Hata dhahabu ilifichwa Kenya lakini ilirudishwa, Rais Samia rudisha hela zilizofichwa China

Hata dhahabu ilifichwa Kenya lakini ilirudishwa, Rais Samia rudisha hela zilizofichwa China

Kulwa Jilala

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2022
Posts
3,891
Reaction score
8,448
Rais Kikwete alirudisha hela tuliyopigwa kwenye ununuzi wa rada na hela hiyo ikapelekwa kununua madawati.
Rais Magufuli alirudisha dhahabu iliyokuwa imefichwa Kenya kwa miaka mingi.

Rais Samia unashindwa nini kurudisha hela uliyodai wewe mwenyewe kuwa imefichwa China? Aliyekuwa DPP Biswalo Mganga si bado yupo hai?

Miaka ya nyuma baada ya hayati Benjamini Mkapa kuingia madarakani tulianza kusikia juu ya ukwapuaji wa pesa za umma uliofanyika. Moja ya watuhumiwa alikuwa ni Prof Kighoma malima ambaye alishafariki. Tukaanza kusoma kwenye magazeti kuwa alificha pesa nyiki huko Uingereza. Na baadae tuliskia serikali ilifreeze akaunti yake na kurejesha hizo pesa.

Sasa mkuu wa nchi kusimama hadharani na kutamka kuwa kuna mabil ya pesa yamefichwa China, maana yake anafahamu benki, akaunti na hata walioficha.

Serikali iyarudishe hayo mabil na wahusika walio hai wachukuliwe hatua. Zaidi ya hapo kuna lingine nyuma ya pazia.
 
Hakuna mtu aliyeficha pesa china hakuna hakuna msidanganyike ni uongo na ni ulongo

Muulize aliyewambia pesa zimefichwa china awambie zimefichwa na nani?

Walioficha pesa china wapo china au Tanzania? Au wote wamekufa?

Hakuna pesa ya kurudisha kutoka china maana hakuna pesa china ni uongo.
 
Correction, raisi Kikwete hakurudisha iliyoitwa fedha ya rada bali Waingereza wenyewe ndiyo waliopigania ikarudishwa ilijadiliwa mpaka Bungeni kwao na masharti ikawa hela zikirudi ziwekwe kwenye Elimu hivyo kila kitu kilifanywa na Waingereza wenyewe na hakukuwa na input yoyote ile kutoka Serikali ya Tanzania, kama wa Uingereza wangekaa kimya hakuna hata Shilingi ingerudi, kama hata ni kweli ilirudishwa hiyo fedha na Waingereza walikuwa na nia ya dhati kutupigania jambo ambalo binafsi siliamini hilo ni swala lingine!
 
Hivyo pia kwenye dhahabu kutoka Kenya, Kenyatta ndio aliamua kuzirudisha.
Correction, raisi Kikwete hakurudisha iliyoitwa fedha ya rada bali Waingereza wenyewe ndiyo waliopigania ikarudishwa ilijadiliwa mpaka Bungeni kwao na masharti ikawa hela zikirudi ziwekwe kwenye Elimu hivyo kila kitu kilifanywa na Waingereza wenyewe na hakukuwa na input yoyote ile kutoka Serikali ya Tanzania, kama wa Uingereza wangekaa kimya hakuna hata Shilingi ingerudi, kama hata ni kweli ilirudishwa hiyo fedha na Waingereza walikuwa na nia ya dhati kutupigania jambo ambalo binafsi siliamini hilo ni swala lingine!
 
Swali, mwenzie ni Jibu.

Kama mkuu wa nchi amesema kuna pesa zilizofichwa China, maana yake amejua kiasi, wapi na nani amehusika, sasa
  • Serikali yenye utawala bora na sheria, inashirikiana na wezi wa fedha za umma? Kama sivyo, hatua zipi zimeshachukuliwa?
  • Kuja kusema hadharani wizi, nini serikali inafanya/imefanya kuadhibu na kurudisha mali iliyoibwa? Inakuaje siri baada ya kuzua taharuki?
  • Ni sahihi kwa wezi kufichwa, kulindwa?

Huu sio muendelezo wa siasa UMIMI?

Si ajabu kushindwa kuwashughulikia wezi hao kwa kudhani Polisi hawa hawa wanaoshindwa kuwadhibiti Panya road wasio na kitu wataweza kuwadhibiti wenye pesa za kuficha China.

Kama mtawala aliua, alinyang'anya, alionea, kisha mtawala huyo akatoka, waliotumika KUUA, KUNYANG'ANYA n.k hawapo? Watawala walioingia, nu jukumu lao kutuambia sisi yaliyotokea ambayi hatukuyaona au kuchukua hatua kwa waliohusika na kuweka mechanism ya kuzuia yasije kujirudia? Wamefanya nini?

Kama kuna pesa zilikwapuliwa, na waliokwapua hawana tena madaraka, wenye mamlaka sasa hawana NIA ya kuweka mambo sawa kupitia MAHAKAMA? Au na wao wanajiandaa/ndi waliofanya hayo?

Kama kuna mtu alipigwa risasi na hakufa, yupo na ni mbobezi wa sheria, kupitia serikali hii inayosikia, inayolipa stahiki zilizominywa, si wakati muafaka kuhakikisha UKWELI UNAJULIKANA na HAKI INATENDEKA dhidi ya uhalifu huo? Kwanini upambanie maslahi yako tu bila kuthibitisha pasi na shaka, kupitia mahakama kuwa huyo unayemtangaza ndiye mhusika wa shambulio?

Nje ya nje ya mada kabisa, nimesikia bajeti inayokuja, trilioni 10.8 zinaenda kuwa za mishahara na marupurupu, TRA wanakusanya ngapi mpaka sasa kwa mwezi? Tunaweza jua tumepiga hatua kiasi gani kwenda mbele tukijua namba za kweli!
 
Hivyo pia kwenye dhahabu kutoka Kenya, Kenyatta ndio aliamua kuzirudisha.

Ofcourse kama angetaa isingewezekana, lkn hapa kuna tofauti dhahabu ni sisi tulishinikiza lkn rada ni Waingereza wenyewe ndiyo waliolivalia njuga, kama Waingereza wangekaa kimya maisha yangeendelea kama kama kawaida, na binafsi siamini kwamba walilivalia njuga swala la rada kwa sababu walituonea huruma bali ni Siasa zao tu walikuwa wanasurubishana na Upinzani wakapata cha kuisubushia Serikali, …
 
Akina nani walitoroshea mapesa China? Umemtaja Malima na wengineo. Hawa wa kuficha mapesa China ni akina nani na nani? Kwa hiyo mnatafuta shida halafu mnajitafuta wa kulitatua?
Kumbe hawajulikani?

Si kawataja kwa majina hapo? BSwalo huoni hilo jina au dhebeza?
 
Mama SSH ukirudisha hizi hela mwendazake na wahuni wenzake walizoficha China utakuwa umepaa sana kisiasa Tanzania!
Ungejua yeye kaficha mamilioni ngap8 oman hadi sasa ni mmoja wapo wa marais matajiri sana africa na duniani
 
Back
Top Bottom