Hatimaye bondia kutoka Ufilipino avalishwa gloves zenye rangi ya bendera ya Tanzania ya jiwe Tanzania ya viwanda

Hatimaye bondia kutoka Ufilipino avalishwa gloves zenye rangi ya bendera ya Tanzania ya jiwe Tanzania ya viwanda

Pongezi kwa serikali ya awamu ya tano kwa ushindi wa bondia Hassan Mwakinyo.
 
Mleta mada hujui mchezo wa ngumi kaangalie marudio kisha uje utoe huu uchafu wako.

Ngumi za mfilipino zilikuwa hazina maana yoyote ile katika pointi, pia tizama ngumi za mwankinyo zilikuwa zinalenga kichwani.

Ngumi sio kupiga piga tu ili mradi, kuna maeneo muhimu ya kupiga.
mkuu soma mada vizuri ...nilipost kabla ya pambano mkulungwa
 
Mwakinyo uwezo wake ni wa kawaida sana kuliko tunavyoaminishwa....hayuko vizuri kwenye kushambulia (mikono ni mizito sana) hata kujilinda pia(anapaki basi sana)...ameruhusu ngumi nyingi za tumboni ambazo zinakata pumzi...kwa kifupi amejitahidi lakini amebebwa....Dogo Mfaume...yule aliepigana pambano la mwisho la utangulizi ni bondia mzuri sana....anajua kushambulia na kujilinda pia anajiamini sana...Mwakinyo aachane na mapromo makubwa wakati uwezo wa kawaida...afanye mazoezi kwanza.

Kweli kabisa, watu hawataki kusema ukweli
 
Nakumbuka vizuri lile pambano lake na muagentina lililopigiwa Kenya, nami niliona kama jamaa hana kasi sana, ila ninaamini kwa umri wake, ana mengi ya kujifunza na huenda akawa bora sana huko mbeleni, tumpe muda na sapoti yetu atafika tu.
Yah! Muhimu akubali kujifunza zaidi na zakdi. Arekebishe makosa yake nadhani kambi yake inapaswa kurekebisha makosa haya kabla ya pambano jingine, sababu anavyoshinda anazidi kupanda, atakutana na mabondia wa viwango vya juu zaidi makosa kama haya atakuwa anaambulia vipigo tu.
 
Watanzania wengi tu wajuaji ila hatujui. Pambano la ngumi hawahesabu ngumi za tumbo na mikono
 
Sisi tulioanza kufuatilia ndondi enzi za kina George Lister Sabuni, Koba Kimanga, Joseph Marwa, Rashid Matumla, Mbwana Matumla, Maneno Oswald "mtambo wa gongo", Hassan Matumla, Haji Matumla, Mzonge, Michael Yombayomba ni dhahiri huyu bwana mdogo anatudanganya
 
Sijawahi kuwaelewa Wabongo 99.5% ni majitu ya hovyo, majuaji na yasiyopenda vya kwao ni malimbukeni sana.

Big up Mwakinyo umefanya vema sana.
Ndugu yangu wala usipate tabu ..boxing inamakundi na kunawatu hata mwakinyo angefanya vizuri vipi bado wangesema kapendelewa. Kumbuka walikuja hapa na kusema Tinampay ni bondia mchovu hivyo wamemtafuta aje ili kumpaisha mwakinyo, leo gemu limekuwa zuri wanasema tena Mwakinyo kashindwa. Mimi binafsi najua kunawatu wa makundi mengi ya boxing wanachuki sana na mwakinyo kwa yale mafanikio ameyapata. Niseme tu walimbeza sana myweather alipopigana na pac na nikwasababu wanafikiri kurusha mangumi mengi ndio ushindi. Watanzania muache chuki pindi mnapokuwa hamjapata nafasi fulani kama za wenzenu..hiyo itawasaidia kupata maendeleo. Linapokuja suala la taifa tuwe pamoja..ni mambo ya ajabu sana ya watu hawa.
 
Yah! Muhimu akubali kujifunza zaidi na zakdi. Arekebishe makosa yake nadhani kambi yake inapaswa kurekebisha makosa haya kabla ya pambano jingine, sababu anavyoshinda anazidi kupanda, atakutana na mabondia wa viwango vya juu zaidi makosa kama haya atakuwa anaambulia vipigo tu.
Kabisa mkuu, anatakiwa atafute makocha bora na watu sahihi wa kumuunga mkono apate kutimiza ndoto zake.
 
Back
Top Bottom