Harmonize: Nilipewa Mkataba wa kuonewa na WCB na nilisingiziwa kumroga Diamond Platnumz

Leo nakuto... totoo, nakutoa kwenu uje kwangu
Nina hamu yakuto... totoo, kutoa mahali uwe wangu (nyau)

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Tueleweshane.

Harmonize alimpigia simu Rais ili amsaidie katika kuuvunja mkataba?

Huo mkataba haukua na get out clause?

alimpia ili amuamuru diamond akabidhi nyaraka za watu,ambazo si mali yake tena.
 
Nyimbo mbili kwa mwaka na unajigaramia vitu vingine...so na wewe ukaamini aliyosema mmakonde ni ya kweli?

Yaani mtu aliyekuja label hana kitu.....aliwezaje kujigharamia mambo mengine...?

kwamba alisema uongo sababu aliingia akiwa hana hata kitu!!!

kwahiyo hizo 60% zilikuwa zinakatatwa kwenye kaptura ama!!!!
 
11. Diamond anataka awe mwanamuziki yeye yu TZ

12.Diamond hawezi ushindani
 
Idara Ya auandishi wa Habari Ni Janga lingine kubwa katika Nchi hii....Yaani Mwandishi anauliza Ukiwa Unaandika huwa unafikiria nini....Jamani yaani hilo swali lina mana gani?? Nyie mnaojiita waandishi siku hizi jaribuni Kusoma vitabu..Jaribuni kuwaasikiliza akina Tido Mhando kidogo mpate mwanga..Mko shallow sana sana na mnatia aibu.

Kingine Wewe Harmonize Ongea tu kiswahili unaeleweka....Achana na Kiswanglish cha nini??
 
kwamba alisema uongo sababu aliingia akiwa hana hata kitu!!!

kwahiyo hizo 60% zilikuwa zinakatatwa kwenye kaptura ama!!!!
Mbona suala rahisi hilo mkuu....aliingia akiwa broke. Label ikaweka mzigo...ndipo makato yakaanza pale alipoanza kuingiza income.

Kumbuka kabla hajaanza kukatwa hiyo 60% kuna muda ulipita ambao alirekodi nyimbo na videos kadhaa kwa gharama za label. Kafanyiwa promotions na other costs kwa gharama za label.
Kwa kipindi hiki cha mpito kabla return of investment haijaanza kuonekana...hakuweza kujigharamia. Aliitegemea label kwa kila kitu.

Kwa hiyo hiyo statement kuwa alikuwa akijitegemea kwa nauli na chochote haiwezekani kuwa ya kweli kwa kipindi hicho ambacho label ilikuwa imewekeza milions na bado aikuwa hajaamza kuingiza chochote.
 
Labda mm Sina masikio ,ivi Kuna sehemu harmonize kalalamika kuwa alikuwa ananyonywa au kulalamikia hiyo 40 percent? Huu ushabik naona watz umetuzid Sana aiseee.
Harmonize kwenye maelezo yake yote amesisitiza kuwa alikuwa hatak kutoka wcb kwa lugha nyepes ariridhika na hiyo 40 percentage ,Ila ishu Ni hao machawa wa mond akina Salam na tale ndio walianza kumfitinisha bwana mdogo na Kaka ake ,na maelezo yake ameongea Waz kuwa alipambana Sana ili wawe sawa lakin ilishindikana so ikawa Ni lazima atoke .

Baada ya kugonga mwamba kwa kila jitihada ikabid waanze kumfanyia fitna Mara lete 300 Mara 200 Mara 100 ,na ukumbuke hiyo Bei walijipangia wao lakin kijana akalipa ,ishu ikaja baada ya kulipa hawakuwa tayal Tena kumpa contract termination ,lengo ni nn hapa yaan wanuue dogo jumla kimziki kwa lugha nyepes walitaka kumtapel ,maana ushalipwa chako hutak kusain mkataba wa kuachana maana ake nn had rais kuingilia Kati.

Kilio Cha harmonize Ni fitna na jinsi alivyogombanishwa na Kaka ake pengine huna jicho la kuona mbali ,harmo Wala hakuwa na mpango wa kutoka wcb Zaid kafitinishwa na tokea hapo ni mwendo wa kumsaka kila angle ,Ni bahat tu kijana nae si haba maana alijua michezo yote ya wcb tofaut na hapo angekuwa km mavoko na yule mrundi Ila kijana nae kaiva .

Ushabik mwingine hapana harmo anaonewa hayo mambo ya pesa unaongea wewe na kuyakuza ili yaonekane ndio ajenda kubwa wakat sio ajenda hapa Ni fitna bac, Kama Ni pesa wcb nao washavuna Sana pesa kutoka kwa bwana mdogo Hilo lipo Waz ,hata hiyo 600m Ni nyongeza tu kwa kile walichovuna kwa harmo ,kapiga show ngap hapo wcb why 600m ndio uone Ni pesa kidogo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…