Hatari kuu inakuja. Wanaume wanatoweka, Wavulana wanaibuka kwa kasi

Hatari kuu inakuja. Wanaume wanatoweka, Wavulana wanaibuka kwa kasi

Umeshawahi kujiuliza ni kwa nini nyakati hizi watoto wengi wazuri wanaolewa au wana date na wazee au wastaafu..??????

Jibu ni rahisi....Wanaume ni wachache na wameshaoa...Wamebaki wavulana ambao hawawezi chochote.

1. Mvulana ananyoa kiduku, anavaa mlegezo, hataki kazi lakini anataka maisha mazuri...fala mkubwa

2. Mvulana hawezi kazi yoyote ngumu ya kutumia mikono...hata bulb pale nyumbani ikiungua hawezi kubadilisha....pumbaf sana

3.Kutwa kudhurura mtaani na begi mgongoni....sijui humo ndani ya hayo mabegi wanabebaga nini...ukisingiziwa ni supplier wa bangi utakataa...lofa mkubwa..

4. Basi ukikutana na hawa wavulana waliomaliza vyuo ndiyo kero kabisa...wao ni kudhurura kwa ndugu wenye pesa zao na kuwabana bana na familia zao....leo yupo Dar, kesho Arusha, kesho kutwa Mwanza....na wanachqgua miji ya kutembelea....hawataki kwenda Simiyu.

5.Wavulana hawawazi maisha....simu yake haishiwi bando la kuchati na warembo na kuposti picha mitandaoni wamechafua meza kwa chupa za pombe....wanawaza ngono na pombe....shubamiti

6.Ukimshauri atafute kibarua cha kufanya, anadai ana vyeti vyake...ipo siku atakuwa HR wa kampuni kubwa.....

7.Basi hawa wavulana wanasumbua sana kwa kuwapiga mizinga kaka au dada zao mpaka kero...kaka au dada yake anaishi chumba kimoja na mwenzi wake....mvukana mmoja mpumbavu anajibana hapo hapo.

Kwa hali hii kizazi cha miaka 3 ijayo kitatawaliwa na hawa wavulana....
Nawasikitikia dada zangu ambao hawajaolewa maana hawa ndiyo waume zao watarajiwa miaka 3 au 5 ijayo..

Wanaume wa kweli wameshaenda umri..wengi wao wako 30+ na wameshaoa..

Kundi kubwa limebaki la hawa wavulana ambao wako -29....
yaani ni shida....hakuna wanachokijua zaidi ya pombe, mademu na vumbi la Congo.

Kwa hali hii, warembo wakiolewa na wastaafu, tutawalaumu...?.Ni nani yupo tayari kuolewa na lijitu ambalo halikomai akili..? mvulana yupo radhi ashinde njaa lakini apate pesa ya kuweka bleach.
Wavulana badilikeni...mnaiangusha jinsia ya kiume.View attachment 1179156
Kila jambo na wakati wake. Acha vijana wafurahie ujana wao, majukumu yatawafunza kila kitu it's the matter of time. Nyingine ni nyakati tu kwani hao wanawake/wasichana wa maana wako wapi siku hizi?
 
Sawa kijana...
Endeleeni kujibanza kwa mashemeji zenu...
Siku dada akiwa period, shemeji akidau mzigo usimtose..
Maana hakuna namna nyingine,
We ule bata mwanaume mmwenzako atafute ugali...?

We unazeeka vibaya...

We unadhani kila anayekula bata anakaa kwa shemeji..
 
We unazeeka vibaya...

We unadhani kila anayekula bata anakaa kwa shemeji..
Fala kigraduate, hatakj kazi zingine eti anataka kazi aliyosomea...kwa nini msirundikane kwa mashemeji, ndugu na wazazi....

Kwa kifupi watu wa namna hii wameshakiwa mizigo...
 
Fala kigraduate, hatakj kazi zingine eti anataka kazi aliyosomea...kwa nini msirundikane kwa mashemeji, ndugu na wazazi....
Kwa kifupi watu wa namna hii wameshakiwa mizigo...
Wewe inaonekana kwenye ukuaji wako kuna hatua uliziluka ndo maana umekuja kutoa mapovu,kauli za hovyo na matusi mengi,sasa kama we mzee hujielewi nani atakuelewa...
Waache vijana waishi maisha yao wanayotaka,kama wewe hukupitia maisha hayo, usitulazimishe tuishi maisha unayoishi wewe
 
Aisee hii mada imekupenya...
We utakuwa mmoja wa hawa wavulana..
Pambana utoke huko.

Nina duka la urithi,faza kadanja kaniachia ndinga, mimi na mademu,mademu na mimi,mimi ni mwendo wa bata kuanzia leo,kesho ni mapenzi ya MUNGU,nina miaka 26,nina watoto wawili kila mmoja na mama yake...nalewa kila weekend,nakula bata mwanzo mwisho,nikikaribia uzee nitaokoka,nitakuwa nashinda na kukesha kanisani,lakini kwa sasa ni bata mwanzo mwisho..

Pambana na uzee wako faza
 
Nyie wazee muda wenu ushaisha acheni vijana tutambe...

Nyie subirini wajukuu muwalee..😁😁😁
 
Nina duka la urithi,faza kadanja kaniachia ndinga, mimi na mademu,mademu na mimi,mimi ni mwendo wa bata kuanzia leo,kesho ni mapenzi ya MUNGU,nina miaka 26,nina watoto wawili kila mmoja na mama yake...nalewa kila weekend,nakula bata mwanzo mwisho,nikikaribia uzee nitaokoka,nitakuwa nashinda na kukesha kanisani,lakini kwa sasa ni bata mwanzo mwisho..

Pambana na uzee wako faza
Ahaa...kumbe una mali za urithi...
Basi si kosa lako ....
 
Nina duka la urithi,faza kadanja kaniachia ndinga, mimi na mademu,mademu na mimi,mimi ni mwendo wa bata kuanzia leo,kesho ni mapenzi ya MUNGU,nina miaka 26,nina watoto wawili kila mmoja na mama yake...nalewa kila weekend,nakula bata mwanzo mwisho,nikikaribia uzee nitaokoka,nitakuwa nashinda na kukesha kanisani,lakini kwa sasa ni bata mwanzo mwisho..

Pambana na uzee wako faza
Mada imepenya....naona kabisaa ilivyokugusa...
Hatujamnyima mtu kula bata....wakati unakula bata uwe na uwezo wa kutafuta pesa...
 
Yeye naye ni wale wale...ila amesema ana mali za urithi mkuu,,, sishangai akiwa na hizo akili.
Yeah....mwanaume unatamba kwa mali za urithi....
Huwezi jua dingi alitoa mmoja wa wanafamilia kafara ndiyo hizo mali zikapatikana, Au alidhulumi watu...
Mali ya jasho lako ni tamu sana hata iwe kiduchu kiasi gani
 
Kuna huyu mvulana hapa anajiita massachusett naona kanikomalia....ila nimependa coz najua nimempenyezea ukweli
Kuwa mvulana si dhambi,we mwenyewe leo hii ni mzee,lakini ushawahi kuwa mvulana,tuache wavulana tuutumie uvulana wetu...

Halafu faza,mwanaume huwa hajitangazi,utamuona tu matendo yake...ogopa sana mtu anayejipiga kifua akitamba "mimi ni mwanaume,mimi ni mwanaume!!!"..hao mara nyingi ndo huwa mashoga nyuma ya pazia...
 
Yeah....mwanaume unatamba kwa mali za urithi....
Huwezi jua dingi alitoa mmoja wa wanafamilia kafara ndiyo hizo mali zikapatikana, Au alidhulumi watu...
Mali ya jasho lako ni tamu sana hata iwe kiduchu kiasi gani
Faza wewe wazazi wako walifeli kukutengenezea maisha,ndo maana hadi leo hii unayumba,mzazi mwerevu huwekeza kwa ajili ya wanawe..usione kula bata ni gharama sana,ni kitu cha kawaida tu
We mzee ulipaswa uwaandalie mazingira watoto wako,sio unawasimanga!!wewe umefeli na watoto wako pia watafeli kama ulivyofeli wewe...
Kumbuka hata tajiri namba moja bongo anatamba kwa sababu ya mali za baba yake
 
Halafu we dingi una mawazo ya kimaskini sana,yaani we hata ukiwa na mali kiduchu kwako ni poa eti kwa sababu ni ya kutokana na jasho lako...kumbe ndo maana ulifeli maisha!

Kilichobakia ni kwenda kununua uchawi na majini,uroge watoto wa jirani zako..
 
Back
Top Bottom