ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 937
Tulianza vibaya mwaka mpya na Ma msapu. Kisa kidogo tu nilimwambia sitoweza kumsaidia jambo ambalo yeye aliona ni muhimu nami nikasema sio kama vipi nipe muda.Alikasirika akaniambia hiyo ndio tabia yangu kwake na ananijua lakini ingekuwa mwingine ningempapatikia.
Haikunipendeza lakini nilipoonyesha sikufurahia nae akachukia. Tumenuniana toka Desemba,31,2012, nikimpigia simu hapokei, sms hajibu na nyumbani anatimiza majukumu yote kasoro salamu hanipi wala "kikapu" hatoi.
Baada ya kutafakari sana nikijaribu kutafuta tuongee roho wa Bwana kanijia kaniambia nimtumie sms nikiwa hapa ofisi nimweleze sijisikii vizuri. Hii itapima upendo wake kwangu katika kipindi cha hasira. Nilipotuma ikapita dakika tano kanirejeshea ujembe: "vipi tena jamani?!", nikajibu " siwezi, nashindwa hata kuendesha gari". Ghafla akapiga "ehe wee, baba vipi tena jamanii.mungu wangu, nije nikusaidie?!"
Nikazuga nimemwomba jamaa yangu mmoja ofisi anisaidie,.. Naelekea nyumbani, sasa tunaweza kuwasiliana tena kwa ujumbe mfupi wa maandishi kwenye simu (sms), anauliza naendeleaje, najisikiaje, nikifika nitamweleza nilikosa mbinu ya kurejesha mawasiliano hilo lilinilazimu kuongopa naumwa!
Raha ya maisha ya ndoa ni kama hivi, mwenzio hata akinunaje itafika wakati ataongea tu kama sio roho yake na kinywa, basi kiungo cha mwili kilichowaunganisha kitamlazimisha kuongea tu..... Huwezi kuzuia kiungo kikidhamiria kutumika, ataonge kwa kinywa au matendo mtawasiliana tu!! Upendo wa kweli katika ndoa hujidhihirisha katika matukio, mwenzio uumia sana juu yako, mke au mume wa kweli hawezi kuvumilia akisikia mwenzie kapatwa na jambo baya, anaumwa, amekosa raha, ametukanwa, anasemwa vibaya nk...mke/mume wa ukweli yu radhi kusimama hata katikati ya nduguze ili kumtetea mwenzie, yu tayari kuonekana hafai kwa maslahi ya mwenzie..
Yu tayari kufia ndoa yake, kudhalilika hata akiitwa "Bw.e.ge" yu radhi!
Haikunipendeza lakini nilipoonyesha sikufurahia nae akachukia. Tumenuniana toka Desemba,31,2012, nikimpigia simu hapokei, sms hajibu na nyumbani anatimiza majukumu yote kasoro salamu hanipi wala "kikapu" hatoi.
Baada ya kutafakari sana nikijaribu kutafuta tuongee roho wa Bwana kanijia kaniambia nimtumie sms nikiwa hapa ofisi nimweleze sijisikii vizuri. Hii itapima upendo wake kwangu katika kipindi cha hasira. Nilipotuma ikapita dakika tano kanirejeshea ujembe: "vipi tena jamani?!", nikajibu " siwezi, nashindwa hata kuendesha gari". Ghafla akapiga "ehe wee, baba vipi tena jamanii.mungu wangu, nije nikusaidie?!"
Nikazuga nimemwomba jamaa yangu mmoja ofisi anisaidie,.. Naelekea nyumbani, sasa tunaweza kuwasiliana tena kwa ujumbe mfupi wa maandishi kwenye simu (sms), anauliza naendeleaje, najisikiaje, nikifika nitamweleza nilikosa mbinu ya kurejesha mawasiliano hilo lilinilazimu kuongopa naumwa!
Raha ya maisha ya ndoa ni kama hivi, mwenzio hata akinunaje itafika wakati ataongea tu kama sio roho yake na kinywa, basi kiungo cha mwili kilichowaunganisha kitamlazimisha kuongea tu..... Huwezi kuzuia kiungo kikidhamiria kutumika, ataonge kwa kinywa au matendo mtawasiliana tu!! Upendo wa kweli katika ndoa hujidhihirisha katika matukio, mwenzio uumia sana juu yako, mke au mume wa kweli hawezi kuvumilia akisikia mwenzie kapatwa na jambo baya, anaumwa, amekosa raha, ametukanwa, anasemwa vibaya nk...mke/mume wa ukweli yu radhi kusimama hata katikati ya nduguze ili kumtetea mwenzie, yu tayari kuonekana hafai kwa maslahi ya mwenzie..
Yu tayari kufia ndoa yake, kudhalilika hata akiitwa "Bw.e.ge" yu radhi!