Hans Poppe wa TATOA amchambua Magufuli

duh! angalia avatar bana
 
Hawa watu wa TATOA wanamlaumu sana Magufuli. Lakini wakati wanalaumu ni vema wakakaa kujiuliza kwa nini inakuwa hivyo. Nielewavyo mimi mizigo iko ya aina nyingi lakini maarufu ni makontena na mifuko inayopakiwa kwenye flat bed za maliro kama mbolea, sukari na kadhalika. tukichukulia mfano kama lori linaruhusiwa kubeba tani 30 za mzigo, ni vema mwenye lori akapakia tani 28 ili wakati anapita mizani hata kama mzigo utaelemea upande mmoja au kuzidi kwa bahati mbaya bado hiyo tolerance ya 1.4 inaweza kuwa ndani ya hizo tani 30. Hiyo itamfanya kuruhusiwa kuendelea bila bughudha yoyote. Kama mzigo ni zaidi ya uwezo wa gari lake basi auache. Ni ukweli usiopingika na kwa makusudi kabisa wasafirishaji wanabeba mizigo mizito zaidi ya uwezo wa magari yao. Hilo pia linasababisha magari yao kuchakaa mapema kwa sababu injini inakuwa inavuta mzigo mkubwa zaidi ya uwezo wake. Tuangalie pande zote ili kutatua tatizo. Kwenye hili naamini TATOA watashindwa tu.
 
Hans Pope bado unavuta ile sigara kubwa kaka? shauri yako, yatakukuta yale yale ya enzi zile za Mwalimu si wakumbuka ulipotea sana ' uraiani' kaka?
 
Nashukuru kwa kunifunua macho,just the last one,je ana uhusiano na captain Hanspope aliyeuwawa vita ya Kagera na mwili wake kuzuiliwa na Nduli kwa madai kuwa Tanzania inatumia askari wa kukodi kutokana na uburushi wa marehemu?
 
Ndugu shida Tuliyonayo kwa sasa Ni kuwa Hata Gharama za Ujenzi katika nchi yetu zipo juu kuliko nchi zinazotuzunguka!! Fikiria kwa TZ Mchina anatenda ujenzi wa barabara kwa gharama ya dola 800,000 kwa kilometer kwa Tanzania na akiwa Nchi nyingine Gharama inakuwa $ 500,000 hadi 600,000. Tena Contractor's from EU Community!! NA WACHINA WAPO $ 400,000 HADI 500,000 Tujiulize Tanzania tuna mkosi Gani? pIA Tunapata very poor quality Road!!
 
Ndugu wanajamvi kufuatia kauli za hivi majuzi toka kwa mh.Magufuri,zimezua jambo kuna nchi kama Rwanda barabara zao zinauwezo wa kupitisha tani 80 je hizo barabara mbona bado ni imara?kwanini hizi za hapa kwetu kila siku mh.Magufuri amekua akiongeza masharti ya matumizi ya barabara hizo?kwahyo kilichopo ni kuwa barabara za magufuri ziko chini ya kiwango hivyo anahofia kuumbuka zinapoharibika mapema ndani ya mda wa kawaida.
Hivyo kitendo cha magufuri kuzidisha sheria kila kukicha za magari ya mizigo barabarani zinachangia mfumko wa bei hapa nchini, kwani kama barabara zingejengwa imala magari ya mizgo yangepakia mzigo mkubwa badala ya sasa kwa gharama ileile kwa umbari huska,lakini kwa leo gari linauwezo wa kubeba tani 60 kutoka Dar hadi Mara bila shida ila kwa ubovu wa barabara za magufuri unalazimika kubeba tani 40 kwa gharama ileile,je hapo ni kwa manufaa ya nani?pia sheria hizi za Magufuri zinachangia rushwa sana kwenye mizani nahisi atakuwa ananufaika na rushwa kwa namna moja ama nyingine bila shaka .
 
Enheeeeee,,,,,anasema barabara zinazojengwa na serikali ya ccm chini ya utawala wa Dr Jakay Mrisho Kikwete zinajengwa kwa fedha nyingi sana,tena za walipa KODI
 
Kama ungekuwa na uthibitisho wa kutosha ningeweza kukuelewa lakini habari ya kizandiki tu ni maneno matupu yasiyo na mantiki.
 
Kama ungekuwa na uthibitisho wa kutosha ningeweza kukuelewa lakini habari ya kizandiki tu ni maneno matupu yasiyo na mantiki.

Mlivyo zero brain hamtakawia kusema madereva wa malori waliogoma mpaka serikali ikaingia hasara ya mabilioni ni Wanachama wa Chadema
 
TATOA, kile chama cha wenye malori, kimesema "Magufuli alipaswa kupelekwa kwenye propaganda za chama kwa sababu ndio sehemu inayomfaa kwa ajili ya kupiga propaganda na sio kuwa waziri".
Pia wanajiandaa kumpeleka mahakamani kwa kuwaletea hasara.
Source: Gazeti la Mwananchi tarehe 12 Oktoba
 
Hii akili ya bavicha haina maana hata chembe.

We mporipori sikushangai kwani unachofanya ni ushabiki hata kwenye hakuna,ila hizo ni akili za kuzimu sio za mtu aliye hai,unadhani viongoz wa kitanzania walivyo wajinga basi kila nchi itafanana na viongoz wenu wsiojitambua,kwanza bw.Simiyo leo kiongoz wako wa ccm akisema soda ya koka haina sukuri utakubari tu huna uwezo wa kupinga kwani huna maamzi na we sio mtu huru pole sana mfu unayetembea.
 
Natamani taifa langu lingekuwa na Rais na Mawaziri wote including Prime Minister aina ya Magufuli...Tungeshanyoka
Bila watu wa aina hiyo maendeleo tutayasikia redioni na kuyataeama kwenye TV.
 
Kama ungekuwa na uthibitisho wa kutosha ningeweza kukuelewa lakini habari ya kizandiki tu ni maneno matupu yasiyo na mantiki.

Ubaya vijana wa lumumba niwavivu kutafiti nakutembea. Wanapopajua nilumumba tu. Mimi nina ushahidi wakueleweka kabisa. Nenda pale biharamulo angalia barabara iliyojengwa na wachina hata mwaka haiwezi maliza sasa ndio ipite gari ya tani30 unategemea nini. Toka pale biharamulo mjini mpaka rusaunga utajionea maajabu ya barabara za magufuli. Zote kiwango cha chini. Anzia chato mpaka bukoba mashimo kibao barabarani. Hyo nimifano michache. Tokeni lumumba jifunzeni kujua hata mkija hapa mnakitu cha kuongea
 

Wajinga watakupinga ila hii ni kweli. Design ya sasa ya highways inalenga maximum loading in a sense ukizidisha uzito unaharibu gari yako mwenyewe na si barabara. Hapa kuna uchakachuaji mkubwa. Huyu jamaa ni mtu wa ajabu sana kila maamuzi yake ya ajabu lazima yaligharimu taifa
1. Meli ya samaki bahari ya Hindi tumevuna nini zaidi ya hasara?
2. Bomoa bomoa?
3. Mizani ni zaidi nadhani kila m2 amesikia loss yake.
The issue is they are constructing roads below the design std ndo maana anabweka hovyo. Ngapi zinatitia hovyo kabla hata ya robo ya design life? Chalinze - Segera, Minjingu - Singida nk. Aibu. Mimi siko KISIASA. Mwenye macho na aone
 

Sheria zipo kuhudumia watu sio watu kuhudumia sheria ndio mana zinatungwa na kurekebishwa na kufutwa tena makufuli wako huyo anang'ang'ania sheria inayoshibisha tumbo lake; wao wanapiga mihela na wakandarasi barabara zinajengwa chini ya kiwango halafu analeta vizogo mbuzi na kutunishia wachukuzi misuli; kwani mabarabara mangapi yamebomokabomoka hata mwaka bado? au hatujui? na huyo makufuli ni waziri wa barabara tuuuu mbona magorofa yanaanguka na watu kibao kufa hatumsikii akin'gaka? anachumia tumbo tu huyo hafai hata kuwa mjumbe wa nyumba kumi mtu kakalia ufisadi tuuuu nyumba za serikali kauza milioni 15 na waliouziwa hata deni hawajamaliza wanaziuza bilioni 15 anafaa kunyongwa tu ni mhujumu uchumi ndio mana mawazo yake mafupi hawezi hata kutafakari athari ya uropokaji wake. Badala ya kujiona yeye ni mhudumu wa wadau anajiona yupo kwa ajili ya kujihudumia na kujikweza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…