Uchaguzi 2020 Hapa Kazi tu ni CCM, Kazi na Bata ni ACT-Wazalendo na Kazi na Uhuru ni CHADEMA

Uchaguzi 2020 Hapa Kazi tu ni CCM, Kazi na Bata ni ACT-Wazalendo na Kazi na Uhuru ni CHADEMA

Mao Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2018
Posts
210
Reaction score
231
Tupate Maoni, tujitambue, tujuane
1. Hapa Kazi Tu (CCM)
2. Kazi na Bata (ACT)
3. Kazi na Uhuru (CHADEMA)

Kazi bila mapumziko Ni tabu, mapumziko bila kazi ni umasikini.

Wewe Ukowapi katika hizo?
 
Wote wanatuchukulia poa Sana...yaani wanatuona Sisi ni wavivu hatupendi KAZI...CCM ndio wenye KAZI zote zenye miradi mikubwa lakini wanazigawa Kwa wachina na wafungwa, Chadema wanataka wapate Uhuru wa kupiga pesa Kwa mikataba kandamizi na kuhodhi njia za uchumi, ACT wanasema na wao ni zamu Yao Kula BATA...yaani wote wanatubeba ujinga.
 
Wote slogan zao ni copy ‘nd paste ya CCM..... upinzani hawajawahi fikiria kazi kama first priority. Asante magufuli watu kazi wanaiyona.

Ukifnya kazi bata utakula tu, ukifanya kazi pesa yako hupangiwi matumizi (utakuwa huru tu mwishowe)
Kumbe wanakubali kuwa sasa Kazi zinafanyika ! Ndo maana wameongeza neno BATA sijui UHURU. Yaani wana maana ya kwamba maendeleo yapo ila hakuna uhuru na bata ! .Wapinzani wanachekesha sana , alafu eti ndo Wanataka washinde Urais kwa slogans hizi !!
 
Tupate Maoni, tujitambue, tujuane
1. Hapa Kazi Tu (CCM)
2. Kazi na Bata (ACT)
3. Kazi na Uhuru (CHADEMA)

Kazi bila mapumziko Ni tabu, mapumziko bila kazi ni umasikini.
Wewe Ukowapi katika hizo
KAZI TU, kodi inakusanywa mwenzio anakwenda kugaia watu barabarani maburrungutu, kwenye mkoa anaotaka na kugawa mapapai
 
Kwa nini nembo ya taifa haikuandikwa "Kazi na barabara ?" Aliuliza Mheshimiwa Lissu !!

Uchaguzi huu utakuja na ajenda za ajabu sana. Ajenda hiyo ya lissu inaweza kuwafanya wafuasi wake kuanza kuvunja barabara zilizojengwa hasa wale wasiokuwa na magari kwa vile inawajenga kuamini kuwa barabara siyo za muhimu. Vile vile inajenga sana kasumba kuwa serikali inatakiwa kuwa inawawekea pesa wananchi pesa mifukoni wakati contract baina ya serikali na wanachi ni kodi+infrastructure, yaani raia analipa kodi, halafu serikali inajenga miundo mbinu na kujenga ulinzi wa nchi na raia wake; jambo mabalo haliwezi kufanywa na mtu binafsi.

Sasa ukianza kubeza kuwa barabara na madaraja siyo ya muhimu, halafu akaja mtu akaanza kuyalipua kwa mabomu ya kigaidi, itakuwa ni hatua nyingi sana za kurudi nyuma. Wakati tunapata uhuru hatukuwa na barabara yoyote yenye lami, ndipo Nyerere akaaza kujenga pole pole; hadi anaodoka alikuwa ameacha Dar-Tunduma, Morogoro-Dodoma, Chalinze-Tanga-Arusha, na Mwanza-Sirari. Leo hii zipo nyingi sana karibu nchi nzima na ni muhimu tujivune kuwa nazo siyo kuzibeza kuwa siyo za muhimu kwa maisha yetu. Cheap politics huweza kuleta unintended consequences kwa jamii.

Halafu nembo inasema "Uhuru na Kazi", haisemi "Kazi na Uhuru."
 
Kwa nini nembo ya taifa haikuandikwa "Kazi na barabara ?" Aliuliza Mheshimiwa Lissu !!

Uchaguzi huu utakuja na ajenda za ajabu sana. Ajenda hiyo ya lissu inaweza kuwafnay wafuasi wake kuanza kuvunja barabara zilizojengwa hasa wale wasiokuwa na magari kwa vile inawajenga kuamnini kuwa barabara siyo za muhimu. Vile vile inajenga sana kasumba kuwa serikali inatakiwa kuwa inaweweka pesa wanachi pesa mifukoni wakati contract baina ya serikali na wanachi ni kodi+infrastructure, yaani raia analipa kodi, halafu serikali inajenga miundo mbinu na kujenga ulinzi wa nchi na raia wake; mjambo mabalo haliwezi kufanywa na mtu binafsi...
lissu hana wafuasi, ana wapenda mageuzi. MATAGA mnasema Lissu na wanamageuzi wanapinga ndege lakini ukweli ni kwamba wanataka ukweli na ueazi kwenye manunuzi ya ndege.

Wanapinga barabara, hapana , wanataka uwiano wa maendeleo ya vitu na watu
 
Huyu Lissu hana hekima zaidi ya kupayuka payuka hovyo bila ya staha. Anatumia barabara anazo zikashifu na kukebehi maendeleo ya miundo mbinu yaliyo fanyanywa na serikali za ccm.

Wanasahau tangu JPM achaguliwe 2015 kuwa mgombea wa CCM hata baadaye akiwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa JMT kila alipoongea na Watanzania hakuacha kuwasihi kwa maneno haya, Katika mambo yetu yote tumtangulize Mungu.

Hivyo basi mafanikio yote serikali ya CCM waliyoyapata chini ya JPM yana mkono wa Mungu. Yoyote anaye simama na kuyakejeli hadharani ama akiwa mafichoni ajue anamkejeli na kumdharau Mungu pengine bila kujua. Lissu na wa aina yake wasubiri hasira ya Mungu, maana kwa hakika ijuu yao na imewaka.
 
Wote wanatuchukulia poa Sana...yaani wanatuona Sisi ni wavivu hatupendi KAZI...CCM ndio wenye KAZI zote zenye miradi mikubwa lakini wanazigawa Kwa wachina na wafungwa, Chadema wanataka wapate Uhuru wa kupiga pesa Kwa mikataba kandamizi na kuhodhi njia za uchumi, ACT wanasema na wao ni zamu Yao Kula BATA...yaani wote wanatubeba ujinga.
Sema uko upande gn acha kulia lia mkuu
 
Kumbe wanakubali kuwa sasa Kazi zinafanyika ! Ndo maana wameongeza neno BATA sijui UHURU. Yaani wana maana ya kwamba maendeleo yapo ila hakuna uhuru na bata ! .Wapinzani wanachekesha sana , alafu eti ndo Wanataka washinde Urais kwa slogans hizi !!
Onyesha uko upande upi?
 
Yaani hata slogan zimeundwa kupingana slogan za CCM. Kwanini wapinzani wasiwe tu independent, waje na slogan ambazo haziko influenced na CCM?
 
Back
Top Bottom