Harufu ya manukato porini na nywele kusisimka ina maana gani?

Harufu ya manukato porini na nywele kusisimka ina maana gani?

kyagata

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2016
Posts
10,406
Reaction score
19,892
Habari JF,

Kwa wenye uzoefu wa hili jambo naomba mnisaidie ni ishara ya nini?

Siku tatu nyuma nilienda kijijini kwetu kusalimia,sasa kama mjuavyo ndugu kijijini huwa ni wengi na ukifika huko basi ni lazima ujitahidi uwatembelee wote kuepusha lawama.

Kilichonishangaza ni kwamba kuna siku nikawa nimeenda kumsalimia ndugu yangu flani ambae anaishi upande wa pili wa kijiji, na ili ufike huko lazima uvuke mto flani unaotenganisha.

So baada ya kufika huko tukaongea mawili matatu then me nikaaga kuondoka, wakati narudi navuka ule mto nilikuwa mwenyewe tu na sikuona kiumbe mwingine yeyote pale, na lile eneo pale mtoni ni eneo ambalo lina miti mingi sana, ikumbukwe pia muda huo ilikua ni saa 6 mchana.

Kwanza ghafla nikahisi nywele zangu za kichwani zimesisimka na hapo hapo nikaanza kusikia harufu ya manukato, nimeshindwa kuelewa mpaka leo manukato yale yalitoka wapi na kwa nini nywele zangu zilisisimka ghafla?

Asante
 
Kwanza Lazima ujue na kufahamu hauko pekeyako na si lazima uwaone walio pamoja nawe. Itoshe tu kusema ishara na hisia ulizozihisi zilithibitisha hivyo 🐒

Hata hivyo, mchanganyiko wa harufu mbalimbali za maua porini huzalisha harufu zenye manukato ya kipekee sana 🐒 🐒
 
kwanza Lazima ujue na kufahamu hauko pekeyako na si lazima uwaone walio pamoja nawe. Itoshe tu kusema ishara na hisia ulizozihisi zilithibitisha hivyo 🐒

hata hivyo,
mchanganyiko wa harufu mbalimbali za maua porini huzalisha harufu zenye manukato ya kipekee sana 🐒 🐒
Sawa mkuu
 
Habari jf.
Kwa wenye uzoefu wa hili jambo naomba mnisaidie ni ishara ya nini?
Siku tatu nyuma nilienda kijijini kwetu kusalimia,sasa kama mjuavyo ndugu kijijini huwa ni wengi na ukifika huko basi ni lazima ujitahidi uwatembelee wote kuepusha lawama.
Kilichonishangaza ni kwamba kuna siku nikawa nimeenda kumsalimia ndugu yangu flani ambae anaishi upande wa pili wa kijiji,na ili ufike huko lazima uvuke mto flani unaotenganisha.so baada ya kufika huko tukaongea mawili matatu then me nikaaga kuondoka,wakati narudi navuka ule mto nilikua mwenyewe tu na sikuona kiumbe mwingine yeyote pale,na lile eneo pale mtoni ni eneo ambalo lina miti mingi sana,ikumbukwe pia muda huo ilikua ni saa 6 mchana.kwanza ghafla nikahisi nywele zangu za kichwani zimesisimka na hapo hapo nikaanza kusikia harufu ya manukato,nimeshindwa kuelewa mpaka leo manukato yale yalitoka wapi na kwa nini nywele zangu zilisisimka ghafla?
Asante
Huyo alikuw ani jini mwanamke hapo uliposikia harufu alikuwa anajipaka mwilini mwake ndio maana umesikia mwili kusisimka.
 
Wewe ni mwili,nafsi na roho,kuna vitu macho yako ya kawaida hayawezi kuona lkn roho yako inaona,ndio maana mwili ukasisimka kwa kitu usichokiona,hivyo amini kuwa palikua na kitu hapo....
 
Back
Top Bottom