Hatimae Flora Mbasha awa Flora Kusweka

Hatimae Flora Mbasha awa Flora Kusweka

Hapo kwa kweli ukioa wa hivyo,usinipe kadi ya mwaliko....huo ubest wa u team popo na ufe tu.
hahahaha
yaan nimecheka had nimeamsha majirani
nimeona hata hapo kwa flora viti vitupu
 
KWANI HUYU KUSEKWA NDO KAMUOA FLORA AU FLORA NDO KAMDANGANYA HUYO "MINOR" NA KUMUOA ! KWANI HUYU KUSEKWA NI KUSEKWA YUPI JAMANI ANA ROHO NGUMU HIVI! HII NDOA IMEFUNGWA KWENYE MADHABAHU YA KISHETANI NA SIO YA MUNGU HATA KAMA MADHABAHU HIYO IPO NDANI YA KANISA LA KILOKOLE.NI YA KISHETANI KWA SABABU EMANUEL MBASHA BADO YUPO HAI.HIYO SPIRIT ILIYOMTENGANISHA FLORA NA MBASHA BADO IPO NA SUALA TU LA MUDA,ITAIVUNJA TENA HII NDOA YA SASA HIVI.BAADA YA MUDA MFUPI UJAO, HII SPIRIT YA KISHETANI ITAMFANYA HUYU DOGO KUSEKWA AJITAMBUE.AKISHAJITAMBUA TU ATAONA DAH ! KUMBE NIMEPIGA CHINI HIVII ! DOGO HAPO ATAANZA KUCHEPUKA MAANA ATAONA KUMBE FLORA HAKUWA SIZE YAKE HASA AKILINGANISHA AGE, NA HISTORIA YA HUYO FLORA....HAPO NDO HIYO UNCLEAN SPIRIT ITAIBUA UGOMVI MKUBWA KATIKA NDOA HII MPYA KULIKO ILE YA KWAKE NA MBASHA.
Prophecy... Prophecy.. Prophecy...... [emoji23] [emoji23]
 
KWANI HUYU KUSEKWA NDO KAMUOA FLORA AU FLORA NDO KAMDANGANYA HUYO "MINOR" NA KUMUOA ! KWANI HUYU KUSEKWA NI KUSEKWA YUPI JAMANI ANA ROHO NGUMU HIVI! HII NDOA IMEFUNGWA KWENYE MADHABAHU YA KISHETANI NA SIO YA MUNGU HATA KAMA MADHABAHU HIYO IPO NDANI YA KANISA LA KILOKOLE.NI YA KISHETANI KWA SABABU EMANUEL MBASHA BADO YUPO HAI.HIYO SPIRIT ILIYOMTENGANISHA FLORA NA MBASHA BADO IPO NA SUALA TU LA MUDA,ITAIVUNJA TENA HII NDOA YA SASA HIVI.BAADA YA MUDA MFUPI UJAO, HII SPIRIT YA KISHETANI ITAMFANYA HUYU DOGO KUSEKWA AJITAMBUE.AKISHAJITAMBUA TU ATAONA DAH ! KUMBE NIMEPIGA CHINI HIVII ! DOGO HAPO ATAANZA KUCHEPUKA MAANA ATAONA KUMBE FLORA HAKUWA SIZE YAKE HASA AKILINGANISHA AGE, NA HISTORIA YA HUYO FLORA....HAPO NDO HIYO UNCLEAN SPIRIT ITAIBUA UGOMVI MKUBWA KATIKA NDOA HII MPYA KULIKO ILE YA KWAKE NA MBASHA.
Acha ujuaji.Huyo anayefundisha dini.ndo kaharibu ndoa ya huyo Dada.ni maamuzi sahihi.kama mbasha hamtaki.mke wake.ulitaka flora awe anazini?
 
lakini ni option ya kifo tuuu, ndio huruhusu ndoa ya pili.
ila masuala ya talaka yanataka mlo talikiana mkae hvo hvo single.
Uko sahihi kabisa! Biblia haijaruhusu kabisa kuacha mke/mume kisha ukaoa tena.
Biblia imeruhusu kuacha mke/mume kwa ajili ya zinaa lakini huyo aliyeacha/achwa asioe/asiolewe ili kutoa nafasi ya kusameheana na kurudiana. Hakuna kuoa/kuolewa tena mpaka kifo kitakapowatenganisha!
Lakini kuna mazingira ambayo biblia huruhusu kuoa/kuolewa. Mazingira menyewe ni kuwa ikitokea mmoja ya wanandoa si mwamini wa ukristo, na huyo asiyeamini akaamua kuondoka kwenye ndoa, yule aliyeachwa katika mazingira hayo anaruhusiwa kuoa/kuolewa tena! Lakini mwamini haruhusiwi kuondoka kwenye ndoa hata kama mwenzi wake si muumini wa ukristo ili maadam yuko tayari kukaa naye!
 
Naomba Mnaojua misingi ya Ndoa hasa za Kikristo mnijibu yafuatayo,
Hivi kila Ndoa inayofungwa kanisani na kunukuu viapo Kwa kuvitamka Kwa mdomo huwa kweli zote ni halali na anakuwa kaunganisha MUNGU?
hivi mtu tapeli anaelenga maslahi Wakati maslahi si msingi wa Ndoa nae kukarili viapo na Kutamka anakuwa kaunganishwa na mwenzake Mwenye nia ya dhati na inapaswa Aina hii tuseme kaunganisha MUNGU?,
Iwapo mwanandoa mmoja hakuwa na Nia toka awali ya kuishi milele ktk Ndoa Lkn akakarili kitapeli viapo na kukubali kiuongo ili tu atimize malengo na hii tutasema kaunganisha MUNGU,
Km ni Mpaka kifo kitenganishe Kwa nini mnanukuu kifungu cha uzinzi kinachohalarisha talaka?inamaana uzinzi ndo kifo,
Inakuaje Kwa akina dada na kaka wanaofunga Ndoa Kwa kufuata Mali, na hawa wanapaswa kuhesabiwa km wanandoa ambao Mungu kaunganisha au Mali na tamaa zao zimeunganisha?
Kwa hayo maswali Yangu yanayo akisi kinachofanyika ktk ufungaji wa Ndoa je mnauhakika gani kuwa kila inayoitwa Ndoa huwa kweli imeunganishwa na MUNGU?
Je ni sahihi Ndoa ambayo ilikuwa na utapeli wa misingi na lengo la Ndoa ikivunjika tunapaswa Kusema alichounganisha MUNGU?
Mnajuaje Sasa km ni Ndoa ipi mmoja alimtapeli mwenzake ili iwape usahihi wa kutumia fungu la alichounganisha MUNGU binadamu asitenganishe maana Siri ya dhamira ya MTU kufunga Ndoa anayo muhusika?
Mnaonaje tukisema MUNGU ndo anajua uhalali wa kila Ndoa maana zipo zinazofungwa kibatili Toka mwanzo?
Na hii ya Mbasha mnauhakika gani kuwa ilikuwa si batili since day one au ilikuwa batili since day one?
Nikimdanganya MTU kuwa nipo tayari kuishi nae milele Kwa shida na raha Wakati najua Moyoni sipo tayari na sintadumu nae nimelenga kitu je Ndoa hii nayo imeunganishwa na Mungu?
Mambo ni mengi Sana
MTU hufungwa kwa kamba za kinywa chake! Ukiapa inakuwa hivyo hata kama ulikuwa unadhani unatania! Ukiunganishwa umeunganishwa maana umetoa nafasi kwa kinywa chako kuunganishwa! Suala kuwa ulikuwa unadanganya halipo Bali ulikuwa unaidanganya nafsi yako mwenyewe! Na utavuna matunda ya udanganyifu kwa kujifunga kwenye ndoa mpaka kifo kikutenganishe! Vinginevyo utakuwa umeikana IMANI na sahau habari ya kufika mbinguni!
 
Sitakaa nifanye huo upuuzi wa kubadili jina la ubin wangu! Ndoa zenyewe ni za kukaa mguu ndani mguu nje.
Mbali na hapo nchi yenyewe haieleweki unaweza shangaa unatumbuliwa bure eti watumia cheti feki.
Uwe na IMANI kwanza ndo Mungu anakupa unachokiamini! Ukiamini katika ndoa ya mguu mmoja ndani na mwingine nje ni kweli utapata ndoa ya mguu mmoja ndani na mwingine nje!
Ukiamini kuwa utapata ndoa ya kudumu hadi kifo kiwatenganishe Mungu atakujalia ndoa ya kudumu! Maamuzi ni yako maana siku zote utapata kile unachomiamini!
 
Hivi ninyi mnaobwabwaja humu wangapi Mko kwenye ndoa? Na mmedumu kwa muda gani? Biblia ni Isigeuke kuwa mzigo, kwa habari ya uzinzi na uasherati ni ruhusa kudai au kutoa talaka sasa ninyi mnazijua changamoto zilizokuwa ktk hiyo ndoa hadi wakakubaliana kupeana talaka? Mambo mengine muachage ujuaji
Kwa habari ya uzinzi ni halali kuachana na si kutalikiana! Hakuna kitu kama talaka kwenye ukristo! Lakini pia hakuna ruhusa ya kuoa au kuolewa kwa walioachana kwa sababu ya zinaa Bali wana ruhusa ya kurudiana!
Andiko linaloruhusu kuachana kwa sababu ya zinaa halijaruhusu kuoa tena! Kasome tena biblia yako!
 
Hiyo ilikuwa harusi kati grandmother and grandson
Shame on you Flora Mbashaaaaaass
 
Ndoa ya kikristo inavunjika kwa sababu mbili
Uasherati
Kifo
Sasa kama mbasha alibaka, unataka nini tena!
Ndoa ya kikristo haivunjiki kwa sababu ya uasherati/zinaa. Kwa mujibu wa biblia kuachana si kuvunjika kwa ndoa! Kinachovunja ndoa ni kifo tu maana baada ya kifo hakuna tena nafasi ya kurudiana! Lakini biblia inatoa ruhusa ya walioachana kwa sababu yoyote ile ikiwemo zinaa kurudiana tena maana kuachana kwao hakukuvunja ndoa!
Anayeamini katika ukristo huwa havunji ndoa! Kuvunja ndoa ni alama mathubuti ya kuuasi ukristo na imani yake! Wahusika tuendelee kuwaombea!
 
Back
Top Bottom