Harakati za wagonga ulimbo kwenye kutafuta ajira

Harakati za wagonga ulimbo kwenye kutafuta ajira

Asante sana mkuu mapambano yanaendelea
Mboni haujamaliza au ndio itaendelea? Kuna limwanasiasa linapitapita kwenye uzi wako linasema nenda kajiajiri wewe masikini nenda kafie kule wewe masikini kafie mbele na umasikini wako bila kujua wewe ndie uliempigia kura kumamamakezake
 
Msoto bado unaendelea mkuu w wakuu nikijipata nitakuja kutoa ushuhuda

kwa ground mambo magumu sana sana
Kuna limwanasiasa linakwambia kafie mbele kule wewe masikini nenda kajiajiri wewe masikini kesho hilo hilo linamwanasiasa linakufuata kukuomba kura
 
Ni kauli za kisiasa zaidi zisizotambua au kudogosha ukweli kwamba kujiajiri kunataka maandalizi, mtaji, support ya kimfumo etc. Watu hao hao ukiwaendea una business plan nzuri sana unahitaji mkopo au hata mtu wa kuwekeza naye hawakupi mkopo, na wanaweza hata kukuibia idea yako wakaifanyia kazi wao kivyao.
Mikopo ya Halmashauri wanapeana wao wenyewe na watoto wao
 
Mkuu hapa umeongea ukweli mchungu sana na kiuhalisia hata ile mikopo ambayo huwa wanaipigia chapuo kuwa ni kwa ajili ya vijana mara nyingi haiwafikii walengwa.
Hio mikopo ni ya kwao wenyewe kwa changa la macho complications ni nyingi sana nilishawahi kuandaa proposal ya kuomba mkopo kwa kikundi cha vijana kwenye Halmashauri fulani oyaa ngoja nipite hivi
 
Hio mikopo ni ya kwao wenyewe kwa changa la macho complications ni nyingi sana nilishawahi kuandaa proposal ya kuomba mkopo kwa kikundi cha vijana kwenye Halmashauri fulani oyaa ngoja nipite hivi
Mpaka uwe na kadi ya chama.
 
Mifumo yetu ya ajira sio rafiki sana na mzizi wa kujuana inapaswa ufe.
Hili suala la mfumo wewe mtoto wa mzazi wa kipato cha chini hakuna mzazi utamwambia atakuelewa sana sana atakwambia mbona yule mtoto wa fulani nyumba ile amepata ajira na sasa ni pharmasia kwenye hospitali fulani unabakia kutokwa na macho tu maana hata umuelekeze kuhusu ajira portal utumishi sekretari ya ajira ofisi ya rais sijui amefanya nini katibu hakuna mzazi atakuelewa kwanza anakuona unamletea dharau kwa kumuona yeye hajui mambo ya mitandao
 
Mpaka uwe na kadi ya chama.
Sisi ndio wale ikitokea Mama akigongwa na nyoka na hospital wakadai 150,000 basi ukoo mzima inabidi ujichange na bado pamoja na wote kujichanga haitimii hio 150,000 sana sana Mama atafia hospitali kwa kukosa 150,000 za kulipia dawa ili apone
 
Mboni haujamaliza au ndio itaendelea? Kuna limwanasiasa linapitapita kwenye uzi wako linasema nenda kajiajiri wewe masikini nenda kafie kule wewe masikini kafie mbele na umasikini wako bila kujua wewe ndie uliempigia kura kumamamakezake
Nimeliona mkuu imebidi nikaushe na kulisamehe bure nyuzi itaendelea si unajua tena harakati zetu wagonga ulimbo nakuwa nakosa nafasi ila kwa ground mkeka bado haujatoa😁yaani ngoma bado mbichiiii
 
Sisi ndio wale ikitokea Mama akigongwa na nyoka na hospital wakadai 150,000 basi ukoo mzima inabidi ujichange na bado pamoja na wote kujichanga haitimii hio 150,000 sana sana Mama atafia hospitali kwa kukosa 150,000 za kulipia dawa ili apone
Kaka acha tu, mwingine atahisi ni meme ila sisi ndo wale tulitafuta kazi ya laki na hamsini tukaambiwa tutafute laki nne ili tuipate
 
Endelea kusimulia bado upo kaunta km barmedi au sasa hivi umehamia kwenye idara ya ubaunsa na ulinzi au umekua dalali mtu wa kati mzee wa kutembeza mikasi almaarufu km winga teleza?
Tunaendelea wakati ule nikiwa waiter kwenye bar ile yenye utulivu mwingi na ilikuwa ni sehemu ambayo ni rahisi sana kuwaona hata viongozi wa chama na serikali wakija kupata moja baridi moja moto kulingana na mazingira yake ya utulivu,Naweza sema ilikuwa ni bar ya watu waliostaarabika.

Mgonga ulimbo kama kawaida yangu nilikuwa najitahidi sana kutoa huduma bora sana kwa wateja ikiwemo kuwachangamkia na kuwakaribisha kwa heshima na adabu kwa waliokulia kijijini wanaelewa vile huwa tunafundishwa vijana wa mikoa ya kusini wanaelewa hili

Mungu sio faru john basi wengine walikuwa wanakuachia tips kiumbe cha Mungu napata walau nauli na hela kidogo ya kuwatumia wazee kijijini lakini kwa wazoefu na bar hili wanalijua sana kwa mhudumu wa kiume tips huwa ndogo ukilinganisha na waitress maana iko wazi wanaume hatuna cha kuoffer kwa watoa tips hivo mtu akinipa hata jero nilikuwa nashukuru vibaya mno.

Siku zikasonga masaa yakasogea akilini mwangu nikawa nasema hapa ndio sehemu sasa ya kutengeneza connection maana watu wazito wengi wanakuja hivo nilikuw nahakikisha nikikupiga service yangu mpaka unafeel kuniuliza hivi umeishia form ngapi hapo ndipo nilikuwa nafunguka kuwa mimi ni graduate basi swali linalofuata ilikuwa lazima uulizwe kwani umesoma kozi gani.

Nilipokuwa nawatajia kozi yangu walikuwa wanashtuka like either wanahisi nimefeli au laa sipambani kutafuta michongo,Ila mimi ndio nilikuwa najua uhalisia wa ground ulivo na hiyo ni kawaida sana kwa waliojipata kuona wanaopambana na maisha kama hawapo serious hivi.

Basi bhana kama kawaida ya pombe ikishamkolea mtu maboss wengine ilikuwa wakilewa wanakupa mausia mengi na kukuahidi mambo makubwa hadi unahisi kesho utaamka upo ofisi fulani maana unakuta anakutajia maboss wakubwa wa mji anaofahamiana nao huku akikwambia kijana usijali mimi nitakusaidia😁Kiumbe wa Mungu nashikwa na imani kumbe pombe anyway ni maisha.

To be continued wakuuu wa wakuu...hii ni true story no fake detail, tunashare experience za maisha
 
Hio mikopo ni ya kwao wenyewe kwa changa la macho complications ni nyingi sana nilishawahi kuandaa proposal ya kuomba mkopo kwa kikundi cha vijana kwenye Halmashauri fulani oyaa ngoja nipite hivi
Huwaga kuna ukiritimba sana

Tushawahi jaribu kujiorganize vijana kadhaa peleka proposal ya kuomba hiyo mikopo🤣Tukatafuta hadi zile kadi za kijani si unajua tena tukaaminishwa ile ni grisi italainisha vyuma.

Hiyo mizunguko tulizungushwa ilikuwa inatuma ujumbe wa moja kwa moja kuwa hizi pesa zina wenyewe jiongezeni ikaishia juu juu
 
Tunaendelea wakati ule nikiwa waiter kwenye bar ile yenye utulivu mwingi na ilikuwa ni sehemu ambayo ni rahisi sana kuwaona hata viongozi wa chama na serikali wakija kupata moja baridi moja moto kulingana na mazingira yake ya utulivu,Naweza sema ilikuwa ni bar ya watu waliostaarabika.

Mgonga ulimbo kama kawaida yangu nilikuwa najitahidi sana kutoa huduma bora sana kwa wateja ikiwemo kuwachangamkia na kuwakaribisha kwa heshima na adabu kwa waliokulia kijijini wanaelewa vile huwa tunafundishwa vijana wa mikoa ya kusini wanaelewa hili

Mungu sio faru john basi wengine walikuwa wanakuachia tips kiumbe cha Mungu napata walau nauli na hela kidogo ya kuwatumia wazee kijijini lakini kwa wazoefu na bar hili wanalijua sana kwa mhudumu wa kiume tips huwa ndogo ukilinganisha na waitress maana iko wazi wanaume hatuna cha kuoffer kwa watoa tips hivo mtu akinipa hata jero nilikuwa nashukuru vibaya mno.

Siku zikasonga masaa yakasogea akilini mwangu nikawa nasema hapa ndio sehemu sasa ya kutengeneza connection maana watu wazito wengi wanakuja hivo nilikuw nahakikisha nikikupiga service yangu mpaka unafeel kuniuliza hivi umeishia form ngapi hapo ndipo nilikuwa nafunguka kuwa mimi ni graduate basi swali linalofuata ilikuwa lazima uulizwe kwani umesoma kozi gani.

Nilipokuwa nawatajia kozi yangu walikuwa wanashtuka like either wanahisi nimefeli au laa sipambani kutafuta michongo,Ila mimi ndio nilikuwa najua uhalisia wa ground ulivo na hiyo ni kawaida sana kwa waliojipata kuona wanaopambana na maisha kama hawapo serious hivi.

Basi bhana kama kawaida ya pombe ikishamkolea mtu maboss wengine ilikuwa wakilewa wanakupa mausia mengi na kukuahidi mambo makubwa hadi unahisi kesho utaamka upo ofisi fulani maana unakuta anakutajia maboss wakubwa wa mji anaofahamiana nao huku akikwambia kijana usijali mimi nitakusaidia😁Kiumbe wa Mungu nashikwa na imani kumbe pombe anyway ni maisha.

To be continued wakuuu wa wakuu...hii ni true story no fake detail, tunashare experience za maisha
Kweli mkuu simulizi ni nyingi wengine walishachoka kupambana wakaamua kurudisha mpira kwa kipa, ngoja tuone muendelezo ulirudisha mpira wa kipa?
 
Huwaga kuna ukiritimba sana

Tushawahi jaribu kujiorganize vijana kadhaa peleka proposal ya kuomba hiyo mikopo🤣Tukatafuta hadi zile kadi za kijani si unajua tena tukaaminishwa ile ni grisi italainisha vyuma.

Hiyo mizunguko tulizungushwa ilikuwa inatuma ujumbe wa moja kwa moja kuwa hizi pesa zina wenyewe jiongezeni ikaishia juu juu
Hio nilishafanya na proposal niliandika mwenyewe nikaandaa kila kitu sio mimi kuna vijana waliji-organize ila weee zile Pesa zina wenyewe hakuna cha kadi ya chama wala cha mama yake kadi ya chama
 
Hio nilishafanya na proposal niliandika mwenyewe nikaandaa kila kitu sio mimi kuna vijana waliji-organize ila weee zile Pesa zina wenyewe hakuna cha kadi ya chama wala cha mama yake kadi ya chama
Zile hela bila maelekezo ya baba kanituma utakuwa unazisikia tu redioni kuwa vijana kadhaa wapata mikopo ya vijana
 
Back
Top Bottom