Spain?!

Basi kama kuna utata kutakuwa kuna mahali historia zao hazijawekwa sawa japo zimejaribu kutufanya tumjue Hannibal na familia yake kiujumla tangu walivyochukua utawala kutoka kwa Tiro wa Etruria

images-32-jpg.805635

angalia kielelezo cha ramani aliyoitoa mkuu zitto junior
dola hiyo inaambaa hadi Sehemu ya Hispania.
Wakati wanajitanua hadi huko, warumi hawakujua kwa nini lakin Ulikuwa ni mkakati wa Muda mrefu ili washambulie italy na roman republic kutokea huko.
Huyo alikuwa mtoto sio mke wake kwa mujibu wa chanzo cha taarifa. na aliongoza majeshi ya Carthage kutokea sehemu ya spain (part of carthage empire). ni miongoni mwa watoto watatu wa kiume wa Barca Sr.

nadhani hakuna mkanganyiko.

ngoja wajuvi na wataalam waje waweke sawa na kuongeza madini zaidi.
 
Habari za asbuhi wana jukwaa bila kupoteza muda embu twende moja kwa moja kwenye mada
View attachment 805630

MWANZO
Hannibal barca alizaliwa mnamo mwaka 247 BC... alikua jenerali wa jeshi la CARTHAGE yaani Tunisia ya leo na alipata umaarufu hasa kwenye vita vyake dhidi ya dola ya kirumi na mataifa mengine makubwa ya ulaya kwa wakati huo zilizofahamika kama PUNIC WARS
View attachment 805635
Jenerali huyu Alitoka afrika na kuweza kuvamia bara la ulaya kupitia Iberia yaani ureno na spain akiwatandika wote waliomzuia njiani kwa kutumia mbinu za kimedani bora zaidi kuwahi kushuhudiwa wakati ule.... Na umaarufu ulipanda zaidi alipovamia ITALIA kwenye moyo kabisa wa dola la kirumi na kushinda vita tatu muhimu dhidi ya dola hiyo kwenye miji ya trebia,trasimene na cannae. Nguvu zake ziliweza kuitia hofu dola hii kiasi walikuwa wakisikia jina lake wanatetemeka!!!

Katika moja ya vita kubwa kabisa ni vita ya cannae ambayo kihistoria ndio vita ambavyo Dola ya kirumi ilipoteza wanajeshi wengi zaidi kati historia ambapo wanajeshi elfu 80 walifia hapo huku masenator 80 wakichinjwa.... Kibaya zaidi alilizunguka jeshi zima la Rumi hivyo hakuna masalia waliopona na tokea hapo jeshi la Rumi liliogopa kupigana vita ya uso kwa uso na Hannibal Barca

Hannibal Barca Aliendelea kuitawala italia kwa miaka 15 lakini jambo ambalo mimi najiuliza mpaka leo na nimekosa majibu ni kwanini General Hannibal Barca aliyeogopeka dunia nzima ya kale aliwatandika warumi kwenye vita zote alizokutana nao ila alisita kuvamia Rome?? Je nini kilimzuia asivamie?? Aliogopa nini??

MBINU ZAKE VITANI
View attachment 805632
Hannibal anafahamika zaidi kwa kutumia tembo kwenye uwanja wa vita.... Alikuwa anatumia tembo mkubwa wa jamii ya syria ambao kwa sasa wametoweka hivyo ukubwa wake ulikuwa ni kama vifaru vya kijeshi vya sasa..... Aliwatanguliza mbele tembo kama 80 kiasi kwamba mpaka mnamalizana na tembo mnakuta mshazingirwa na kupewa kipigo cha mbwa mwizi

MWISHO WAKE
Baada ya kupata taarifa kuwa nchini mwake wamevamiwa ikabidi arudi kuokoa jahazi na kufikia muda huo mbinu zake za medani zilikwisha somwa vizuri na jenerali scipio Africanus wa dola ya Rumi ambaye alitaka kulipa kisasi baada ya Hannibal kumjeruhi vibaya baba yake kwenye ile vita ya trebia hivyo akampiga hannibal huko mjini ZAMA nchini Carthage (Tunisia) na baada ya hapo Hannibal Barca aliranda randa sana ulaya na mwishowe alisalitiwa na kurudishwa kwa warumi ila aliamua kujiua kwa kunywa sumu ili kuepuka dhahama ya kuangukia mikononi mwa maadui zake.

HITIMISHO
Jenerali huyu anatazamiwa kuwa mwanajeshi bora kuwahi tokea katika historia za kijeshi hapa duniani ila swali nalotaka mnisaidie great thinkers je ni kwanini General Hannibal pamoja na kuwatandika dola ya rumi huko italia aliogopa kuvamia roma ambayo ingeifuta rasmi dola ya kirumi kwenye uso wa dunia????

Naomba kuwasilisha
View attachment 805636
Asante sana chief kwa maarifa mapya haya, kiukweli sijawahi kumsoma huyu jenerali shujaa kabisa wa kiafrica....ila naahidi kutafuta historia kidogo tuweze kujua ilikuaje.
 
Asante sana chief kwa maarifa mapya haya, kiukweli sijawahi kumsoma huyu jenerali shujaa kabisa wa kiafrica....ila naahidi kutafuta historia kidogo tuweze kujua ilikuaje.
Pamoja sana mkuu ni vizuri kukumbushana kuhusu watu waliofanya makubwa hapa duniani ili tuweze kujifunza mambo machache kutoka kwao nimefurahi pia uwepo wa magwiji kwenye huu uzi kuanzia Malcom Lumumba mitale na midimu Red Giant Kudo wametiririka madini ya kutosha hadi nmejikuta nageuka mwanafunzi..... Long live JF
 
Back
Top Bottom