Harmonize: Nilipewa Mkataba wa kuonewa na WCB na nilisingiziwa kumroga Diamond Platnumz

Cannabis

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
11,557
Reaction score
33,535



Mwanamuziki wa kizazi kipya, Harmonize afunguka kuhusu mkataba alioingia na WCB amesema alikuwa akipewa 40% ya mapato yoyote anayoingiza na WCB kuchukua 60% ameamua kuelezea hayo yote kutokana na watu kuwa dhana ya kwamba yeye ni msaliti. Amesema alifanyiwa fitna nyingi zilizopelekea yeye kuondoka kwenye record label hiyo.

Amesema management nzima ya WCB walikuwa wanamuogopa yeye (Harmonize) kwamba anaelekea kumshinda Diamond Platnumz kimuziki, amenongezea pia baba yake Harmonize alivyokuwa akija kumtembelea nyumbani WCB walikuwa wanasema kwamba alikuwa anakwenda kumroga Diamond.

Harmonize ameongezea pia alikwenda Nigeria kwa gharama zake kufanya collabo na Reekado Banks nchini Nigeria na akakatwa dola 5000 na WCB. Alipoona fitna zimezidi alijaribu kutafuta amani lakini ilishindikana, amesema mkataba wake na WCB alishauriwa na Joseph Kusaga kwamba akitafuta mwanasheria asingelipa chochote lakini hakutaka kupambana kwa njia hiyo na akaamua kulipa hela tu (Milioni 600) ili tu kupata amani.

------ Maoni ya Wadau -----------




 
Huyu mziki ushamshinda,album inafanya vibaya.

Sasa Diamond kama angetaka kila siku kuwa yy.

Kaanzisha lebo ambayo imemtoa yy.
Kampeleka nje kufanya video kubwa.
Kamkutanisha na wasanii wakubwa Africa.
Kamtoa Rayvanny mpaka kufikia hatua ya Colabo na Maluma na kuchukua BET,Tz hii Rayvanny ndiye mwenye nyimbo yenye streams nyingi, kapiga show jukwaa la essence, mafanikio ambayo Diamond hajawahi kuya fikia.

Angeamua kuto kuanzisha label tusinge mjua na Diamond ni mfanyabiashara, always ana angalia faida na label zote duniani zina angalia faida, hata yy na JembeniJembe wanaangalia faida.

Yeye mwenyewe kuimba aliambiwa hajui, Diamond kakaa nae zaidi ya miaka mitatu, akimfundisha na kumpika kimuziki na kuna watu walimwambia hajui kuimba ila Mondi hakukata nae tamaa, kula,kuvaa na kulala kwa Diamond.

Anadai WCB walikuwa wana muogopa yy, haya leo zaidi ya miaka miwili nje ya WCB, yupo yy peke yake,free habanwi je kafika wapi,kampita Diamond?Anapata airtime ktk media zote kubwa zilizo kuwa hazipigi nyimbo zake.

Halafu haja tuambia wasanii wake wanapata kiasi gani, mikataba yao miaka mingapi,wana miaka miwili hawa heleweki wanafanya nini.
 

Asante kwa kumaliza kila kitu mdau
 
Hii fungulia thread mpya.
 
Mwenye akili hapa atakuelewa mkuu
 
Anadai WCB walikuwa wana muogopa yy, haya leo zaidi ya mwaka wa pili, yupo yy peke yake,free habanwi je kafika wapi,kampita Diamond?Anapata airtime ktk media zote kubwa zilizo kuwa hazipigi nyimbo zake.
Mashabiki wake wanamdanganya kwa sasa yeye ndo msanii mkubwa zaidi Tanzania...

Anasahau hata huku kufurukuta kwake ni kwa sababu tu Kiba amelala usingizi...

Wiki chache zilizopita Kiba akaamua kutoka usingizini na hapo hapo Harmonize akaanza kusahaulika... thanks to Kiba kajirudia zake kuvuta shuka!!

Harmonize ashukuru sana relaxation ya Kiba lakini Kiba akirudisha nguvy japo kwa 50%, Harmonize atabaki kushindana na akina Rayvanny!
 

Rayvanny yupo Maili 100 mbali mno
 
Nimeamini kuna watu wanaweza kukuchukia na hujawafanyia lolote baya,

Harmonize
1. Aliutekeleza mkataba wake WCB vizuri
2. Waliposhindwana wakamalizana vizuri na wcb wakavuta pesa waliyokuwa wanaitaka (600M)

Choko choko za nini sasa?mtu ana demand respect kwa mtu ambaye alitaka kumuangusha??? Naamini mmoja wenu hapa ndiye angekuwa Harmonize uvuliwe milioni 600 si ajabu hata mngekuwa mmeshamloga Diamond kafia mbali
 
Rayvanny yupo Maili 100 mbali mno
Hilo nalifahamu fika...

Tangu enzi Harmonize yupo Wasafi, nilikuwa namkubali Rayvann mara 100 kumlinganisha na Harmonize

Na kilichokuwa kinanikera zaidi kuhusu Harmonize ni ile kuiga kila kitu toka kwa Diamond.... yaani alikuwa Clone ya Diamond; hakuwa unique kama Rayvann ambae hata kama umepiga mtungi na kuzima, ukisikia ngoma mpya ya Rayvann utajua tu huyo ni Rayvann!!
 
Pale ambapo mziki unagoma, na kuamua kuzigeukia kiki....
Hakuna shughuli hapo

Harmonize inabidi atoe respect kwa mtu aliyemuokota baada ya kuambiwa na BSS kuwa hajui kuimba ila Diamond akaamini kipaji chake na kumsaidia kufika alipofika leo hii

Huyo rayvanny mwenyewe alikuwa ameachwa na Madee kwenye ile label yao kwa kuambiwa hajui kitu ila Simba akamchukua na kuamini kipaji chake na leo hii yupo juu

Muangalie Mbosso khan leo hii wenzake wa kundi la Ya moto band wapo wapi na wanafanya nini kwenye industry? Aslay na yule Beka flavour

Tuje tumsuguse Zuchu right now, one of the top female artist in East and Central Africa

Ooooh!, This Dude Simba need appreciation kwa kutengeneza wasanii wakubwa ambao wanaweza kufanya competition na yy mwenyewe coz label nyingi hapa bongo wameshindwa kufanya ambacho amekifanya yy

Pia wakumbuke ile music label yake sio kwa ajili ya social charity Ila ipo for profit gain
 
Sijasikiliza hata nyimbo zake....ndo kile kiingereza cha ago kill u??? Akankill ma self???
Kaongeza misamiati siku hizi kuna matusi , huu ndio wimbo wake wa kwanza kwenye album katoa video juzi juzi, haueleweki anaimba nini, hapo kwenye sleep sleep nafikiri alimaanisha halali lali, hiyo outside sijui ndio ametoka😆

"Yeah hustle everyday I never sleep sleep coz am outside
When am falling love I go deep deep coz am outsidee
Time for the money two for the show enzi za kuuza maji na wanangu wa kariakoo
That was before long time ago I wish you know I wish you know yeaah
"

Chorus:
"We are outside outside outside outside
B*tch am outside outside outside outside
Am outside outside outside (Eeeh)
Kondegang we are outside outside outside (Yah yah yah)
"
 
Summer Walker ni msanii mkubwa tu Marekani kwa sasa kwenye mkataba wake kapewa advance ya $110,000, kwenye mauzo ya album kwa kila $1 atakayotengeneza yeye atapewa 16 cents baada ya kuirudisha advance aliyopewa. Record labels hazina huruma, ndio soko la kibepari hapo penyewe bongo bado mziki unapelekwa kishikaji na kibinadamu sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…