Hapa nishaibiwa au niendelee kujifariji?

Hapa nishaibiwa au niendelee kujifariji?

Mimi ni mwanafunzi wa chuo kikuu hapa Morogoro(SUA) nina mpenzi wangu ambaye naye yupo chuo kikuu Moshi (Mweka), lakini tangu aende chuo nimekua simuelewi kabisa.

Nikipiga simu anasema amechoka wakati zamani alikuwa anapiga hadi saa 7, sms nikituma hajibu nisipoanza hata anitafuti lakini nampenda sana.

Naombeni ushauri nifanye nini ili penzi letu lisivunjike?
Pole ila we komaan na shule, demu sio wako huyo washamchukua.
 
Acha kuwazia kiumbe dhaifu huyo, hakuongezei wala kupunguza chochote. Tafuta mwingine achana na mawazo yasiyo kufikisha popote.
 
Back
Top Bottom