Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hapo ni kaka,kaka k mnyoko unafki mbaya sana
Wewe huoni watu wanaomuattack harmo hata baada ya kutoka WCB, Baba levo, juma lokole, alisitote, Issa Azam, middle Simba, au wewe unapenda asemwe yeye tu lakini yeye asisemeKwa Sasa si ameshatoka WCB? Why for 3 years kila siku yeye Ni WCB WCB
Afanye kazi aone Kama hajatengeneza fanbase yake Na yy
Mbona alikiba Yupo Na Anatoa Ngoma Kali Ana fanbase yake Mpaka Leo
Msukule, hivi kwani huyo Domo ni mungu kwamba hatakiwi kuambiwa akiwakosea watu.Awekeze Nguvu kwenye kufanya Kazi nzuri Na Atengeneze fanbase yake
Mbona Diamond aliweza hilo, kipindi WCB na Clouds Wana bifu Diamond hakuwenda kwenye media kila siku kulalamika
Bali alifanya kazi na akatengeneza fanbase yake,
Harmonize yeye anashindwa nn?
H Baba, Mwijaku, Carrymastory, hawa kazi yao kila siku ni kumtukana Diamond na wanatumwa na nani?Wewe huoni watu wanaomuattack harmo hata baada ya kutoka WCB, Baba levo, juma lokole, alisitote, Issa Azam, middle Simba, au wewe unapenda asemwe yeye tu lakini yeye asiseme
Haya ww ambaye ni mkubwa nieleze Diamond alipomkosea huyo Mmakonde wenuMsukule, hivi kwani huyo Domo ni mungu kwamba hatakiwi kuambiwa akiwakosea watu.
Hivi vijana akili mmepeleka wapi ?
Kwani mungu domo naye alishawahi kukosea watu ???Haya ww ambaye ni mkubwa nieleze Diamond alipomkosea huyo Mmakonde wenu
Mimi nadhani Diamond labda kama anashindana na kina Davido, Wizkid and likes, lakini kwa Tanzania kashawapiga gape ukubwa hakuna fair competition, watu huwa hawaupendi tu ukweli.Harmonize Ana force kushindanishwa na Diamond apo ndo anakosea saana Diamond ni mkubwa kuliko Harmonize, Diamond mshindani wake ni Ali kiba na Sio Harmonize. Mmakonde atulie saana mda wake bado kushindana na Diamond.
Asante kwa kuweka hiyo link hapo.Hakika amefunguka
Jizuie ku_comment kabla hujamsikiliza mwanzo mwisho, ili ujue ukweli, Hizo clip mbili hapo juu zimeacha sehemu kubwa ya maelezo yake.
Sasa swali linakuja unapomrekodi mwanaume mwenzio kwenye simu malengo yako ni nini?Asante kwa kuweka hiyo link hapo.
Nimemsikiliza Kondeboy na nimechuja pumba, chuya na mawe bado nimebaki na kama 60 - 70% mchele safi. Kuna ukweli katika maelezo yake japo limau, ndimu na chumvi havikosi kwa mbaaaaali na kapilipili.
Kuna jambo hapo, ushauri wangu kwako, watafute wote wawili ukae nao wamalize tofauti zao wakajenge nchi hayo mambo yao hayatapata mshindi na hata jamii ikijua ukweli bado haita wasaidia wote wawili zaidi ya kila mmoja kutaka kuonewa huruma na jamii na mwingine aonekane ndio mbaya.
Kaa nao tafadhari myamalize. Ni hayo tu!
Basi wote wanashambuliana, hamna wa kulaumiwa kuhusu mashambuliziH Baba, Mwijaku, Carrymastory, hawa kazi yao kila siku ni kumtukana Diamond na wanatumwa na nani?
Au ndo nyani haoni kundule
mtu akiongea ukweli mnakimbilia mziki mmemshinda tuna na uwelewa wa kufikiri watanzania dogo jinsi alivyo kavumilia mengi.Huyu mziki ushamshinda,album inafanya vibaya.
Sasa Diamond kama angetaka kila siku kuwa yy.
Kaanzisha lebo ambayo imemtoa yy.
Kampeleka nje kufanya video kubwa.
Kamkutanisha na wasanii wakubwa Africa.
Kamtoa Rayvanny mpaka kufikia hatua ya Colabo na Maluma na kuchukua BET,Tz hii Rayvanny ndiye mwenye nyimbo yenye streams nyingi, kapiga show jukwaa la essence, mafanikio ambayo Diamond hajawahi kuya fikia.
Angeamua kuto kuanzisha label tusinge mjua na Diamond ni mfanyabiashara, always ana angalia faida na label zote duniani zina angalia faida, hata yy na JembeniJembe wanaangalia faida.
Yeye mwenyewe kuimba aliambiwa hajui, Diamond kakaa nae zaidi ya miaka mitatu, akimfundisha na kumpika kimuziki na kuna watu walimwambia hajui kuimba ila Mondi hakukata nae tamaa, kula,kuvaa na kulala kwa Diamond.
Anadai WCB walikuwa wana muogopa yy, haya leo zaidi ya miaka miwili nje ya WCB, yupo yy peke yake,free habanwi je kafika wapi,kampita Diamond?Anapata airtime ktk media zote kubwa zilizo kuwa hazipigi nyimbo zake.
Halafu haja tuambia wasanii wake wanapata kiasi gani, mikataba yao miaka mingapi,wana miaka miwili hawa heleweki wanafanya nini.
Hivi mkuu kwenu Mara au Ukerewe?Sasa swali linakuja unapomrekodi mwanaume mwenzio kwenye simu malengo yako ni nini?
Je huyo Rayvanny kampa go ahead huyu mmakonde kuongea faragha zake?
Unajiongelesha mwenyewe kutwa na mwenyewe kaweka ukweli unataka aseme nini.Harmonize ni mtu wakujiliza liza sana, na ni mtu ambae anataka sana kuonewa huruma! Kulikua na haja gani ya kuonge hivo?. Au ndo alivoshauriwa na washauri wake?? Sasa kaongea kapata faida gani? Hii ni fedheha kwa msanii mkubwa kama yeye,alitakiwa kutulia na kufanya kazi
Watu wengi ni misukule.Mimi huwa nawashangaa sana mashabiki wa kibongo,mnachokihitaji kutoka kwa msanii ni mziki wake au yeye kuwa label flani? Mimi naona mtu kuwa label flani ni swala binafsi zaidi hatupaswi kuliingilia sana kwani linalenga kumjenga msanii ili aendelee kukuburudisha zaidi. Hapo hapo WCB kuna wasanii mnawaponda hawafai kuwepo kwenye label lakini akishatoka mnaleta nongwa,embu wekeni wazi mnataka nini?
Waache wapambane wao
Mwanamuziki wa kizazi kipya, Harmonize afunguka kuhusu mkataba alioingia na WCB amesema alikuwa akipewa 40% ya mapato yoyote anayoingiza na WCB kuchukua 60% ameamua kuelezea hayo yote kutokana na watu kuwa dhana ya kwamba yeye ni msaliti. Amesema alifanyiwa fitna nyingi zilizopelekea yeye kuondoka kwenye record label hiyo.
Amesema management nzima ya WCB walikuwa wanamuogopa yeye (Harmonize) kwamba anaelekea kumshinda Diamond Platnumz kimuziki, amenongezea pia baba yake Harmonize alivyokuwa akija kumtembelea nyumbani WCB walikuwa wanasema kwamba alikuwa anakwenda kumroga Diamond.
Harmonize ameongezea pia alikwenda Nigeria kwa gharama zake kufanya collabo na Reekado Banks nchini Nigeria na akakatwa dola 5000 na WCB. Alipoona fitna zimezidi alijaribu kutafuta amani lakini ilishindikana, amesema mkataba wake na WCB alishauriwa na Joseph Kusaga kwamba akitafuta mwanasheria asingelipa chochote lakini hakutaka kupambana kwa njia hiyo na akaamua kulipa hela tu (Milioni 600) ili tu kupata amani.
Una akili timamu ??Yaani Diamond atake kumwangusha Harmonize?
Like serious?!
Yaani Harmonize aliyekuwa ana-copy kila kitu kutoka kwa Diamond... kuanzia style ya kuimba hadi swagga halafu bado anaye-copy ndie awe threat kwa mwanzilishi?!
Like serious?!
Mkiweka utimu pembeni... hivi Harmonize anamfikia hata hRayvann kwa uwezo wa kimuziki?! Kuanzia mashairi hadi melody?
Kwanini basi huyo Diamond asifanye struggles za kumwangusha Rayvann, ambae kwa vocals, hata Diamond mwenyewe hajafika levels za Rayvann?!
FYI, ambae alikuwa na matatizo na Harmonize ni Sallam....
Na Sallam ndivyo alivyo... yaani huwa hakopeshi!!!
Na hata Harmonize alipotoka WCB, Diamond alikuwa kimya!!
Harmonize alipotoa album, Diamond alii-post lakini alichoambulia "Oh, Diamond anaanza shobo na kutafuta kiki"!
Na ni huyo huyo Harmonize ndie alianza vijembe kwenye nyimbo zake....
Akaja H Baba nae akanunua "ugomvi"