Copy paste kutoka fb......
Tanzania kuna "𝐭𝐚𝐩 𝐤𝐢𝐝𝐝𝐢𝐞𝐬" wengi wanaojiita "𝐇𝐚𝐜𝐤𝐞𝐫𝐬" , hii ni sawa na panya kujifananisha na simba wakati hamwezi hata nyau.
Kumekua na tabia ya ajabu sana siku hizi, mtu anajijua kabisa hafikii hata theluthi ya hacker ila anaamua kujipachika jina la hacker, huu ni ushamba wa hali ya juu sana.
𝐇𝐀𝐂𝐊𝐄𝐑– 𝘏𝘢𝘸𝘢 𝘯𝘪 𝘬𝘢𝘮𝘢 𝘮𝘢𝘧𝘶𝘯𝘥𝘪 𝘮𝘢𝘨𝘢𝘳𝘪 𝘸𝘢𝘯𝘢𝘰𝘫𝘶𝘢 𝘬𝘶𝘵𝘦𝘯𝘨𝘦𝘯𝘦𝘻𝘢 𝘯𝘢 𝘬𝘶yaendesha.
sifa yake kuu anaweza kujitengenezea tools zake yeye mwenyewe, ku modify tools za wengine kwa kuongeza manjonjo yake n.k. na hata akitumia scripts za wengine ni kuokoa tu muda, sio kwamba hawezi kujitengenezea yake.(no need to re invent the wheel)
anaujua mtiririko wa system, anajua nini kinafanyika mpaka kinatokea kitu Fulani, maswali yake huwa ni kwanini au inakuwaje tool hii iko hivi na hivi, sio kama kundi la pili wanakimbilia kuulizia tool ipi watumie bila kuwa na understanding ya work flow.
𝗦𝗖𝗥𝗜𝗣𝗧 𝗞𝗜𝗗𝗗𝗜𝗘– 𝘩𝘢𝘸𝘢 𝘯𝘪 𝘬𝘢𝘮𝘢 𝘮𝘢𝘥𝘦𝘳𝘦𝘷𝘢 𝘸𝘢 𝘮𝘢𝘨𝘢𝘳𝘪 ya automatic.
Hawa huwa wanajua kutumia script lakini hawajui nini kilicho nyuma ya hizo scripts mpaka zinaleta matokeo flani maana hawana hata elimu ya fundamentals za mtiririko wa process zinazoendelea pindi wanapozitumia scripts, hii inamfanya akose ubunifu.
Wanachojua ni kutumia scripts ambazo zimetengenezwa na hackers.
script ikiharibika ama ikileta matatizo hua hawezi kuirekebisha, yeye kakariri tu commands kwamba akichapa hivi kwenye keyboard basi kitakuja kitu Fulani.
ila kidogo wana nafuu maana angalau wanajua ku tumia hzo scripts za lugha mbali mbali kama JavaScript,PHP, Python, Ruby, Groovy, Perl, Lua,Bash, n.k. kundi linalofata hata kutumia scripts ni shughuli nzito, wanachukia sana scripts.
𝗧𝗔𝗣 𝗞𝗜𝗗𝗗𝗜𝗘- 𝘩𝘢𝘸𝘢 𝘯𝘪 𝘬𝘢𝘮𝘢 𝘮𝘵𝘰𝘵𝘰 𝘢𝘯𝘢𝘦𝘱𝘢𝘬𝘢𝘵𝘸𝘢 𝘯𝘢 𝘥𝘦𝘳𝘦𝘷𝘢, yeye 𝘢𝘯𝘢𝘯𝘺𝘰𝘰𝘴𝘩𝘢 𝘵𝘶 𝘶𝘴𝘶𝘬𝘢𝘯𝘪.
Ewaaa!! sasa hiki ndio kichaka cha wabongo wengi wanaojiita hackers, Mtu anajiita hacker kwenye ishu za kawaida kabisa.
-kapewa file la hatunnel kaanza kutumia freenet, anajiona hacker.
-kadownload app ya kuroot simu yenye kisehemu cha kuminya root, anajiona hacker
-kadownload software iliyovunjwa ili itumike bure, anajiona hacker
-anatumia firmware ya dtb kwenye kingamuzi ili akwepe malipo, anajiona hacker
-kaingiza window ya ubuntu au kali linux kwenye laptop, tayari anajiona hacker
-ka unlock modem / simu kwa maelekezo ya youtube, anajiona hacker, 😂😂😂😂
GASTA DI ELOO NYAMBAFU! hebu acheni kushusha thamani za taaluma za watu aisee.
Hawa wengi hata umpe script atabaki anaishangaa, ni weupe Zaidi ya script kiddies.
huwa wanazikwepa scripts, huwa wanapenda kutumia program/ app kwasababu huwa zimerahisisha mtitririko wa sctipt, wanagonga tu sehem kazi imeisha, hakuna mambo ya kuumiza kichwa wala kuandika command lines za kutumua script, ni mwendo wa kubofya tu.
hapa ndio kuna mambo ya kuminya kwa mouse… next, next, accept terms, done, finish.
.............................................................................
SASA TUELEWANE.
Msiwe mnawaita hackers, muwe mnawaita "TAP KIDDIES" 😂😂😂. mnapowaita hackers huwa wanavimba vichwa sana na hilo ndio huwa lengo lao
wao wanapojiita hackers, kuweka profile picture za hackers na kuleta fujo kwenye groups ili wasifiwe ni hackers huwa ni kama mtoto mdogo kavaa ndevu bandia ili aamkiwe, Msiwatimizie lengo lao kirahisi, kwanza hua inaua kipaji 😂, waiteni tap kiddies wapate hasira ya kupiga hatua..