Hatimae sasa hoja zote za upinzani zinajibika ‘With high confidence and logic’ ikiwemo suala la Katiba

Hatimae sasa hoja zote za upinzani zinajibika ‘With high confidence and logic’ ikiwemo suala la Katiba

Na hao wanaccm walipojaribu kubadilisha na kutaka kwenda peke yao bado walishindwa. Katiba sio issue ya kikundi cha watu fulani tu. Ikiwa hivyo haitapatikana. Ile ya Warioba ilienda vizuri kwa sababu ilikuwa ya watanzania wote.
Hili jambo ni rahisi, tunapoteza muda bure. Tupigie kura ya maoni rasimu ya warioba.
 
Ila najua na ninaamini wapo wanakijani Tena wengi ambao ndio tatizo wapo tayari kuhujumu au ama wanaihujumu Nia hiyo njema inayoanza kuchomoza kwambaaali🤔
Mkuu, Tatizo sio CCM, tatizo ni kwamba kwenye jamii yetu kuna watu wengi wa ovyoo, wengine wachawi (hawapendi kuona vitu vikienda)n.k hao ndio wanaojiunga kwenye vyama vya siasa randomly (kwa sababu ndio watu tulio nao). Ndio maana tunasisitiza sana, kwamba pamoja na umuhimu wa kuwa na kiongozi bora ambaye sasa angalau tunaye, ni muhimu tukawekeza vile vile kuibadili jamii ambayo ndio domain.
 
Asingeshindwa kulazimisha rasimu ya warioba ipite.
Mkuu, hata ukiwa na nguvu, sio kila mahali unatakiwa kutumia nguvu zako. Utumiaji wa nguvu kulazimisha watu wakubaliane na mawazo yako (yawe mazuri au mabaya) huo ni udikteta.

Aidha, Katiba ni maridhiano ya watu/umma (ndivyo inavyopaswa kuwa) sio enforcement ya mtu fulani mwenye nguvu. Tukitaka liwe zao la mwenye nguvu inawezekana, ila hiyo maana yake ni nini?
 
Yaani wanaweza kujibu hata mwenendo wa uchaguzi na uchaguzi wenyewe uliowaweka madarakani?
 
Mkuu, hata ukiwa na nguvu, sio kila mahali unatakiwa kutumia nguvu zako. Utumiaji wa nguvu kulazimisha watu wakubaliane na mawazo yako (yawe mazuri au mabaya) huo ni udikteta.

Aidha, Katiba ni maridhiano ya watu/umma (ndivyo inavyopaswa kuwa) sio enforcement ya mtu fulani mwenye nguvu. Tukitaka liwe zao la mwenye nguvu inawezekana, ila hiyo maana yake ni nini?
Nimemaanisha kulazimisha kwa hao unaosema walimzuia. Ile ilikuwa na uungwaji mkono wa wananchi kwahiyo isingekuwa udikteta.
 
Nimemaanisha kulazimisha kwa hao unaosema walimzuia. Ile ilikuwa na uungwaji mkono wa wananchi kwahiyo isingekuwa udikteta.
Kwa maana ulitaka mzee Kikwete a override bunge la katiba? sasa bunge la katiba si lisingekuwa halina maana yoyote ya kuwepo katika mazingira kama hayo? Lakini pia huoni ni jambo la hatari kutegema mtu mmoja ku force mambo yanayohusisha watu wengi badala ya mifumo kufanya kazi yake? sasa hii ya ku force siku tukipata rais mwenda wazimu na ndio tukawa tushajijengea huo utamaduni, nini kitatokea?

Kwa uzoefu wa maeneo mengine duniani mfano Kenya walifanyaje?
 
Kwa maana ulitaka mzee Kikwete a override bunge la katiba? sasa bunge la katiba si lisingekuwa halina maana yoyote ya kuwepo katika mazingira kama hayo? Lakini pia huoni ni jambo la hatari kutegema mtu mmoja ku force mambo yanayohusisha watu wengi badala ya mifumo kufanya kazi yake? sasa hii ya ku force siku tukipata rais mwenda wazimu na ndio tukawa tushajijengea huo utamaduni, nini kitatokea?

Kwa uzoefu wa maeneo mengine duniani mfano Kenya walifanyaje?
Wabunge wa ccm walikuwa wanakutana na kupewa maelekezo nini waseme bungeni. Jk ndiye alikuwa kinara wa kubadilisha maoni ya wananchi kule bungeni. Wangekuwa huru kuchangia isingefikia pale.
 
katiba mpya NI muhimu Sana hasa kwa nyakati hizi .kwani tatizo ni nn mpaka hili suala la katiba ,lichukue muda mrefu bila kufanyiwa kazi!? Nini shida!?
 
Wabunge wa ccm walikuwa wanakutana na kupewa maelekezo nini waseme bungeni. Jk ndiye alikuwa kinara wa kubadilisha maoni ya wananchi kule bungeni. Wangekuwa huru kuchangia isingefikia pale.
Unamuonea bure JK. Kumbuka yeye ndio aliunda tume ya Warioba na akamchagua kuwa wenyekiti, hivyo alikuwa na total control ya tume. Kwa maana hiyo angataka chake ndio kiwe conclusion, angeiagiza tu tume iandike ripoti kama atakavyo yeye, na tume idai ndio maaoni ya wananchi kisha awaambie wajume waipitishe kwa nguvu moja.

Asingekuwa na sababu ya kuacha tume iandike ripoti asiyotaka halafu awapangie wajumbe cha kusema kupinga ripoti ambayo yeye alikuwa na uwezo wa kuifanya iandikwe atakavyo toka mwanzo.

Hivyo, dhamira yake ilikuwa ipatikane katiba halisi na sio ya kubumba ndio maana yeye akakaa pembeni.
 
katiba mpya NI muhimu Sana hasa kwa nyakati hizi .kwani tatizo ni nn mpaka hili suala la katiba ,lichukue muda mrefu bila kufanyiwa kazi!? Nini shida!?
Shida ni kukosekana kwa uelewa wa pamoja na makundi hasa vyama vya siasa kuitizama kwa maslahi ya vyama badala ya maslahi ya Taifa. Hiki pia ndicho kilichokwamisha mchakato 2014.

Kwa hiyo tatizo hilo ni lazima litatuliwe kwanza kwa kujenga uelewa wa pamoja na kuaminiana ili kuepuka kurudia makosa yale yale.
 
Unamuonea bure JK. Kumbuka yeye ndio aliunda tume ya Warioba na akamchagua kuwa wenyekiti, hivyo alikuwa na total control ya tume. Kwa maana hiyo angataka chake ndio kiwe conclusion, angeiagiza tu tume iandike ripoti kama atakavyo yeye, na tume idai ndio maaoni ya wananchi kisha awaambie wajume waipitishe kwa nguvu moja.

Asingekuwa na sababu ya kuacha tume iandike ripoti asiyotaka halafu awapangie wajumbe cha kusema kupinga ripoti ambayo yeye alikuwa na uwezo wa kuifanya iandikwe atakavyo toka mwanzo.

Hivyo, dhamira yake ilikuwa ipatikane katiba halisi na sio ya kubumba ndio maana yeye akakaa pembeni.
Lakini akaweza kubadilisha maoni ya wana ccm wengi juu ya kumpitisha lowassa kama mgombea.

Uwezo alikuwa nao sana na akaamua kwa makusudi kuliingizia taifa hasara ya zaidi ya bilioni 300.
 
Lakini akaweza kubadilisha maoni ya wana ccm wengi juu ya kumpitisha lowassa kama mgombea.

Uwezo alikuwa nao sana na akaamua kwa makusudi kuliingizia taifa hasara ya zaidi ya bilioni 300.
Mkuu, sio kila kitu kinachopendwa na wengi ni sahihi. Mtu anaweza kuchaguliwa na watu wengi na akawa na changamoto ambazo wapiga kura hawazijui.

Hivyo usiamini sana kinachoitwa 'wengi' hasa bongo. Wabongo wanaulizwa kwenye mkutano wa hadhara 'Nimtumbue huyu au nisimtumbueeeee" wanajibu mtumbueeeeeee...... halafu ukiwauliza kosa lake nini hakunaanayejua.

Kwa mfano, nenda mtaani waulize watu, tuwe na serikali au tusiwe na serikali uone wengi watakuambia nini!

Hivyo kwenye vitu vya msingi ni lazima pawe na watu wenye uelewa mzuri wanaoongoza wengine na kura tu au maoni tu haitoshi.
 
Mkuu, sio kila kitu kinachopendwa na wengi ni sahihi. Mtu anaweza kuchaguliwa na watu wengi na akawa na changamoto ambazo wapiga kura hawazijui.

Hivyo usiamini sana kinachoitwa 'wengi' hasa bongo. Wabongo wanaulizwa kwenye mkutano wa hadhara 'Nimtumbue huyu au nisimtumbueeeee" wanajibu mtumbueeeeeee...... halafu ukiwauliza kosa lake nini hakunaanayejua.

Kwa mfano, nenda mtaani waulize watu, tuwe na serikali au tusiwe na serikali uone wengi watakuambia nini!

Hivyo kwenye vitu vya msingi ni lazima pawe na watu wenye uelewa mzuri wanaoongoza wengine na kura tu au maoni tu haitoshi.
Hoja hapa ni kwamba uwezo alikuwa nao sana na akaamua kuacha kukamilisha mchakato wa katiba iliyoletwa na Jaji Warioba.
 
Uko sahihi kabisa mkuu, sema kunakuwa na tofauti juu ya namna ya kulishughulikia suala hilo miongoni mwa vyama vya siasa, kwa sababu licha ya vyama vya siasa kudai katiba mpya ni kwa maslahi ya taifa, kuna wanaoliangalia kwa jicho la maslahi ya vyama. Ndio maana inahitajika kutengenezwa mazingira rafiki na ulewa wa pamoja kabla ya kuanza tena mchakato huo ili tusije kukwama kama tulivyokwama 2014. Hivyo dhamira ni njema kabisa kwamba sasa tuende kisayansi badala ya emotions.
Kwa hiyo katiba mpya siyo baada ya 2025 tena?
 
Ccm ni kama nyoka kuna wakati anakuwa na gamba la kigaidi, gamba la kifisadi na sasa amevaa gamba la utapeli wa kisiasa.
Chuki tu bro. Acha chuki zisizokuwa na mantiki. Ukiwa na chuki huwezi ukaona vitu kwa jicho halisia. Utakuwa unaona mauza uza tu.
 
Wapo wengi sana. Wana woga na hofu kwamba mambo yao yataharibika. Lakini mi watoe wasi wasi tu hakuna kitakachoharibika.

Ncho itaongozwa kwa misingi ya Utawala bora
Hofu si kuongozwa kwa nchi, bali hofu ya wana CCM wengi hasa wabunge ambao ndiyo wenye kufanya maamuzi, ni kwamba kama kutakua na demokrasia nzuri, ikifika kipindi cha uchaguzi wengi wao watapoteza majimbo. Kumbuka wengi walibebwa na udictator wa JPM dhidi ya vyama vya upinzani. Kuna majimbo ambayo demokrasia ikirudi na wahusika wa vyama vya upinzani wakagombea, hakuna hata kujiuliza, walioko sasa wa CCM lazima wapoteze. Sasa watu kama hao huwezi kutegemea wapende maridhiano na hali ya siasa inayojengwa sasa na SSH.
 
Uchamadola wa CCM ndio tatizo. JKN na JMK wote hawa kuwa tayari kuachana nao. JPM ndio alitaka kuturudisha chama kimoja kabisa. Mama akiliweza hili ataiokoa tanzania. Kuondoa uchamadola inahitaji mapambano na watanzania kutoka kwenye "ukondoo wa nyerere" .
 
Maoni yangu ni kwamba jk hakuwa na nia ya kuleta katiba mpya. Aliweza kumuibia lowassa ushindi ndani ya chama na nje ya chama ingawa alikuwa na nguvu sana. Asingeshindwa kulazimisha rasimu ya warioba ipite.
Uko sahihi kabisa. Rasimu ya katiba mpya chini ya Jaji Warioba, alimaarufu "Rasimu ya Warioba" au wakati mwingine hata ikiitwa "Katiba ya Warioba", ni mwiba mkali sana kwa CCM. Ukipenda waweza kuiita ni sumu kali sana kwa CCM.

Waliovuruga mchakato wa katiba mpya ni CCM baada ya kuona hatima yao (hatima ya CCM) kama rasimu ile ikipitishwa na kuwa KATIBA.

Waelewe kwamba vyama huzaliwa na kufa lakini nchi hubaki. Watapata vyama vingine na maisha kuendelea... Waangalie Kenya na nchi zingine, vyama vya awali vya nchi hizo havipo, lakini wale waliokua katika vyama hivyo wanagombea na kupata uongozi na nchi inaendelea.

Hapo Kenya tu, huwezi kuamini kwamba kulikua na KANU, lakini maendeleo yao yako mara dufu kutuzidi sisi wenye lichama la tangu uhuru.

Watanzania tunahitaji Katiba mpya.
 
Hili jambo ni rahisi, tunapoteza muda bure. Tupigie kura ya maoni rasimu ya warioba.
Rahisi kabisa na hiyo itapunguza gharama, kuliko kupeleka rasimu ikajadiliwe na eti bunge la katiba ambalo majority ni CCM. Rasimu ya Warioba ni maoni ya wananchi, na katiba ni ya sisi wananchi. Sasa haya maoni kwa nini tena yakajadiliwe na wabunge wa CCM? Kumbuka, kwa muundo wa bunge la katiba, hata iwe vipi, majority huwa ni CCM, ndiyo maana nasema bunge la katiba la CCM. Wakati wa kuchukua maoni kwa wananchi, hawakua wanawafuata watu kivyama, waliwahoji watanzania.

Rasimu ya Warioba ndiyo katiba bora kwa watanzania.
 
Back
Top Bottom