Hapa ni eneo gani kati ya Ubungo na Kariakoo - DSM

Hapa ni eneo gani kati ya Ubungo na Kariakoo - DSM

Ingawaje mwinuko inaonesha ni kwa Macheni (kama tuta-sticky Ubungo to K/koo) lakini sitaki kuamini kwamba ndo penyewe unless kama ni far back enzi za ukoloni. Miongoni mwa sehemu ambazo zilijengwa mapema sana ni Magomeni. Ninachokiona hapo kabla hilo lilikuwa "daladala" la Ubungo to Kariakoo lakini lilipochoka kupita kiasi, likawa linapiga route za shamba, labda from Ubungo to Kibaha or anywhere along Morogoro Rd kuelekea Kibaha. Sema dereva ili awatafune kiulaini watoto wa shamba, akaamua kuacha kibao kuwaeleza "yeye ni mtu wa Dar"! Asikuambie mtu, unaambiwa hadi miaka ya 80 tu hapo, mtu angeweza kutafuna mtaa mzima kwa kofia ya "anatoka Dar"!
Kweli , sijui kwa nn naufananisha na mlima wa kibo ukitokea ubungo , kwa Miaka ya 80 ulikuwa ni mlima haswa
 
inachokiona hapo kabla hilo lilikuwa "daladala" la Ubungo to Kariakoo lakini lilipochoka kupita kiasi, likawa linapiga route za shamba,
Lakini wangechomoa kibao, ikumbukwe enzi hizo sheria zilikuwa kali, mfano ni pale magari madogo yote yalikuwa hayaruhusiwi kutembea Jumapili baada ya saa 7 au 8 kama sijakosea, kwahiyo hata kibao kisingeachwa hapo iwapo bus lilikuwa linakwenda shamba
 
Naona kuna mlima nyuma kule, Magomeni mlima upo eneo gani Mkuu
milima ya pembezoni mwa morogoro road pale Kibanda cha mkaa bado ipo?

sa imagine miaka hio pale kama unapanda kutokea Jagwani kenda Magomeni Mapipa Hamna miinuko??

Enzi hizo Sinza ilikuwa mashamba ya mpunga
 
Pembeni naona kuna jamaa anatongoza demu. Watakuwa wameshafariki hao maana muda umepita sana au ni wazee sana umri wa Mzee Mwinyi
Una macho mazuri sana ni kweli binti anaonekana anatafuna kucha kama ishara ya "niangusage tu sambi sako mwenyewe"😂🤣
 
Pembeni naona kuna jamaa anatongoza demu. Watakuwa wameshafariki hao maana muda umepita sana au ni wazee sana umri wa Mzee Mwinyi
Sio zamani kivile,mwaka 1991 nikiwa pale kivukoni ilikuepo stand ya mabasi mikangafu kama hilo,,daladala za kawaida ilikuwa ni chai maharage,,
 
Sisiemu Revolution!!! Hongera sana awamu ya 5 kwa kuleta mabadiliko & maendeleo makubwa yanayoonekana since 2016!!!
 
Back
Top Bottom