Ukiwa ndani ya CCM hauwezi kuikosoa na kuisahihisha kwa sababu never outshine your master lkn ni rahisi sana kupush ajenda nje ya CCM kuna mwafizikia Newton aliwahi kusema nguvu ya ndani haileti mwelekeo bali ni nguvu ya nje mm nimezaliwa kusimamia ukweli lkn sio kujipendekeza ili nipate madaraka kwangu mm furaha yangu ni kuona matokeo
Well said, wanasiasa wengi wa kitanzania wanapenda kujipendekeza ili kupata nafasi za uteuzi. Kama unamaanisha anza taratibu za kutafuta wanachama wa mwanzo wanao takiwa ili kupata usajili. Usisubiri karibu na uchaguzi. Tanzania hii wanaweza kufanya zengwe usajili usipatikane kama walivyofanyiwa kile chama cha Sitta.
Uungwaji mkono upo! Tumechoka na siasa za kujipendekeza na kutafuta umaarufu. Tanzania tunahitaji mabadiliko ya kiuongozi na mfumo. Kwasasa uongozi unabadilika kwa watu kupeana na mfumo huko pale pale. Hakutakuwa na jipya katika Tanzania yetu.
Tunahitaji kusimama kama nchi inayojitambua. Si kujipendekeza ati tuonwe wazuri. Tunahitaji kukua kiuchumi, na kinguvu kuwa Taifa kubwa. Tufute omba omba kama nchi, tujitegemee, tusomeshe vijana wetu na kuwatumia ktk kuendeleza nchi.
Magufuli alileta mabadiliko chanya. Sasa tunarejea enzi za nyuma. Wanaosema Magufuli aliuwa wanaushahidi? Mauwaji yamekuwepo katika hii nchi toka uhuru.
Kuanzia kwa Nyerere, nakumbuka nikiwa mdogo kuna mwanasiasa mmoja, alipigwa Risasi hadharani katika mkoa fulani. Wakati wa Mwinyi kuna mauaji yalitokea yakiwalenga Maprofesa Kadhaa.
Wakati wa Mkapa, watu waliuliwa na hasa ktk maandamano ya Mwembe Chai, na kule Zanzibar.
Wakati wa Kikwete kulikuwa na utekaji, Ulimboka, na baadhi ya waandishi wa habari, Mauaji ya Albino, Mwandishi wa habari aliyeuwawa huko Iringa. Hata Mauaji ya Kibiti yalianza JK akiwa madarakani.
Haya mambo hutokea katika nchi yoyote ile. Hakuna binadamu asiye na mapungufu. Hizo lawama anazopewa Magufuli ni kwa wale waliomchukia. Na kwa kawaida uwezi pendwa na binadamu wote. Au kuwafurahisha wote.
Hongera kwa wazo hili na anzisha hicho chama nauhakika wafuasi wengi wapo. VIva Tanzania Viva!