Harakati za wagonga ulimbo kwenye kutafuta ajira

Harakati za wagonga ulimbo kwenye kutafuta ajira

kante mp2025

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2022
Posts
631
Reaction score
1,192
Mbele yenu ni kijana wa kitanzania mpambanaji ninayechukia kukata tamaa, Kwani kukata tamaa ndio mwanzo wa umaskini.

Leo nimeona nishare visa tunavyokumbana navyo wagonga ulimbo hasa graduates katika kutafuta ajira rasmi hasa sisi tuliotokea kwenye familia duni ambazo ikihitajika laki moja basi ukoo mzima lazima mjichange.

Basi bhana tokea nimalize chuo kichwani nilikuwa tayari nimejiandaa kisaikolojia kuhusu changamoto ya ajira kwani nilikuwa napenda sana kusikiliza visa na mikasa vya mabraza ambao tayari walinitangulia kumaliza jinsi walivyokuwa wanapambana walau kupata japo hata mchongo wa laki mbili na bado wanaikosa.

Hivyo basi wakati wenzangu hasa wale watoto wa Dady Me I Want To Party"" walipokuwa wakizimimina shampeni kwa fujoo siku ya mahafali ya chuo pale makao makuu, Mimi kiumbe wa Mungu nilikuwa kwenye msongo mkubwa wa mawazo maana sikuwa hata na ndugu ambae alikuja kwenye mahafali yangu nikajikuta najutia uamuzi wa kufanya sherehe ile.

Lakini niliazimia kufanya sherehe ya kuhitimu maana kitendo cha mimi kuhitimu ilikuwa ni muujiza mkuu ukizingatia ndio msomi pekee wa taaluma hiyo katika ukoo wangu, lakini pia mapito niliyopitia hadi kumaliza chuo yalinipa nguvu ya kuhisi ninapaswa nishiriki graduation maana hapo kati nilihairisha mwaka kwa kukosa ada, pili yale maisha ya kula ili niishi nikimaanisha ile kula mara moja kwa siku kama niko kwaresima yote hayo yalinipa sababu ya kushiriki sherehe ile ya mahafali chuoni.

Nikiwa katika dimbwi zito la mawazo ndipo nikawa nasikia wazazi wa watoto wa Dady me i want to party wakiwaahidi mambo makubwa makubwa vijana wanaomaliza pale, Niliwasikia baadhi wakiwaambia watoto wao kuwa nishaongea na yule mkurugenzi ukipata tu cheti chako kuna nafasi pale Mloganzila, wengine wakazitaja sehemu kubwa kubwa tu.

Hapo mimi mgonga ulimbo na joho langu nikawa na simanzi sana hasa nikiwa sina ramani yeyote ile ya kujua nitaelekea wapi, nikiyakumbuka mazingira ya kule kijijini kwetu ambako kupata network ya mtandao hadi upandishe vilima nikawa nayaona tu mashamba ya mahindi yakiningojea kwenda kuyakatua.

Lakini pia nikakumbuka wazazi na wanakijiji wananiona mimi kama kijana wa mfano, ukizingatia kule kijijini msomi anaheshimika vibaya mno na wanaamini elimu ndio ufunguo wa maisha.

Nikawaza nikiwa chini ya mti nimejiinamia je nirudi bush, Nikakumbuka hata nauli ya kunirudisha tu bush sina mfukoni nina elfu ishirini tu niliyopatiwa na mwalimu wangu kama zawadi ya kunipongeza kuhitimu, huku geto nikiwa na kiroba cha unga alioniagizia mama toka kijijini na kipeto cha viazi na gesi ipo nikasema hapa ni kukaza tu sina connection ila Mungu hutengeneza connection.

Basi wengine wakiwa wanaelekea kwenye kumbi za kisasa kusherekea sherehe yao ya kuhitimu na familia zao wengine wakiwa na misafara ya magari, Mimi kwa kutumia usafiri adhimu wa miguu nikaanza kujirudisha magetoni huku nikiwa na msongo mzito wa mawazo.

Nikiwa njiani wakati naelekea magetoni ghafla nikasimamishwa na chombo kimoja cha usafiri ambacho ndani yake kulikuwa na mtu anaenifahamu na anayewafahamu wazazi wangu kule kijijini, akaniuliza vipi hukuwaambia nduguzo kuwa uko na sherehe mbona upo mwenyew mwenyew nikabrush kuwa aah niliona nisiwasumbue, kwa kuwa yule ni mtu mzima akajiongeza na kunambia nawe ingia humu akaniunganisha kwenye sherehe ya ndugu yao mmoja aliekuwa anamaliza pale

Ambapo ilifanyika sehemu moja nzuri sana hivyo kiumbe wa Mungu nikapata kula vyuku na soda siku hiyo kwa hisani ya watu wema na si haba walinipa na zawadi japo kimoyo moyo nilikuwa najisikia vibaya maana kwa kila kinachotokea nikawa nasema huenda tungekuwa na mapesa kama watoto wa Dady Me i want to party basi nami ningepigwa kasherehe fulani hivi ka kitaita, Nawashukuru sana watu wale.

Ile sherehe ilipokwisha nikarudi kwenye zone yangu "Stress zone* nikiwa najirudisha kwenye kiota changu na si haba na zile zawadi za watu wale wema nikajikuta nina kama elfu sitini mfukoni.Kichwani nikawa na swali moja kubwa NAANZIA WAPI KUJITAFUTA BAADA YA KUHITIMU....

Fuatana nami kiumbe wa Mungu kwenye safari hii ya harakati za wagonga ulimbo💉
 
Mbele yenu ni kijana wa kitanzania mpambanaji ninayechukia kukata tamaa, Kwani kukata tamaa ndio mwanzo wa umaskini.

Leo nimeona nishare visa tunavyokumbana navyo wagonga ulimbo hasa graduates katika kutafuta ajira rasmi hasa sisi tuliotokea kwenye familia duni ambazo ikihitajika laki moja basi ukoo mzima lazima mjichange.

Basi bhana tokea nimalize chuo kichwani nilikuwa tayari nimejiandaa kisaikolojia kuhusu changamoto ya ajira kwani nilikuwa napenda sana kusikiliza visa na mikasa vya mabraza ambao tayari walinitangulia kumaliza jinsi walivyokuwa wanapambana walau kupata japo hata mchongo wa laki mbili na bado wanaikosa.


Hivyo basi wakati wenzangu hasa wale watoto wa Dady Me I Want To Party"" walipokuwa wakizimimina shampeni kwa fujoo siku ya mahafali ya chuo pale makao makuu, Mimi kiumbe wa Mungu nilikuwa kwenye msongo mkubwa wa mawazo maana sikuwa hata na ndugu ambae alikuja kwenye mahafali yangu nikajikuta najutia uamuzi wa kufanya sherehe ile.

Lakini niliazimia kufanya sherehe ya kuhitimu maana kitendo cha mimi kuhitimu ilikuwa ni muujiza mkuu ukizingatia ndio msomi pekee wa taaluma hiyo katika ukoo wangu, lakini pia mapito niliyopitia hadi kumaliza chuo yalinipa nguvu ya kuhisi ninapaswa nishiriki graduation maana hapo kati nilihairisha mwaka kwa kukosa ada, pili yale maisha ya kula ili niishi nikimaanisha ile kula mara moja kwa siku kama niko kwaresima yote hayo yalinipa sababu ya kushiriki sherehe ile ya mahafali chuoni.

Nikiwa katika dimbwi zito la mawazo ndipo nikawa nasikia wazazi wa watoto wa Dady me i want to party wakiwaahidi mambo makubwa makubwa vijana wanaomaliza pale, Niliwasikia baadhi wakiwaambia watoto wao kuwa nishaongea na yule mkurugenzi ukipata tu cheti chako kuna nafasi pale Mloganzila, wengine wakazitaja sehemu kubwa kubwa tu.

Hapo mimi mgonga ulimbo na joho langu nikawa na simanzi sana hasa nikiwa sina ramani yeyote ile ya kujua nitaelekea wapi, nikiyakumbuka mazingira ya kule kijijini kwetu ambako kupata network ya mtandao hadi upandishe vilima nikawa nayaona tu mashamba ya mahindi yakiningojea kwenda kuyakatua.

Lakini pia nikakumbuka wazazi na wanakijiji wananiona mimi kama kijana wa mfano, ukizingatia kule kijijini msomi anaheshimika vibaya mno na wanaamini elimu ndio ufunguo wa maisha.

Nikawaza nikiwa chini ya mti nimejiinamia je nirudi bush, Nikakumbuka hata nauli ya kunirudisha tu bush sina mfukoni nina elfu ishirini tu niliyopatiwa na mwalimu wangu kama zawadi ya kunipongeza kuhitimu, huku geto nikiwa na kiroba cha unga alioniagizia mama toka kijijini na kipeto cha viazi na gesi ipo nikasema hapa ni kukaza tu sina connection ila Mungu hutengeneza connection.

Basi wengine wakiwa wanaelekea kwenye kumbi za kisasa kusherekea sherehe yao ya kuhitimu na familia zao wengine wakiwa na misafara ya magari, Mimi kwa kutumia usafiri adhimu wa miguu nikaanza kujirudisha magetoni huku nikiwa na msongo mzito wa mawazo.

Nikiwa njiani wakati naelekea magetoni ghafla nikasimamishwa na chombo kimoja cha usafiri ambacho ndani yake kulikuwa na mtu anaenifahamu na anayewafahamu wazazi wangu kule kijijini, akaniuliza vp hukuwaambia nduguzo kuwa uko na sherehe mbona upo mwenyew mwenyew nikabrush kuwa aah niliona nisiwasumbue, kwa kuwa yule ni mtu mzima akajiongeza na kunambia nawe ingia humu akaniunganisha kwenye sherehe ya ndugu yao mmoja aliekuwa anamaliza pale ambapo ilifanyika sehemu moja nzuri sana hivyo kiumbe wa Mungu nikapata kula vyuku na soda siku hiyo kwa hisani ya watu wema na si haba walinipa na zawadi japo kimoyo moyo nilikuwa najisikia vibaya maana kwa kila kinachotokea nikawa nasema huenda tungekuwa na mapesa kama watoto wa Dady Me i want to party basi nami ningepigwa kasherehe fulani hivi ka kitaita, Nawashukuru sana watu wale.

Ile sherehe ilipokwisha nikarudi kwenye zone yangu "Stress zone* nikiwa najirudisha kwenye kiota changu na si haba na zile zawadi za watu wale wema nikajikuta nina kama elfu sitini mfukoni.Kichwani nikawa na swali moja kubwa NAANZIA WAPI KUJITAFUTA BAADA YA KUHITIMU....


Fuatana nami kiumbe wa Mungu kwenye safari hii ya harakati za wagonga ulimbo💉
Basi bhan mida ya saa mbili usiku mgonga ulimbo nikafika kwenye kiota changu kujipumzisha huku nikitambua siku mbili mbele napaswa kurejesha joho na hivo kuanz kutambulika kama mwananchi wa kawaida rasmi😁

Kiukweli kwangu mimi ilikuwa tofauti sana na wengine ambao wakimaliza chuo eti huwa wanalikumbuka bata la chuo mimi kumaliza chuo ilikuwa ni kama kushusha gunia la moto kichwani ,maisha ya chuo kwangu yalikuwa jehanamu ndogo wakati wengine siku za ijumaa wakienda out za usiku usiku mimi mgonga ulimbo hizo weeknd nilikuwa nina usajiri rasmi kwa bakhresa kama muuza ukwaju aliyetukuka hivo zilikuwa ni siku za kwenda kuswampa kuuza ukwaju nipate walau ya kula.

Wakati wengine wakimiliki mademu wakali pale chuo mimi Mapenzi niliyaona kama anasa hata nilipojaribu kutongoza nilijibiwa majibu ya kwenda kulilia chooni maana baadhi hawakuogopa kunambia ukweli mchungu wa kuwa am not their type, and it was true lol😂

Hivo basi nikaazimia kazi yeyote itakayojitokeza mbele yangu baada ya kumaliza chuo mimi nipo tayari kuifanya, Kituo cha kwanza ikawa ni harakati zangu za Mungu nipe pesa ya kula za kuuza ukwaju kwa yale mabegi unatembea mchana wa jua kali mpaka nyayo na utosi vinaanza kupumua kama hirizi huku vikifuka moshi wa mvuke wa jua.

Ashukuriwe bakhresa ile harakati ni rahisi sana kuipata na kwa wale wapambania tumbo ilituokoa sana kutupa buku mbili za kula kwa mama ntilie.Punde si punde nikaona tangazo la kazi kwenye bar & restaurant kali sana mjini nikajisemea lahaula hapa naenda kurusha nyavu, kumbuka mimi ni mkristo ninayenena hadi kwa lugha ila nikajisemea hata hii naomba Mungu baba nisaidie.

Guess what nilipata kazi pale kama waiter bila hata kuwa na cheti cha hotel management , kazi ikaanza na niliipenda na kufanya kwa moyo ila nikajisemea sitakunywa pombe ijapokuwa nauza pombe...😁Sio kazi rahisi wagonga ulimbo wenzangu, kwa kuwa kazi ile ilikuwa inafanyika ndani ya very comfortable environment with full A.C included asee hata ka ngozi kangu kalianza kunawiri ukizingatia kuna kuonja onja vyakula vya watoto wa Dady Me I Want To Party nikapata na shavu la kuzugia.

Changamoto ilikuwa pale unakutana na mates wenzako ambao ndani ya muda mfupi washapata michongo ya dollari maana walishaingia kwenye mfumo kwa tiketi ya baba kanituma, Walipokuwa wanakuja kujivinjari na wapenzi wao, Kiumbe wa Mungu nilikuwa nawanawisha mikono kwa bashasha kubwa sana lakini moyo una maumivu makali ya kumuuliza Mungu ni lini saa yangu ya kutimiziwa haja za moyo wangu??....
 
Basi bhan mida ya saa mbili usiku mgonga ulimbo nikafika kwenye kiota changu kujipumzisha huku nikitambua siku mbili mbele napaswa kurejesha joho na hivo kuanz kutambulika kama mwananchi wa kawaida rasmi😁

Kiukweli kwangu mimi ilikuwa tofauti sana na wengine ambao wakimaliza chuo eti huwa wanalikumbuka bata la chuo mimi kumaliza chuo ilikuwa ni kama kushusha gunia la moto kichwani ,maisha ya chuo kwangu yalikuwa jehanamu ndogo wakati wengine siku za ijumaa wakienda out za usiku usiku mimi mgonga ulimbo hizo weeknd nilikuwa nina usajiri rasmi kwa bakhresa kama muuza ukwaju aliyetukuka hivo zilikuwa ni siku za kwenda kuswampa kuuza ukwaju nipate walau ya kula.

Wakati wengine wakimiliki mademu wakali pale chuo mimi Mapenzi niliyaona kama anasa hata nilipojaribu kutongoza nilijibiwa majibu ya kwenda kulilia chooni maana baadhi hawakuogopa kunambia ukweli mchungu wa kuwa am not their type, and it was true lol😂

Hivo basi nikaazimia kazi yeyote itakayojitokeza mbele yangu baada ya kumaliza chuo mimi nipo tayari kuifanya, Kituo cha kwanza ikawa ni harakati zangu za Mungu nipe pesa ya kula za kuuza ukwaju kwa yale mabegi unatembea mchana wa jua kali mpaka nyayo na utosi vinaanza kupumua kama hirizi huku vikifuka moshi wa mvuke wa jua.

Ashukuriwe bakhresa ile harakati ni rahisi sana kuipata na kwa wale wapambania tumbo ilituokoa sana kutupa buku mbili za kula kwa mama ntilie.Punde si punde nikaona tangazo la kazi kwenye bar & restaurant kali sana mjini nikajisemea lahaula hapa naenda kurusha nyavu, kumbuka mimi ni mkristo ninayenena hadi kwa lugha ila nikajisemea hata hii naomba Mungu baba nisaidie.

Guess what nilipata kazi pale kama waiter bila hata kuwa na cheti cha hotel management , kazi ikaanza na niliipenda na kufanya kwa moyo ila nikajisemea sitakunywa pombe ijapokuwa nauza pombe...😁Sio kazi rahisi wagonga ulimbo wenzangu, kwa kuwa kazi ile ilikuwa inafanyika ndani ya very comfortable environment with full A.C included asee hata ka ngozi kangu kalianza kunawiri ukizingatia kuna kuonja onja vyakula vya watoto wa Dady Me I Want To Party nikapata na shavu la kuzugia.

Changamoto ilikuwa pale unakutana na mates wenzako ambao ndani ya muda mfupi washapata michongo ya dollari maana walishaingia kwenye mfumo kwa tiketi ya baba kanituma, Walipokuwa wanakuja kujivinjari na wapenzi wao, Kiumbe wa Mungu nilikuwa nawanawisha mikono kwa bashasha kubwa sana lakini moyo una maumivu makali ya kumuuliza Mungu ni lini saa yangu ya kutimiziwa haja za moyo wangu??....
Kwa kuw kazi ile ya waiter nilikuw naifanya kw moyo kweli na nilikuwa nakuwa inspired na watu wenye magari mazuri sana wakiwa wameyapaki nje huku wakipata moja baridi moja moto ndani kwangu mimi ile sehemu niliibatiza jina la "Inspirational Zone" sehemu ile ilinifanya niamini ile kauli ya sema sina hela usiseme hatun hela, Ilikuwa ni kawaida sana kwa watoto wa Dady Me I Want To Party kuagiza kuku mzima akaishia kula kipaja tu na asitake umfungie arudi nayo nyumbani...U can imagine mgonga ulimbo hiyo kuku nilikuwa naenda kuidust wapi😁😁kama sio around duodenum & colon sphincter...Kiukweli kwa wakati ule nilikuwa natamani kupata harakati ya kunipa kula tu na harakati ile ilinisaidia sana sana hapo nasubiria mavyeti yangu yatoke huku pia nikijiandaa na pepa la leseni nikiamini nikishakuwa na nyaraka zote muhimu basi kazi hii hapaaa🤣Kumbe kwa ground huwa kuna maelekezo bhana sio rahisi kihivo.

Namshukuru Mungu pamoja na kufanya kazi katika mazingira yale sikujiingiza kuvuta bhangi , sigara ila pombe nilishawahi zionja onja hasa pale watoto wa Dady Me I Want To Party walipokuwa wanaagiza St .Ann Wine kubwa wanakunywa glass moja iliyobaki wanaacha nikawa nagusa gusa wine pombe kali sikuwahi na sitawahi...hapa niko honest.

Siku nazo zikasonga nikafanya hiyo pepa ya leseni na Mungu sio nyau mara nyingi wagonga ulimbo hata katika nyakati ngumu huwa tunatoboa nikafaulu na kukamilisha michakato yote ya kuipata, nikaandaa CV na kusema kwa kuwa sasa nyaraka zote zipo ni ile saa ya kuanza kutuma ballistic missisles kwenye taasisi ,mashirika n.k

Hapa ndipo safari ya mtumbwi wa vibwengo inaanza😁
 
Mkuu kante mp2025

Shukurani kwa habari hii inayotupa moyo wengi.

Nchi yetu inajinyima vipaji vya watu wengi wenye uwezo kazini lakini ambao hawana connections.

Habari ya kupata kazi imekuwa ngumu mpaka watu wengi hawajui kuwa mtu kupata kazi aliyoisomea au aliyo na uzoefu nayo ni haki ya kikatiba na kibinadamu.

Inasikitisha sana kuona watu wanakosa kazi katika nchi yenye potential kubwa sana.
 
Mkuu kante mp2025

Shukurani kwa habari hii inayotupa moyo wengi.

Nchi yetu inajinyima vipaji vya watu wengi wenye uwezo kazini lakini ambao hawana connections.

Habari ya kupata kazi imekuwa ngumu mpaka watu wengi hawajui kuwa mtu kupata kazi aliyoisomea au aliyo na uzoefu nayo ni haki ya kikatiba na kibinadamu.

Inasikitisha sana kuona watu wanakosa kazi katika nchi yenye potential kubwa sana.
Mkuu acha tu kupata kazi imekuwa changamoto sana

Kuna muda huwa naviangalia vyeti vyangu vya kuhitimu nabaki kushika tama tu na kusikitika

Hasa nikikumbuka wazazi walivojinyima na wakauza mashamba ili nisome lakini mpaka muda huu mambo bila bila
 
Mkuu acha tu kupata kazi imekuwa changamoto sana

Kuna muda huwa naviangalia vyeti vyangu vya kuhitimu nabaki kushika tama tu na kusikitika

Hasa nikikumbuka wazazi walivojinyima na wakauza mashamba ili nisome lakini mpaka muda huu mambo bila bila
Pigania hivyo hivyo tu.

Kawaida ni kwamba mtu mpiganaji huwa anaonekana, mtu smart huwa anaonekana, kitu kibaya ni kukata tamaa.

Umenifurahisha kwa spirit yako ya kutochagua kazi. Humo humo katika kutochagua kazi kuna sehemu watu wanaojua kuangalia kitu kinaitwa "human potential" wanaweza kukuona na kushangaa inakuwaje mtu mwenye uwezo mkubwa na aliyesoma anafanya kazi ambayo haitumii hata nusu ya uwezo wake.

Kuna watu wema wakiona hivyo wanatoa michongo. Wengine wamepitia humo humo wakiona story yako wanakumbuka na wao walivyokuwa wanapambana kabla ya kutoboa, wanakushika mkono na kukufungulia njia.

Nchi yetu tunapigana sana, tunatekana sana, tunabaguana sana, tunahitaji kufadhiliana zaidi, kushikana mikono zaidi na kuoneshana njia zaidi.

Mimi bahati mbaya siku hizi najikuta napoteza sana networks za home hapo, na washua wa zamani wale ma Godfather kina Mzee Malai, Mzee Mengi, Mzee Mufuruki etc wengi washatangulia tayari wanaibuka watu wapya hatuwajui tumekaa Marekani miaka mingi sana sasa mpaka network zinahama wanakuja wageni tusiowajua kuchukua nchi.
 
Mambo kwenye ground sio mepes
Tunaendelea na safaru yet
Kwa kuw kazi ile ya waiter nilikuw naifanya kw moyo kweli na nilikuwa nakuwa inspired na watu wenye magari mazuri sana wakiwa wameyapaki nje huku wakipata moja baridi moja moto ndani kwangu mimi ile sehemu niliibatiza jina la "Inspirational Zone" sehemu ile ilinifanya niamini ile kauli ya sema sina hela usiseme hatun hela, Ilikuwa ni kawaida sana kwa watoto wa Dady Me I Want To Party kuagiza kuku mzima akaishia kula kipaja tu na asitake umfungie arudi nayo nyumbani...U can imagine mgonga ulimbo hiyo kuku nilikuwa naenda kuidust wapi😁😁kama sio around duodenum & colon sphincter...Kiukweli kwa wakati ule nilikuwa natamani kupata harakati ya kunipa kula tu na harakati ile ilinisaidia sana sana hapo nasubiria mavyeti yangu yatoke huku pia nikijiandaa na pepa la leseni nikiamini nikishakuwa na nyaraka zote muhimu basi kazi hii hapaaa🤣Kumbe kwa ground huwa kuna maelekezo bhana sio rahisi kihivo.

Namshukuru Mungu pamoja na kufanya kazi katika mazingira yale sikujiingiza kuvuta bhangi , sigara ila pombe nilishawahi zionja onja hasa pale watoto wa Dady Me I Want To Party walipokuwa wanaagiza St .Ann Wine kubwa wanakunywa glass moja iliyobaki wanaacha nikawa nagusa gusa wine pombe kali sikuwahi na sitawahi...hapa niko honest.

Siku nazo zikasonga nikafanya hiyo pepa ya leseni na Mungu sio nyau mara nyingi wagonga ulimbo hata katika nyakati ngumu huwa tunatoboa nikafaulu na kukamilisha michakato yote ya kuipata, nikaandaa CV na kusema kwa kuwa sasa nyaraka zote zipo ni ile saa ya kuanza kutuma ballistic missisles kwenye taasisi ,mashirika n.k

Hapa ndipo safari ya mtumbwi wa vibwengo inaa

Pigania hivyo hivyo tu.

Kawaida ni kwamba mtu mpiganaji huwa anaonekana, mtu smart huwa anaonekana, kitu kibaya ni kukata tamaa.

Umenifurahisha kwa spirit yako ya kutochagua kazi. Humo humo katika kutochagua kazi kuna sehemu watu wanaojua kuangalia kitu kinaitwa "human potential" wanaweza kukuona na kushangaa inakuwaje mtu mwenye uwezo mkubwa na aliyesoma anafanya kazi ambayo haitumii hata nusu ya uwezo wake.

Kuna watu wema wakiona hivyo wanatoa michongo. Wengine wamepitia humo humo wakiona story yako wanakumbuka na wao walivyokuwa wanapambana kabla ya kutoboa, wanakushika mkono na kukufungulia njia.

Nchi yetu tunapigana sana, tunatekana sana, tunabaguana sana, tunahitaji kufadhiliana zaidi, kushikana mikono zaidi na kuoneshana njia zaidi.

Mimi bahati mbaya siku hizi najikuta napoteza sana networks za home hapo, na washua wa zamani wale ma Godfather kina Mzee Malai, Mzee Mengi, Mzee Mufuruki etc wengi washatangulia tayari wanaibuka watu wapya hatuwajui tumekaa Marekani miaka mingi sana sasa mpaka network zinahama wanakuja wageni tusiowajua kuchukua nchi.
Asante sana ndugu yangu kwa maneno ya kunitia moyo na kunifariji nami sikati tamaa naamini siku yangu yaja
Pigania hivyo hivyo tu.

Kawaida ni kwamba mtu mpiganaji huwa anaonekana, mtu smart huwa anaonekana, kitu kibaya ni kukata tamaa.

Umenifurahisha kwa spirit yako ya kutochagua kazi. Humo humo katika kutochagua kazi kuna sehemu watu wanaojua kuangalia kitu kinaitwa "human potential" wanaweza kukuona na kushangaa inakuwaje mtu mwenye uwezo mkubwa na aliyesoma anafanya kazi ambayo haitumii hata nusu ya uwezo wake.

Kuna watu wema wakiona hivyo wanatoa michongo. Wengine wamepitia humo humo wakiona story yako wanakumbuka na wao walivyokuwa wanapambana kabla ya kutoboa, wanakushika mkono na kukufungulia njia.

Nchi yetu tunapigana sana, tunatekana sana, tunabaguana sana, tunahitaji kufadhiliana zaidi, kushikana mikono zaidi na kuoneshana njia zaidi.

Mimi bahati mbaya siku hizi najikuta napoteza sana networks za home hapo, na washua wa zamani wale ma Godfather kina Mzee Malai, Mzee Mengi, Mzee Mufuruki etc wengi washatangulia tayari wanaibuka watu wapya hatuwajui tumekaa Marekani miaka mingi sana sasa mpaka network zinahama wanakuja wageni tusiowajua kuchukua nchi.
Asante sana mkuu na nimekuelewa sana sana mapambano yanaendelea na hakuna kukata tamaa.

Naamini ipo siku nitakuja kutoa ushuhuda hapa wa "from trench to triumph" kwa kuwa bado niko hai basi zawadi hii ya uhai lazima niitumie vema kwenye mapambano.


Muhimu ni kuhakikisha nawasaidia wale wazee maana wana imani sana na kijana wao sema ndio vile mambo hayajajipa bado.Walijinyima sana kwa ajili yangu sema ni kama serikali huwa haitambui hilo.

Kupata ajira limekuwa suala gumu sana na wanasiasa wanaosema vijana wajiajiri wengi huwa hawawazi wapi watapata hiyo mitaji.

Wakuu wa ajira portal kiumbe wa Mungu sitochoka kutuma maombi😄labda ipo siku nami nitapata kuingia kwenye mifumo ya kumiliki checknumber

Sisi ndo wale tunaotamani kupata hata michongo ya laki mbili tutume pesa za matibabu kijijini kwa wazee wetu.
 
Tunaendelea na safaru yet



Asante sana ndugu yangu kwa maneno ya kunitia moyo na kunifariji nami sikati tamaa naamini siku yangu yaja

Asante sana mkuu na nimekuelewa sana sana mapambano yanaendelea na hakuna kukata tamaa.

Naamini ipo siku nitakuja kutoa ushuhuda hapa wa "from trench to triumph" kwa kuwa bado niko hai basi zawadi hii ya uhai lazima niitumie vema kwenye mapambano.


Muhimu ni kuhakikisha nawasaidia wale wazee maana wana imani sana na kijana wao sema ndio vile mambo hayajajipa bado.Walijinyima sana kwa ajili yangu sema ni kama serikali huwa haitambui hilo.

Kupata ajira limekuwa suala gumu sana na wanasiasa wanaosema vijana wajiajiri wengi huwa hawawazi wapi watapata hiyo mitaji.

Wakuu wa ajira portal kiumbe wa Mungu sitochoka kutuma maombi😄labda ipo siku nami nitapata kuingia kwenye mifumo ya kumiliki checknumber

Sisi ndo wale tunaotamani kupata hata michongo ya laki mbili tutume pesa za matibabu kijijini kwa wazee wetu.
Hizo kauli za "vijana jiajirini" za wanasiasa kwa kiasi kikubwa ni kauli za mtu aliyeshiba ambaye hamjui mwenye njaa.

Ni kauli za kisiasa zaidi zisizotambua au kudogosha ukweli kwamba kujiajiri kunataka maandalizi, mtaji, support ya kimfumo etc. Watu hao hao ukiwaendea una business plan nzuri sana unahitaji mkopo au hata mtu wa kuwekeza naye hawakupi mkopo, na wanaweza hata kukuibia idea yako wakaifanyia kazi wao kivyao.
 
Hizo kauli za "vijana jiajirini" za wanasiasa kwa kiasi kikubwa ni kauli za mtu aliyeshiba ambaye hamjui mwenye njaa.

Ni kauli za kisiasa zaidi zisizotambua au kudogosha ukweli kwamba kujiajiri kunataka maandalizi, mtaji, support ya kimfumo etc. Watu hao hao ukiwaendea una business plan nzuri sana unahitaji mkopo au hata mtu wa kuwekeza naye hawakupi mkopo, na wanaweza hata kukuibia idea yako wakaifanyia kazi wao kivyao.
Mkuu hapa umeongea ukweli mchungu sana na kiuhalisia hata ile mikopo ambayo huwa wanaipigia chapuo kuwa ni kwa ajili ya vijana mara nyingi haiwafikii walengwa.


Hivo chain ya umaskini kubaki pale pale na matajiri kuendelea kuneemeshana hata kwa kile ambacho maskini alipaswa akipate ili ajikwamue na hali yake ya maisha.

Ukweli ni kwamba asilimia kubwa ya graduates wetu wana msongo wa mawazo hasa wale wanaotokea familia za kipato cha chini, Mtu anayetokea familia ya kipato cha juu hawezi nielewa maneno yangu na ndio hao wanasema vijana hawapo serious "Mwenye shibe hamjui mwenye njaa"

Ila uzuri ni kwamba hatujakata tamaa tunapambana na tunaamini watu wema bado wapo, Watu wema ambao wanaweza kukutoa kwenye giza na kukupeleka kwenye mwanga.

Wakati fulani 2021 nilipohairisha masomo kwa kukosa ada, wapo watu wema ambao walinishika mkono dogo nikarudi shule na kumaliza masomo yangu "Wema wao hausahauliki kwangu nami nitawatendea hivo wengine katika siku zijazo"

Mifumo yetu ya ajira sio rafiki sana na mzizi wa kujuana inapaswa ufe.


Sisi wagonga ulimbo tunaamini ipo siku yetu muhimu tusipoteze focus tu tutachelewa ila tutafika.
 
Back
Top Bottom