Hatari kwenye soko la ajira

Hatari kwenye soko la ajira

Nangu Nyau

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2022
Posts
5,015
Reaction score
14,139
Moja kwa moja kwenye hoja.

Ni wakati sasa wa kuangalia kwa jicho kali ulinzi wa ajira za vijana wa Kitanzania na Watanzania kwa ujumla.

Milango tulioifungua kwa kuruhusu wageni kuingia na kupata ajira kwa hoja ya kadili muwekezaji aonavyo inaanza kuwa hatari kwa ajira za wazawa na mustakabali wa wasomi wa kitanzania.

Hali imeaanza kuwa mbaya mitaani kwa ajira nyingi kupewa wageni sasa hata pale ambako hapastahili.

Serikali inapaswa kuweka jicho kali sasa ili kulinda ajira za wazawa, Waajiri wengi sasa wameanza kuleta wageni hasa indians kutoka India kwa kazi ambazo watanzania wanaweza kuzifanya.

Kenyans, Ugandans nao hawako nyuma wamechangamkia fursa hiyo hasa makampuni ambayo ni mali ya wakenya na waganda. Wahindi wameanza kumiminika kwa wingi saana, na makampuni ya kihindi yanatoa priority kwa indians wenzao bila kujali wako ardhi yenye watu pia.

Kwenye constructions na mining pia kumekuwa na hii changamoto kwa sasa kwa expert wengi kuletwa kwa kigezo cha wazawa hakuna, hata kwa zile kazi ambazo unaweza kufundisha mtu ndani ya mwezi akazifanya au ukapromote mtu ndani ya organization husika.

Upande wa biashara, wageni wanaachwa kuingia ndani kabisa huko kufuata bidhaa za kilimo na kufanya biashara nyinginezo ambazo wazawa wanapaswa kufanya, mkenya hapaswi kufuata parachichi Njombe au nanasi bagamoyo bali ni mtanzania anapaswa kupeleka Kenya au Mkenya asubiri border kwenye soko.

Mchina hapaswi kuwa na duka kariakoo bali ni mtanzania anapaswa kuagiza bidhaa china na kuleta hapa, Mturuki hapaswi kuwa na duka kariakoo bali mtanzania anapaswa kuagiza bidhaa na kuzileta hapa.

Tusipolinda ajira za vijana wetu basi kuna hatari ya vijana wetu kuwa watumwa na wapagazi ndani ya ardhi yao, Jicho kali sana linahitajika hapa na watanzania tuwe wazalendo sasa kulinda ajira za wenzetu hata kama sisi tuna nafasi ya kuishi.

Kenya huwezi kupeleka bidhaa hovyohovyo kwenye masoko yao kama sio mkenya, Kenya huwezi mtanzania kuomba ajira ukapata kirahisirahisi. Kenya ni mfano tu katika mifano mingi katika nchi nyinginezo kama West Africa.
 
mfano rahisi.

kwa wale ambao wanatafuta au wameshawahi kufanya kazi nchi za GCC mfano UAE, Oman, Qatar nk mtakubaliana na mimi recruitments agents nyingi ni zawahindi na hutoa priority kwa wahindi wenzao haijalishi umemdhidi au hujamdhidi uwezo, uelewa na experience labda itokee kabisa hayupo mhindi kwenye hiyo nafasi.

tusipolinda ajira za vijana wetu hapa nyumbani ambao huko nje wanakwama kwa kuzidiwa na kukosa wakuwabeba basi tutakiwa watu wa ajabu sana.
 
Ni tatizo sugu Sana , na linaanzia kwenye mamlaka zenyewe hasa immigration na wizara ya ajira kuna rushwa kiwango kikubwa cha kutisha na loop holes za kuruhusu Huu upuuzi kufanyika , hii nchi inatia hasira Sana , Mimi sijui hawa wapumbav kwenye hizo wizara na mamlaka kazi Yao huwa ni nini , na si wahindi Tu kuna wachina nao na wapuuz wengine wachina mahindi wanaletwa humu kama experts na wanapewa vibali vya kazi kabisa bila hata assessment yeyote wakati kuna Lundo la watu wenye hizo qualifications na experience humu za hizo kazi nchini .


Mtu mweusi kalaaniwa ,huwa hatujifunzi hata Kwa wenzetu jinsi migration na wizara ya ajira Kwa wenzetu zilivyostrict ? ,Hivi mtanzania unaweza toka hapa ukaenda hapo Kenya au Uganda ukapata ajira kipumbavu kama inavyofanyika humu ?
 
mfano rahisi.

kwa wale ambao wanatafuta au wameshawahi kufanya kazi nchi za GCC mfano UAE, Oman, Qatar nk mtakubaliana na mimi recruitments agents nyingi ni zawahindi na hutoa priority kwa wahindi wenzao haijalishi umemdhidi au hujamdhidi uwezo, uelewa na experience labda itokee kabisa hayupo mhindi kwenye hiyo nafasi.

tusipolinda ajira za vijana wetu hapa nyumbani ambao huko nje wanakwama kwa kuzidiwa na kukosa wakuwabeba basi tutakiwa watu wa ajabu sana.
Sijui kwanini huwa hata watu hawafungui nyuzi zakujadili mambo muhimu yanayogusa maisha ya wazawa wa hili Taifa directly hasa hili
 
Ni tatizo sugu Sana , na linaanzia kwenye mamlaka zenyewe hasa immigration na wizara ya ajira kuna rushwa kiwango kikubwa cha kutisha na loop holes za kuruhusu Huu upuuzi kufanyika , hii nchi inatia hasira Sana , Mimi sijui hawa wapumbav kwenye hizo wizara na mamlaka kazi Yao huwa ni nini , na si wahindi Tu kuna wachina nao na wapuuz wengine wachina mahindi wanaletwa humu kama experts na wanapewa vibali vya kazi kabisa bila hata assessment yeyote wakati kuna Lundo la watu wenye hizo qualifications na experience humu za hizo kazi nchini .

Mtu mweusi kalaaniwa ,huwa hatujifunzi hata Kwa wenzetu jinsi migration na wizara ya ajira Kwa wenzetu zilivyostrict ? ,Hivi mtanzania unaweza toka hapa ukaenda hapo Kenya au Uganda ukapata ajira kipumbavu kama inavyofanyika humu ?

Inasikitisha sana kwa Mtanzania kuchukua rushwa na kuruhusu mgeni kuingia kufanya kazi ilihali akijua kabisa kwa nafasi hiyo wapo watanzania weengi wanaweza kufanya kazi na kufanya hivyo watanzania wenzako watakuwa nje bila ajira.

Nchi nyingine huwezi kuingia kirahisi namna hiyo na wahusika wote wakakuangalia tu huku wakijua umekuja kuchukua ajira za ndugu zao na wewe huna kipya unacholeta kwao, yaani utaishia airport mfano Zambia, Ghana au Nigeria, Kenya automatically tu mgeni hasa Mtanzania hupati ajira kirahisirahisi aisee.

Haina maana kuwaacha watu wasome na kuwapeleka shule huku nyumbani kwao ambako wanapaswa kuanzia kufanya kazi na kupata uzoefu ajira ni mali ya wageni.
 
Mkuu huu uzi ni muhimu sana kwa mustakali wa taifa letu, lakini kwa kua vijana wenyewe tajwa wako kwenye usingizi mzito sana tegemea uzi huu kukosa wa hangiaji
 
Tatizo linaanzia watu waliowepewa mamlaka kusimamia lakini pia watanzania wengi sio watu wakuchangamkia fursa.

Hili inabidi watanzania wenyewe tupaze sauti..
 
Wachangiaji wa huu uzi wanaweza kuwa wachache. Ila kula tunda kimasihara vijana utawakuta, Nchi hii Mungu ndiyo anajua!!
 
Njooni tulime tuu wazee

Chief wote hatuwezi kulima, na tukilima sijui tutauza wapi maana kila mtu hatakuwa na shida ya chakula.

Pia, naamini huwezi kulima peke yako lazima uwe na wanaokusaidia na kuwalipa ujira ili nao waishi na familia zao.

Ardhi haiwezi kutosha kwa Watanzania wote zaidi ya 60mil tukiamua kulima, kulima pia kwa ufanisi tunahitaji zana bora na za kisasa, nani atengeneze sasa na wote tunalima chief.
 
Ki ukweli kwenye hili tumevamiwa ukizingatia wenzentu wapo vizuri si tuu kwenye kujieleza na hata kwenye maeneo mengine,
 
Tatizo linaanzia watu waliowepewa mamlaka kusimamia lakini pia watanzania wengi sio watu wakuchangamkia fursa.

Hili inabidi watanzania wenyewe tupaze sauti..

mkuu hata mwanao au familia yako unaipeleka shule ili kupata maarifa na kuziona fursa, hawa wasioziona fursa ni watanzania na tatizo litabaki Tanzania, hatuna budi kuwasaidia ili wazione na kuzifikia fursa ili watanzania wote tuishe kwa faraja. Ukiwa na faraja na wanaokuzunguka hawana faraja automatically tu na wewe utakosa faraja.
 
Ki ukweli kwenye hili tumevamiwa ukizingatia wenzentu wapo vizuri si tuu kwenye kujieleza na hata kwenye maeneo mengine,

Ifike mahala hata baadhi ya makampuni ambayo kwa kiasi kikubwa yanaoperate sana ndani ya nchi na wafanyakazi wake wengi ni watanzania basi usahili/Interview ifanyike kwa kiswahili kufavor wazawa.

Serikali ianzishe program maalum za lugha ya kiingereza bure maeneo mbalimbali watanzania wajifunze lugha mbalimbali hasa Kiingereza, French na kichina.
 
Mlio kwenye nafasi ya kutoa vibali vya kazi muuvae uzalendo na kuangalia ndugu zenu. Rushwa ndogo ndogo ambazo zinaumiza ndugu zenu ni laana ambayo haitawaacha salama kwenye uzao wenu, hii ni karma mbaya sana.

Waliobahatika kufanya kazi nje wanafahamu namna wenzetu walivyo makini juu ya kulinda ajira zao, hata wenzetu baadhi ya WaAfrica wamekuwa wakali kwenye hili.

Tuwe serious zaidi kulinda maisha ya familia za wenzetu ambao pia ni watanzania wamesoma, hawakusoma lakini nao wanahitaji kuishi vizuri kwenye ardhi yao.
 
Moja kwa moja kwenye hoja.

Ni wakati sasa wa kuangalia kwa jicho kali ulinzi wa ajira za vijana wa Kitanzania na Watanzania kwa ujumla.

Milango tulioifungua kwa kuruhusu wageni kuingia na kupata ajira kwa hoja ya kadili muwekezaji aonavyo inaanza kuwa hatari kwa ajira za wazawa na mustakabali wa wasomi wa kitanzania.
Hali imeaanza kuwa mbaya mitaani kwa ajira nyingi kupewa wageni sasa hata pale ambako hapastahili.

Serikali inapaswa kuweka jicho kali sasa ili kulinda ajira za wazawa, Waajiri wengi sasa wameanza kuleta wageni hasa indians kutoka India kwa kazi ambazo watanzania wanaweza kuzifanya.
Kenyans, Ugandans nao hawako nyuma wamechangamkia fursa hiyo hasa makampuni ambayo ni mali ya wakenya na waganda. Wahindi wameanza kumiminika kwa wingi saana, na makampuni ya kihindi yanatoa priority kwa indians wenzao bila kujali wako ardhi yenye watu pia.

Kwenye constructions na mining pia kumekuwa na hii changamoto kwa sasa kwa expert wengi kuletwa kwa kigezo cha wazawa hakuna, hata kwa zile kazi ambazo unaweza kufundisha mtu ndani ya mwezi akazifanya au ukapromote mtu ndani ya organization husika.

Upande wa biashara, wageni wanaachwa kuingia ndani kabisa huko kufuata bidhaa za kilimo na kufanya biashara nyinginezo ambazo wazawa wanapaswa kufanya, mkenya hapaswi kufuata parachichi Njombe au nanasi bagamoyo bali ni mtanzania anapaswa kupeleka Kenya au Mkenya asubiri border kwenye soko.
Mchina hapaswi kuwa na duka kariakoo bali ni mtanzania anapaswa kuagiza bidhaa china na kuleta hapa, Mturuki hapaswi kuwa na duka kariakoo bali mtanzania anapaswa kuagiza bidhaa na kuzileta hapa.

Tusipolinda ajira za vijana wetu basi kuna hatari ya vijana wetu kuwa watumwa na wapagazi ndani ya ardhi yao, Jicho kali sana linahitajika hapa na watanzania tuwe wazalendo sasa kulinda ajira za wenzetu hata kama sisi tuna nafasi ya kuishi.

Kenya huwezi kupeleka bidhaa hovyohovyo kwenye masoko yao kama sio mkenya, Kenya huwezi mtanzania kuomba ajira ukapata kirahisirahisi. Kenya ni mfano tu katika mifano mingi katika nchi nyinginezo kama West Africa.
Nchi imefunguliwa na kuwa shamba la Bibi. Ajira chache zilipo, zachukuliwa na wageni tena wasio na sifa kisa wenye kampuni ni watu wa kwao Kuna kampuni, kipindi cha magu wafanyakazi wao wengi walikuwa na mikataba ya mwisho. Baada ya kufariki ile sheria imekanyagwa na wamepewa mikataba mipya na maslahi manono. Viongozi wetu dhaifu sana.
 
kuna nchi zimeendelea sana lakini bado mgeni unahitaji utulize kichwa na utulie ili uweze kupata kazi halali na kuishi na hapo lazima uwe na vibali vyote na ikiwezekana hata kusoma upya, tumekuwa wepesi sana kuruhusu watu kuingia na kufanya kazi hovyohovyo.

Mgeni aje na mtaji wake, awekeze, atoe ajira kwa wazawa hela ibaki na wazawa wajenge na kuwekeza kwao nao.
 
Moja kwa moja kwenye hoja.

Ni wakati sasa wa kuangalia kwa jicho kali ulinzi wa ajira za vijana wa Kitanzania na Watanzania kwa ujumla.

Milango tulioifungua kwa kuruhusu wageni kuingia na kupata ajira kwa hoja ya kadili muwekezaji aonavyo inaanza kuwa hatari kwa ajira za wazawa na mustakabali wa wasomi wa kitanzania.
Hali imeaanza kuwa mbaya mitaani kwa ajira nyingi kupewa wageni sasa hata pale ambako hapastahili.

Serikali inapaswa kuweka jicho kali sasa ili kulinda ajira za wazawa, Waajiri wengi sasa wameanza kuleta wageni hasa indians kutoka India kwa kazi ambazo watanzania wanaweza kuzifanya.
Kenyans, Ugandans nao hawako nyuma wamechangamkia fursa hiyo hasa makampuni ambayo ni mali ya wakenya na waganda. Wahindi wameanza kumiminika kwa wingi saana, na makampuni ya kihindi yanatoa priority kwa indians wenzao bila kujali wako ardhi yenye watu pia.

Kwenye constructions na mining pia kumekuwa na hii changamoto kwa sasa kwa expert wengi kuletwa kwa kigezo cha wazawa hakuna, hata kwa zile kazi ambazo unaweza kufundisha mtu ndani ya mwezi akazifanya au ukapromote mtu ndani ya organization husika.

Upande wa biashara, wageni wanaachwa kuingia ndani kabisa huko kufuata bidhaa za kilimo na kufanya biashara nyinginezo ambazo wazawa wanapaswa kufanya, mkenya hapaswi kufuata parachichi Njombe au nanasi bagamoyo bali ni mtanzania anapaswa kupeleka Kenya au Mkenya asubiri border kwenye soko.
Mchina hapaswi kuwa na duka kariakoo bali ni mtanzania anapaswa kuagiza bidhaa china na kuleta hapa, Mturuki hapaswi kuwa na duka kariakoo bali mtanzania anapaswa kuagiza bidhaa na kuzileta hapa.

Tusipolinda ajira za vijana wetu basi kuna hatari ya vijana wetu kuwa watumwa na wapagazi ndani ya ardhi yao, Jicho kali sana linahitajika hapa na watanzania tuwe wazalendo sasa kulinda ajira za wenzetu hata kama sisi tuna nafasi ya kuishi.

Kenya huwezi kupeleka bidhaa hovyohovyo kwenye masoko yao kama sio mkenya, Kenya huwezi mtanzania kuomba ajira ukapata kirahisirahisi. Kenya ni mfano tu katika mifano mingi katika nchi nyinginezo kama West Africa.
Wakenya wapo agrressive sana katika kutafuta pesa,wanajua kujiuza vzr,communications skills(sio kizungu)yao imekaa vzr,mtu anajielezea vzr utakiri ana PHD,kumbe ka diploma tu.
Makampuni mengi ya nje,huanzia kuweka base Kenya,harafu yanasambaa East Afrika,wakitaka mfanyakazi bongo,wanakuja nae kutoka Kenya,Kuna kampuni ya USA ilipata kazi Zenj,lakini ofisi zipo Dar,basi ikachukua wafsnyakazi kibao Dar ikaenda nao Zenj kupiga kazi!!sasa wenyeji wakawa wanashangaa kwanini hiyo kampuni haikuqnzia Zenj iajiri Zenj?maana kazi tulizokuwa tunafanya hata wenyeji wangeweza kufsnya,wao wakaishia kuwa vibarua tu,Wakenya wanatafuta fulsa mpaka SA!!nimekutana nao huko,wameishaoa wenyeji wanapiga maisha balaa!!vijana wabongo inabidi kujifunza hustle technic za Wakenya sio kuwachukia,kama Mganda,Mkenya anakuja shqmbani kwangu ananunua nanasi,mahindi,ndizi kwa bei poa,kwanini nimkatalie?
Wakenya wananunua mahindi hapa,wanaenda wanasaga unga wanauza Sudan,kwanini na sie tusiuze Malawi??
 
Wakenya wapo agrressive sana katika kutafuta pesa,wanajua kujiuza vzr,communications skills(sio kizungu)yao imekaa vzr,mtu anajielezea vzr utakiri ana PHD,kumbe ka diploma tu.
Makampuni mengi ya nje,huanzia kuweka base Kenya,harafu yanasambaa East Afrika,wakitaka mfanyakazi bongo,wanakuja nae kutoka Kenya,Kuna kampuni ya USA ilipata kazi Zenj,lakini ofisi zipo Dar,basi ikachukua wafsnyakazi kibao Dar ikaenda nao Zenj kupiga kazi!!sasa wenyeji wakawa wanashangaa kwanini hiyo kampuni haikuqnzia Zenj iajiri Zenj?maana kazi tulizokuwa tunafanya hata wenyeji wangeweza kufsnya,wao wakaishia kuwa vibarua tu,Wakenya wanatafuta fulsa mpaka SA!!nimekutana nao huko,wameishaoa wenyeji wanapiga maisha balaa!!vijana wabongo inabidi kujifunza hustle technic za Wakenya sio kuwachukia,kama Mganda,Mkenya anakuja shqmbani kwangu ananunua nanasi,mahindi,ndizi kwa bei poa,kwanini nimkatalie?
Wakenya wananunua mahindi hapa,wanaenda wanasaga unga wanauza Sudan,kwanini na sie tusiuze Malawi??

Ni kosa kuruhusu Mkenya kuingia ndani mpaka shambani na kufuata nanasi eti kwasababu yeye ni hustler, hii sio kweli, kwao hawakuruhusu kufanya hili lazima ukutane na vikwazo kuanzia kwa raia na mamlaka,

Huwezi kuruhusu mhindi kuingia geita eti kununua dhahabu pale Nyarugusu na kuuza nje, aje atoke India na kuwa mchimbaji mdogomdogo, utaratibu lazima ulamzimishe kuwa na mtaji mkubwa wa kuwekeza in large scale.

Mtanzania sio mjinga kama alivyo Mkenya sio mjinga, Mtanzania mfumo umemfanya mnyonge kuanzia shule na mifumo yake, mpaka taratibu za kuishi alizowekewa.
Naamini Mtanzania akiwekewa utaratibu mzuri na kujengewa utaratibu mzuri kuanzia chini kwa maana ya shule hata yeye anawez a kuwa aggressive.

Wakenya wakikutana na Mtanzania mjanja kama wao huwa hawataki urafiki naye na lazima kukwepe maana wanajua wewe ni hatari kwao wakiwa hapa, hupenda sana kudeal na wenzetu wasio na uelewa au uelewa mdogo.

Kenya walichagua mfumo wa ubepari na Mzungu akapafanya kama nyumbani kwake, hili limewabeba sana, ndio maana unaona makampuni mengi yanaanza kuweka base Kenya maana favourable kwao, hapa nasisi inabidi tuje na sytle yetu ya kulazimisha kampuni yeyote kutoka Europe na America yenye operations Tanzania zaidi ya 70% basi headquarter lazima iwe Tanzania.
 
Back
Top Bottom