Hapa duniani starehe ziko chache, majanga ndiyo mengi

Hapa duniani starehe ziko chache, majanga ndiyo mengi

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
21,643
Reaction score
51,642
Mungu ametuwekea mambo ya kutupa raha machache sana yaani ukifikiria raha ni kunywa pombe, kula chakula, kufanya mapenzi na kulala usingizi.ila cheki majanga yalivyo mengi magonjwa, majanga ya asili, umaskini, ajali n.k

At least kidogo tungekuwaga na uwezo wa kupaa Kama ndege yaani unaruka angani ile ni raha kwa kweli.
 
Hizo changamoto zinapoongezeka na maendeleo yanaongezeka

Pombe unabidi kuwa nazo makini Mimi kuna ndugu yake alikuwa master Wa pombe Ila zilimpolaza chini hakuweza kuamini macho yake.

So drink responsibly
 
Kikubwa ni kuwa na amani ya moyo tu.

Pia kila jambo kulifanya kwa kiasi nafikiri iyo ndio starehe na utaishi raha mustareheeee.

La sivyo starehe zako ndio yatakuwa mapigo yako.

Watch Out
 
Mungu ametuwekea mambo ya kutupa raha machache sana yaani ukifikiria raha ni kunywa pombe, kula chakula, kufanya mapenzi na kulala usingizi.ila cheki majanga yalivyo mengi magonjwa, majanga ya asili, umaskini, ajali n.k


At least kidogo tungekuwaga na uwezo wa kupaa Kama ndege yaani unaruka angani ile ni raha kwa kweli.
Mkuu, kwa mujibu wa huu uzi; kila kitu ni STAREHE narudia tena kila kitu ni STAREHE. Hapo ninamaanisha kile ambacho kwako ni kero au hakikupi raha , basi kwa mwenzio ni starehe kubwa sana hadi moyo unasuuzika kabisa. Nitatoa mfano;- 1.
Wewe ukipata ajali say ya gari na kuumia sana yupo atakayetoa comment "Yes, na akome, alizidi mno kuturingia na kigari chake" i.e. amefurahia kuumia kwako.
2. Wewe ukilala njaa, yupo atakayesema "nilijua tu- huyo hatoboi"
3. Mwanao au Jamaa yako akiugua halafu akafa, ukienda kwa muuza majeneza (yah. kwa wakristo) baada ya kununua usishangae akakuambia "..karibu tena ndugu yangu 😀
4. Ukiachika (kwa Ke) au ukitelekezwa (kwa Me) wapo watakaoshangilia kwa furaha sana.......
5. Yanapotokea mafuriko, hiyo ni fursa (furaha iliyojificha) kwa waokoaji n.k.
Wahenga walisemaga "One man's meat is another man's poison"
Ndio maana utakuta wapo watu wanafurahia vita, wanaobaka, wauaji n.k. na ndipo likawepo neno la Husda, Wachawi n.k.......
Kwa kifupi Furaha yako ni Kero kwa wengine. Ni mtizamo wako tu ili kitu kiwe ni majanga.
 
Mungu ametuwekea mambo ya kutupa raha machache sana yaani ukifikiria raha ni kunywa pombe, kula chakula, kufanya mapenzi na kulala usingizi.ila cheki majanga yalivyo mengi magonjwa, majanga ya asili, umaskini, ajali n.k


At least kidogo tungekuwaga na uwezo wa kupaa Kama ndege yaani unaruka angani ile ni raha kwa kweli.
Mh? Sio kweli! Raha jipe mwenyewe! Binadamu ana milango 5 ya fahamu! Kila mlango unaweza kukupa starehe jinsi unavyotaka! Macho (yape macho kile ambacho kitakustarehesha mfano movies n.k), masikio (unastareheshwa ukisikia nini? Mziki, n.k, basi yape), pua( unastareheshwa ukinusa nini? Papuchi/mbususu? Yape! Ulimi (chakula/vinywaji, pombe? Juice? Yape), ngozi (inastareheshwa kugusana na nini? Mke/mme? Upe). Naongeza na kingine! Viungo vya uzazi (mambo kwichikwichi, ni starehe number moja), heshima/vyeo/kumiliki mali, n.k jipe! N.k, n.k, sasa shida hiko wapi mleta uzi?
 
Ila tungekuwa tunapaa magari na ndege visingehitajika kabisa. Maana kuna ndege wanasafiri kila mwaka kutoka Australia kwenda Kitulo Makete Njombe. Wengine wakati wa baridi kali Ulaya wanasafiri kwenda kisiwa cha kule Muleba Kagera kula raha
 
Hii dunia nadhani hatukuumbiwa sisi, tumekuja bahati mbaya tu. Manake kila kitu kilichopo apa duniani ukikaa vibaya kinakuua!
Prof janabi anatukataza kula ili hali yeye ni dakitari bingwa! Sasa mtu asipokula nguvu za kifanyakazi, na mwili kujengeka itakuwaje? Eti ni dakitari!
 
Ila tungekuwa tunapaa magari na ndege visingehitajika kabisa. Maana kuna ndege wanasafiri kila mwaka kutoka Australia kwenda Kitulo Makete Njombe. Wengine wakati wa baridi kali Ulaya wanasafiri kwenda kisiwa cha kule Muleba Kagera kula raha
Prof janabi anatukataza kula ili hali yeye ni dakitari bingwa! Sasa mtu asipokula nguvu za kifanyakazi, na mwili kujengeka itakuwaje? Eti ni dakitari!
Hilo nalo ni mojawapo ya majanga?
 
At least kidogo tungekuwaga na uwezo wa kupaa Kama ndege yaani unaruka angani ile ni raha kwa kweli.
Njoo hapa Katavi utapewa uwezo wa kupaa na kufika popote duniani kwa kufumba macho kwa sekunde 5 tu.

Muda na umbali (time and distance) havina uhusiano kwa maarifa ya kupaa ya hapa Katavi.
 
Back
Top Bottom