Hapa ni Gbadolite, Kijijini kwa dikiteta Mobutu Sesseko Kuku Wazabanga, nyumba zimegeuka Magofu na mahame

Andika vitu kwa facts sio unaongea kama upo kijiweni. Huyu mtoa mada ameweka mpaka vielelezo vya picha. Na wewe tupe facts zako
Inawezekana mleta mada umri wake ni mdogo, ni kijana. Sidhani kama anajua huyo Mobutu alikaa ikulu kwa miaka mingapi.

Uhakika uliopo ni kwamba JPM mwaka 2025 atamuachia kiti mrithi wake pale uwanja wa Uhuru kama Mungu akipenda.

Msuya aliendeleza upareni, Mrema akaendeleza uchagani, ukipewa nafasi ya urais ukashindwa hata kusomesha ndugu zako au kujenga mazingira yao ya maendeleo katika siku zijazo basi wewe ni mpumbavu wa mwisho.
 
Magufuli anachota hela bila kufuata sheria na utaratibu.

Hata kama angepeleka hela kwenye most deserving location (which he doesn't) angekuwa bado aakosea kwa kupeleka hela nje ya utaratibu.

Kwa hivyo, kwa sasa anafanya makosa mawili.

1. Anapeleka miradi kwake, kwa sababu ni kwake, si kwa sababu kuna priority ya kiuchumi.

2. Anapeleka miradi kwa kuchota fedha nje ya utaratibu, open tender, na bajeti.

Huu si uongozi bora, labda bora uongozi.
 

Ahahahhaha. Sawa mkuu. Mamlaka zote duniani zimetoka kwa Mungu kwa hiyo twapaswa kuziheshimu. Ila zile tetesi za kutawala milele zote ndo inabidi tuzipinge kwa nguvu zote. Maana huko kunakopelekewa pesa bila utaratibu kutakua kama ulaya ilihali wengme ni maskini wa kutupwa.

Ebu muone huyu member maoni yake juu ya watu weusi.

Hua naamini waafrika tukibebwa kama tulivyo tukapelekwa US na US wakabebwa kama walivyo wakaletwa africa haitapita mwezi tutakuja kuomba msaada Africa tena msaada wa tech mpya kutoka Africa manake hizo za tutakazokuta kule tutaua ndani ya mwezi
 
Unasema mamlaka zote zimetoka kwa Mungu.

Unaweza kuthibitisha huyo Mungu yupo na hizo habari si uongo tu unajazwa na watu kama wewe?
 

Kama kuendeleza kwenu au kuwasaidia ndugu zako ufanye kwa pesa yako lakini sio ya walipa kodi. Hayo waliyoyafanya Msuya na Mrema yalikuwa ni makosa.
 
Kuna siku nilitembelea Butiama. Kulikuwa na Kampuni ya Ujenzi wa barabara ikifanya kazi kujenga barabara ya Makutano - Natta. Project Manager, raia wa Ethiopia akanikaribisha ofisini. Katika mazungumzo akaniambia kuwa hapo tulipokaa ndio palikuwa Ikulu ya Butiama. Na kwamba meza hiyo na chumba hicho ndiyo ilikuwa ofisi ya Mwalimu. Walikuwa wamepewa jengo lile na mke wa Baba wa Taifa watumie kama ofisi. Mwisho akaniambia kwa Kiingereza: "Your first President was a humble and a down to earth person. It is as if God wanted you Tanzanians to be a benchmark to the rest of Africa; a place where our leaders would come and learn the lessons of humbleness and humility."
Nikiifikiria CCM ya hawa mbwa mwitu wanaovaa ngozi ya kondoo, machozi yalinitoka!!!
Hakuendelea tena na mazungumzo, ikabidi kuaendelea na shughuli iliyonipeleka pale.
 
Mkuu hakuna mimi na wewe tunachoweza kufanya katika kubadilisha hali iliyopo. Ni kujitakia sononeko na maumivu ya moyo pasipo kuwa na ulazima.

Wewe kama huna moyo wa kupigania haki wapishe watu wengine waendelee. Vitu vingine sio vya kufumbia macho
 
Wewe kama huna moyo wa kupigania haki wapishe watu wengine waendelee. Vitu vingine sio vya kufumbia macho
Yale yale ya Dada Mange Kimambi, keyboard warrior. Wenye kudai haki wapo Sudan, wanakwenda barabarani kudai mabadiliko mpaka wanakuja kuyapata. Watanzania tunachokiweza ni kulialia hovyo tu.
 
Yale yale ya Dada Mange Kimambi, keyboard warrior. Wenye kudai haki wapo Sudan, wanakwenda barabarani kudai mabadiliko mpaka wanakuja kuyapata. Watanzania tunachokiweza ni kulialia hovyo tu.

Hakuna anayelia hapa. Ndio maana nikakwambia kama huna moyo wewe vaa shanga ukalale waache wanaume wa shoka wafanye kazi.
 
Hakuna anayelia hapa. Ndio maana nikakwambia kama huna moyo wewe vaa shanga ukalale waache wanaume wa shoka wafanye kazi.
Bwana mdogo unaingiza matusi baada ya kuishiwa ya hoja, ushujaa wa watu wa aina yako ni wa kulalama humu mitandaoni, hamna jeuri ya kuidai hiyo haki mnayosema kuwa imeminywa kwa kuingia mtaani.

Za kwenu ni kelele za chura, hazina uwezo wa kuyafanya maji yakawa sio matamu kwenye mdomo wa Tembo.

Sio uwanja wa ndege tu, sasa kuna hifadhi ya wanyama inayokwenda kuongeza pato la taifa kupitia utalii.
 

Hizo "kelele za chura" ndizo zilizofanya serikali kuufyata na kubadili sheria za takwimu. Nchi yetu bado ni ombaomba kwahiyo wapinzani wao wanaongea moja kwa moja na walioshika mpini ambao nyie mnawaita mabeberu halafu wao wanatoa amri kifanyike nini.
 
Tujikumbushe vituko vya huyu jamaa aliyewahi kuwa Raisi wa zamani wa Zaire. Mobutu Sese Seko Kuku Gbendu Wa Za Banga. Moja ya vitu alifanya huyu bwana mkubwa vilivyoushangaza uliwengu ni kitendo chake cha kutumia mamilioni ya dola na kwenda kubadilisha Gbadolite ( kijijini alipozaliwa) kuwa paradiso ndogo. Kwanza Alijenga bwawa la kuzalisha umeme karibu na mto Ubangi, uwanja wa ndege wa Gbadolite, Kasri kubwa na hoteli alotumia kama makazi na sehemu ya kupokelea wageni wake. Gbadolite pia kulikuwa na makampuni makubwa kama vile CDIA Zaire kwa ajili ya kilimo. SOZAGEC kampuni ya ujenzi wa barabara na SAFRICAS kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za makazi kulikuwa pia na hospitali kubwa iliyokuwa na vifaa vya kisasa ambayo iliharibiwa vibaya mwaka 1997. Mobutu pia alijenga kanisa kubwa sana lililojulikana kama Chapelle Marie la Misericorde ambapo huko ndipo alimzika mkewe mama mobutu.
Mwandishi na mpiga picha wa gazeti Guardian la uingereza bwana Sean Smith alisafiri mpaka Jamhuri ya kidemokrasia ya kongo iliyokuwa zaire na kutuletea picha ya yaliyomo Gbadolite ya sasa.

https://www.theguardian.com/cities/...e-mobutu-ruined-jungle-city-in-pictures#img-1

Hii ni iliyokuwa air-traffic control tower ya Gbadolite international airport, ambayo runway yake ilikuwa ndefu kuwezesha ndege aina ya Concorde kutua (concorde zilikuwa ndege maarufu kubwa za abiria miaka ya 1979 hadi 2003 zilizokuwa na uwezo wa kubeba abiria 92 hadi 128.
Picha zote na Sean Smith wa gazeti la Guardian la uingereza



  • hapa ni ndani ya air control tower iliyotelekezwa kama inavyoonekana.


  • Hii ni VIP arrivals terminal: sehemu ya kupokelea wageni muhimu ambapo watu maarufu kama vile Pope John Paul II, UN secretary-general Boutros Boutros Ghali walipita hapa.


    Hapa ni ndani main airport terminal






  • hili ni jengo la wizara ya Maji ambalo halikumalizika na sasa linatumika kama shule.
  • ndani ya shule




  • Hii inaitwa Motel Nzekele, iliyojengwa na mobutu kijijini kwao. ilikuwa na hadhi ya nyota tano kipindi inafunguliwa mwaka 1979.


  • Bwawa tupu la kuogelea kama linavyoonekana kwa picha. wageni mblimbali mashuhuri wanaoripotiwa kufika katika moteli hii ni pamoja na Papa wa kanisa katoliki, mfalme wa Ubelgiji, na raisi wa ufaransa , François Mitterrand


  • kumbi ya kuangalia cinema Motel Nzekel


  • Picha ya daraja ambalo halikufanikiwa kumalizika kwatika kijiji cha Gbadolite





  • Hili ni geti la kuingilia makazi binafsi ya Mobutu kijijini kwao. wakazi wa hapa wanatoza dola 20 kwa wageni kuingia na kutazama.







  • Kwa majina mengine walipaita Mobutu’s palace. katika makazi haya waliajiriwa wafanyakazi zaidi ya 700 staff wakiwemo wapishi, vijakazi na wanajeshi 300 soldiers


  • Ndani ya viwanja vya kasri la mobutu ambapo taratibu pameanza kumezwa na vichaka.


  • Hii ilikuwa chemchem ya ndani ya kasri hilo iliyokuwa na sanamu la simba lililochongwa wa ustadi wa hali ya juu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…